Askofu Nyaisonga avishangaa Vyama vya Upinzani kususia uchaguzi. Ahimiza waumini kujitokeza kupiga kura na kuchagua viongozi

Askofu Nyaisonga avishangaa Vyama vya Upinzani kususia uchaguzi. Ahimiza waumini kujitokeza kupiga kura na kuchagua viongozi

Mwezi February kanisa katoliki lilitoa waraka watu wajiandikishe uchaguzi.

Mbona hili kanisa halikujitokeza kuhamasisha waumini wakajiandikishe kupiga kura?!

Leo wanawahamasisha wakapige kura vipi ikiwa hawakujiandikisha?!

Kura wanapiga za nini ikiwa mgombea ni mmoja?!
 
Kasome historia ya vita za Yerusalemu,dark ages na mauaji ya wakristo ulaya,uongozi wa madikteta ka Musolini na Hitler,mauaji ya wayahudi Ujerumani,Rwandan genocide,Ireland crisis,utawaelewa vizuri viongozi wa kikatoliki.Ni watu very controversial yanapokuja mambo ya aina hii na mara nyingi husimama na upande wenye nguvu.Ni wanafiki na nyoka wabaya.Pole kwa waumini wao.
 
Kabisa, usisahau mambo mema kama kumuunga mkono kuchinja na kupora mali za Wayahudi zaidi ya elfu nane na kuwapeleka Borgo San Dalmazzo Camp na Fossoli ili Kanisa lipewe mji wa Vatican.
Ninafikiri Kanisa Katoliki liliunga mkono mambo mema pekee.

Hata leo, kuna mambo hayaendi sawa katika awamu tuliyonayo. Lakini haimaanishi kuwa hakuna mambo mema mengi yanayotendeka.

Kwa mtazamo wangu; busara ni kuunga mkono hayo mema na kutumia njia nzuri kukosoa mapungufu. Ukosoaji huu sio lazima uwe public.

Tufanye kususia uchaguzi; what will be our next plan?
 
Kasome historia ya vita za Yerusalemu,dark ages na mauaji ya wakristo ulaya,uongozi wa madikteta ka Musolini na Hitler,mauaji ya wayahudi Ujerumani,Rwandan genocide,Ireland crisis,utawaelewa vizuri viongozi wa kikatoliki.Ni watu very controversial yanapokuja mambo ya aina hii na mara nyingi husimama na upande wenye nguvu.Ni wanafiki na nyoka wabaya.Pole kwa waumini wao.
Vipi kuhusu DRC na Kabila?
 
Kuna tatizo hapo.
Na ukiona hivyo tunaelekea kubaya sana.
Kama kuna waumini humu wa Kanisa hilo wamwambie kabisa huyo askofu wao kuwa amebariki dhulma katika Taifa hili.
Dhulma siku zote unaishia kwenye vurugu,ghasia na mwishowe vifo vingi.

Siku zote nilikua sijaelewa kuwa ni kwa nini Viongozi wa Dini hasa wa kanisa Katoliki wamekua wakihusishwa na vita za kimbari sasa nimepata jibu .
Askofu anaposimama upande wa Mdhulumaji mwenye nguvu zote kama Mabunduki ,majeshi na kila aina ya mabavu na kumwacha mlalamikaji asiye na nguvu basi amebariki ugandamizaji.Matokeo yake mlalamikaji dhaifu hata akijaribu kuandamana ataishia kupigwa risasi na hata kumwagiwa kemikali za sumu na kufa kama Panya. Mwishowe mlalamikaji mnyinge ataamua kujitetea dhudi ya binadamu mwenzake anayeamua kumuua na kumwona kama sisimizi.Hapo vita inaingia ya kimbari na wenyewe kwa wenyewe . Chanzo ni viongozi wa dini waliosimama upande wa Wenye nguvu dhidi ya wanyongo na dhaifu.

Lakini kama askofu angesimama na wanyonge angeepusha vurugu na kuuawa kwa wanyonge mana wenye nguvu wangejichunguza na kuona makosa yao na kuwatendea haki wanyonge.

Waafrika tumeamua kutumia kila mbinu za kikoloni kutawaliana kimabavu kwa faida ya watawala na dini viongozi wa dini za kikoloni.
Ubeberu umehamia kwa watawala.

Nadhani watakua wanapata migao ya mafungu ya dhulma yanayopatikana nje ya bajeti.

