Askofu Dkt. Bagonza amshukia Lugola kwa kumfananisha Magufuli na Yesu. Asema hii laana lazima itafune mtu na Taifa

Askofu Dkt. Bagonza amshukia Lugola kwa kumfananisha Magufuli na Yesu. Asema hii laana lazima itafune mtu na Taifa

Mimi binafsi naona wazi Lugola anakera sana sana kuanzia kwa wananchi wa kawaida naamini vile vile anamkera sana Mh Rais wetu, lugha za Lugola ni za hovyo, hafai kuwa kiongozi, ni bahati mbaya tu alipewa uwaziri, naamini pia Oct 2020, CCM sitegemei impe nafasi ya kupita kugombea tena, Lugola ana maneno ya kufuru sana, mengi na anamkera sana Mh. Rais naamini hivyo, Lugola hapimi maneno yake vema kabla ya kuongea, na ana uwezo mdogo sana wa kufikiri
 
We unaongea kwa hisia. Wenzio tunaongea kwa kuona. Yaani unatumia hearsays.

Jibu Hoja usirahisishe mambo ,unaposema jambo flani ina maana unataka kufilisha ujumbe flani uio ukusudia.

Lugola amemfananisha Mh Rais na Yesu ,je ni sahihi ?
 
Mimi binafsi naona wazi Lugola anakera sana sana kuanzia kwa wananchi wa kawaida naamini vile vile anamkera sana Mh Rais wetu, pia naamini lugha za Lugola ni za hovyo, hafai kuwa kiongozi, ni bahati mbaya tu alipewa uwaziri, naamini pia Oct 2020, CCM sitegemei impe nafasi yq kupita kugombea tena, Lugola ana maneno ya kufuru sana, mengi na anamkera sana Mh. Rais naamini hivyo, Lugola hapimi maneno yake vema kabla ya kuongea, na ana uwezo mdogo sana wa kufikiri
Mh rais anapenda kutukuzwa ndio maana akina Lugola, Kessy na wengineo wasaka vyeo wanajua ukimsifu bwana mkubwa anakuteua.
Na wenyewe wanapiga mule mule sema huyu Kange amepitiliza
 
Mwanzo ulikuwa una tetea kitu gani na sasa unasema nini ..!!
Haya kangi kashasema ni kama yesu je kuna cha kubadilisha kwenye kauli yake? au ndio kupotezeana muda kujadili jambo ambalo limeshasemwa na hakuna wa kulibadili, Mimi ninachojua ni kwamba, MAGUFULI SIO YESU KIRISTO, bali ni mwanadamu kama alivyokuwa Yesu kiristo akiwa hapa duniani.
 
Anaandika Baba Askofu Rev.Dr.Benson Bagonza (PhD), Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
___________
Kufuru haina kinga. Kwa Wakristo, dhambi isiyosameheka katika Agano Jipya ni kumkufuru Roho Mtakatifu. Na katika Agano la Kale ni ibada ya sanamu (idolatry). Amri ya kwanza aliyopewa Musa inasema, "Mimi ni Bwana Mungu wako, usiwe na miungu mingine" (Kutoka 20:3-6).
_
Kufuru haina kinga duniani wala mbinguni. Ghadhabu ya Mungu iko wazi katika vitabu vyake vyote.

Tuzitendee haki kumbukumbu zetu;

1. Mwaka 2005 mjinga mmoja alitumia uhuru wake vibaya huko Denmark. Akachora katuni yenye kumdhihaki Mtume Muhammad (S.A.W). Dunia nzima iliwaka moto.

2. Mwaka 2010 mpuuzi mwingine huko Marekani akachoma moto Quran tukufu. Hakuna jiwe lililosalia juu ya jiwe.

3. Mwaka 2012 huko Mbagala utoto ukavuka mipaka. Msahafu ukakojolewa. Amani yetu ilitoweka kwa muda. Majivu yakawa majivu.

4. Huko Sumbawanga, msimu wa uchaguzi kama huu, ulimi wa mmoja uliteleza. Akaufananisha UTATU mtakatifu na mafiga matatu ya chama chake. Hapakutosha. Mzee Pinda (mtu wa amani), ana cha kusimulia mpaka leo.

Mungu wetu hafananishwi. Mungu wetu halinganishwi. Mungu wetu hashindanishwi. Ni ibada ya sanamu kupenda kitu kingine kuliko unavyompenda Mungu wako. Ni ibada ya sanamu kuchukia kitu kingine kuliko unavyomchukia shetani. Ni ibada ya sanamu kumlinganisha Muumbaji na uumbaji wake.

Hatumtendei haki Mungu kumlinganisha na aliowaumba. Hatuwatendei haki wale tuwapendao kwa kuonesha kuwa tunawapenda kuliko tunavyompenda aliyewaumba.

