#COVID19 Askofu Gwajima: Ni ujinga kuruhusu Taifa zima kuwa 'Experiment' kwa sababu tuna haraka ya Corona

#COVID19 Askofu Gwajima: Ni ujinga kuruhusu Taifa zima kuwa 'Experiment' kwa sababu tuna haraka ya Corona

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Mbunge wa Jimbo la Kawe, Askofu Josephat Gwajima ametaka kuwepo umakini wa kuchagua Chanjo dhidi ya Ugonjwa wa COVID-19. Amesema hayo akiwa Bungeni Dodoma leo wakati wa Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Afya iliyowasilishwa na Waziri Dorothy Gwajima.

Amefafanua, "Mimi sipo kinyume na Chanjo za Corona wala chanjo yoyote. Mtu asininukuu napinga chanjo, hapana. Tanzania tulishachanjwa Chanjo ya Kifua Kikuu, Surua, Kifaduro na Polio''.

Amesema ni kweli Tanzania ikikataa Chanjo inaweza kuwekewa zuio la kwenda Ulaya. Ameeleza, "Tunakabiliwa na uchaguzi mbaya sana, tuchanjwe kitu tusichokijua sawa sawa au tusichanjwe tuzuiwe kwenda Ulaya".

Ameiomba Wizara ya Afya kuangalia suala la Chanjo kwa umakini, akisema waangalie madhara ya sasa, ya siku zijazo na ya Taifa. Ameongeza kuwa, tatizo lililopo ni kufikiri kila kinachotoka Ulaya kinafaa.

Amesema, "Before we venture into what kind of vaccine we should take, tunatakiwa tuwe na wataalamu wetu wa hapa".
 
Hivi Corona ipo au haipo kwa upande wa Tanzania?

Sasa hivi tunashuhudia chanjo! Wakati mwanzo Tanzania ilisema inafanya tafiti!

Majibu ya hiyo tafiti bado tu? Au kuna mengine nyuma ya pazia!

Na kama tafiti bado, kwanini Tanzania ikimbilie kwenye chanjo.

Kama Corona ipo siitangazwe tujue moja!

Kuliko kuficha ficha huku Watanzania wengi wakiendelea kupukutika.
 
Jamani US wameanza mchakato wa kuomba patent zilegezwe ili manufacturers wa chanjo waongezeke.

Sasa nilitegemea wabunge waombe serikali ipewe patent ili tuwe na pattern zote sie tutengeneze chanjo yetu. Sie tumekalia kulalamika tu na kukosoa chanjo kila siku.

Kwani nani amekataza waTZ kuwa na chanjo yetu? China wanatumia chanjo za UK? mbona EU haijawekea vikwazo nchi yao?

Huyu jamaa toka apotoshe eti 5G ndio inaleta Covid 19 na akaahidi Covid 19 itaishia kenya haitowahi tua Dar najiuliza nani bado anamuamini?? Kama nabii tu hawezi kupatia ubashiri je hta uchambuzi tu ndio ataweza.

Masuala ya kitaaluma tuachie wataalam ni hatari sana HKL kujadili epidemiology
 
Chanjo hizi zimeharakiswa mno hata waliozitengeneza hawajuwi madhara ambayo bado hayajajitokeza kwenye mwili wa mwanadamu.
Homa ya manjano ile Vaccine yake imeua watu zaidi ya laki 5 directly kabisa tokea iwe introduced mbona sijasikia mkiipiga marufuku na ndio kwanza tunatumia hiyo kila tukisafiri nje!!

Mkatae kwa sababu tu hamtaki ila msijustify eti madhara cjui nini.... Coz ikiwa hivyo inapaswa mpaka Radiotherapy isitishwe pale ocean road maana ile madhara yake ni makubwa sana kwa kila anayetumia tiba ile.

Tuache double standard
 
Homa ya manjano ile Vaccine yake imeua watu zaidi ya laki 5 directly kabisa tokea iwe introduced mbona sijasikia mkiipiga marufuku na ndio kwanza tunatumia hiyo kila tukisafiri nje!!

Mkatae kwa sababu tu hamtaki ila msijustify eti madhara cjui nini.... Coz ikiwa hivyo inapaswa mpaka Radiotherapy isitishwe pale ocean road maana ile madhara yake ni makubwa sana kwa kila anayetumia tiba ile.

Tuache double standard
Kwa nini tusifast track majaribio ya chanjo ya ukimwi pale Muhimbili?
 
Hivi Corona ipo au haipo kwa upande wa Tanzania?

Sasa hivi tunashuhudia chanjo! Wakati mwanzo Tanzania ilisema inafanya tafiti!

Majibu ya hiyo tafiti bado tu? Au kuna mengine nyuma ya pazia!

Na kama tafiti bado, kwanini Tanzania ikimbilie kwenye chanjo.

