kifupi kirefu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2018
- 539
- 3,507
Mbunge wa Korogwe Vijijini Timotheo Mzava anatarajiwa kufunga ndoa na Binti wa Mbunge wa Arumeru Mashariki Dr. Jonh Pallangyo. Ndoa hii inalalamikiwa na mtu anayetambulika kwa jina la Anna na wachungaji huko Arusha na Tanga wanafahamu upo mgogoro. Mgogoro huu nimeusoma kwenye gazeti kwamba Mzava ameishi na mwanamke kinyumba kwa miaka mitatu na amezaa naye mtoto Kisha akamwacha na kuanza mahusiano na mtoto wa Mbunge mwenzie.
Mimi sina shida na mahusiano mapya ila kwa mujibu wa Taarifa zilizotolewa na Raia Mwema na nikiwa Kama muumini wa kikristo nimeona Kama kanisa halifanyi kazi yake Kama linavyopaswa kufanya. Kanisa linachafuka kwa kuandikwa vibaya kwenye magazeti lakini pia skendo ikihusisha watu wenye vyeo na fedha kwenye jamii.
Tunapoona haya yanaandikwa kwenye vyombo vya habari na kwa kuwa yanagusa imani zetu za dini pamoja na nyumba za ibada, tunalazimika kuwaomba viongozi wa dini watoke adharani kukana tuhuma hizi zilizoelekezwa kwao au kuzikubali na kuzirekebisha kwa kuzingatia maandiko na Katiba ya kanisa.
Utaratibu wa kanisa upo wazi, kabla ya kufunga ndoa lazima ndoa itangazwe siku 21 na likitokea pingamizi Basi lipatiwe ufumbuzi na TAASISI husika, je inakuwaje Kuna pingamizi na taratibu za kufunga ndoa next week kwa mujibu wa gazeti zinaendelea.
Endapo muumini atabainika kufanya uzinzi na ushahidi kuwepo (kwa mazingira haya ushahidi ni mtoto wa mzava na Anna) muumini lazima asimame mbele ya kanisa na kutubu Kisha kurejeshwa kundini ndipo taratibu za ndoa ziendelee, huyu Mzava hajawahi kufanya haya.
Panapowekwa pingamizi mweka pingamizi uitwa na suluhu upatikana, kwenye hili hakuna hiyo suluhu. Je, siku ya ndoa Anna akisimama akasema anapingamizi ndoa itafungwa? Kanisa halina walinzi, je siku hiyo familia hizi mbili zitakuja na walinzi kanisani kwa sababu Wana nafasi serikalini na Wana fedha? Kwanini Mkuu wa KKKT usubiri hadi Hali ichafuke kwenye hekalu wakati una nafasi yakusimama imara na kuzitetea nguzo za imani?
Nikuombe wewe na viongozi wa kanisa msiruhusu mambo haya kufanyika sirini, tokeni adharani msafishe kanisa kwenye tuhuma hizi za wanasiasa kutumia madara na pesa kupindisha utaratibu wa kanisa.
Tendeni haki, Kama Mzava na Pallangyo Wana haki tokeni adharani tuelezeni kwa haki yao ni ipi, na Kama huyo mwanamke Anna ana haki na mtoto wake kuweka pingamizi sikilizeni pingamizi ilo. Msipowatendea wenye fedha na madaraka Kama mnavyowatendea watu wa chini dhambi hii italipasua kanisa. Wapo waumini wametengwa kwa zinaa, Wapo waumini ndugu zao wamezikwa bila kanisa kushiriki kisa tu alikuwa ajarudishwa kundini, Wapo watu wametengwa na huduma za kanisa baada ya kubainika Wana vimada au mke zaidi ya mmoja lakini watu hao wote kwa miaka ya hivi karibuni wamekuwa na waumini wa Hali ya chini.
Matajiri na wenye nyadhifa hakuna sehemu mmewatenga Wala kukataa kuwazika. Simamieni misingi ya kanisa acheni kuwaona waumini flani Wana haki kuliko wengine.