Walinzi na waangalizi wa imani (viongozi wa dini), kama hatuwezi kukemea hili (la Lugola) basi angalau tuchukie na tuonekane kweli tumechukizwa.!
Na spika akakaa kimya bila kukemea na kuamuru hiyo kauli ifutwe. Ina endelea kubaki kwenye kumbukumbu za bunge kwamba kuna mpuuzi mmoja alimuita Magufuli ni sawa na Kristo na maneno ya huyo mpuuzi yana ishi kwenye kumbukumbu za bunge la ajabu la Tanzania lililo ongozwa na Ndugai... Hii ni aibu
 
Hivi hamjui kwamba Yesu ni mwana wa Adamu na ni mwanadamu kama wanadamu wengine?? Yesu Kiristo "Mwana wa Adamu" ni kwamba Yesu alikuwa kweli binadamu. Mungu alimwita nabii Ezekia "mwana wa Adamu " mara 93. Mungu kwa njia nyingine alikua anamwita Ezekia binadamu. Mwana wa Adamu ni binadamu. Yesu alikuwa Mungu kamili (Yohana 1:1), lakini pia alikuwa binadamu (Yohana 1:14). Sasa neno "KAMA" Linapelekea mfanano wa moja kwa moja wa Magufuli kuwa YESU KIRISTO hapo ndipo sjui.
 
Haya kangi kashasema ni kama yesu je kuna cha kubadilisha kwenye kauli yake? au ndio kupotezeana muda kujadili jambo ambalo limeshasemwa na hakuna wa kulibadili, Mimi ninachojua ni kwamba, MAGUFULI SIO YESU KIRISTO, bali ni mwanadamu kama alivyokuwa Yesu kiristo akiwa hapa duniani.

Upotoshwaji na Ujinga hauwezi kuachwa bila ya kukemewa Sababu utaharibu Taifa ,imagine ingekuwa amemfanisha na wa upande ule unafikiri ni nini kinge tokea !?.

Katika maneno ya Busara ya Baba Askofu ametoa mifano iliyo sababisha kutokea Mauaji na uharibifu wa Mali pia na kuchochea Chuki kwa baadhi ya Wajinga kufanya kama alivyo fanya Lugola,nimeahindwa kujua ni unasoma tu kama isha au tatizo ni uelewa wako.
 
Utatu mtakatifu ni mambo yaliyosukwa tu na wajanja! Kamwe huwezi kumgawa Mungu eti nafsi tatu!! Najibu swali! Alimlinganisha JPM na Yesu (nabii) kwa kuwa amejitoa mhanga kama Yesu alivyoteseka ili kuukomboa ulimwengu. Anaikomboa Tz kutoka mikononi mwa mafisadi. Ni hatari kwake ila amejitoa mhanga.
KOMA kumfananisha YESU na midude mingine
 
Shida ya Mzee wangu Bagonza amejaa chuki, Chuki Imemjaa hata kwenye vitu vidogovidogo tu.
Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni, hiyo ni kufuru ya wazi we unadai ana chuki? We kwako ni sawa Magu ni kama Yesu? Huko kusifia ndiko kunasababisha mnashindwa kumkemea pindi akoseapo huyo mpenda sifa kipofu wewe
 
Upotoshwaji na Ujinga hauwezi kuachwa bila ya kukemewa Sababu utaharibu Taifa ,imagine ingekuwa amemfanisha na wa upande ule unafikiri ni nini kinge tokea !?.

Katika maneno ya Busara ya Baba Askofu ametoa mifano iliyo sababisha kutokea Mauaji na uharibifu wa Mali pia na kuchochea Chuki kwa baadhi ya Wajinga kufanya kama alivyo fanya Lugola,nimeahindwa kujua ni unasoma tu kama isha au tatizo ni uelewa wako.
Halafu bagonza sio mwema kiasi cha kuwanyooshea wengine vidole.
 
Bagonza anafikili anaweza kuchukua nafasi ya mungu? Hawezi ku finally hukumu ya mungu kwa binadamu hata siku moja, pia akumbuke kuna watu wanaitwa yesu hapa duniani kwa maana hiyo hao hawatasamehewa kwa vile wamejiita jina la yesu?

Pia lazima ajue mfano sio lazima iwe kitu halisi,
Ujuaji anaotaka kujifanya anao Bagonza unamuondolea hadhi ya kuwa Askofu.

