Askofu Shoo, Wabunge Timotheo Mzava wa Korogwe na Dkt. Pallangyo wa Arumeru wanalichafua kanisa au wanachafuliwa?

Askofu Shoo, Wabunge Timotheo Mzava wa Korogwe na Dkt. Pallangyo wa Arumeru wanalichafua kanisa au wanachafuliwa?

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Mbunge wa Korogwe Vijijini Timotheo Mzava anatarajiwa kufunga ndoa na Binti wa Mbunge wa Arumeru Mashariki Dr. Jonh Pallangyo. Ndoa hii inalalamikiwa na mtu anayetambulika kwa jina la Anna na wachungaji huko Arusha na Tanga wanafahamu upo mgogoro. Mgogoro huu nimeusoma kwenye gazeti kwamba Mzava ameishi na mwanamke kinyumba kwa miaka mitatu na amezaa naye mtoto Kisha akamwacha na kuanza mahusiano na mtoto wa Mbunge mwenzie.

Mimi sina shida na mahusiano mapya ila kwa mujibu wa Taarifa zilizotolewa na Raia Mwema na nikiwa Kama muumini wa kikristo nimeona Kama kanisa halifanyi kazi yake Kama linavyopaswa kufanya. Kanisa linachafuka kwa kuandikwa vibaya kwenye magazeti lakini pia skendo ikihusisha watu wenye vyeo na fedha kwenye jamii.

Tunapoona haya yanaandikwa kwenye vyombo vya habari na kwa kuwa yanagusa imani zetu za dini pamoja na nyumba za ibada, tunalazimika kuwaomba viongozi wa dini watoke adharani kukana tuhuma hizi zilizoelekezwa kwao au kuzikubali na kuzirekebisha kwa kuzingatia maandiko na Katiba ya kanisa.

Utaratibu wa kanisa upo wazi, kabla ya kufunga ndoa lazima ndoa itangazwe siku 21 na likitokea pingamizi Basi lipatiwe ufumbuzi na TAASISI husika, je inakuwaje Kuna pingamizi na taratibu za kufunga ndoa next week kwa mujibu wa gazeti zinaendelea.

Endapo muumini atabainika kufanya uzinzi na ushahidi kuwepo (kwa mazingira haya ushahidi ni mtoto wa mzava na Anna) muumini lazima asimame mbele ya kanisa na kutubu Kisha kurejeshwa kundini ndipo taratibu za ndoa ziendelee, huyu Mzava hajawahi kufanya haya.

Panapowekwa pingamizi mweka pingamizi uitwa na suluhu upatikana, kwenye hili hakuna hiyo suluhu. Je, siku ya ndoa Anna akisimama akasema anapingamizi ndoa itafungwa? Kanisa halina walinzi, je siku hiyo familia hizi mbili zitakuja na walinzi kanisani kwa sababu Wana nafasi serikalini na Wana fedha? Kwanini Mkuu wa KKKT usubiri hadi Hali ichafuke kwenye hekalu wakati una nafasi yakusimama imara na kuzitetea nguzo za imani?

Nikuombe wewe na viongozi wa kanisa msiruhusu mambo haya kufanyika sirini, tokeni adharani msafishe kanisa kwenye tuhuma hizi za wanasiasa kutumia madara na pesa kupindisha utaratibu wa kanisa.

Tendeni haki, Kama Mzava na Pallangyo Wana haki tokeni adharani tuelezeni kwa haki yao ni ipi, na Kama huyo mwanamke Anna ana haki na mtoto wake kuweka pingamizi sikilizeni pingamizi ilo. Msipowatendea wenye fedha na madaraka Kama mnavyowatendea watu wa chini dhambi hii italipasua kanisa. Wapo waumini wametengwa kwa zinaa, Wapo waumini ndugu zao wamezikwa bila kanisa kushiriki kisa tu alikuwa ajarudishwa kundini, Wapo watu wametengwa na huduma za kanisa baada ya kubainika Wana vimada au mke zaidi ya mmoja lakini watu hao wote kwa miaka ya hivi karibuni wamekuwa na waumini wa Hali ya chini.

Matajiri na wenye nyadhifa hakuna sehemu mmewatenga Wala kukataa kuwazika. Simamieni misingi ya kanisa acheni kuwaona waumini flani Wana haki kuliko wengine.

