ATCL Kwenda India ni ukatili kwa Watanzania

ATCL Kwenda India ni ukatili kwa Watanzania

..serikali ilitakiwa iwachukue hao wagonjwa bila kuwatoza fedha.

..hili ni suala la KIBINADAMU / HUMANITARIAN na UOKOAJI na serikali inatakiwa ibebe mzigo wa gharama.
 
Tembeeni vifua mbereee tumenunua ndegee kwa kashi.

Nauli za Ndege zimekuwa juu kuliko awamu iliyopita. Nakumbuka mwanza to dar nilipanda ndege kwa 90k.

Ndege inatumwa madagascar kuchukua box 13 za dawa ambazo hata sisi tunazo. Yani majani yametuzunguka kila kona. Tulivutiwa na packaging.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kutumia ndege yake ya Boeing 787 Dreamliner inataraji kwenda nchini India kuwachukua watanzania 255 waliokuwa wagonjwa wakipatiwa matibabu nchini humo. Suala hili ukiliangalia juu juu unaweza kusema ni upendo wa Serikali ya Tanzania kwa wananchi wake kwa kuwachukua watanzania hao baada ya kunasa huko kwa sakata la LOCKDOWN la Ugonjwa wa CORONA ulioathiri Dunia Nzima.

Lakini laghasha, Watanzania hawa wanaoenda kuchukuliwa wameingia gharama kubwa saaaaaana za kulipia nauli ya ndege na kuwa mara 2 au 3 zaidi ya ile waliotumia awali kwenda India kutibiwa, kiasi ambacho wengi wao walioko huko wenye kipato kidogo kushindwa kulipia nauli hiyo ya kurudi nyumbani. Kama kweli Serikali inania ya dhati ya kuwasaidia wananchi wake kurudi nyumbani wafanye “COST SHARING” kwa hao wagonjwa ili kuwasaidia kurejea nyumbani. Ikumbukwe kwamba hao wagonjwa walikwenda India kutibiwa huko kwa gharama zao wenyewe na walishaingia gharama kubwa za kutibiwa wakiwa huko sasa sidhani kuwasaidia kurudi nyumbani napo waingie gharama nyingine kubwa zaidi.

Hili kwa maoni yangu naona sio kuwasaidia wananchi bali ATCL kuendelea kuingiza mapato licha ya Janga la CORONA kuendelea kuwepo. Hii inaitwa kufa kufaana kuwepo kwa janga la CORONA imekuwa ni manufaa kwa ATCL kuendelea kuingiza mapato na sio kuwasaidia wananchi wake. wakati huo ikumbukwe kuwa ndege hizi zimenunuliwa kwa Kodi za wananchi ambao ni watanzania wenyewe kati yao ndio hao walionasa huko India.

Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL Mhandisi Ladislaus Matindi alisema “Sisi ni wafanya biashara, ndege yetu gharama yake ni hizi kwahiyo tunahitaji utupe kiasi hiki, hata wakiwa watu wawili wakiwa na uwezo wa kuichukua ndege tunawapa” Kwa kusema hivi inaonesha kuwa ATCL wako kimaslahi zaidi na sio kuwasaidia watanzania.

ATCL na Serikali kwa ujumla kwa hili hata siwasifu eti mnawajali au kuwasaidia watanzania bali nawapongeza kwa kuendele kuwaumiza wananchi hali ya kuwa ndege hizo ni Kodi zao.
View attachment 1447667
Waingereza wao walitozwa Pauni 1,600/= na nyongeza.
 
msemaji wa serikali alisema ndege imekodiwa na mtu mmoja, huyo mtu mmoja yeye atajuana na abiria hao. kwenda kutibiwa nje inamaana unakuwa huelewi utarudi lini nchini kwahiyo unakuwa umejiandaa kikamilifu financially ukiwa huko, imetokea dharula unatakiwa urudi nitashangaa ukishindwa kujilipia nauli hata kama ni mara 3, hiyo kwako ni ndogo mno. Ungekuwa na pesa za wasiwasi ungebakia uhangaike na hospitali za ndani hadi mwisho wa maradhi yako
 
Juzi hapa niliona taarifa moja kwamba Nchi ya Uturuki ilituma ndege yake Sudan kwenda kumchukua raia wake mmoja aliyekuwa anaumwa na corona. Nikafikiri nikasema sisi waafrika tumekosea wapi maana kwa nchi zetu hizi ni ndoto. Hata hilo la kutoa ndege kwenda kuwachukua tushukuru tu.
 
Je sisi ni waingereza? unakijua kipato cha muingereza wa hali ya chini?
Serikali yao imewapa miezi mitano (5) ya kuzilipa baada ya wengi kudai hawana uwezo wa kuzilipa kwa mkupuo. Nadhani nimejibu swali lako.
 
almost 2 millions huku bei ya kawaida mpka India inachezea laki 7 mpaka 9
IMG-20200507-WA0001.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao watu wa India nimewaona kule facebook wakilalamika ,kinachowauma ni kwamba kwanini one way ni dollar 850,ikiwa wakati safari za anga zipo one way ilikuwa 350$

Hapo watakuwa hawatendi haki wakilalamika, maana kabla serikali kuamua kutoa ndege kuwafuata gharama zao za kuishi huko zilikuwa kubwa mno, na wasingefuatwa bado gharama za kuishi huko zingeendelea kuwa kubwa sana kuliko wanacho kilalamikia.

Wangeweza kufikria tu kuwa, hapa ndege inaondoka tupu hadi india hailipiwi. Kwahiyo nafikr hiyo bei ni kama imegharamikia to and fro
 
Mkuu asante kwa taarifa ila hakuna jipya hapo. Hapa hapa ndani no body cares sebuse walokuwepo India? Acha kabisa
 
Hii kitu ina harufu kubwa ya rushwa, kama siasa hazitaingizwa tu, basi takukuru wanatakiwa kufuatilia kwa undani. Kwanza ni kweli kuna ruti ya India au ilikufa kimyakimya na hii ruti imekodiwa tu? Nani kakodi? Kwanini iwe gharama maratatu ya ruti za kawaida?
 
Kutokana na janga hili kuna nchi nyingi zimefanya yafuatayo
Kufuta baadhi ya kodi
Kutoa ruzuku kwa raia wake
Kurudisha raia wake wote waliokwama nje ya nchi
Umeme/maji kitolewa bure
Kigawa sanitaiza, pep na baràkoa bure
Kupandisha mishahara ya afya maradufu
Kusitisha shughuli zote za uazalisha zenye mikusanyiko

Lakini sisi Tz tumeruhusu yooote ila tumetoa ndege ifuate watu wetu waliokwama kwasababu ya lockdown tunaanza kulalamika.......hivi nani katuloga lakini?
Mleta mada hana tofauti ya roho mbaya kama aliyonayo mgogo anayeongoza bunge letu
 
Du wabongo bwana! ndo maana hatuendelei, sasa shirika likipata hasara mtoa mada atakuwa wa kwanza kutoa post ya kufurahia huku alisema kwa mbwembwe "tulimwambia" .
 
Back
Top Bottom