Atajitahidi lakini watega mitego na wacheza Amapiano 2025 wamedhamiria

Atajitahidi lakini watega mitego na wacheza Amapiano 2025 wamedhamiria

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema wakuu!

Kila nikijitahidi kumtetea naona inakataa. Kila nikijaribu kuona Kama itawezekana naona haiwezekani.

Anaweza fanya mazuri kuliko waliopita lakini jicho langu kutoka nyota ya Tibeli halimuoni kama atakubalika na wacheza Amapiano.

Sapoti ni Kama itaanza kuyeyuka Sirius kuanzia 2023, mivurugano mikali na mafarakano yapo waziwazi.
Lango litakuwa wazi lakini litakuwa na mitego mingi mibaya. Ataingia lakini atajikuta yupo nje. Atasema lakini ataona anajifokea mwenyewe. Atajipamba lakini atajiona dhalili. Sijui kwakweli!

Kama atakuwa mjanja ataaga na kuacha lango Kwa wategaji lakini wapiga Amapiano nao watavurugana na watega mitego. Hapa kazi ipo.

Sisi tutaangalia tuu.
Labda akinambia nimshauri; anaweza zichanga karata zake na Makuhani wavaa majoho huko madhabahuni ingawaje jicho langu linawaona makuhani mwakani 2022 wakitema dhabihu na kuchoma uvumba, akiwawahi mapema hawezitema nyongo, na hiyo inaweza kuwa Dalili nzuri.

Akiwashika Mkono maliwali, makadhi, maakida na jemadari huenda ikawa Kheri kwake lakini asichelewe Sana.

Hofu yangu ipo Kwa watega mitego, na wacheza Amapiano ambao wanataka kutrend Kwa kila Ngoma wanaoiachia hawa wanataka mpaka 2025 wawe wamekubalika.

Niishie hapa tuu

Kumbuka 2022 ni mwaka wa Makuhani kutema nyongo na kufukiza uvumba. Bahati sio mbali ni wiki moja ijayo.


Wasalamu!
 
2025 tunampa tena, na akitaka kuwakomesha atupe Katiba mpya, tena Ile ya Warioba.

Akae akijua ni Mungu ndiye kamuweka pale Ili atupatie nuru na machweo mapya (Katiba mpya).....katika waliobaki sioni wa kukalia kile kiti kisha tukasalimika, lazima tuwe na Katiba ya kuwadhibiti.

Samia tunakuomba tuvushe, Mungu amekuchagua utuvushe, tuachie Katiba ya Warioba.
 
Niliwahi kutabiri na thread imo humu kwamba mwaka 2025 Rais atakuwa mwanamke.

Na kweli Mungu kafanya jambo ambalo mwaka 2025 utamkuta Rais ni mwanamke ila kitachotokea baada ya 2025 bado sijapata ufunuo.

Ngoja nijichimbie zaidi kwenye maombi Mungu atanifunulia.
 
2025 tunampa tena, na akitaka kuwakomesha atupe Katiba mpya, tena Ile ya Warioba.
Akae akijua ni Mungu ndiye kamuweka pale Ili atupatie nuru na machweo mapya (Katiba mpya).....katika waliobaki sioni wa kukalia kile kiti kisha tukasalimika, lazima tuwe na Katiba ya kuwadhibiti.
Samia tunakuomba tuvushe, Mungu amekuchagua utuvushe, tuachie Katiba ya Warioba.
Ndio ziro sasa!!!
 
Imani yako ni potofu. Wale tu waliokua wanafanya vikao vya ndani kuhusu katiba salikamatwa wakalala selo
Mwingine kapewa ugaidi.
Katiba kuleta kwa kupenda yeye hilo halipo, yeye yupo pale kwa sababu ya CCM.
Wale hata Mimi walinikera, mtu kaingia madarakani miezi sita hana mnamdai Katiba? Mtu mwenyewe kaachiwa mamiradi mikubwa ambayo pesa za kuiendeleza haijulikani inatokea wapi, ndo yanakuja haya ya asikope, tukamuane.

wakati huo huo miaka iliyopita Katiba ilikuwa inasiginwa kweli kweli walinyamaza, tena walikimbia nchi wakituacha tusio na Kwa kukimbilia tuteseke peke yetu.