Kuna wanasiasa wanasema uongo na anajuwa wanasema uongo na wengine ni waumini wake mbona hatujaona andiko kuwakemea ili waache uongo kwa kuwa vitabu vya dini vinasema usimsemee mtu uongo, pia uongo ni zaidi ya mchawi, sasa hilo halijui?
Mapenzi yake kisiasa hayamzuii kuacha uaskofu ili aje apambane kama mwanasiasa kwa kuwa yeye hatakuwa wa kwanza, kuna Dr slaa, kuna marehem rwakatale kuna msigwa na wengine wengi.
Yeye anashambulia upande wa CCM tu je huko Upinzani ni watakatifu?
Maaskofu wa hivi laana zao watazibeba wenyewe maana mungu anaiona mioyo yao inavyohangaika na maovu wanayowaza kika siku.
Bagonza ajitathimini.
Mbona mifano aliyoiainishi pale mwanzo iko wazi? lakini Yesu alofananishwa na Magu sio hao binadamu wanaoitwa yesu vile vile ukumbuke kauli ya mkuu wa mkoa wa tabora siku za nyuma kuhusu Mungu amshukuru Magu japo aliitolea ufafanuzi. Anaepinga na askofu ndo ana chuki
 
Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni, hiyo ni kufuru ya wazi we unadai ana chuki? We kwako ni sawa Magu ni kama Yesu? Huko kusifia ndiko kunasababisha mnashindwa kumkemea pindi akoseapo huyo mpenda sifa kipofu wewe
Mkuu tukubaliane kwamba Magu sio Yesu, ila kangi amesema RAIS MAGUFULI ni kama Yesu, kwa maana hyo ni kwamba, Magu(ulivyomtaja wewe) sio Yesu.
 
Halafu bagonza sio mwema kiasi cha kuwanyooshea wengine vidole.

Umeshindwa kutetea ulicho kuwa ukikisema mwanzo na kurukia Maisha binafsi ya Mtu ,jifunze kujadili Hoja na sio kumjadili mleta Hoja.

Lugola kumfananisha Mh Rais na Yesu ni sahihi !?
 
Anaandika Baba Askofu Rev.Dr.Benson Bagonza (PhD), Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
___________
Kufuru haina kinga. Kwa Wakristo, dhambi isiyosameheka katika Agano Jipya ni kumkufuru Roho Mtakatifu. Na katika Agano la Kale ni ibada ya sanamu (idolatry). Amri ya kwanza aliyopewa Musa inasema, "Mimi ni Bwana Mungu wako, usiwe na miungu mingine" (Kutoka 20:3-6).
_
Kufuru haina kinga duniani wala mbinguni. Ghadhabu ya Mungu iko wazi katika vitabu vyake vyote.

Tuzitendee haki kumbukumbu zetu;

1. Mwaka 2005 mjinga mmoja alitumia uhuru wake vibaya huko Denmark. Akachora katuni yenye kumdhihaki Mtume Muhammad (S.A.W). Dunia nzima iliwaka moto.

2. Mwaka 2010 mpuuzi mwingine huko Marekani akachoma moto Quran tukufu. Hakuna jiwe lililosalia juu ya jiwe.

3. Mwaka 2012 huko Mbagala utoto ukavuka mipaka. Msahafu ukakojolewa. Amani yetu ilitoweka kwa muda. Majivu yakawa majivu.

4. Huko Sumbawanga, msimu wa uchaguzi kama huu, ulimi wa mmoja uliteleza. Akaufananisha UTATU mtakatifu na mafiga matatu ya chama chake. Hapakutosha. Mzee Pinda (mtu wa amani), ana cha kusimulia mpaka leo.

Mungu wetu hafananishwi. Mungu wetu halinganishwi. Mungu wetu hashindanishwi. Ni ibada ya sanamu kupenda kitu kingine kuliko unavyompenda Mungu wako. Ni ibada ya sanamu kuchukia kitu kingine kuliko unavyomchukia shetani. Ni ibada ya sanamu kumlinganisha Muumbaji na uumbaji wake.

Hatumtendei haki Mungu kumlinganisha na aliowaumba. Hatuwatendei haki wale tuwapendao kwa kuonesha kuwa tunawapenda kuliko tunavyompenda aliyewaumba.

Walinzi na waangalizi wa imani (viongozi wa dini), kama hatuwezi kukemea hili (la Lugola) basi angalau tuchukie na tuonekane kweli tumechukizwa.!
Hatochelewa kujibu soon. Keep cool.
 
Lugola kumfananisha Mh Rais na Yesu ni sahihi !?
Hakuna mahali Kangi amemfananisha Yesu Kristo mwana wa Adamu na Rais Magufuli, bali ametumia neno kama, neno ambalo halina mfanano wa moja kwa moja na kitu husika, Sasa wewe kwa akili yako unadhani YESU KRISTO MWANA WA ADAMU Anaweza kufananishwa na Mwandamu hapa duniani ingawa na Yeye YESU KRISTO alikuwa ni mwanadamu???? 😫👂
 
Back
Top Bottom