Natumai utamwomba Mwenyenzi Mungu akusaidie kuliponya kanisa pale ambapo walio chini yako wamekuwa wakipotoka. Nakupenda nakutakia tafakuri njema huku ukilinda imani na kanisa ulilokabidhiwa.
Mimi sina shida na mahusiano mapya ila kwa mujibu wa Taarifa zilizotolewa na Raia Mwema na nikiwa Kama muumini wa kikristo nimeona Kama kanisa halifanyi kazi yake Kama linavyopaswa kufanya. Kanisa linachafuka kwa kuandikwa vibaya kwenye magazeti lakini pia skendo ikihusisha watu wenye vyeo na fedha kwenye jamii.
Tunapoona haya yanaandikwa kwenye vyombo vya habari na kwa kuwa yanagusa imani zetu za dini pamoja na nyumba za ibada, tunalazimika kuwaomba viongozi wa dini watoke adharani kukana tuhuma hizi zilizoelekezwa kwao au kuzikubali na kuzirekebisha kwa kuzingatia maandiko na Katiba ya kanisa.
Utaratibu wa kanisa upo wazi, kabla ya kufunga ndoa lazima ndoa itangazwe siku 21 na likitokea pingamizi Basi lipatiwe ufumbuzi na TAASISI husika, je inakuwaje Kuna pingamizi na taratibu za kufunga ndoa next week kwa mujibu wa gazeti zinaendelea.
Endapo muumini atabainika kufanya uzinzi na ushahidi kuwepo (kwa mazingira haya ushahidi ni mtoto wa mzava na Anna) muumini lazima asimame mbele ya kanisa na kutubu Kisha kurejeshwa kundini ndipo taratibu za ndoa ziendelee, huyu Mzava hajawahi kufanya haya.
Panapowekwa pingamizi mweka pingamizi uitwa na suluhu upatikana, kwenye hili hakuna hiyo suluhu. Je, siku ya ndoa Anna akisimama akasema anapingamizi ndoa itafungwa? Kanisa halina walinzi, je siku hiyo familia hizi mbili zitakuja na walinzi kanisani kwa sababu Wana nafasi serikalini na Wana fedha? Kwanini Mkuu wa KKKT usubiri hadi Hali ichafuke kwenye hekalu wakati una nafasi yakusimama imara na kuzitetea nguzo za imani?
Nikuombe wewe na viongozi wa kanisa msiruhusu mambo haya kufanyika sirini, tokeni adharani msafishe kanisa kwenye tuhuma hizi za wanasiasa kutumia madara na pesa kupindisha utaratibu wa kanisa.
Tendeni haki, Kama Mzava na Pallangyo Wana haki tokeni adharani tuelezeni kwa haki yao ni ipi, na Kama huyo mwanamke Anna ana haki na mtoto wake kuweka pingamizi sikilizeni pingamizi ilo. Msipowatendea wenye fedha na madaraka Kama mnavyowatendea watu wa chini dhambi hii italipasua kanisa. Wapo waumini wametengwa kwa zinaa, Wapo waumini ndugu zao wamezikwa bila kanisa kushiriki kisa tu alikuwa ajarudishwa kundini, Wapo watu wametengwa na huduma za kanisa baada ya kubainika Wana vimada au mke zaidi ya mmoja lakini watu hao wote kwa miaka ya hivi karibuni wamekuwa na waumini wa Hali ya chini.
Matajiri na wenye nyadhifa hakuna sehemu mmewatenga Wala kukataa kuwazika. Simamieni misingi ya kanisa acheni kuwaona waumini flani Wana haki kuliko wengine.
Natumai utamwomba Mwenyenzi Mungu akusaidie kuliponya kanisa pale ambapo walio chini yako wamekuwa wakipotoka. Nakupenda nakutakia tafakuri njema huku ukilinda imani na kanisa ulilokabidhiwa.