Hii ni kawaida yenu mwisho wa siku mnalegea
Mlizuia gari za Tanzania.kuchukua watalii Jomo Kenyatta,tukapunguza safari za KQ toka 49,mpaka 7 kwa wiki Uhuru alikuja mwenyewe kwa miguu kuomba suluhu
Mpaka umefungwa siku moja tu balozi kaita waandishi,safari hii mtakiona cha moto maana simu haIpokelewi,ile kabudi alipokea kwa sababu kazungu alitumia simu ya mkeqw,lakini jibu alilopewa kuwa waziri yupo bize mpaka wiki ijayooo
Machungwa,nyanya,vitunguu vimeshapotea kwa sasa,bado.mahindi
Mpaka wa Silali na wenyewe tumeshapiga pini, imebakia Namanga tu.
Tutaelewana tu ngoja tuoneshane makali (Dr Shika, 2017)View attachment 1454606
Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna anaekataa kupimwa,tatizo ni kwamba kila mtanzania mnasema.ana.corona,lakini mkenya akitoka Tanzania hana!tumestukia lengo lenu ni kutuchafua ili watalii waogope,sasa tushindane tuone nani atanyanyua mikonoLazima mpimwe, hakuna kuingia kwetu hapa ukinuka corona, balozi kuja kuwatekenya hilo halibadilishi kitu.
Lazima mpimwe.... majirani zenu wote wamelazimisha mpimwe...
Ulifikiri sisi hatuwapimi? Sema sisi tunajielewa hatukuona umuhimu wa kuweka wazi taarifa zenu za ugonjwa. Haya sasa Namanga haifungwi lakini ni mwendo wa kupimana tu mpaka kieleweke.Lazima mpimwe.... majirani zenu wote wamelazimisha mpimwe...
Mkuu wa Mkoa wa Arusha kawaumbua akarudia kupima Madereva 19 ambao Kenya iliona wana Corona na Majibu yameonyesha kuwa hawana CoronaKama mnashuku kits za majirani zenu mbona msiwe na wataalam wenu hapo mpakani wa kuthibitisha, mnaogopa nini. Au mje na kits zenu.
Mnapong'ang'ania kuingia kwenye nchi za watu lazima mkubali kufuata masharti yao, ukija unanuka corona lazima ugeuzwe papo hapo, hata ukipiga ukunga hautasklizwa.
Rais wenu amejibiwa na MaRC tu wala si Rais wetu! Sasa mnahaha ile mbaya!! Ni dharau iliyoje!! Balozi wenu ameambiwa na Prof. Kabudi hana nafasi ya kumwona mpaka after 2 weeks yuko busy!! Hahaha!Kuna video inasambaa kwenye mitandao inayomuonyesha RC wa Tanzania akimtukana rais wa Kenya na Wakenya, binafsi sijahangaika kuitazama maana nawafahamu Watanzania ndivyo walivyo, kwao hakuna tofauti ya malofa wa vijiweni na viongozi wa ngazi ya juu, kila mmoja huropokwa bila kuzingatia diplomasia au utaalam.
Muhimu sana asitokee kiongozi wa Kenya hata kwenye level ya mbunge kujishusha hadhi na kumjibu huyo mkuu wa mkoa, au kama vipi yule mbunge anaitwa Jaguar ndiye ajibu, maana yeye akiongea hujadiliwa na Tanzania yote hadi bungeni hadi na waziri mkuu.
Watanzania lazima waelewe kwetu hapa afya ya Wakenya lazima ilindwe kwa nguvu zote, wao kama viongozi wameamua kuwarubuni wananchi kisa umaskini wa nchi, na kuachia watu wajifie kwa corona eti hawataki kuchukua tahadhari maana nchi itaadhirika kiuchumi, sisi hapa lazima kila mtu anayeingia ndani ya nchi apimwe, apimwe apimwe na apimwe....haijalishi watatulilia kwa kiasi gani, lazima wapimwe.
Hizo hasira zao ni cha mtoto sana na haziwezi kusababisha tubadilishe sera, huku tunapima hata wanaosafiri baina ya majimbo au gatuzi iwe kajamba kutoka nje ya nchi ndiye aruhusiwe kutuletea corona. Mambo ya hasira na mizuka ndio zetu tunafahamika Afrika, hivyo hamna jipya hapo, kumtukana rais wetu au Wakenya ni kitu kidogo sana.
Hayo mahindi mnakuja kutuuzia huku na malori tunanunua kwa hela yetu, hivyo haiwezekani tutumie hela zetu kununua corona pia, jeuri ya pesa inatuwezesha kununua mahindi popote tunataka, wewe unatuletea mahindi hakikisha unatii sheria na masharti yetu. Fika mpakani ufanye aidha mojawapo wa haya
- Upimwe corona na kuruhusiwa kupita au
- Upokeze lori lako kwa dereva wa huku ikiwemo hata kuwapa Watanzania walio huku, na lipulizwe kabisa na mtupiane funguo
Madereva wetu wasiruhusiwe kuingia Tanzania maana wakienda kule lazima wageuze na corona.
Inashangaza sana wataalam wa Tanzania wote chali, hakuna anayesema wala kushauri nchi, wameachia wanasiasa waseme vitu vya ajabu ajabu ambavyo haviendani na elimu yoyote ya sayansi.
Hii imesababisha Tanzania itengwe na majirani wote kuanzia SADC hadi EAC.
Mkulu wa Tanzania nilimsikia akisema dereva aliyejiendeshea lori kilomita 1,000km hana haja ya kupimwa, hiyo kuendesha gari kwa umbali ni ishara tosha kwamba ni mzima.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha kawaumbua akarudia kupima Madereva 19 ambao Kenya iliona wana Corona na Majibu yameonyesha kuwa hawana Corona
Mbinu zenu chafu zimekwama
Rais wenu amejibiwa na MaRC tu wala si Rais wetu! Sasa mnahaha ile mbaya!! Ni dharau iliyoje!! Balozi wenu ameambiwa na Prof. Kabudi hana nafasi ya kumwona mpaka after 2 weeks yuko busy!! Hahaha!
Mtanyooka tu na mbinu zenu za kijinga sasa tunaendelea kuwaliamingo wakenya wote wanaofanyakazi hapa TZ ukifika wakati muafaka tuwarudishe kwenu!Nimeona comments za watu nikachoka hata sikutaka kuitazama maana nawafahamu mlivyoo, kwenu kiongozi yeyote hurupokwa tu.....
Halafu hao Wakenya 19 mliwagundua vipi kuwa na corona ilhali mliacha kupima corona baada ya tikitaka la mapaipai.
Anyway kama kweli mliwagundua na corona, mlichokifanya ni jambo la busara na hatuwezi kulialia kama mnavyofanya tukiwapima, kila anayekuja huko aidha mumpime au mzuie asiingie, hayo ndio maamuzi ya busara.
Vipi mmeacha kupika mawe?Rais wetu wala hana mudda na hizo show zenu, akiwa na nia ya kuongea na mataifa majirani kuhusu Corona huwa anafanya video call, wale ambao kingereza kinawatatiza wanaishia mitini.
Balozi aliwakuna ili muache kulialia kwanini mnapimwa, na mpaka hapo hatubadilishi kitu, mtapimwa kwa kwenda mbele.
Huko kwenu mktaka mpime msipime mtajua wenyewe, nchi ni yenu na sheria ni zenu.