#COVID19 Askofu Gwajima: Ni jambo baya sana kuwapa Chanjo ya Corona Wanajeshi, Polisi na watu wa Usalama

#COVID19 Askofu Gwajima: Ni jambo baya sana kuwapa Chanjo ya Corona Wanajeshi, Polisi na watu wa Usalama

Umenena vyema mkuu
Huyu mtu ni mjinga kabisa tena he is fool maneno anayo sema unahisi kichwani kuna funza... lkn ukweli anajua kila kitu isipokuwa anatengeneza attention kwake ili aendele kuwa na wa waumini wengi. Unajua kama huja pata msiba wa ndugu au jamaa aliyefarika na CORONA unaweza kuleta masikhara sn kwenye jambo hili lkn kama umepata misiba huwezi kufanya masikhara hata kidogo.
 
Huyu Rashid anafilimbwa nini?
*Corona naifunga haitaingia Tanzania- ikaingia
* Siwezi kugombea ubunge, Urais -kagombea ubunge.
*Naizimisha corona haitakaa Tanzania- Imeua watu na bado iko.
Sasa huyu mbona ni kigeugeu kuliko watu wote nchini?
 
Kwa hio Gwajima ana maanisha kwamba Rais Samia ni kigeugeu. Ila yeye hajioni alivyo kigeugeu na alivyo muongo (Waumini wanasubiri ile treni aliowaahidi kununua).


Hongera zake Gwajima kwa kumrushia mawe SSH.
Miaka ya sabini Rais Nyerere alipoanzisha Sera ya vijiji vya ujamaa, kuna mbunge mmoja machachali alitoka hadhalani na kumpinga Mwl. Nyerere kuwa hiyo Sera haifai.
Mwl. Nyerere alikasirishwa sana na kitendo hicho cha mbunge huyo wa jimbo la Karagwe Mhe.Kaneno ambae kwa sasa ni marehemu.

Alimfuta uanachama wa TANU na hivyo akupoteza ubunge Moja kwa moja na ukaitishwa uchaguzi na akachaguliwa mbunge mwingine.

Sasa yetu macho, ngoje tuone huu mnyukano wenye viashiria vya uasi na uchochezi kati ya Mama na mbunge wa chama chake.
Muda utaongea na historia itahukumu.
 
Tunaambiwa tukachanje ila waziri mkuu, rais au makamu hawachanji tukawaona...
Tunaambiwa inakuja chanjo fulani kisha tunamuona waziri wa zamani anachanja chanjo ya urusi...

Kwani mtu yeyote kuchanjwa wewe inakuhusu nini? Chanjo si hiari?

Inasemekana vigogo wote wakiwamo kina Jobo walishachanjwa. Unavyowaona hawana pressure. Ile ni nguvu ya chanjo wala si nguvu ya buku.

Kwamba kuwaona wakichanjwa?Labda kama una maana wachanjwe kwa mara nyingine tena?
 
Wewe Unajuaje kama anapotosha????? Hivyi askofu gwajima sio mtanzania kama alivyo rais samia???? Au wewe ukiambiwa na waziri wa afya ndo unamwamini sana kuliko askofu gwajima!! Utofauti wao ni madaraka ndugu lakini kwenye swala la ufahamu yamkini askofu gwajima yupo mbali sana, atakayezikubali hizi chanjo ni mtu asiyeelewa tu!!! Unataka uniambie hao wote akina kigwangala walikuwa wapi wakati wa Magufuli!! Wewe huoni kuwa ni wanafiki tu!! Kutetea matumbo yap tu, wakati wa maombolezo watu wamejazana kila mahari, mpaka leo wamejazana!! Pale kigoma! Hiyo corona ipo wapi???? Msifanye wantanzania wajinga

??????

Kwenye mada, kauli ya serikali (inayowajibika na mustakabala wa afya zetu) kuhusiana na protokali za kushughulika na Ugonjwa huu umeiona?

Serikali inayowajibika ni ile inayotimiza kajukuu yake kwa mujibu wa protokali mbalimbali za kimataifa. Kauli ya serikali anayoibeza gwajima inavyo vigezo vyote vyenye kuendana na protokali hizo.

Kauli ya serikali inatokana na mapendekezo ya tume ya wataalamu wabobezi iliyokuwa imeundwa na SSH.

Kauli ya gwajima haina mashiko isiyokuwa na tofauti na kauli za kibwetere zilizopelekea msiba mkubwa.

Kauli ya gwajima inaelekea kule kule ilikoishia kauli ya kibwetere.
 
