#COVID19 Askofu Gwajima: Nitabaki risasi ya mwisho kwenye uwanja wa vita, kuchanjwa wengine tumekataa

#COVID19 Askofu Gwajima: Nitabaki risasi ya mwisho kwenye uwanja wa vita, kuchanjwa wengine tumekataa

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Ibada inaendelea.

Askofu Gwajima amesema kamati ya Corona ilipendekeza wananchi washawishiwe na serikali kuvhagua kuchanjwa ama LA na yeye Gwajima amechagua LA niko sahihi.

Rais Samia amechagua kuchanja naye yuko sahihi.

Msinigombanishe na mwenyekiti wangu wa chama.
========

Josephat Gwajima: Viongozi wanaoangalia kuweni makini, kuna wachonganishi hapa. Mimi naweka msimamo nchi iwe salama, watanzania wawe na afya, chama changu kipite salama.

Kanisa ambalo halina ufumbuzi dhidi ya Korona, litoeni msaada liwe hospitali, sasa la nini?

Mimi nawaza, wakakupima joto likawa juu, wanakwambia uingie usiingie? Sasa wale walioingia wanaombewa? Ni kashfa kwenye ufamlme wa Yesu kubwa sana.

Nitabaki risasi ya mwisho kwenye uwanja wa vita, mimi wa kwanza kuweka mguu uwanja wa mapambano na nitakuwa wa mwisho kuondoa. I will not quit from the battle front, Never.

Hii nchi sasa hivi, Rais wake ni mama Samia Suluhu Hassan, Mungu ndio kamchagua. Biblia inasema hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu, lazima tumsupport.

Ni Rais anaetawala wakati mgumu sana kuliko wowote, kwanza kuna Rais mwingine alikuwa anaelekea hivi, bwana John alikuwa ana tabia zake. Wale ambao hamjajua, John alikuwa akikupigia simu, utafikiri kuzimu imefunguliwa leo. Kuna watu wengine wanasema tu Magufuli Magufuli, Magufuli alikuwa akikupigia simu unasema Mungu wangu, utafikiri kiama imeanza, akiongea anaongea kwa Mamlaka, akikupigia simu anajua vyote.

Huyo ameshaondoka, tuangalie nchi yetu na hatima yetu kwasasa. Tumwambie maam Samia tunakubeba twende na wewe, tupeleke ila tumesema, kuchanjwa wengine tumekataa, wengine wamekubali lakini mama twende.
 
Ibada inaendelea.

Askofu Gwajima amesema kamati ya Corona ilipendekeza wananchi washawishiwe na serikali kuvhagua kuchanjwa ama LA na yeye Gwajima amechagua LA niko sahihi.

Rais Samia amechagua kuchanja naye yuko sahihi.

Msinigombanishe na mwenyekiti wangu wa chama.
Hapo ni kanisani au jukwaa la siasa.
Waumini wako ni mchanganyiko wa itikadi tofauti.Neno Mkiti wako wa chama nenda jimboni kaongelee hayo
 
Huku chanjo, kule CDC inatoa maelekezo mapya kua hata kama umechanjwa vaa barakoa iwe nje ama ndani, social distance kama kawaida na sanitize.

Serikali inategemea kuchanja watu 12M, tutanye hii chanjo ni effective na salama 100%, lakini bado wanasema wataalam kua bado hata kama umechanjwa unaweza kuambukizwa ila hutapata matatizo makubwa kama ambae hajaambukizwa, sasa kuchanja 12M people unaacha 48M hawajachanjwa, maana yake hawa 48M wanaweza kuwaambukiza hawa 12M waliochanjwa na bado nchi nzima ikawa na covid.

Hii covid na chanjo issue bado ni sarakasi zisizo na maana.
 
Ibada inaendelea.

Askofu Gwajima amesema kamati ya Corona ilipendekeza wananchi washawishiwe na serikali kuvhagua kuchanjwa ama LA na yeye Gwajima amechagua LA niko sahihi.

Rais Samia amechagua kuchanja naye yuko sahihi.

Msinigombanishe na mwenyekiti wangu wa chama.
Hizo hatua mpya ameanza kuzitangaza?
 
Back
Top Bottom