Natumai utamwomba Mwenyenzi Mungu akusaidie kuliponya kanisa pale ambapo walio chini yako wamekuwa wakipotoka. Nakupenda nakutakia tafakuri njema huku ukilinda imani na kanisa ulilokabidhiwa.
 
Kama Anna na Mzava waliishi kama mume na mke Kwa zaidi ya miaka miwili, hapo Kuna presumption of marriage.

Anna ana pingamizi halali, asikilizwe.
Mkuu, Sheria ya ndoa katika kifungu cha 160 inaeleza juu ya mahusiano haya kwamba endapo mwanamke akiishi na mwanaume kwa miaka miwili au zaidi mfululizo na jamii inayowazunguka ikawatambua na kuwapa hadhi ya mume na mke, basi mahusiano hayo yaweza kupata dhana ya kuchukuliwa kama wana ndoa na wawe wanafanya matendo ya kindoa
 
Wote chama tawala, wabunge Kama wamechanga wasikilizie Kwanza wasipeleke ma V8 yao ukumbuni harusi ikapingwa. Haya mambo yakuachana na mademu kwa kuwakoromea ndo matatizo yake haya, ndoa inakosa amani fresh sendoff day
 
Katika sheria ya Ndoa ya 1971, Kifungu cha 160 kinaeleza dhana hii kwa ndani zaidi kwa kuanishi vigezo vinavyoweza kuchukuliwa maanani ili kudhibitisha dhana ya uwepo wa ndoa.

Vigezo vinavyothibitisha Uwepo wa Dhana ya Ndoa

Udhibitisho wa kuishi kwa mwanamke na mwanaume kwa kipindi kisichopungua miaka 2 na zaidi. Ili dhana hii ithibitike ni lazima uwepo ushahidi wa maisha ya pamoja kati ya mwanamume na mwanamke.

Lazima kuwe na udhibitisho kuwa umma au jamii inayowazunguka wanawachukulia na kuwapa heshima kama mke na mume. Hapa swali la kijamii lazima lijibiwe ni kwa namna gani maisha yao yanaonekana mbele ya watu.

Lazima ithibitishwe kuwa watu hao walikuwa na uwezo wa kuwa mke na mume wakati walipoanza kuishi pamoja na kama walikuwa na umri unaokubalika kisheria. Umri wa kuweza kuingia kwenye ndoa ni miaka 18 hivyo walio chini ya hapo dhana hii haiwezi kusimama.

Ni lazima pia ithibitishwe kuwa kati yao au wote wawili hakuna aliye na ndoa iliyokuwa inaendelea. Hii ni muhimu dhana hii haitasimama pale mwanaume ana mke mwengine eneo lingine na akaende kuishi na mwanamke mwengine katika eneo lingine hata kama ni zaidi ya miaka 2.

Sasa Endapo dhana hii itadhibitishwa mahakamani kulingana na vigezo vilivyoainishwa hapo juu basi haki na wajibu wa mwanamke na mwanamume utahesabika kama walio katika ndoa halali;

Haki ya mwanamke kudai matunzo kwa ajili yake na watoto waliozaliwa katika kipindi chote

Haki ya mwanamke au mwanaume kuomba mahakama kuvunja ndoa hiyo au kutoa amri ya kutengana

Haki ya kupewa kukaa na watoto

Haki juu ya mali na machumo yaliyopatikana katika kipindi chote walichokaa pamoja.

Sheria ya Ndoa ya 1971 imeainisha dhana hii ya uwepo wa ndoa ili kutoa ulinzi kwa mwanamke na watoto watakaozaliwa katika mazingira hayo.

Hata hivyo dhana hii haiondoi umuhimu wa wahusika kuchukua hatua na kufunga ndoa halali kwa mujibu wa sheria kwa taratibu za kidini au kimila au kiserikali kama watakavyoona inafaa.

