KingCobra95
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 3,249
- 5,863
Vaccine shilling threads will be on a high note this coming month
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Watanzania mlio wengi (isipokuwa Mimi na wenzangu wachache) bila shuruti hamtii na kufanya mambo yenye faida kwenu.Shari peleka kwenu chanjo ni hiari wacha watu watumie hiari yao
Tanzania pamoja na kukandamizwa na viongozi wengi walio na UBINAFSI (dhambi kuu ya nchi hii) bado Mungu anatuhesabu kama wanadamu wenye kiwango kikubwa cha Imani(high spiritual sensitivity) ndio maana tumebarikiwa sana.Watanzania mlio wengi (isipokuwa Mimi na wenzangu wachache) bila shuruti hamtii na kufanya mambo yenye faida kwenu.
Hakuna ubinafsi zaidi ya huo anaoufanya Gwajima, anawarubuni waumini wake ambao huenda walio wengi ni wajinga.Tanzania pamoja na kukandamizwa na viongozi wengi walio na UBINAFSI (dhambi kuu ya nchi hii) bado Mungu anatuhesabu kama wanadamu wenye kiwango kikubwa cha Imani(high spiritual sensitivity) ndio maana tumebarikiwa sana.
Sasa hivi wenye upendo mkubwa na nchi hii wako wanaanda namna ya kugeuza idadi kubwa ya watu tuliobarikiwa na mwenyezi Mungu kuwa rasilimali. Mara tukifanikiwa Jambo hilo Africa na dunia itatambua ukuu wetu.
Mungu huwalinda na kuwabariki wenye maarifa Mithali imeandika hivyo tuongezee bidii kuyatafuta maarifa ya kweli.
#ONYO: Usimdhihaki Gwajima kama huwezi kujibu maswali yake. Amefanyika kuwa sauti ya wengi.
Mbona nyie makada mmeshupaza shingo kuipakiki Corona na hayo machanjo yenuNimeona video inayomuonesha Mchungaji Gwajima (Mbunge wa Kawe) akiwahimiza waumini katika kanisa lake kutokuchoma chanjo ya UVIKO.
Kwa namna nyingine amewatishia Wataalamu watakaohusika kuhamasisha matumizi ya chanjo hiyo kuwa wakifanya hivyo watakufa. Anadai anataka Wataalamu hao wajiridhishe na contents za chanjo hiyo kama ni salama kwa matumizi yetu.
Mheshimiwa Rais tumeshuhudia jitihada zako katika kupambana na janga hili la Corona, ni katika awamu yako tumeona pia Waziri wa afya akihamasisha wananchi kuzingatia ushauri wa wataalamu kujikinga na UVIKO.
Rais ulienda mbali na kuunda kamati maalumu ya Wataalamu ili wakushauri namna bora ya kukabiliana na ugonjwa huo, ripoti na mapendekezo ya Wataalamu ndiyo chanzo cha uagizaji wa chanjo baada ya kuthibitika zina faida kubwa katika kupambana na UVIKO 19.
Pamoja na kuwa mmeelekeza kuwa chanjo hiyo ni hiari lakini bado wanatokea watu kama Gwajima anawarubuni Watanzania bila kufikiria madhara makubwa yanayoweza kuwakumba.
Nimesikia kuwa Jumanne tarehe 28 July utakuwa unazindua matumizi ya chanjo hizo.
Ninashauri iundwe kamati ndogo ya uhamasishaji wa chanjo ya UVIKO itakayoundwa na Wataalamu, Viongozi wa dini na Wanasiasa.
Mojawapo ya watu watakaoshiriki katika kamati hiyo awe Mchungaji Gwajima.
Wanakamati hao wapewe elimu na waelewe vizuri maana halisi ya chanjo inayotolewa, matumizi yake na madhara yake. Kamati hiyo uitangaze siku hiyo ya Jumanne.
Nawasilisha.