Elimu yetu Tanzania haijatutendea haki. Bado tu wajinga kupita kiasi. Sasa ona JF ambao tunaona wanauelewa kidogo lakini wanaakili kama au chini ya Gwajima. Inakuwaje hadi mtu anamaliza hadi form four hajui basics za chanjo?
Na kitu kimoja nimegundua, wajinga huwa paranoid sana. Kazi sana kureason nao.

Chanjo wandugu zipo za aina nyingi sana. Kuna chanjo ya Typhoid. Chanjo ya Typhoid kila baada ya miaka mitatu inaisha nguvu. Inatakiwa kuchoma kila baada ya miaka mitatu.
 
Huyu mtu ni mjinga kabisa tena he is fool maneno anayo sema unahisi kichwani kuna funza... lkn ukweli anajua kila kitu isipokuwa anatengeneza attention kwake ili aendele kuwa na wa waumini wengi. Unajua kama huja pata msiba wa ndugu au jamaa aliyefarika na CORONA unaweza kuleta masikhara sn kwenye jambo hili lkn kama umepata misiba huwezi kufanya masikhara hata kidogo.
Uzuri wa corona inaweza kupita naye yeye mwenyewe
 
Tuanze naye, alituambia Corona haitaingia Tanzania, ikaingia, sasa hivi anatuambia tumuachie Corona apambane nayo, nani atamuamini?

Kama anajiamini anafufua wafu aanze kumfufua yule alietangulia mwezi wa tatu, kinyume na hapo aache kusema wenzake wakati na yeye ni msanii tu.
Huyu ni askofu wa wajinga tuu!
 
Uzuri wa corona inaweza kupita naye yeye mwenyewe
Tena naomba kwa MMUNGU nayeye impate ili ajue kuna mambo ya mchezo yakutafutia umaarufu na Majanga yaliyo kuwa serious hayataki masikhara .
 
Njia zilizotumika kumpatia Ubunge anajua hazikuwa sahihi na haki haikutendeka lakini Leo hii hajawahi popote kuukataa ubunge wake Wala japo kuukubali lakini kutumia kanisa kukemea pale ambapo hakukuwa na haki

Amekywepo kwenye utawala wa awamu iliyopita ambapo tulishuhudia na kusikia watu wakipoteza uhai na kutekwa na watu wasiojulikana, tulishudia risasi adharani lakini hakuna siku amewahi kutoka adharani kukemea uvunjivu wa sheria na katiba ya nchi

Alikuwepo BUNGENI juzi wakati tozo kandamizi zinapitishwa hakuna siku tulimsikia akipinga na kura alipiga ya ndiyo. Hata hao waoumini wake hajawahi kuwaonea huruma, mshahara wake alipi Kodi na hatumsikii akikemea.

Leo anaibuka anaanza kumjadili JPM kwamba wakati wake hakuna aliyeleta chanjo. Je wakati wa JPM wakati watu wanabambikiwa kesi yeye hakuwepo? Alitusemea? Wakati watu wanakufa kwa corona alisema? Wakati tunaficha data alisema? Leo ametoa wapi ujasiri wakutumia nyumba za ibada kutaka kujifanya yeye ni daktari?

Tunaporuhusu watu wa aina ya Gwajima waongoze jamii ndipo tunapozalisha mawazo mgando. Yeye anaamini JPM alikuwa Mungu na kwamba maarifa ya JPM lazima yaheshimiwe hata Kama yalikuwa hayafai, kwamba Leo badala atueleze Mungu anasemaje anatulazimisha tufuate nyayo za binadamu ambaye ana mapungufu mengi ya wazi. Hii dini gani yakuelekeza watu wamwabudu mtu?

Leo ndipo amekuwa na msimamo, mbona huo msimamo upo kwa mambo ya mwendazake haupo kwa wengine?

Huyu mtu apuuzwe, siyo kiingozi wa dini Bali ni Kiongozi wa walafi wa madaraka. Kwenye siasa anataka, kwenye dini anataka na kwenye ushirikina anataka. Yeye Nani wakuombea watu wafe kisa awakubaliani naye? Unasiamama madhabauni unabiri kuua watu unadhani waumini wako wanajitunza Nini? Kwamba wanaokwenda kinyume na mtizamo wako na JPM wafe? Nani kakwambia ninyi ni miungu? Kwamba wewe utokufa?

Nadhani huyu mtu kwa kuwa tu Ni mwana ccm anayo haki yakutumia kanisa anavyojisikia yeye Tena kwa mambo ya hovyo kinyume kabisa na imani yake. Ila ipo siku ataadhibiwa
Huyu bwana ni hatari sana kwa nchi hii sijui kwanini hata ameruhusiwa kugombea ubunge!
 