Upungufu wa kufunga ndoa unaweza kusababisha matatizo makubwa endapo mmoja wapo atafariki na kupelekea watoto na mwenzi kutishiwa kupoteza haki zake za urithi kwa kigezo cha kukosa ndoa.... I stand to be corrected guys
 
Waache Waoane
Screenshot_2021_0706_230736.jpg
 
Endapo muumini atabainika kufanya uzinzi na ushahidi kuwepo (kwa mazingira haya ushahidi ni mtoto wa mzava na Anna) muumini lazima asimame mbele ya kanisa na kutubu Kisha kurejeshwa kundini ndipo taratibu za ndoa ziendelee, huyu Mzava hajawahi kufanya haya
Atatubu kwa nani wakati wenye kuongoza toba ni wachafu?
 
Katika sheria ya Ndoa ya 1971, Kifungu cha 160 kinaeleza dhana hii kwa ndani zaidi kwa kuanishi vigezo vinavyoweza kuchukuliwa maanani ili kudhibitisha dhana ya uwepo wa ndoa.

Vigezo vinavyothibitisha Uwepo wa Dhana ya Ndoa

Udhibitisho wa kuishi kwa mwanamke na mwanaume kwa kipindi kisichopungua miaka 2 na zaidi. Ili dhana hii ithibitike ni lazima uwepo ushahidi wa maisha ya pamoja kati ya mwanamume na mwanamke.

Lazima kuwe na udhibitisho kuwa umma au jamii inayowazunguka wanawachukulia na kuwapa heshima kama mke na mume. Hapa swali la kijamii lazima lijibiwe ni kwa namna gani maisha yao yanaonekana mbele ya watu.

Lazima ithibitishwe kuwa watu hao walikuwa na uwezo wa kuwa mke na mume wakati walipoanza kuishi pamoja na kama walikuwa na umri unaokubalika kisheria. Umri wa kuweza kuingia kwenye ndoa ni miaka 18 hivyo walio chini ya hapo dhana hii haiwezi kusimama.

Ni lazima pia ithibitishwe kuwa kati yao au wote wawili hakuna aliye na ndoa iliyokuwa inaendelea. Hii ni muhimu dhana hii haitasimama pale mwanaume ana mke mwengine eneo lingine na akaende kuishi na mwanamke mwengine katika eneo lingine hata kama ni zaidi ya miaka 2.

Sasa Endapo dhana hii itadhibitishwa mahakamani kulingana na vigezo vilivyoainishwa hapo juu basi haki na wajibu wa mwanamke na mwanamume utahesabika kama walio katika ndoa halali;

Haki ya mwanamke kudai matunzo kwa ajili yake na watoto waliozaliwa katika kipindi chote

Haki ya mwanamke au mwanaume kuomba mahakama kuvunja ndoa hiyo au kutoa amri ya kutengana

Haki ya kupewa kukaa na watoto

Haki juu ya mali na machumo yaliyopatikana katika kipindi chote walichokaa pamoja.

Sheria ya Ndoa ya 1971 imeainisha dhana hii ya uwepo wa ndoa ili kutoa ulinzi kwa mwanamke na watoto watakaozaliwa katika mazingira hayo.

Hata hivyo dhana hii haiondoi umuhimu wa wahusika kuchukua hatua na kufunga ndoa halali kwa mujibu wa sheria kwa taratibu za kidini au kimila au kiserikali kama watakavyoona inafaa.

Upungufu wa kufunga ndoa unaweza kusababisha matatizo makubwa endapo mmoja wapo atafariki na kupelekea watoto na mwenzi kutishiwa kupoteza haki zake za urithi kwa kigezo cha kukosa ndoa.... I stand to be corrected guys
Umeandika essay ndeefu lakini inaonyesha bado dhana ya ndoa (presumption of marriage) haijakukaa sawa

PRESUMPTION OF MARRIAGE IS MARRIAGE DEFACTO BUT NOT DEJURE

Ndio maana Judge Mwalusanya katika kesi ya ZACHARIA LUGENDO vs SHADRACK LUMILANGOMA alipinga vikali watu wanaodhani hiyo ni ndoa na wengine wanakosea zaidi kuiita ndoa ya kimila. Yeye aliharamisha uhusiano wa namna hiyo na kuuita UHAWARA (CONCUBINAGE) hata kama wameishi pamoja zaidi ya miaka 30 na kupata hiyo reputation ya jamii bado haitoshi kuitwa ndoa itatumika tuu kama kakigezo cha kugawana mali walizochuma pamoja kama joint venture nyingine na kuangalia welfare ya mtoto if any but sio ndoa maana ndoa ina taratibu zake iwe ya kimila lazima mahari yalipwe pombe ipikwe ngoma ichezwe na mashuhuda wawepo

