Black Butterfly
Senior Member
- Aug 31, 2022
- 130
- 368
"Ninaona na ninaamini mchakato ule wa maridhiano umetekwa, siwezi kusema Rais ndiye ameuteka kwa sababu yeye ndiye aliyeuanzisha ila ninahisi kuna nguvu nyingine tusiyoiona ambayo imeteka mchakato ule wa maridhiano na kutaka kulirudisha taifa letu katika sintofamu"- Dkt. Bagonza.
Dkt. Benson Bagonza ambaye ni Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Dayosisi ya Karagwe akizungumza na kituo cha habari cha Busokelo TV hivi karibuni hasa baada ya viongozi waandamizi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wanachama wa chama hicho, wanaharakati na wanahabari kukamatwa na Jeshi la Polisi maeneo mbalimbali ya Tanzania.