LGE2024 Askofu Ruwa'ichi: Kuandikisha watoto kupiga Kura ni Hatari kwa Taifa, Tunalea Wahuni na Wezi

LGE2024 Askofu Ruwa'ichi: Kuandikisha watoto kupiga Kura ni Hatari kwa Taifa, Tunalea Wahuni na Wezi

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Askofu Jude Thaddeus Ruwa'ichi kupitia mahojiano aliyofanya na Tumaini TV amesema:

"Uchaguzi wa serikali za mitaa ni zoezi la kiraia, ni fursa ya kidemokrasia, lakini zoezi hilo ni lazima litekelezwe kwa uadilifu, kwa uzalendo na kwa uaminifu, ni Sala yetu kwamba kama zoezi la kupata viongozi wa serikali za mitaa raia wenye haki ya kupiga kura wapate fursa ya kupiga kura halali, nasema kura halali kwa sababu ilishatokea yakaweko manung'uniko kwamba umefanyika uchaguzi lakini waliochaguliwa hawakuchaguliwa kwa kura halali, hilo halitaifaa nchi yetu, jamii yetu katika maendeleo na halitasaidia katika maendeleo."

"Ili tuendelee kama raia wa Tanzania tunahitaji kufanya mambo kwa namna ambayo ni ya haki, uadilifu, safi na ni sahihi, nilipokuwa Roma (Italia) nilikuwa nafuatilia taarifa za habari na ilinisikitisha niliposikia kwamba hapa na pale imegundulika kwamba kuna mbinu za kuwaandikisha watoto ambao hawajafikisha umri wa kupiga kura, kitendo kama hicho ni kitendo cha hatari sana kwa sababu ni kuwafundisha watoto kuwa wezi, ni kuwafundisha watoto kuwa waongo, ni kuwafundisha watoto kuwa wahuni, sasa tukilea watoto wetu kuwa waongo, kuwa wezi, kuwa wahuni, maana yake tunatia mbegu ya mahangaiko yetu wenyewe, tupende kufanya vitu kwa usahihi na ukweli na namna hiyo ya kufanya vitu itujenge."
 
Kama unabisha angalia Wanasiasa na watumishi wa Umma walioiba Mitihani au kuiba Majina ya wanafunzi Wenzao walipokuwa Primary school au O level

Mzazi unaweza kujiona mjanja Leo kumtumia Mwanao kwa matamanio Yako ya Kisiasa lakini ukumbuke kuwa " hiyo ni mbegu umeshapanda"

Askofu Ruwaich Mungu wa mbinguni akutunze, amen!

Baadaye Mlale Unono 😀
 
Kama unabisha angalia Wanasiasa na watumishi wa Umma walioiba Mitihani au kuiba Majina ya wanafunzi Wenzao walipokuwa Primary school au O level

Mzazi unaweza kujiona mjanja Leo kumtumia Mwanao kwa matamanio Yako ya Kisiasa lakini ukumbuke kuwa " hiyo ni mbegu umeshapanda"

Askofu Ruwaich Mungu wa mbinguni akutunze, amen!

Baadaye Mlale Unono 😀Lam
January Mkamba, Daudi Albert Bashite aka Paul Christian Makonda, Saidi Bagaile aka Khamis Kigwangwala, Lameck Madelu aka Mwigulu Nchemba, list ni ndefu sana muda mchache.
 
Kama unabisha angalia Wanasiasa na watumishi wa Umma walioiba Mitihani au kuiba Majina ya wanafunzi Wenzao walipokuwa Primary school au O level

Mzazi unaweza kujiona mjanja Leo kumtumia Mwanao kwa matamanio Yako ya Kisiasa lakini ukumbuke kuwa " hiyo ni mbegu umeshapanda"

Askofu Ruwaich Mungu wa mbinguni akutunze, amen!

Baadaye Mlale Unono 😀
sema kizimkazi, sema wazi wazi, acha porojo kijana
 
Kama unabisha angalia Wanasiasa na watumishi wa Umma walioiba Mitihani au kuiba Majina ya wanafunzi Wenzao walipokuwa Primary school au O level

Mzazi unaweza kujiona mjanja Leo kumtumia Mwanao kwa matamanio Yako ya Kisiasa lakini ukumbuke kuwa " hiyo ni mbegu umeshapanda"

Askofu Ruwaich Mungu wa mbinguni akutunze, amen!

Baadaye Mlale Unono 😀
Nasikia Waziri wa Katiba na Sheria wa Kenya hakuwa na cheti cha form four. Ni waziri wa kenya Tanzania
 
Back
Top Bottom