Askofu Mwamakula: Sikutarajia yaliyoandikwa na Kabendera yangewekwa hadharani wakati wa uhai wangu

Kwa haya tunayoyasikia ni dhahiri kifo cha Magufuli kilikuwa ushahidi wa upendo wa Mungu kwa watanzania.
Ndugu Kifo si Adhabu ni Mlango kila Mtu atapita kwa Wakati wake hata hivyo Mungu wetu ni mwema kwa wasioshukrani na wenye shukran wapo watakatifu waliokufa wakiwa na umri mdogo na wapo watenda zambi waliokufa wakiwa na umri mkubwa Mungu Hapangiwi
 
Mwingine huyu limempata, inaanza kama upepo baadae kimbunga
 
Kazi ndio imeanza.
Sina mashaka na andiko la askofu Mwamakula. Mashaka yangu ni kuwa aliye achiwa kiti lazima alikuwa anayajua yote haya na yale asiyoyajua wakati ule sasa ameyajua kutokana na source mbalimbali alizo nazo.
Lakini kutamka "mimi na yule ni kitu kimoja" inaacha maswali! Jee aliropoka au ni kweli yuko hivyo?
Najua sio rahisi naye kumpiga za kichwa asiyempenda, lakini jee hawezi kuagiza bila moyo kustuka?
Acha niendelee kujiuliza!
 
Sio vema kumsema au kusema maovu ya mtu aliye fariki kwani huwa unamjengea mazingira magumu huko aliko wewe ukiwa kama askofu unalijua hilo tunajifunza nini kwako, lakini kwanini haya mambo usiyaseme kipindi yupo hai na sifa moja wapo ya askofu ni kutofumbia maovu yanapofanyika🙄
 
Humu jf kuna id kadhaa zilishawahi kuzungumzia hayo masuala ya kutisha. Ila watu walizipuuzia. Ila kama kabendera kasema, askofu kasema nasubiria comment ya lissu. Inawezekana zile id za jf zilizosema hayo masuala ni za watu waliopo kwenye inner circle ya mfumo.
 
Fikiri kama mtu huru usisukumwe na USUKUMA.
Chawa wa marehemu kashikwa na uchungu wa ghafla maana haamini kama mabaya ya jiwe hatimaye yapo hadharani na kila mtu anajisomea.
Kutetea marehemu jiwe kuwa alikuwa mwema saana na hawezi kufanya mabaya inahitaji kuwa taahira wa kiwango cha juu sana.
Mfalme Daudi wa kwenye biblia pamoja na utakatifu wake alichukua mke wa mwanajeshi wake na akampiga mimba na akaamuru mumewe yaani huyo mwanajeshi apangwe mstari wa mbele vitani ili afe.
Na Daudi akauchuna ila Mungu kupitia nabii Nathan akamuumbua.

Sasa kama Daudi alipotoka kiasi hicho jiwe mvuta bhangi kichaa ni nani hata awe mtakatifu kiasi cha mtu kusema anasingiziwa why asisingiziwe Nyerere, Mkapa, Mwinyi, Kikwete?
 
Uchafu wa jiwe upo wazi kitambo tu na wengi wanaujua wala si siri. Makada, watumishi serikalini wengi wamekuwa wakisema mauchafu ya jiwe japo kwa kunong'ona.
Issue ya sa8 ipo hewan kitambo sana.
 
Umewakaanga kijani kibichi a.k.a wafuasi wa mtakatifu balaa, sijui wataficha wapi nyuso zao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…