Tumpe muda, dereva azoee gari, kisha tumuelekeze tunataka kupita njia gani.
 
Niliwahi kutabiri na thread imo humu kwamba mwaka 2025 Rais atakuwa mwanamke.

Na kweli Mungu kafanya jambo ambalo mwaka 2025 utamkuta Rais ni mwanamke ila kitachotokea baada ya 2025 bado sijapata ufunuo.

Ngoja nijichimbie zaidi kwenye maombi Mungu atanifunulia.
Kitakachotokea mafisi yatafocus 2030, yatamdharau mama, na mama Ili kuwaonyesha yeye ndo Rais na wakati huo Hana cha kupoteza ataanzisha mchakato wa Katiba mpya, tena Ile rasimu ya Warioba...mafisi yote chali.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Wale hata Mimi walinikera, mtu kaingia madarakani miezi sita hana mnamdai Katiba? Mtu mwenyewe kaachiwa mamiradi mikubwa ambayo pesa za kuiendeleza haijulikani inatokea wapi, ndo yanakuja haya ya asikope, tukamuane.....wakati huo huo miaka iliyopita Katiba ilikuwa inasiginwa kweli kweli walinyamaza, tena walikimbia nchi wakituacha tusio na Kwa kukimbilia tuteseke peke yetu.
Tumpe muda, dereva azoee gari, kisha tumuelekeze tunataka kupita njia gani.
Walikukera kudai katiba? Alafu hapohapo unataka katiba?
Kazi ya wapinzani ni kusubiri hisani ya raisi?
 
Kitakachotokea mafisi yatafocus 2030, yatamdharau mama, na mama Ili kuwaonyesha yeye ndo Rais na wakati huo Hana cha kupoteza ataanzisha mchakato wa Katiba mpya, tena Ile rasimu ya Warioba...mafisi yote chali.
Unajipa mmoya mnachadema
 
2025 tunampa tena, na akitaka kuwakomesha atupe Katiba mpya, tena Ile ya Warioba.
Akae akijua ni Mungu ndiye kamuweka pale Ili atupatie nuru na machweo mapya (Katiba mpya).....katika waliobaki sioni wa kukalia kile kiti kisha tukasalimika, lazima tuwe na Katiba ya kuwadhibiti.
Samia tunakuomba tuvushe, Mungu amekuchagua utuvushe, tuachie Katiba ya Warioba.
MBOWE SIO GAID
 
Walikukera kudai katiba? Alafu hapohapo unataka katiba?
Kazi ya wapinzani ni kusubiri hisani ya raisi?
Kwa Katiba hii chakavu tulonayo kupata mpya Kwa njia ya Amani ni hisani ya Rais....niamini Mimi.
 
Kuna watu wanaona umri unakimbia kabla hawajakikalia kile kiti.
 
2025 tunampa tena, na akitaka kuwakomesha atupe Katiba mpya, tena Ile ya Warioba.
Akae akijua ni Mungu ndiye kamuweka pale Ili atupatie nuru na machweo mapya (Katiba mpya).....katika waliobaki sioni wa kukalia kile kiti kisha tukasalimika, lazima tuwe na Katiba ya kuwadhibiti.
Samia tunakuomba tuvushe, Mungu amekuchagua utuvushe, tuachie Katiba ya Warioba.
Hii nchi ilishapata katiba yenye uafadhali tatizo cdm ndio waliikataa kisa hoja ndogo sana eti serikali tatu!! Stupid mpk wenyewe ccm wakawashangaa chadema.

Yaani hoja serikali tatu waliyodai cdm ndio ikaturudisha nyuma sana.
 
Back
Top Bottom