Kwa hiyo wewe hujawahi KUCHANJWA chanjo yoyote maishani ?!!!Mbona nyie makada mmeshupaza shingo kuipakiki Corona na hayo machanjo yenu
Nenda kachanjwe buda wwWengi wanakifahamu au wamewahi kukisikia kisa cha Joseph Kibweteere wa Uganda mshirika aliyejitenga kutoka kanisa katoliki na akaanzisha huduma yake iliyokuwa na mafundisho mengi ya ajabu lakini ikijitambulisha kama dhehebu la Kikristo.
Kilele cha huyu bwana ilikuwa March 17,2000 alipowafungia waumini wake takribani 700 ndani ya kanisa akawaaminisha mwaka 2000 ulikuwa mwisho wa dunia na wakakubali kuchomwa moto wote hadi kufa huko Kanungu Uganda.
Kibwetere mwenyewe haiweleweki mpaka leo kama alijichoma moto na washirika wake au yeye alichoropoka, mpaka leo amebaki katika listi ya mojawapo wa watu wanaotafutwa sana Uganda.
Nikirudi hapa nyumbani katika video na taarifa ziliozasambaa sana leo ni pamoja na ya Askofu Gwajima akihubiri kanisani kwake akiwasisitiza sana wafuasi wake wakatae chanjo kwa sababu wanaweza kugeuka mazombi.
Ameenda mbali zaidi akiipuzulia mapendekezo ya kamati ya wataalamu wa serikali iliyondwa kumshauri Rais katika suala la Corona.
Njia inayoonekana bora katika kukabiliana na Corona mpaka sasa ni chanjo, ikiwa Gwajima atasikilizwa na kutiliwa maanani na maelfu ya watu katika makundi hatarishi ya kupata na kufa kwa korona atakuwa hana tofauti na Kibweteere wa Uganda
Mimi nayewaambia watu kuhusu ukweli wa chanjo wasichanjwe wasichokijua Vs wewe unayewahamasisha watu wachanjwe wasichokijua yaani watu milioni 60 wageuzwe majaribio ya wazungu ni nani hatari kwa usalama wa taifa?Acha UPOTOSHAJI wewe unataka kumpinga mtu anayekusanya takwimu za wanaolazwa ná kufa kwa COVID-19!? Watu kama wewe ni hatari sana ni hasara kubwa Kwa Taifa. Ulichoandika ni UONGO MTUPU!!!
Kuna chanjo kamaUnaonaje ukitoa takwimu za chanjo zenye ahueni zisizofuata kanuni ya MRNA ili tuanze kuzifuatilia kabla hatujalazimishwa kukinga mabega
Kwahiyo wewe unatuletea stori zako zinazopromotiwa na watengenezaji chanjo na big pharma? Kwani unalipwa shilingi ngapi eti[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]waambie hao wenzako kwamba hatuchanjwi mrna ng'oo[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]wewe kweli taahira unaenda kuokoteza vitu vya kipumbavu vinavyoandikwa na wahuni wa conservative!?
![]()
Fact check: No evidence Bill Gates said ‘at least 3 billion people need to die’
A video viewed thousands of times on social media attributes to Bill Gates a quote about “sterilization and population control”. The clip shows a man saying: “In the words of Bill Gates, at least 3 billion people need to die”. Reuters found no evidence Gates ever made such...www.reuters.com
[emoji13][emoji13][emoji13][emoji13][emoji13][emoji13]kumbe!!!!!!!!!!hakuna chanjo ilotengenezwa kwa nia mbaya
chanjo zinatengenezwa kwa nia ya kutibu
na kabla hawajaruhusu zitumike huzifanyia majaribio, zinapokutwa hazina sumu na madhara kwa miili ya wanaadam ndipo huruhusiwa zisambazwe na kutumika/kutumiwa.
Vilevile hiyo ni fursa kwa watengenezaji wa chanjo hizo maana huuzwa kwa mataifa mbalimbali, ndo maana kuna makampuni mengi yanayotengeneza chanjo hizo na majina ya chanjo hizo yanatofautiana kulingana na makampuni zinapotengenezewa.
Hivyo msiwe na wasiwasi chanjo zote ni salama kwa matumizi ya wanaadam.