Lakini tuwalaumu viongozi dhaifu wa upinzani wasio na weledi na Elimu ya siasa kama alivyodai.

Chadema ndicho chama tegemeo la Watanzania lakini Mbowe amevuruga Chama hakina dira wala uongozi mpaka sasa.
Chama hakina Intelijensia ya kutosha.
Chama hakitumii fedha kujenga Chama ngazi za chini zaidi ya kumlinda Mbowe na maslahi yake.
Wasomi ndani ya Chadema wamejitenga na Chama na wamekaa kimya.
Hata Lisu ameamua kukaa kimya mana anaona anahatarisha maisha yake kwa manufaa ya Mtu Mmoja Mbowe na Mali zake .
Akili kubwa kama Komu inawekwa pembeni kwa sababu ya akili ndogo.
Komu ni kati ya wasomi wenye uwezo mkubwa sana kiakili na anauwezo wa kupambanua mambo na uwezo wa kubadili mwelekeo wa siasa za Tanzania kwa kuja na mbinu mpya.

Kubenea amewekwa kapuni ,MTU mwenye historia ya kuichachafya serikali mpaka akataka kupoteza maisha yake. Akisema tunaletewa hadithi za Mbowe amepoteza Mali zake wakati anapewa stahiki yake ya kukwepa Kodi . Ufisadi wa Mbowe wa kukwepa kodi umekigharimu chama. Na hawezi kuachia uongozi mana anaishi kwa ruzuku za Chama ili afidie hasara alizopata kupitia siasa.
Wenzake wamenusurika kuuawa kwa akili ya Chama lakini wanatumikia Chama nje ya madaraka lakini Mbowe ameguswa kwenye kodi na ufisadi wake analia lia na kusema akiondoka chama kitakufa wakati anakiua mana chama kinakosa dira.

Wapo watu jasiri wasio hofia mali zao wala maisha yao kama alivyo Lema, Heche,Juma Mwalimu, Msigwa ,Esta Matiku n.k Lakini bado tu Chama kina mkumbatia Mbowe na usanii wake.
Hapo kweli Chama hiki kitategemea Kauli toka kwa Kanisa Katoliki.?? Kweli ??? Are serious ???
Komu amesoma na Mapadri wengi na walikua wanamheshimu kwa Uwezo wake aliokua nao Darasani. Hata Mkuu Fulani wa taasisi nyeti anamfahami vilivyo Komu alivyokua anawachachafya kule Seminary. Leo anakimbizwa na wawekezaji wa kisiasa.

Hata hivyo siungi mkono kauli ya Askofu kwa sababu hata kama wapinzani wangeshiriki uchaguzi hali ingekua ni hiyo hiyo mana CCM wangekata rufaa na kuwaengua wote hata kama wangeshinda mana wameshaelekezwa kosa lilipo kuwa ni majina ya Vyama na kwa mtego hawakusema kuwa form zijazwe upya Bali waruhusiwe kugombea. Mtego ulikua hapo bado.

Lakini pia ukimfumania mpishi anataka kukuwekea sumu kwenye chakula huwezi kukubali kuendelea kupikiwa chakula na mpishi huyo huyo eti kwa sababu chakula kimemwagwa.

Wapinzani wajichunguze.
Serikali ijichunguze.
CCM ijichunguze.
Wananchi wajichunguze.
Kanisa Katoliki lijichunguze kama limesimama katika haki au upande wenye dhulma na nguvu ya fedha na mabavu?
 
Sina hakika kama aliyozungumza Rais wa TEC yametokana na maazimio ya TEC.Rais wa TEC anapaswa kufahamu kuwa ana kofia mbili,ya Uaskofu wa jimbo lake na uakilishi wa kanisa katoliki Tanzania.Nina mashaka kama tamko lake linatokana na Baraza la TEC.Kama sivyo sakretariati ya TEC (kama ipo)inapaswa kujitenga na kauli ya Askofu Mwaisonya.Ni kauli isiyokuwa na tafakuri ya kina na isiyojua ni nini kinachoendelea kwenye jamii.Kama huna uhakika na jambo,usizungumze.Busara ni kukaa kimya.
Kabla ya yote lazima ujiulize katika viongozi wa vyama vya upinzani walioazimia kususia uchaguzi umemwona MTU mwenye uwezo wa kutoa hoja ya kulishawishi kanisa Katoliki . Kanisa lililofungamana serikali tangu enzi na enzi.
Lazika pawe na mtu anayejua filosofia ya Kanisa na mtizomo wake ili aweze kutoa hoja zenye kuweza kulishawishi kanisa hilo kwa mapana yake.
Vyama vyenye nguvu vijifunze kupata viongozi wanye maono mapana yanayoweza kujichimbia mpaka ndani ya kanisa Katoliki na sio kubaki kulia lia tu wakati wanajua wazi kuwa kanisa hilo tangu ukoloni lina ndimi mbili.
 