Samia naye ndiye wale wale. Karibu wiki sasa hajasikika sijui naye COVID-19 imeshamsarandia? Alifanya kosa kubwa kuwaacha Mawaziri wote wa dhalimu mwendazake. Sasa dharau zao kwake nje nje. Akiona yamenshinda abwage manyanga. Kwani hii vuta nikuvute ya timu Kikwete na timu mwendazake siyo kabisa.
hahaaaaaa alisambaza usalama kila kona.alijiona yeye ndo yeye kuna mtu alisema Mungu amshukuru magufuli kwa aliyoyafanya.akafuta uchaguzi mkuu wabunge wote wa chadema akafukuza akateka watu akapiga risasi wapinzani.leo mdude yupo huru nje bora tuongozwe na mwanamke
kuliko magufuli
 
Mbunge wa bunge la JMT kupitia jimbo la Kawe mh Josephat Gwajima amesema ni balaa kubwa kuchagua Kigeugeu kuwa kiongozi katika jambo lolote lile.

Mkiwa na Kiongozi anayebadilikabadilika kulingana na maslahi yake binafsi basi mjihesabu " mmekwisha" maana yeye anaijua kesho yake tu na siyo kesho yenu, amesema.
Ujumbe uwafikie wanalumumba wote na kule Mwanakwerekwe
 
Kwamba?

"...na sio group la waswahili ni hao hao wazungu mnao waamini na kuwaabudu."

Madhara ya porojo za mwendazake.

😂😂😂!

Hiiiiii bagosha!
Ujinga wa aina hii, no wonder hili bara lina zaidi ya miaka 50 ya uhuru lakini zaidi ya asilimia 70 ya watu wake ni masikini wa kutupwa..akili kama hizi hizi
 
Wewe kilaza hata chanjo ya pepopunda huwa inarudiwa rudiwa, ukichanjwa mara moja haimaanishi hutapata kabisa pepopunda.
Mambo ya Roho acha yaende kiroho. Anaongoza kundi kubwa la watu anapenda hawavushe.

unapewa chanjo bado utakufa kwa Corona ukipata na pia utaambukizwa Corona, sasa kazi ya Chanjo ni nini mwako.

“Madhara ya hiyo Chanjo yatabaki kwa mhusika na siyo Serikali “ hata hii kauli hauelewi
Siyo yeye hata mi sitachoma na Family yangu
 
Wengi wanakifahamu au wamewahi kukisikia kisa cha Joseph Kibweteere wa Uganda mshirika aliyejitenga kutoka kanisa katoliki na akaanzisha huduma yake iliyokuwa na mafundisho mengi ya ajabu lakini ikijitambulisha kama dhehebu la Kikristo.

Kilele cha huyu bwana ilikuwa March 17,2000 alipowafungia waumini wake takribani 700 ndani ya kanisa akawaaminisha mwaka 2000 ulikuwa mwisho wa dunia na wakakubali kuchomwa moto wote hadi kufa huko Kanungu Uganda.

Kibwetere mwenyewe haiweleweki mpaka leo kama alijichoma moto na washirika wake au yeye alichoropoka, mpaka leo amebaki katika listi ya mojawapo wa watu wanaotafutwa sana Uganda.

Nikirudi hapa nyumbani katika video na taarifa ziliozasambaa sana leo ni pamoja na ya Askofu Gwajima akihubiri kanisani kwake akiwasisitiza sana wafuasi wake wakatae chanjo kwa sababu wanaweza kugeuka mazombi.

Ameenda mbali zaidi akiipuzulia mapendekezo ya kamati ya wataalamu wa serikali iliyondwa kumshauri Rais katika suala la Corona.

Njia inayoonekana bora katika kukabiliana na Corona mpaka sasa ni chanjo, ikiwa Gwajima atasikilizwa na kutiliwa maanani na maelfu ya watu katika makundi hatarishi ya kupata na kufa kwa korona atakuwa hana tofauti na Kibweteere wa Uganda
Wengi wanakifahamu au wamewahi kukisikia kisa cha Joseph Kibweteere wa Uganda mshirika aliyejitenga kutoka kanisa katoliki na akaanzisha huduma yake iliyokuwa na mafundisho mengi ya ajabu lakini ikijitambulisha kama dhehebu la Kikristo.