Kwenye kanisa linalotumia Canon law sina uhakika kama martin luther wakati amekimbia RC alikumbuka kuondoka nayo lakini kwa kanisa Moja Takatifu Katoliki la Mitume hakuna kizuizi chochote cha ndoa hapo kama mlikuwa hamjafunga ndoa hata kama mliishi pamoja miaka 40 ,unaweza ukachagua kabinti ilafuata taratibu za ndoa ya kanisa na ukafunga naye ndoa bila tatizo. Yule wa zamani atatambulika kama hawara jambo ambalo kikanisa halitambuliki na ni dhambi
 
Umeandika essay ndeefu lakini inaonyesha bado dhana ya ndoa (presumption of marriage) haijakukaa sawa

PRESUMPTION OF MARRIAGE IS MARRIAGE DEFACTO BUT NOT DEJURE

Ndio maana Judge Mwalusanya katika kesi ya ZACHARIA LUGENDO vs SHADRACK LUMILANGOMA alipinga vikali watu wanaodhani hiyo ni ndoa na wengine wanakosea zaidi kuiita ndoa ya kimila. Yeye aliharamisha uhusiano wa namna hiyo na kuuita UHAWARA (CONCUBINAGE) hata kama wameishi pamoja zaidi ya miaka 30 na kupata hiyo reputation ya jamii bado haitoshi kuitwa ndoa itatumika tuu kama kakigezo cha kugawana mali walizochuma pamoja kama joint venture nyingine na kuangalia welfare ya mtoto if any but sio ndoa maana ndoa ina taratibu zake iwe ya kimila lazima mahari yalipwe pombe ipikwe ngoma ichezwe na mashuhuda wawepo

Kwenye kanisa linalotumia Canon law sina uhakika kama martin luther wakati amekimbia RC alikumbuka kuondoka nayo lakini kwa kanisa Moja Takatifu Katoliki la Mitume hakuna kizuizi chochote cha ndoa hapo kama mlikuwa hamjafunga ndoa hata kama mliishi pamoja miaka 40 ,unaweza ukachagua kabinti ilafuata taratibu za ndoa ya kanisa na ukafunga naye ndoa bila tatizo. Yule wa zamani atatambulika kama hawara jambo ambalo kikanisa halitambuliki na ni dhambi
Hivi lile la Tangazo la Siku 21 kukaribisha endapokuna pingamizi no kwa mujibu wa Sheria ya Serikali au Kanisa!???
Hata hivyo maadam wahusika ni Wabunge wa CCM Acha wapambane na hali yao!
 
Huyo dogo mzava kwanza hawezi tena kurudi Bungeni hao ndio wabunge walioingia kwa mbeleko za Mwendazake ali pokea kijiti bila hata uchaguzi baada ya Reprofessor Maji marefu kufariki!! Hana influence wala Hela yoyote ya kumfanya aendelee kuhold hio position 2025 Sio mbali naona Ana stretch his muscles kwa Kutataka awe circled Na watu wenye exposure Na icho cheo, Kijana atafute kazi ya kufanya
 
Umeandika essay ndeefu lakini inaonyesha bado dhana ya ndoa (presumption of marriage) haijakukaa sawa

PRESUMPTION OF MARRIAGE IS MARRIAGE DEFACTO BUT NOT DEJURE

Ndio maana Judge Mwalusanya katika kesi ya ZACHARIA LUGENDO vs SHADRACK LUMILANGOMA alipinga vikali watu wanaodhani hiyo ni ndoa na wengine wanakosea zaidi kuiita ndoa ya kimila. Yeye aliharamisha uhusiano wa namna hiyo na kuuita UHAWARA (CONCUBINAGE) hata kama wameishi pamoja zaidi ya miaka 30 na kupata hiyo reputation ya jamii bado haitoshi kuitwa ndoa itatumika tuu kama kakigezo cha kugawana mali walizochuma pamoja kama joint venture nyingine na kuangalia welfare ya mtoto if any but sio ndoa maana ndoa ina taratibu zake iwe ya kimila lazima mahari yalipwe pombe ipikwe ngoma ichezwe na mashuhuda wawepo

