ATCL bado hawajajipanga vizuri

biashara za serikali hata wangeanzisha singeri lazima ikose dosari
 
Naunga mkono hoja bei za ticket kwenda Dubai bila kujali unaanza safari Dar, Mwanza au mkoa wowote ilitakiwa iwe sawa ni kama connection feed ya route ya Dubai sio unamcharge kama anatoka mwanza to Dar then Dar to Dubai, huu ni ujinga sana. Na sio kutoka mikoani tu wangewavuta nchi jirani kama Comoro, Congo sijui zambia unawapa cheap option za connection watu wanatafuta cheap ticket. Hilo na wahudumu kama mama ntilie sina comments. Kwenye Lugha yes naunga mkono.
 
Sijakuelewa, unasema atcl hawana connection nzuri halafu unasema kwa upumbavu hawaioni waitumie, hiyo ambayo hawana lakini unataka waitumie ni ipi?
Ukianzisha safari za UAE huwezi kutegemea abiria wa Dar pekee yake.

Unatakiwa kutengeneza connection ya kupata abiria wa Zanzibar,Mwanza,Kilimanjaro & Arusha.....

ATCL walitakiwa kuanza safari kuanzia Kilimanjaro na Zanzibar then Dar hapo ndege lazima ijae.Huwezi kuamini ndege ya abiria zaidi ya 200 ilikuwa na abiria 30 au 40.Hapo hapo unasikia matangazo fly dubai inaelekea Zanzibar then Dubai !.
 
Masha ameombewa na kiboko ya wachawi, tuvute subira labda fastjest inaweza kurudi.
huyu jamaa kama Mama atamtumia vizuri mfano kumpa ndege zetu halafu kwenye kila mia moja serikali inachukua 65 na Masha anachukua 35....Atcl ingeshine sana,Uyu Masha jinsi alivyokuwa anaiendesha Fastjet ni bonge ni moja la akili,inakuwaje Atcl kwamwaka haina tiketi za ofa misimu yote kwa mwaka
 
Siku moja natoka Mumbai kuja Dar, choo cha Business Class hakikuwa na maji. Wakawa wanazuia watu kuingia chooni. Imagine. Mabinti na Captain walikuwa wanasogoa mpaka nikawakaripia na kumweleza Captain kuwa analofanya kama kiongozi si sahii kupiga story na subordinates wake. Akanielewa akarudi katika kachumba kake. ATCL ni tatizo
 
Dawa ya hili shirika ni serekali kuuza hisa zake na kuingia ubia kama ilivyokuwa Crdb & NMB.
 
Pamoja na kuwa tuna soko kubwa la ndani ambalo hatulitumii, bado kwenye soko la kimataifa ndipo tumelaa kabisa. Ukitumia Flightradar24, utagundua kuwa anga la Afrika linatawaliwa na mashirika matatu tu: KQ, ETH na THY; ambapo hata Rwanda inachukua anga kubwa kuliko Tanzania.

Muda mfupi kabla sijaandika hapa, niliona kuwa Rwandair ilikuwa na ndege 8 angani wakati ATCL ina ndege2 tu angani ATCL 403 kutoka china kwenda Zanzibar na ATC134 kwenda KIA; vile vile na kulikuwa na ATCL 110 iliyokuwa uwanja wa ndege ikijiandaa kwende Ndola. Wakati ATCL110 inaingia anganim ATCL403 itakuwa imeshatua Zanzibar, na kuacha ndege mbili tu angani tena. Wakati huo ndege 8 za Rwandair zilizokuwa angani ni pamoja na RWD711, RWD701, RWD710, RWD103, RWD303, RWD444, RWD9306 (hii nadhani inapeleka mizigo Dubai) na nyingine ya nane ilikuwa inatokea Dubai kwenda Kigali sikuweza kupata call sign yake; ilikuwa inaionyeshwa ??
 
Mbona CCM ilikufa akaizindua jiwe kwa kuiwekea dripu ya ruzuku toka serikalini.
 
Sijakuelewa, unasema atcl hawana connection nzuri halafu unasema kwa upumbavu hawaioni waitumie, hiyo ambayo hawana lakini unataka waitumie ni ipi?
Jamaa kaishia kutaja locals tena! Aliposema Zanzibar nilimwelewa lakini kutaja Mwanza hapana bwana. Yaani unataka wawe wanabeba na abiria wa Mwanza halafu wawapitishe ndiyo waende Dar au wawe na ndege maalum ya kwenda huko? Mbona hao abiria wakishushwa Dar wanapata usafiri fresh tu!
 
Mashirika haya ya serikali ni tatizo.
Siku moja Niko mpanda katavi,nilikuwa na mzigo WA maharage kama gunia 100 za 120kg. Nikataka nisafirishe Kwa Kutumia train πŸš† Hadi mwanza.

Ajabu nilipofika kutaka kujua gharama Yule mhusika alinisikitikia Sana.
"Nakuhurumia,usitumie usafiri WA train, ni gharama Sana ni Bora Kutumia malori. Mzigo wako utafika haraka....."
Rate ilikuwa 1kg/250tsh.
Nikajiuliza maswali mengi Sana Kwamba hawa TRC wanakosa Sana hela ya mizigo Kwa hivi viwango vyao vya gharama.
Next ni SGR.
 
Mabinti na Captain walikuwa wanasogoa mpaka nikawakaripia na kumweleza Captain kuwa analofanya kama kiongozi si sahii kupiga story na subordinates wake. Akanielewa akarudi katika kachumba kake. ATCL ni tatizo

Madhara yake ni nini? Ama una hofu ya kupaa kumuona captain nje ya cockpit. Ingekuwa airline nyingine wala usingefanya chochote kwa captain.
 
Hapa Tanzania tunawapa wajinga kuendesha mambo.
 
Madhara yake ni nini? Ama una hofu ya kupaa kumuona captain nje ya cockpit. Ingekuwa airline nyingine wala usingefanya chochote kwa captain.
Airline nyingine huwezi kuona captain anaweka kijiwe na cabin crews! Sana sana ndege ikiwa angani utamuona anaenda maliwatoni na kurudi kwao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…