Kilele cha huyu bwana ilikuwa March 17,2000 alipowafungia waumini wake takribani 700 ndani ya kanisa akawaaminisha mwaka 2000 ulikuwa mwisho wa dunia na wakakubali kuchomwa moto wote hadi kufa huko Kanungu Uganda.

Kibwetere mwenyewe haiweleweki mpaka leo kama alijichoma moto na washirika wake au yeye alichoropoka, mpaka leo amebaki katika listi ya mojawapo wa watu wanaotafutwa sana Uganda.

Nikirudi hapa nyumbani katika video na taarifa ziliozasambaa sana leo ni pamoja na ya Askofu Gwajima akihubiri kanisani kwake akiwasisitiza sana wafuasi wake wakatae chanjo kwa sababu wanaweza kugeuka mazombi.

Ameenda mbali zaidi akiipuzulia mapendekezo ya kamati ya wataalamu wa serikali iliyondwa kumshauri Rais katika suala la Corona.

Njia inayoonekana bora katika kukabiliana na Corona mpaka sasa ni chanjo, ikiwa Gwajima atasikilizwa na kutiliwa maanani na maelfu ya watu katika makundi hatarishi ya kupata na kufa kwa korona atakuwa hana tofauti na Kibweteere wa Uganda
Bora kibwetere hakuwa kiongozi serikalini
 
Njia zilizotumika kumpatia Ubunge anajua hazikuwa sahihi na haki haikutendeka lakini Leo hii hajawahi popote kuukataa ubunge wake Wala japo kuukubali lakini kutumia kanisa kukemea pale ambapo hakukuwa na haki

Amekywepo kwenye utawala wa awamu iliyopita ambapo tulishuhudia na kusikia watu wakipoteza uhai na kutekwa na watu wasiojulikana, tulishudia risasi adharani lakini hakuna siku amewahi kutoka adharani kukemea uvunjivu wa sheria na katiba ya nchi

Alikuwepo BUNGENI juzi wakati tozo kandamizi zinapitishwa hakuna siku tulimsikia akipinga na kura alipiga ya ndiyo. Hata hao waoumini wake hajawahi kuwaonea huruma, mshahara wake alipi Kodi na hatumsikii akikemea.

Leo anaibuka anaanza kumjadili JPM kwamba wakati wake hakuna aliyeleta chanjo. Je wakati wa JPM wakati watu wanabambikiwa kesi yeye hakuwepo? Alitusemea? Wakati watu wanakufa kwa corona alisema? Wakati tunaficha data alisema? Leo ametoa wapi ujasiri wakutumia nyumba za ibada kutaka kujifanya yeye ni daktari?

Tunaporuhusu watu wa aina ya Gwajima waongoze jamii ndipo tunapozalisha mawazo mgando. Yeye anaamini JPM alikuwa Mungu na kwamba maarifa ya JPM lazima yaheshimiwe hata Kama yalikuwa hayafai, kwamba Leo badala atueleze Mungu anasemaje anatulazimisha tufuate nyayo za binadamu ambaye ana mapungufu mengi ya wazi. Hii dini gani yakuelekeza watu wamwabudu mtu?

Leo ndipo amekuwa na msimamo, mbona huo msimamo upo kwa mambo ya mwendazake haupo kwa wengine?

Huyu mtu apuuzwe, siyo kiingozi wa dini Bali ni Kiongozi wa walafi wa madaraka. Kwenye siasa anataka, kwenye dini anataka na kwenye ushirikina anataka. Yeye Nani wakuombea watu wafe kisa awakubaliani naye? Unasiamama madhabauni unabiri kuua watu unadhani waumini wako wanajitunza Nini? Kwamba wanaokwenda kinyume na mtizamo wako na JPM wafe? Nani kakwambia ninyi ni miungu? Kwamba wewe utokufa?

Nadhani huyu mtu kwa kuwa tu Ni mwana ccm anayo haki yakutumia kanisa anavyojisikia yeye Tena kwa mambo ya hovyo kinyume kabisa na imani yake. Ila ipo siku ataadhibiwa
Acha zako fanya mambo yako. Kwani wewe ndiye uliyempa huo ubunge. Kama alipewa ubunge na mtu mwingine mwache afanye anavyotaka yeye.
 
GWAJIMA ANAPAMBANA VITA NGUMU SANA NA MABEBERU NA MAKAMPUNI YAO MAKUBWA YA DAWA ANATAKIWA AONGEZEWE ULINZI ILI AENDELEE KUSEMA UKWELI WATANZANIA AMKENI CHANJO NI HATARI KURIKO KORONA
 
Back
Top Bottom