Askofu Bagonza: Wabunge wamekubaliana na Serikali kuwanyonya wananchi

Askofu Bagonza: Wabunge wamekubaliana na Serikali kuwanyonya wananchi

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
4,016
Reaction score
6,759
"Tozo za miamala ya simu zimeunganisha mihimili bunge na serikali dhidi ya wananchi na walaji. Katiba inatenganisha mihimili hii miwili. Tozo zimeiunganisha. Ni kinyume cha katiba. Wabunge wamekubaliana na serikali kuwanyonya wananchi. Nani mtetezi wa wananchi?"

Askofu Bagonza
 
Watanzania wengi wanataka kufanya kazi Kama polisi. Hata wabunge wenyewe wameingia mkumbo huo. TRA, TCRA, TANESCO hata makatibu muhtasi kwenye ofisi za serikali wote siku hizi wamekuwa mapolisi.

Sent from my Infinix X656 using JamiiForums mobile app
 
"Tozo za miamala ya simu zimeunganisha mihimili bunge na serikali dhidi ya wananchi na walaji. Katiba inatenganisha mihimili hii miwili. Tozo zimeiunganisha. Ni kinyume cha katiba. Wabunge wamekubaliana na serikali kuwanyonya wananchi. Nani mtetezi wa wananchi?"

Askofu Bagonza
ETI ndio WAWAKILISHI wa WANANCHI
4f39d9bc1ca7277d2210a03bfc610604.jpg
 
Mwambie atulie!

Si ndio huyu nae alikuwa anademka tu siku Mwigulu anasoma bajeti?
 
Wananchi Tanzania miaka yote hawana mtetezi, na hata wananchi wakiamua kukimbilia kwenye mhimili wa tatu (mahakama) nako watashindwa kwasababu hizo tozo tayari zipo kisheria, hapa wananchi ni sawa na tumefungwa pingu mikononi na miguuni.
 
Hio ndio tafsiri ya "USHINDI WA KISHINDO (Kupita Bila Kupingwa)" Baba Askofu. Acha watanzania mpaka akili ziwasogee. Serikali yote CCM, Bunge lote CCM, Serikali za mitaa zote CCM, Mahakama zote CCM. Wananchi walitegemea nini??? Kumwita Tundu Lissu msaliti??? Acha sasa waone ni kina nani wasaliti kama sio CCM!!!!

Huko Kahama wamachinga wamechezea virungu kutoka kwa Mkurugenzi na Polisi. Mwanza watu wamekamatwa na Polisi. Mtaani kila sehemu ni vigenge vya kujadili hizi kodi mpya (Wakulima Kupandishiwa Kodi + Kodi Ya Mbolea + Kodi Ya Mafuta + Kodi Ya Mitandao Ya Simu + Kodi Ya Wavuvi).

Ama kweli CCM wana fitina mpaka kwa Mwenyekiti wao, wamejua kumchonganisha na raia, na wameamua sasa asimalize miaka 5 yake kama walivomfanyia Rais Mzee Mwinyi.

Safari hii swala la katiba hakizimiki hata kwa magari ya zima moto. Mtaani pata chimbika dadeki.
 
CAG Kichere katishiwa maisha yake kisa kufanya kazi zake lakini si samia au yeyote yule ndani ya hii Serikali ya waporaji uchaguzi aliyekemea vitisho hivyo.

Tunahimizwa tuchangie kodi lakini ubadhirifu ukifanyika hauwekwi hadharani na wala hakuna anaewajibija. Matokeo ya tume ya wizi wa BoT yamefanyiwa kazi gani?
 
"Tozo za miamala ya simu zimeunganisha mihimili bunge na serikali dhidi ya wananchi na walaji. Katiba inatenganisha mihimili hii miwili. Tozo zimeiunganisha. Ni kinyume cha katiba. Wabunge wamekubaliana na serikali kuwanyonya wananchi. Nani mtetezi wa wananchi?"

Askofu Bagonza
Huyu ni askofu asieelewa nn anakifanya ila anatumia haki yqke kikatiba kutoa maoni yake lkn uenda yeye Ni msomi kuliko Mimi lkn muumba bado hajamfahamisha maana navyotambua mihimili ya nchi iko mitato yaan mahakama bunge na serikal Sasa huyu serkali ndo kila kitu na rahis wa awamu ya tano alituambia ukwel hakuficha kwamba yeye ndo mkuu wa dola wengine mumsikilize yeye lkn Kama haitoshi nimuongezee askofu kwamba Dola Ni ukabaji,uporaji,ujasusi na dhuluma dhidi ya raia wake Sasa ukihubir haki au ukiitaka haki serkalini Ni kupikia jiko la kuni kwenye mafuriko ebu ajikite kwenye kuwaelekeza watu wasiwashangalie viongoz wa serkali pale wanapokuja na uongo isipokuwa wakimbilie kanisani wamuache mwana siasa abwabwaje mwenyewe
 
Back
Top Bottom