Pre GE2025 Askofu Bagonza: Ushahidi wa Marko Ng'umbi unasambaratisha uhalali wa TAMISEMI na tume “huru” kusimamia chaguzi kwa uhuru na haki

Pre GE2025 Askofu Bagonza: Ushahidi wa Marko Ng'umbi unasambaratisha uhalali wa TAMISEMI na tume “huru” kusimamia chaguzi kwa uhuru na haki

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798
Askofu Bagonza

"Jumapili ya 1 September mosi 2024, mmoja wa watekaji wa 4R alijitokeza hadharani na kutoa siri kuwa alihusika katika kuvuruga Nchi na kufanya uhaini wa serikali dhidi ya wananchi, ni aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Longido anayeitwa Marko Henry Ng'umbi, Rais ametengua uteuzi wake ndani ya masaa lakini ni vyema tukatafakari ushahidi alioutoa kwa kina

1. Kwamba, madiwani wote wa wilaya hiyo walipitishwa bila kupingwa kwa njama za serikali. Hawana uhalali (Legitimacy). Je madiwani haramu waweza kutunga sheria halali katika Halmashauri zetu?

2. DC Mtenguliwa anakiri kushiriki operesheni za maporini katika wilaya kadhaa. Je zilikuwa zipi hizo? Haziwezi kuwa za kuiba kura kwa sababu madiwani walipita bila kupingwa. Jinai haiozi; utenguzi ufuatwe na uchunguzi.

3. Kama DC katenguliwa kwa kusema uwongo, taifa haliko salama. Kama katenguliwa kwa kusema ukweli usiotakiwa kusemwa, taifa haliko salama zaidi. Ukweli na uwongo wa DC Mtenguliwa ndicho kiini cha kifo cha 4R.

4. Walioteka 4R na kuzikataa sirini na hadharani, hawawezi kumpenda kwa dhati muasisi wa 4R. Wanaochukia 4R hawawezi kuwapenda watu wanaonufaika na 4R. Kutekana, kutesana hata kuuana maporini ni matokeo ya kuzichukia 4R na muasisi wake. Hata ndani ya serikali na chama tawala, wapenzi wa 4R wako hatarini.

5. Ushahidi wa DC Mtenguliwa unasambaratisha uhalali wa TAMISEMI na tume “huru” kusimamia chaguzi kwa uhuru na kwa haki kwa sababu mapori yapo. Tusishupaze shingo. Naona msururu mrefu wa wanaosubiri kumwaga siri zaidi.

Najiuliza: Nani alimrekodi na kurusha clip hii? Hiyo pia ni dalili ya ugomvi ndani ya chama na serikali kati ya watekaji na watetezi wa 4R.

Mheshimiwa Rais asiishie kutengua waropokaji. Hata KM wa chama asiishie kukanusha wanaojinadi kuteka au kutishia kutumia dola kukimbia na masanduku.

Kinachowawasha waropokaji hatukijui lakini kwa hakika waropokaji hawa ni maadui wa CCM kuliko wapinzani.

Pia soma
 
Askofu Bagonza

"Jumapili ya 1 September mosi 2024, mmoja wa watekaji wa 4R alijitokeza hadharani na kutoa siri kuwa alihusika katika kuvuruga Nchi na kufanya uhaini wa serikali dhidi ya wananchi, ni aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Longido anayeitwa Marko Henry Ng'umbi, Rais ametengua uteuzi wake ndani ya masaa lakini ni vyema tukatafakari ushahidi alioutoa kwa kina

1. Kwamba, madiwani wote wa wilaya hiyo walipitishwa bila kupingwa kwa njama za serikali. Hawana uhalali (Legitimacy). Je madiwani haramu waweza kutunga sheria halali katika Halmashauri zetu?

2. DC Mtenguliwa anakiri kushiriki operesheni za maporini katika wilaya kadhaa. Je zilikuwa zipi hizo? Haziwezi kuwa za kuiba kura kwa sababu madiwani walipita bila kupingwa. Jinai haiozi; utenguzi ufuatwe na uchunguzi.

3. Kama DC katenguliwa kwa kusema uwongo, taifa haliko salama. Kama katenguliwa kwa kusema ukweli usiotakiwa kusemwa, taifa haliko salama zaidi. Ukweli na uwongo wa DC Mtenguliwa ndicho kiini cha kifo cha 4R.

4. Walioteka 4R na kuzikataa sirini na hadharani, hawawezi kumpenda kwa dhati muasisi wa 4R. Wanaochukia 4R hawawezi kuwapenda watu wanaonufaika na 4R. Kutekana, kutesana hata kuuana maporini ni matokeo ya kuzichukia 4R na muasisi wake. Hata ndani ya serikali na chama tawala, wapenzi wa 4R wako hatarini.