Kama Corona ipo siitangazwe tujue moja!

Kuliko kuficha ficha huku Watanzania wengi wakiendelea kupukutika.
Nadhani chanjo huwa haijalishi ugonjwa upo au hamna.... Ni kama homa ya manjano tu huwa tunapigwa chanjo kila miaka 10 whether ugonjwa upo ama lah.

That said issue hapa ni kuomba patent tutengeneze za kwetu kukosoa tu na kejeli za bungeni kwa chanjo za mabeberu ni kujidhalilisha tu.

Kama hawaziamini ni rahisi tu tuombe leseni tutengeneze za kwetu maana tumeshindwa kubuni yetu. Tuache kujificha kwenye madhaifu ya chanjo za wenzetu
 
Huku mtaani kwetu sijui tutamvika nani maana kwa hiari ni ngumuuuu

Tena wanakuambia kabisa mbona tangu mwaka jana tunafanya kazi zetu kariakoo, tandika, ilala na hakuna mfanyabiashara aliyeumwa hiyo corona

Kamvika mtu ambaye ameshajihakikishia corona haiambukizwi kwa kutovaa barakoa uwe na sababu atakazoelewa
 
Yaani vitu vya kitaalamu waachie wataalamu,au mtaishia kutupa low key ideas....
Jamani US wameanza mchakato wa kuomba patent zilegezwe ili manufacturers wa chanjo waongezeke.

Sasa nilitegemea wabunge waombe serikali ipewe patent ili tuwe na pattern zote sie tutengeneze chanjo yetu. Sie tumekalia kulalamika tu na kukosoa chanjo kila siku.

Kwani nani amekataza waTZ kuwa na chanjo yetu? China wanatumia chanjo za UK? mbona EU haijawekea vikwazo nchi yao?

Huyu jamaa toka apotoshe eti 5G ndio inaleta Covid 19 na akaahidi Covid 19 itaishia kenya haitowahi tua Dar najiuliza nani bado anamuamini?? Kama nabii tu hawezi kupatia ubashiri je hta uchambuzi tu ndio ataweza.

Masuala ya kitaaluma tuachie wataalam ni hatari sana HKL kujadili epidemiology
 
Hapa Dj mr zero amenangwa waziwazi kabisa.

Amechanjwa harakaharaka huko Dubai
Hapana. Tatizo ni kuwa Watanzania hatusomi! Tumebaki kulalamika kuwa hatuijui chanjo. Watu wote hadi Rais aliyetangulia mnasema hamjui! Data za majaribio ya chanjo zote zilikuwa zinatolewa mwaka mzima mwaka jana, na ripoti zote za phase ya mwisho ya majaribio, Phase 3 zilielezwa vizuri sana na kuchambuliwa na wataalamu huru kuanzia Desemba 2021.

Sasa tuko Phase 4 ya monitoring, halafu asiyesoma anasema tusubiri wataalamu wetu waseme. Sijui hawa wataalamu watarudi Phase ya kwanza? Watu huko duniani wanatikisa vichwa tu jinsi tulivyoachwa maili maelfu.

Jebu someni New England Journal of Medicine moate hizo ripoti za Pfizer, Moderna, Astrozeneca na J&J. Sisi wengine sasa hivi tunamalizia kusoma za Urusi, China, India (nazo zinatumika), na Soberana ya Cuba.
 
"Mimi sipo kinyume na Chanjo za Corona wala Chanjo yoyote. Mtu asininukuu napinga Chanjo, hapana! Tanzania tulishachanjwa Chanjo ya Kifua Kikuu, Surua, Kifaduro na Polio".
Huyu ndio Leo anasema hivi? Amesahau au anajifanya sisi ndio tumesahau!!
 
Yaani vitu vya kitaalamu waachie wataalamu,au mtaishia kutupa low key ideas....
Hapana mkuu mie nimejifunza kuheshimu taalum hivi kweli madaktari bingwa wa WHO kuanzia yule mama wa kihindi ambaye ni top expert wa epidemiology duniani yaani hajui hayo anayosema Gwajima?

Ukisikia mjenzi wa daraja anatumia miezi 6 kufanya upembuzi watu huwa wanatukana mitandaoni kwamba miezi 6 yote kufanya upembuzi??? Lakini ukikaa na mtaalam atakueleza kwanini miezi 6 maana kuna movement za kitectonic, ama misimu ya mvua ukipita n.k ndio utaweza kujua stability ya eneo husika kujengewa daraja n.k

So nadhani tukiheshimu taaluma za watu nchi itafika mbali. Maadam Rais kaunda tume yenye wataalam husika then watakacho recommend tuheshimu otherwise ujuaji haujatusaidia mpaka hii Leo.
 
Back
Top Bottom