Wewe ndo mpumbavu,mjinga tena brainwashed na hao bwana zako mimi unaniforce nimsikilize dr fauci ambaye an share kwenye hayo makampuni?wewe utakua mgonjwa sio bureWewe ni mpuuzi huna ujualo umeandika maelfu ya waliopata chanjo wanakufa lakini huna ushahidi wowote ule wa kuthibitisha ulichoandika kuhusu vifo hivyo. Nimekuonyesha ushahidi wa kwamba 99% ya wanaokufa ná Covid kwa sasa ni wale ambao hawajapata chanjo maana yake waliopata ná chanjo ná wanakufa ni 1% lakini bado unaleta UBISHI WAKO wa KIPUMBAVU usio na kichwa wala miguu. Wazushi kama wewe ni watu hatari sana ná hasara kubwa kwa Taifa.
Ukija humu kuandika uzushi wako bila kuwa ná chembe ya ushahidi ujue uongo wako hautavumiliwa. Kadanganye kwingine siyo humu.
Akina amfifiro?wewe ni mpumbavu wa mwisho kwahiyo unadhani hizi ni propaganda kama hizo zenu nyie mawakala wa bilgate?Haya tueleze Bwana Molecular Biologist hiyo mRNA inaingia vipi kwenye cytoplasm na kuungana na DNA.
Au ndiyo akina amfifiro????
Gwajima ni mtu mjinga sana.GWAJIMA ANAWASIWASI NA CHANJO YA CORONA TUU! LABDA NI KWA UJINGA WAKE AU KAAMUA KUIPINGA SERIKALI KWA UJEURI TUU.
Kwa Mkono wa, Robert Heriel.
Nimeiona Clip inayomuonyesha Ndugu Gwajima akitoa maoni yake Kanisani kwake kuhusu Masuala ya Chanjo ya Corona.
Katika Hotuba yake hiyo, Gwajima alitoa maudhui yaliyolenga kuwashawishi waumini na wasikilizaji wake kuwa wasikubali Chanjo ya Corona mpaka pale Madaktari wa kitanzania watakapo fanya uchunguzi wa contents akimaanisha Gradients au Chemical composition zilizopo kwenye Chanjo hiyo.
Kauli za Gwajima mbali na kushawishi waumini wake na waliokuwa wakimsikiliza, pia zililenga kutishia na kuwaogopesha baadhi ya watendaji katika sekta ya Afya, Kwa kuwataja Madaktari watakaohusika kuipitisha chanjo hiyo.
Gwajima alitoa kauli ambazo Mimi niliziona za kipuuzi na kitoto, kwani Kwa. Uelewa wake alidhani mungu anayemuamini yeye basi ni mungu wa watu wengine.
Gwajima kupitia kauli yake ya kutisha Madaktari namlimgamisha na Wale masheikhe waliomtishia Afande Sele wakidhani mungu wao ananguvu ya kufanya atakavyo Kwa watu wote Kama afanyavyo kwao. Jambo ambalo ni uongo.
Nikiachana na mambo ya Imani ili nisiguse makundi ya waaminio. Naomba nirejee kwenye hoja.
Gwajima anaongea Kama mtu asiyemtaalamu, anayebebwa na upepo wa propaganda za kitoto na watu wasioenda shule.
Na Kama kaenda shule basi elimu yake itakuwa na Shaka kubwa Sana, sio ajabu Mbunge Msukuma akiwakejeli wasomi ikiwa ndio akili zao zipo Kama hivi.
Gwajima lazima aelewe kuwa ishu ya Corona ipo kitabibu zaidi kuliko porojo zake au Siasa ambazo ni kuongea tuu.
Kuwaambia Madaktari ati wachunguze contents zilizopo ndani ya Chanjo ya Corona ni kujaribu Kueleza kuwa Madaktari WA nchi hii hawajui wajibu na kazi Yao.
Gwajima anataka kuwaambia Waumini na wasikilizaji wake kuwa, Madaktari wa Tanzania huwaga hawafanyagi uchunguzi katika madawa yanayotoka nje.
Gwajima anafikiri kuwa Madaktari WA Tanzania wanaongozwa na Teolojia inayomuongoza yeye ambayo ni Tawi la Falsafa ambayo Wachungaji huitumia kuwafundisha watu habari za Mungu, Jambo ambalo sio kweli. Madaktari huongozwa na Sayansi zaidi kuliko masuala dhahania.