Nimesikiliza mahubiri ya Askofu Mkuu na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tz,Mhashamu Askofu Nyaisonga, ameelekeza lawama zake katika vyama vya upinzani,akijenga hoja kuwa havikutumia busara na elimu katika kufikiri na kujitoa katika uchaguzi.

Amehimiza kuwa kujitoa sio suluhu,wanapaswa kukaa meza moja na serikali kutatua hiyo changamoto,amesisitiza kuwa waliojitoa wamekosea,hivyo kasema msimamo wa maaskofu Wakatoliki ni kutokubaliana na kusisia uchaguzi,na wamehimiza waumini kujitokeza wa wingi jumapili kupiga kura.

Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Peter O'bay naye amehubiri kile alichotumwa na wakubwa zake, kuhimiza watu wajitokeze kwa wingi katika uchaguzi, hii ni kusema, kanisa katoliki linaungana na Polepole, Jafo na TAMISEMI kuubariki uchaguzi wa serikali za mitaa ambao mchakato wake umejaa utata mtupu,utata ambao hata makada wazoefu wa CCM wanaona aibu kwa yaliyotokea. Hili ndio kanisa Katoliki na msimamo wake umetangazwa na Rais wa TEC. Kanisa limeridhika na mchakato, halitaki kugombana na serikali, limewakana waumini wake waliogoma toka mwanzo kujiandikisha kwa kuona ubovu wa demokrasia kwa sasa.

Katika maandishi ya kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed", mwandishi alijaribu kuelezea kwa undani jinsi kanisa, na hasa kanisa la Vatican wakati mwingi lilivyoshiriki kuungana na serikali katika kuisaidia kufikia adhma yake, mwandishi ameeleza nafasi ya wamisionari katika kuitawala Afrika, jinsi walivyotangulia na kuwatengenezea njia wakoloni, kuanzia Congo ya DR mpaka Afrika ya Kusini,Kaskazini na Mashariki ya Afrika. Mwandishi anasema kanisa huangalia kwanza maslahi ya viongozi wake kabla ya waumini wake.

Inaelezwa kuwa wakati wa utawala wa Kifashisti kule Italia, Mussolini aliona tishio la Kanisa Katoliki ktk kufikia malengo yake. Maana kwa wakati ule, kanisa lilikuwa na ushawishi wa kila sekta ya maisha ya kiroho na kimwili na serikali ilikuwa na ushawishi mdogo tu ya maisha ya kisiasa.

Alichokifanya Mussolin ni kujipendekeza kwa kanisa na kutoa "rushwa" ili yote atakayoyafanya kanisa katoliki lililokuwa na nguvu sana Italia libaki kimyaa.Na Alifanikiwa...

Kwanza aliamua kumbatiza mwanae wa kiume, ambaye hapo awali hakuwa amebatizwa.Hapa akaliteka kanisa kwa karata ya kwanza.

Pili alimua kufunga ndoa ya kikanisa,baada ya kuwa amekaa miaka 11 na ndoa ya bomani na mkewe Rachele.Hii ikawa karata ya pili ya kujisogeza na kujiweka karibu na kanisa ili kutimiza malengo yake ya ufashisti.

Karata nyingine;aliamuru kufungwa kwa maduka yote ya vileo(wine shops) na kufuta leseni za clubs zote za usiku ili kuendana na kauli ya kanisa ya kupunguza uovu mitaani kwa ulevi na anasa za usiku.Hapa kanisa katoliki likanasa mtegoni.

