#COVID19 Askofu Gwajima: Nasubiri wataalamu wa ndani wa chanjo ya COVID-19 waongee kisha nitawapiga kwa risasi moja tu watawanyike

#COVID19 Askofu Gwajima: Nasubiri wataalamu wa ndani wa chanjo ya COVID-19 waongee kisha nitawapiga kwa risasi moja tu watawanyike

Gwajima anasema viongozi na wataalamu wetu ni vigeugeu na hawafai kuongoza, Wanafanya mambo kwa kuangalia upepo na sio utaalamu

Anasisitiza wajiuzulu mapema kwenye suala la covid-19

Akihutubia maelfu ya waumini wake leo Gwajima amesema wataalamu wetu ndio hao walijenga pale Muhimbili jiko la kujifukiza nyungu na waliwaaminisha wananchi kuwa chanjo hazifai

Gwajima anasema Leo ghafla wataalamu hao wanahubiri chanjo, Je wanamdanganya nani?

Gwajima anahoji lile jiko sasa wanaalitumia kwa kazi gani pale Muhimbili kwani waliokataa chanjo ndio hao vinara wa kusisitiza chanjo

Gwajima anasisitiza hao wataalamu wa ndani walete Papers au Research zao wamefanya lini na wapi kuhusu chanjo za korona.

Gwajima anasema waje wataalamu hao wa ndani waeleze Madhara ya muda mrefu na mfupi wa chanjo ndio hapo atakuja na Maswali magumu ya kufanya watawanyike

Anasema viongozi makini wangejiuzulu kazi hawafai kuongoza Taifa kwa kuwa vigeugeu kwa kuangalia nani anaongoza juu yao
Huyu Ndugu zamani Nilikuwa namdharau Sana lakini kwa hili la Corona..day...aisee...
 
Hivi kwanini mnashindwa kujibu hoja zake badala yake mnatukana tu. Sasa ukiulizwa kati yake na ninyi nani ni mbuzi utajibu nini? Nafikiri ni vyema kujikita katika kujibu hoja zake. Kweli swali langu pia ni madhara gani yataweza kutokea kwa wale wanaopata hiyo chanjo baada ya miaka kadhaa baada ya kupata hiyo chanjo? Kipi kitatokea kwa watoto watakaozaliwa kwa wazazi hao waliopata chanjo? Tatizo tunaweka siasa mbele. Pia tunaangalia nani kasema. Muda mwingine Mungu anaweza kumtumia huyo mnayemzalau kuwaletea ujumbe na mkaukataa.
Nina mfano ulionikuta mwenyewe tarehe 10/07/2021 nilisimamishwa na ofisa wa usalama barabarani akanipiga faini ya kutovaa mkanda lakini pia akaongea maneno kadhaa nikaondoka kwenda ninakoenda lakini njiani pia kuna mtu nilimchukua alikaa siti ya nyuma na watoto wangu
Kilomita kadhaa tulipata ajali na yule mtu niliyemchukua aliwashikilia watoto wangu muda ajali inatokea. Nilipokuwa nikitafakari ndipo nilipoambiwa kuwa yule ofisa wa usalama barabarani alipewa neno kuniambia mimi kwa sababu mbele kulikuwa kunaenda kutokea ajali. Vile nimefundishwa kusikia sauti ya Mungu sikupuuza na nikawa salama.
Kikubwa tusipuuze tunayombiwa ila ukweli anaujua Mungu kama una mashaka nenda akuoneshe ukweli ni upi maana maneno yamekuwa mengi hata muda mwingine tunakosa utulivu wa kuyachambua na kupata majibu sahihi kabisa. Hivi watu mnapolumbana huku wengine walishapewaga majibu hata kabla chanjo haijafika kama kuna madhara au laa. Nasema hayo kwa sababu mimi mwenyewe nilishapewa majibu ya hiyo chanjo.
Ushauli wangu ni kwamba usiweke tumaini lako kwa mwanadamu maana mwanadamu atakufa atakuacha na shida zako.
Ukweli ni kwamba ndani ya leadership na medical professionals hakuna anayeweza kujibu hoja zake
 
Mpaka hapo wazungu wameweza kutuaminisha kwamba chanjo ni wewe mwenyewe kuchukua tahadhari kama sivyo iweje uchanje afu uteseke na mabarakoa
 
Anachotaka ni nini hasa? Hayo mambo si yaliisha isha?

Amesahahu kama yenyewe iliiambia hiyo misukule yake kwamba haiwezi kugombea ubunge maana ni demotion?

nimeshagundua kinachoisumbua hii mbuzi inataka umaarufu wa kuongelewa mitandao
hatuwezi kutembelea akili za yule mwendawazimu aliedharau korona akafa kwa korona na maujinga yake
Muacheni mtumishi wa mungu. Atakupiga mpaka utawanyike kusikojulikana. Kwani ameongea uongo? Wasomi si vigeugeu kutegemeana rais ni nani au wao wenyewe hawajui lolote bali walikalili tu
 
Dodoma hapakalini. Pale wamemwaga Damu ya Lissu kila wakifika pale miguu inawasha.

Rejea mlima Gilboa alikouawa Mfalme Sauli palilaaniwa pakakosa Mvua na umande na hakuna mtu wa maana anapakaa.
Mkuu hivi mtu wa maana ni mtu gani!
 
Huyu jamaa yeye ndio kigeugeu namba moja, hatofautishi agenda za dini na siasa, afu hiyo chama iliyompa nafasi ya siasa haina hata namna ya kumthibiti, may be thy like the way he is rolling the ball.
Mlimpaje ubunge??? hamkujua kuwa ni askofu na ana imani hiyo. Nyamaza milele hayo mambo ya siasa na dini yaache, you seem stupid
 
Anachotaka ni nini hasa? Hayo mambo si yaliisha isha?

Amesahahu kama yenyewe iliiambia hiyo misukule yake kwamba haiwezi kugombea ubunge maana ni demotion?

nimeshagundua kinachoisumbua hii mbuzi inataka umaarufu wa kuongelewa mitandao
hatuwezi kutembelea akili za yule mwendawazimu aliedharau korona akafa kwa korona na maujinga yake
Kwa nini mijitu mijinga huwamnajianika kiasi hiki, Wewe unaongelea kipi sasa kwenye hoja za gwajima?
 
Kutofautiana mitazamo kunasaidia kurekebisha hali. Serikali ilipashwa kuanza na utoaji elimu kuhusu chanjo. Kuleta taarifa za tafiti mpya kwa sababu kila siku kuna taarifa mpya. Mfano kwanini kuna variant tofauti tofauti kunatokana na nini...then faida za chanjo ni zipi.

Kumshutu Gwajima na kumtusi sio mwisho wa majadiliano.
 
Back
Top Bottom