Gwajima anajifanya anaakili mbele ya waumini na wasikilizaji wake na hawapi nafasi ya kufikiri kuliko upeo ili aonekane kaongea hoja yenye manufaa wakati Kwa akili ndogo ni kuwa ameongea pasipo kufikiri vizuri.
Kama Gwajima angetoa nafasi ya kuulizwa maswali huenda angejidharau pale pale na kujiona ameongea vitu visivyopaswa kuzungumzwa na mtu Kama yeye.
Mfano wa maswali;
1. Tangu nchi imepata Uhuru, ni lini Madaktari walitaja contents zilizopo kwenye madawa yatokayo nje au hata Chanjo ambazo tulichanjwa?
2. Kwa nini Gwajima Hana wasiwasi na Dawa zingine Kama vile ARVs, chanjo wapigwazo watoto wachanga, au wamama wajawazito, Kwa nini iwe Chanjo ya Korona na sio hizo?
3. Gwajima amegusia suala la biashara imejiingiza kwenye suala la Chanjo ya Corona, yupo sahihi. Ni Ugonjwa upo ambao sio biashara?
Na ni Huduma gani isiyobiashara Kwa sasa? Mbona hata kwenye dini biashara imejiingiza, yeye anaona Kwa wenzake haoni upande wake.
Gwajima alikuwa anaelezea Jambo ambalo Hana Uelewa nalo Kwa sababu yeye sio Daktari, hivyo kujifanya anaamrisha mambo asiyo na Uelewa nayo ni Kama kujivua nguo mbele za watu.
Gwajima sijui hajui au anafanya ukaidi, mambo mengi tunayoyatumia iwe Kwa kula au kutumia kawaida yanatoka nchi za nje, Kwa hao hao Wazungu. Hivyo Kama ni kutumaliza wangetumaliza hata kabla Gwajima mwenyewe hajazaliwa.
Gwajima anaweza akawa na hoja lakini uwasilishaji wake umekuwa wakijinga Kwa sababu maoni yake anajaribu kuyalazimisha na kutisha watu, huku akielezea mambo asiyo na utaalamu nayo.
Mahali ninapoungana na Gwajima;
Ninaungana na Gwajima ile siku alipompinga Mbowe kuhusu kauli yake kuwa Chanjo iwe Lazima,
Gwajima anajaribu kuifichua tabia ya Mbowe ya udikteta ya kulazimisha Chanjo ya Corona Kwa wote badala ya kutumia Demokrasia.
Hata hivyo Gwajima naye anajisahau, anataka kulazimisha watu wakatae Chanjo ya Corona badala ya kuruhusu demokrasia Kama Tamko la serikali lilivyoelekeza kuwa; Chanjo ya Corona ni Hiyari.
Anayetaka akapigwe, asiyetaka aache.
Gwajima usiwaze Kama mtu asiye na Uelewa wa mambo.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
MOROGORO
Well said mkuu.....akasome ripoti ya wizara ya afya ya 2013 kuhusu onyo juu ya mlipuko wa mafua yanayoitwa corona ilikua 2013 na huo uzi ulikuwepo humu ngoja niutafuteMkuu, pana wengine hukurupuka tu kupinga hoja bila tafakari. Toka mwanzo umesema HUPINGI hanjo ila si hizi za MRNA! Jamaa kakomaa tu na chanjo chanjo huyu hana tofauti na wanaotupigia kelele za CORONA kana kwamba kirusi hiki kimeanza 2019. Kirusi cha korona kipo duniani hapa miaka nendarudi ila sasa tunapigana na hiki cha CoVid19.
Kaka....ona hiiMkuu, pana wengine hukurupuka tu kupinga hoja bila tafakari. Toka mwanzo umesema HUPINGI hanjo ila si hizi za MRNA! Jamaa kakomaa tu na chanjo chanjo huyu hana tofauti na wanaotupigia kelele za CORONA kana kwamba kirusi hiki kimeanza 2019. Kirusi cha korona kipo duniani hapa miaka nendarudi ila sasa tunapigana na hiki cha CoVid19.