Alienda mbali mpaka akatangaza kuwa "Public Swearing",yaani kujiapiza hadharani jina la Mungu kama "Public Crime"...Yaani mwananchi ukiwa mtaani mnabishana,mtu akikwambia sema Haki ya Mungu...Ukisema tu "Haki ya Mungu sijaenda nyumba ndogo mwezi wa pili sasa".Basi ujue wewe una kesi ya jinai ya kujibu.Hapa alitaka kulifurahisha kanisa kwa amri ile isemayo "Usitaje bure jina la bwana Mungu wako"

Mussolini akaamuru kupigwa marufuku vidonge vya majira na kampeni zote za matumizi ya uzazi wa mpango kama ulivyo msimamo wa kanisa.Wakati huo kanisa lilitaka wanawake wabaki nyumbani ili kulea watoto na kukuza familia vyema.Mussolini akalipigia chapuo hili na kulitungia sheria ili kuwafurahisha wazee wa kanisa.

Akatunga sheria ambayo ilifutilia mbali talaka kwa ndoa hata za bomani.Hii ilikuwa ni njia ya kuungana na kanisa ktk ndoa ya mke mmoja na isiyo na talaka mpaka Mungu awatenganishe.Ndoano hii ikanasa vizuri kwa kanisa.Hawakupepesuka wala kutikisika.Mambo yote ya ndoa yakaondolewa serikalini na kubaki kuwa in "Full Control of the Catholic Church".Wale wapenda mteremko wa ndoa za bomani wakakosa pa kwenda.

Akatoa 109 acres ktk mji wa Roma ili yajengwe makao makuu ya Papa(Vatican) baada ya kuwa yalipokonywa wakati wa "Unification of Italy" ya miaka ya 1870's,na akatoa amri kanisa lilipwe zaidi ya £130 milioni kwa wakati ule.Hii ilikuwa ni ndoano iliyoingia sawasawa kwa kanisa,na kanisa halikusema lolote juu ya "ufashisti" wa Mussolini hadharani;japo liliouona na kuuhisi kwake na kwa waumini wake.

Vatican ikawa nchi ndani ya mji,wakapewa mamlaka juu ya Post Office,jeshi dogo,polisi na "Rail station".Baada ya hapo,ugomvi ukawa ni nani anatakiwa ku-control Elimu?Mussolini alihitaji sekta ya elimu ili apandikize "ufashist" kwa watoto,na kanisa lilitaka elimu ili kupandikiza imani ya kikatoliki kwa watoto.

Mambo haya yote ambayo baadae,waumini wasio rasharasha waliona ni kama rushwa kwa kanisa ili liweze kusifia na kukaa kimya juu ya serikali ya kifashisti ya Mussolin yalifanikiwa.

Si ajabu Papa John Paul II alikuja kuiomba jumuiya ya waumini na wasio waumini ktk jubilei ya miaka 2000 ya Ukristo kwa yale yote kanisa iliyoyakosea ktk kukuwa kwake.Hili la kuukumbatia uonevu wa serikali isiyojali usawa ya Mussolini lilikuwa ni moja ya kosa la Kanisa.

Hakukuwa na Kardinali,askofu wala kasisi(padre) aliyeikemea serikali isiyo ya kidemokarasia ya Utawala wa Mussolini.Mengi yalitokea na kanisa lilikaa kimyaaa.Waumini waliteseka,waliumia na walipata machungu ya maisha...Lakini kanisa lilisema hewalaaa,huu ni utawala mzuri tu,maana umerudisha heshima ya Papa katika nchi ya Italia.

Hatumaanishi kuwa sasa Tanzania tuna ufashisti,lakini tunakubaliana kuwa kwa sasa Tanzania maisha ya chuki za kisiasa,mienendo ya kidemokrasia na ushiriki wa watu katika siasa huru umekengeuka sana.

Kuwa baba wa kiroho na kuongea kinyume cha yale waumini wako ambao ni sehemu ya wananchi wa Tanzania wanalalamika,ni kuwa upande wa pili badala ya ule wa waumini wako.

Ndio maana wale wanafunzi wa historia ya kale,wanaweza kustuka na kuona kuwa kanisa linaendelea kuwa upande tofauti na wanaoonewa.Kanisa libaki kuwa mali ya waumini wanyonge,liachane na urafiki wa mashaka kama ule wa Mussolini na Vatican enzi hizo za zama za giza za Ulaya.