Kwenye kanisa linalotumia Canon law sina uhakika kama martin luther wakati amekimbia RC alikumbuka kuondoka nayo lakini kwa kanisa Moja Takatifu Katoliki la Mitume hakuna kizuizi chochote cha ndoa hapo kama mlikuwa hamjafunga ndoa hata kama mliishi pamoja miaka 40 ,unaweza ukachagua kabinti ilafuata taratibu za ndoa ya kanisa na ukafunga naye ndoa bila tatizo. Yule wa zamani atatambulika kama hawara jambo ambalo kikanisa halitambuliki na ni dhambi

Huu ndio ukweriii hata uishi 100 years kama hujafunga ndoa takatifu, hakuna ndoa hapo.
Mbele ya kanisa Mzava ana haki ya kuanza upyaaa.
Na Pia busara ya kanisa hapo inakuja kuwasuluhisha tu hawa ila hawawezi tena kuwa wanandoa yenye utulivu. Tunaokoa roho sio mapenzi ya mtu mmoja.
 
Umeandika essay ndeefu lakini inaonyesha bado dhana ya ndoa (presumption of marriage) haijakukaa sawa

PRESUMPTION OF MARRIAGE IS MARRIAGE DEFACTO BUT NOT DEJURE

Ndio maana Judge Mwalusanya katika kesi ya ZACHARIA LUGENDO vs SHADRACK LUMILANGOMA alipinga vikali watu wanaodhani hiyo ni ndoa na wengine wanakosea zaidi kuiita ndoa ya kimila. Yeye aliharamisha uhusiano wa namna hiyo na kuuita UHAWARA (CONCUBINAGE) hata kama wameishi pamoja zaidi ya miaka 30 na kupata hiyo reputation ya jamii bado haitoshi kuitwa ndoa itatumika tuu kama kakigezo cha kugawana mali walizochuma pamoja kama joint venture nyingine na kuangalia welfare ya mtoto if any but sio ndoa maana ndoa ina taratibu zake iwe ya kimila lazima mahari yalipwe pombe ipikwe ngoma ichezwe na mashuhuda wawepo

Kwenye kanisa linalotumia Canon law sina uhakika kama martin luther wakati amekimbia RC alikumbuka kuondoka nayo lakini kwa kanisa Moja Takatifu Katoliki la Mitume hakuna kizuizi chochote cha ndoa hapo kama mlikuwa hamjafunga ndoa hata kama mliishi pamoja miaka 40 ,unaweza ukachagua kabinti ilafuata taratibu za ndoa ya kanisa na ukafunga naye ndoa bila tatizo. Yule wa zamani atatambulika kama hawara jambo ambalo kikanisa halitambuliki na ni dhambi
Wwe mwenyewe umefanya maamuzi ya kutoitambua hiyo Ndoa ya kuishi pamoja muda mrefu kwa kuegemea upande wa Kanisa,na tunajua kabisa kidini Kama hamkwenda kanisani au kwa Sheikh hapo hakuna Ndoa hata Kama mliishi miaka mia na Watoto mia,lakini kiserekali itawataambua pamoja na Watoto wenu,wakati ki Dini hadi Watoto wenyewe hawatambuliki,hadi huitwa Watoto wa zinaa!!
 
Hivi lile la Tangazo la Siku 21 kukaribisha endapokuna pingamizi no kwa mujibu wa Sheria ya Serikali au Kanisa!???
Hata hivyo maadam wahusika ni Wabunge wa CCM Acha wapambane na hali yao!
Swali zuri sana hili,nami nasubiri jibu!! Asante!!
 
Kanisa limepoteza muelekeo wake. K.k.k.t mwenye pesa anahabudiwa Bwana. Kama huna pesa haki yako kanisani sahau, tunayo mifano mingi Sana Hadi inssikitisha, na ndiyo maana kina Kakobe and the like imekuwa Ni rahisi kwao kukomba wahumini kutoka kwenye madhehebu haya makubwa. Inssikitisha kwa kweli. Huna fedha huna thsmani fullstop.
 
Back
Top Bottom