Askofu Mwamakula amesema RC Makonda alipopewa nafasi ya kusalimia Waumini kwenye Ibada ya Mwamposa alisema Eliya hakuwa Nabii na Biblia haimtaji popote kama Nabii
Mwamakula amemtaka RC Makonda asome Wafalme 18:22 Ili apate Maarifa Zaidi
Amesema Ukurasani X
Sabato Njema ππΉ
Kuna viongozi wa dini hawaelewi hutumia mifano ya manabii agano la kale kama Eliya, Samuel nk kukemea wafalme watawala wanasahau kuwa kipindi hicho dini ilikuwa moja na nabii aliiuwa juu ya mfalme sababu ndiye aliyekuwa akisimika wafalme na kuwapa madaraka kwa kuwapaka mafuta
Hivyo yeye alikuwa bosi wa watawala hivyo kuwakemea haikuwa issue sababu ya kwanza walikuwa waumini wao ya pili mabosi wao na nchi nzima waliwatambua kama wako juu yao na juu ya mfalme mtawala
Ikafika kipindi cha Yohana mbatizaji akaamua kujitosa kwenye kukemea wanasiasa ambao sio waumini wake wala hakuwaweka yeye akamkemea mfalme Herode ambaye hakuwa dini yake wala siye aliyemuweka madarakani Herode akamkata kichwa Yohana mbatizaji.
Yohana aliacha jukumu lake la kuhubiri na kubatiza watu akajitosa kusikomhusu
Kwenye kuhubiri na kubatiza Yohana mbatizaji alifanikiwa mno Yerusalem na Yudea yote walienda kwake kwa agenda moja tu kutubu dhambi na kubatizwa sio kutafuta maombi ya utajiri vyeo vya siasa au umaarufu alipojitosa siasa umaarufu ukapotea na akafa
Sasa hivi hata kanisa katoliki waungama dhambi kwa padri wamepungua ni kama hawapo tena baada ya kanisa kujitosa kwenye siasa .Padri muungamishaji aweza tandika hata usingizi sehemu ya kitubio jumapili haji mtu Wiongozi wa dini wabaki kwenye reli ya dini
Kujilingajisha na manabii wa zamani wakati mazingira tofauti sana ni kutoijua theolojia vizuri Hata katoliki walikuwa na nguvu kubwa mno mapapa kukemea watawala kipindi wao ndio wanawapa utawala wafalme kwenye Roman empire
Makonda yuko sahihi Tanzania haina dini viongozi wa Dini wapeleke maombi kwa Mungu wakiona kuna shida kubwa wasielekeze serikalini
Environment ya sasa sio kama ya enzi zile za manabii Eliya nk