5. Ushahidi wa DC Mtenguliwa unasambaratisha uhalali wa TAMISEMI na tume “huru” kusimamia chaguzi kwa uhuru na kwa haki kwa sababu mapori yapo. Tusishupaze shingo. Naona msururu mrefu wa wanaosubiri kumwaga siri zaidi.

Najiuliza: Nani alimrekodi na kurusha clip hii? Hiyo pia ni dalili ya ugomvi ndani ya chama na serikali kati ya watekaji na watetezi wa 4R.

Mheshimiwa Rais asiishie kutengua waropokaji. Hata KM wa chama asiishie kukanusha wanaojinadi kuteka au kutishia kutumia dola kukimbia na masanduku.

Kinachowawasha waropokaji hatukijui lakini kwa hakika waropokaji hawa ni maadui wa CCM kuliko wapinzani.

Pia soma
Screenshot_2024-07-16-21-00-20-1.png
 
Askofu Bagonza

"Jumapili ya 1 September mosi 2024, mmoja wa watekaji wa 4R alijitokeza hadharani na kutoa siri kuwa alihusika katika kuvuruga Nchi na kufanya uhaini wa serikali dhidi ya wananchi, ni aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Longido anayeitwa Marko Henry Ng'umbi, Rais ametengua uteuzi wake ndani ya masaa lakini ni vyema tukatafakari ushahidi alioutoa kwa kina

1. Kwamba, madiwani wote wa wilaya hiyo walipitishwa bila kupingwa kwa njama za serikali. Hawana uhalali (Legitimacy). Je madiwani haramu waweza kutunga sheria halali katika Halmashauri zetu?

2. DC Mtenguliwa anakiri kushiriki operesheni za maporini katika wilaya kadhaa. Je zilikuwa zipi hizo? Haziwezi kuwa za kuiba kura kwa sababu madiwani walipita bila kupingwa. Jinai haiozi; utenguzi ufuatwe na uchunguzi.

3. Kama DC katenguliwa kwa kusema uwongo, taifa haliko salama. Kama katenguliwa kwa kusema ukweli usiotakiwa kusemwa, taifa haliko salama zaidi. Ukweli na uwongo wa DC Mtenguliwa ndicho kiini cha kifo cha 4R.

4. Walioteka 4R na kuzikataa sirini na hadharani, hawawezi kumpenda kwa dhati muasisi wa 4R. Wanaochukia 4R hawawezi kuwapenda watu wanaonufaika na 4R. Kutekana, kutesana hata kuuana maporini ni matokeo ya kuzichukia 4R na muasisi wake. Hata ndani ya serikali na chama tawala, wapenzi wa 4R wako hatarini.

5. Ushahidi wa DC Mtenguliwa unasambaratisha uhalali wa TAMISEMI na tume “huru” kusimamia chaguzi kwa uhuru na kwa haki kwa sababu mapori yapo. Tusishupaze shingo. Naona msururu mrefu wa wanaosubiri kumwaga siri zaidi.

Najiuliza: Nani alimrekodi na kurusha clip hii? Hiyo pia ni dalili ya ugomvi ndani ya chama na serikali kati ya watekaji na watetezi wa 4R.

Mheshimiwa Rais asiishie kutengua waropokaji. Hata KM wa chama asiishie kukanusha wanaojinadi kuteka au kutishia kutumia dola kukimbia na masanduku.

Kinachowawasha waropokaji hatukijui lakini kwa hakika waropokaji hawa ni maadui wa CCM kuliko wapinzani.

Pia soma
Ndiyo maana Serikali inampenda sana Askofu Bagonza!

Hoja zake si za kitoto!
 
Naungana na askofu mimi pamoja na Lucas Mwashambwa, johnthebaddest pamoja nae Tlaatlaah bila kusahau timu lumumba buku7fc
mueleze Askofu namuheshimu sana,
na ninaheshimu sana uhuru, haki, maoni na mtazamo wake kuhusu uongozi na mambo ya uchaguzi uliopita....

muelezeni tu kwamba mambo yanabadilika, sasa hivi tinayo serikani ya awamu ya sita na iko kazini chini ya kiongozi shupavu na na kipenzi cha wananchi wote Tanzania Dr Samia Suluhu Hassan...

dhamira ya dhati, nia Njema na mipango mikikati ya Serikali ya awamu ya sita katika kuliunganisha taifa na kuifungua nchi miongoni mwa mataifa ya ulimwengu haihisiani kabisaa na awamu za uongozi zozote zilizopita.....

kiongozi yeyote wa umma sasa, mwenye mindset, mawazo au fikra za awamu zilizopita kwenye awamu hii adilifu na chapakazi ataondolewa mara moja kwenye nafasi yake kwasabb atakua anamuhujumu Rais na ananaturudisha nyuma kama taifa..

hali ya kua sisi waTanzania wote kwa ujumla tunasonga mbele kwa bidii sana 🐒
 
Huyo mbwa achunge kondoo,kutwa siasa, viongozi wenzie wa dini waliposhiriki mauaji ya albino,liwati nk alitia neno!?
mtumishi anapokengeuka na kuwa mwana siasa mchumia tumbo ndiyo hawa wanaacha kondoo wanatawanyika kwa maslahi yao binafsi
 
mwanamwana,

..miaka ya 70 mgombea Uraisi wa chama cha Republican alimfanyia hujuma mgombea wa Democrats huko Marekani.