Kama kanisa la wakati huo lilibaki kimya juu ya ufashisti wa Benitho Mussolini,hili la kwetu la Tanzania,lisibaki kimya juu ya uonevu wa kidemokrasia,vurugu za kuinajisi demokrasia unaonekana kufanywa waziwazi kabisa na serikali.Kutoa kauli za aina hii hadharani,mbele ya mimbari na katika altare takatifu,inatupa mashaka na tutaamua kurudi na kupekua kurasa za kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed"

Tukizifunua kurasa hizi;Tutahitimisha kwa kusema,Rais wa TEC amesimama upande wa serikali,amesimama na wanaodhaniwa kuminya demokrasia na mizizi yake,taswira ya waumini ambao ndio raia wenyewe kutokupendezwa na haya yanayoendelea haujaletwa na vyama vya upinzani,maana waumini walianza kugoma kujiandikisha mpaka pale walipohimizwa kwa lazima.

Hizi ni dalili kuwa si tu hatua ya kugomea uchaguzi imeasisiwa na vyama pinzani,bali ilishaanza kutendwa na waumini ambao ndio wapiga kira wenyewe.

Tutamkumbusha RAIS WA TEC na Askofu Mkuu wa Mbeya Nyaisonga kuwa kuutumikia mwili ni gharama zaidi ya kuitumikia roho.Ndio maana Lugha Mama ya Kanisa ya Kilatini ikasema "Nemo Liber Est Qui Corpori Servit"(No One is Free who is a slave of his body)

Tuitumikie Roho inayodumu milele,kuliko mwili unaooza na kuliwa na nyenyere.View attachment 1265377View attachment 1265378

Nimeumwa ghafla. Sijui nikapime kipimo gani. Siendi tena kanisani. Mitabaki na machozi ya ndugu zangu yeye na ulatili aliousifia ataukuta jehanamu. Shetani andaa kuni au mkaa wa kutosha. Ikiwezekana weka gesi ya kutosha.
 
Kabla ya yote lazima ujiulize katika viongozi wa vyama vya upinzani walioazimia kususia uchaguzi umemwona MTU mwenye uwezo wa kutoa hoja ya kulishawishi kanisa Katoliki . Kanisa lililofungamana serikali tangu enzi na enzi.
Lazika pawe na mtu anayejua filosofia ya Kanisa na mtizomo wake ili aweze kutoa hoja zenye kuweza kulishawishi kanisa hilo kwa mapana yake.
Vyama vyenye nguvu vijifunze kupata viongozi wanye maono mapana yanayoweza kujichimbia mpaka ndani ya kanisa Katoliki na sio kubaki kulia lia tu wakati wanajua wazi kuwa kanisa hilo tangu ukoloni lina ndimi mbili.
'ujiulize katika viongozi wa vyama vya upinzani walioazimia kususia uchaguzi umemwona MTU mwenye uwezo wa kutoa hoja ya kulishawishi kanisa Katoliki'.

Uzuri wananchi wanajionea figisu zinazofanywa na watawala so hakuna hata haja ya wapinzani kutoa hoja zozote za kulishawishi kanisa katoliki.
 
Mimi niliyasikia haya wakati wa kipindi cha kumpata Rais mpya wa TEC. Jambo la kujiuliza, hivi hizi dini zetu zipo kwaajili ya imani au maslahi fulani? Ni dini au watu fulani ndio wanaozifanya dini kuwa syndicate ya matakwa binafsi ya watu fulani?
Mkuu kwa nini unajipa jakamoyo?hamia mito ya baraka au mlima moto,yesu ni yule yule tu
 
Wapinzani wamenusa tu kushindwa suala la kususa ni geresha
Eti UPDP nao wamesusa,sijui hata kama wana kiti hata kimoja katika mitaa yote nchi nzima
 
Niliwahi kueleza hapa jukwaani taarifa kutoka kwa Askofu mmoja kutoka inner circle ya Kanisa Katoliki. Mimi pia ni mkatoliki halisi wa imani aliyewahi kuhudumu ndani ya kanisa.

Askofu yile alieleza kuwa Kanisa Katoliki, baada ya waraka wa kwaresma, ulioeleza mapungufu mengi ya watawala wa awamu hii, uhusiano wake na mtawala mkuu ulififia sana kufikia hatua ya kujenga uadui. Inner circle ya Kanisa waliazimia kuurudisha uhusiano huo uliokuwa umezoeleka.