..tukio hilo lilikuja kugundulika na kujulikana kama kashfa ya Watergate [ Watergate scandal. ].

..waandishi wa habari wa kiuchunguzi, Bob Wooward, na Carl Bernstein,waliibebea bango kashfa hiyo, na mtonyaji wao alikuwa Afisa ndani ya shirika la uchunguzi la FBI.

..Kwa miaka kadhaa mtonyaji hakujulikana ni nani, bali alipewa jina la siri, " DEEP THROAT. "

..Miaka mingi baadae mtonyaji akiwa amezeeka alikuja kujitokeza hadharani.

..Kashfa ya Watergate ilimlazimisha Raisi wa Marekani RICHARD NIXON kujiuzulu.
 
Huyo mbwa achunge kondoo,kutwa siasa, viongozi wenzie wa dini waliposhiriki mauaji ya albino,liwati nk alitia neno!?
Sitaki kuamini hiyo comment yako imemlenga msomi anayeheshimika ndani na nje ya Tz, Dr. Bagonza!

Dr. yupo sahihi kupiga kelele pale anapoona mambo yanaenda ndivyo sivyo! Uchungaji ni kuhakikisha usalama na ustawi wa kondoo. Atanyamazaje anapoona viashiria vinavyohatarisha usalama wa kondoo wake?

Waliofanyiwa figusu na wengine "kupotezwa" ni miongoni mwa kondoo wake!
 
Askofu Bagonza

"Jumapili ya 1 September mosi 2024, mmoja wa watekaji wa 4R alijitokeza hadharani na kutoa siri kuwa alihusika katika kuvuruga Nchi na kufanya uhaini wa serikali dhidi ya wananchi, ni aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Longido anayeitwa Marko Henry Ng'umbi, Rais ametengua uteuzi wake ndani ya masaa lakini ni vyema tukatafakari ushahidi alioutoa kwa kina

1. Kwamba, madiwani wote wa wilaya hiyo walipitishwa bila kupingwa kwa njama za serikali. Hawana uhalali (Legitimacy). Je madiwani haramu waweza kutunga sheria halali katika Halmashauri zetu?

2. DC Mtenguliwa anakiri kushiriki operesheni za maporini katika wilaya kadhaa. Je zilikuwa zipi hizo? Haziwezi kuwa za kuiba kura kwa sababu madiwani walipita bila kupingwa. Jinai haiozi; utenguzi ufuatwe na uchunguzi.

3. Kama DC katenguliwa kwa kusema uwongo, taifa haliko salama. Kama katenguliwa kwa kusema ukweli usiotakiwa kusemwa, taifa haliko salama zaidi. Ukweli na uwongo wa DC Mtenguliwa ndicho kiini cha kifo cha 4R.

4. Walioteka 4R na kuzikataa sirini na hadharani, hawawezi kumpenda kwa dhati muasisi wa 4R. Wanaochukia 4R hawawezi kuwapenda watu wanaonufaika na 4R. Kutekana, kutesana hata kuuana maporini ni matokeo ya kuzichukia 4R na muasisi wake. Hata ndani ya serikali na chama tawala, wapenzi wa 4R wako hatarini.

5. Ushahidi wa DC Mtenguliwa unasambaratisha uhalali wa TAMISEMI na tume “huru” kusimamia chaguzi kwa uhuru na kwa haki kwa sababu mapori yapo. Tusishupaze shingo. Naona msururu mrefu wa wanaosubiri kumwaga siri zaidi.

Najiuliza: Nani alimrekodi na kurusha clip hii? Hiyo pia ni dalili ya ugomvi ndani ya chama na serikali kati ya watekaji na watetezi wa 4R.

Mheshimiwa Rais asiishie kutengua waropokaji. Hata KM wa chama asiishie kukanusha wanaojinadi kuteka au kutishia kutumia dola kukimbia na masanduku.

Kinachowawasha waropokaji hatukijui lakini kwa hakika waropokaji hawa ni maadui wa CCM kuliko wapinzani.

Pia soma
Huyu Rais kawategua Nape, na huyu mkuu wa wilaya, kwa nini hamtumbui Mkwewe kwa kwa kuropoka kwenye ile clip ya kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa? Au kwa sababu damu nzito kuliko maji?
 
Back
Top Bottom