Hatua ya kwanza ilikuwa kumpata Rais wa TEC ambaye ana mahusiano binafsi ya karibu na mtawala, na huyo hakuwa mwingine bali huyu Rais wa TEC wa sasa. Hilo lilifanikiwa.

Na ninarudia tena, chini ya uongozi wa sasa wa TEC, msitegemee kauli yoyote ile kutoka TEC itakayokuwa kinyume na matakwa ya watawala. Kanisa, kama lilivyo bunge na mahakama, wamejumuishwa. Mark my words.

Mimi niliyasikia haya wakati wa kipindi cha kumpata Rais mpya wa TEC. Jambo la kujiuliza, hivi hizi dini zetu zipo kwaajili ya imani au maslahi fulani? Ni dini au watu fulani ndio wanaozifanya dini kuwa syndicate ya matakwa binafsi ya watu fulani?

Mm sio msemaji lakini kwa kauli hii ya huyu askofu tutawaumbua. Hawezi kutetea watu wanne wakati mamilioni wanateseka. Niko tayari kufa na kuteseka jamani. Baba mtakatifu tunakuita nenda Tanzania kaangalie vilio vya watoto wako.
Na mimi ni mkatoliki lakini maweza kuwa na ushawishi duuu!!!!!!!. Jiwe kila mahali anarushiwa stone hata duniani na mbinguni hafai.

Baba nyoosha mkono wako (Il tuo lemani beneffici signore) sisi baba bado tunakupenda ndio maombi yetu.
 
haki ni ku support unachokitaka wewe?
Kumbuka Askofu Ruwaichi alitumiwa ndege kumchumkua huko KCMC Hospital na kumleta hapa Dar kupata matibabu kwa maelekezo ya rais. Katika mazingira hayo unategemea kanisa la Roma liwe upande wa haki au la wanaowalinda viongozi wake?
 
Anza kwa Ngwajima patakufaa..
Usisumbuke kuona aibu. tuko powa
Huku nikutudhalilisha wakatoliki

Yaani nasikia aibu sana mimi kuitwa mkatoliki

Hawa viongozi hovyo sana.

Badala ya kukemea maovu, wanakumbatia waovu

Wakapige wao mapadre mimi nafamilia yangu marufuku
 
Unawalilia RC. utadhani ni chama cha siasa.
Subiri kanisa la wachaga KKKT li support kila wanachotaka chadema..
Mkuu hili ulilolosema liko wazi na ni ukweli mtupu. Wangalau KKKT ndio wamebaki upande wa haki, hao RC wameamua kusimamia upande wa uovu ili kupata faida binafsi. Nadhani huko makanisani kuna mabox ya maoni, ni vyema hiyo kauli ikapigwa kwa nguvu zote na waumini.
 
Nimesikiliza mahubiri ya Askofu Mkuu na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tz,Mhashamu Askofu Nyaisonga, ameelekeza lawama zake katika vyama vya upinzani,akijenga hoja kuwa havikutumia busara na elimu katika kufikiri na kujitoa katika uchaguzi.

Amehimiza kuwa kujitoa sio suluhu,wanapaswa kukaa meza moja na serikali kutatua hiyo changamoto,amesisitiza kuwa waliojitoa wamekosea,hivyo kasema msimamo wa maaskofu Wakatoliki ni kutokubaliana na kusisia uchaguzi,na wamehimiza waumini kujitokeza wa wingi jumapili kupiga kura.
Ahsante kwa andiko hili lenye funzo mhimu, mkuu 'Barafu'.

Linalojitokeza kwa msimamo waliochukua hawa wenye dini yao, ni kwamba waumini wataanza kuhoji. Hili ni jambo jema watu wakianza kuhoji.
Hawa viongozi wa dini, kiukweli sio wenye kanisa; kanisa ni waumini. Waumini wanapoanza kuhoji yanayofanywa au kusimamiwa na viongozi wa dini zao, wanajikomboa na kujitoa kwenye ujinga wa kufuata kila kitu wasemacho viongozi wa dini kama makondoo. Kwa hiyo hili ni jambo zuri kabisa wanalofanya hawa viongozi wa dini.

Ningejua namna ya kumfikishia ujumbe wa bandiko lako hili huyo askofu ningemfikishia, au hata kumtumia kitabu chenyewe ulichotaja hapa ili na yeye ajisomee.
Na kwa bahati mbaya sana, dini zote watu/viongozi kama hawa wamo.
 
Back
Top Bottom