Athari za mishahara duni ya Watumishi wa Umma

Athari za mishahara duni ya Watumishi wa Umma

Mkuu Wewe endelea kufaidi dunia huko uliko. Waachie kilio wenye msiba wao. Usiwakatishe tamaa zaidi.

Hii nchi ilishakuwa ya hatari tangu awali. Nyerere aliposema kwa katiba hii anaweza kuja dikteta mbaya sana, Watanzania walipuuza wakijua “ulaji mezani kwako” waliouzoea utaendelea kama kawa hivyo hakuna haja ya kuhangaika na masiasa.

Tena miaka ile ukiuliza habari za mshahara au pensheni unaonekana kama kibwengo fulani hivi; umefulia kweli kweli. Kazi ya maana ilikuwa ni ile yenye “ulaji” mkubwa. Mishahara karibia yote ilikuwa peanuts. Wafanyakazi hasa serikalini wamshukuru sana JK (awamu ya 4) kwa kuhuisha mishahara na pensheni za sekta ya umma mpaka kufikia kuwa kigezo cha kuvutia ajira hizo. Kiasi cha watumishi wengi kusahau habari za rushwa na fojari za risiti. Watu wakaanza kujadili mishahara na pensheni serikalini!

Leo hii watu wanamdai Magufuli ajira, vyeo, nyongeza za mshahara kwa vile Kikwete aliongeza thamani kubwa katika vipato hivyo vya watumishi wa umma kwa namna ambayo haikufikirika huko nyuma. Waliotumikia awamu za 1 hadi 3 wanajua. JK aliposema “mtanikumbuka” alipokuwa akiaga tukacheka sana nadhani alijua kuhusu “yajayo”. Eti “nawaletea chuma hiki; kinatema cheche!” [emoji23] Bila shaka aliiangalia ile “wage bill” ya sekta ya umma ilivyokuwa na ukubwa wa kutisha akajua chuma kikishakamata hatamu hatua namba moja kitawahi Hazina na kufyekelea mbali maslahi kibao.

Safari ya kurejea awamu za 3 > 1 ndio ilishaanza tena huku sekta za umma na binafsi zikizidi kusinyaa. Haitakaa itokee mishahara iongezwe serikalini Labda selectively kwa “wateule” na “watu maalum”. Kwenye siasa nako ni sauti moja tu ndiyo inayosikika sasa ikihanikizwa na miangwi ya kila aina na shadidi za mapambio ya kusifu na kuabudu. Hakika kama Watanzania wataendelea kukwepa wajibu wao wa kisiasa, basi ni mi-kumi zaidi ya kilio na kusaga meno. Hakuna namna. [emoji22]
Mkuu

Habari ya mishaahara kuwa midogo na watu kutegemea rushwa serikalini inanikumbusha story moja ya enzi za "Fagio la Chuma" la Mzee Ruksa.

Mzee Ruksa, Rais Ali Hassan Mwinyi, mwenyewe alihadithia habari hii katika hotuba kuonesha ukubwa wa tatizo la rushwa.

Alisema kwamba, alikuwa na ndugu yake mmoja anafanya kazi serikalini. Sasa yule ndigu yake, akawa na tuhuma fulani kazini. Akasimamishwa kazi ili ufanyike uchunguzi. Wakati kasimamishwa kazi, analipwa mshahra wote kama kawaida.

Sasa huyo jamaa aliyesimamishwa kazi, akamfuata Mzee Ruksa. Akamwambia Mzee, nakulililia sana. Tafadhali nirudishe kazini, hali ni mbaya nina familia na watoto.

Sasa Mzee Rushwa akamuuliza huyo ndugu yake, wewe umesimamishwa kazi unalipwa mshahara au mshahara hawakulipi?

Ndugu yake akamjibu mshahara analipwa kama kawaida.

Mzee Ruksa akashangaa sana. Akamuuliza tena. Sasa kama mshahara analipwa kama kawaida, tatizo liko wapi?

Ikabidi jamaa afunguke. Akasema kwamba huo mshahara wake ni mdogo sana na siku zote si wa kuutegemea, yeye anachotegemea ni ma deal anayoyafanya akiwa kazini. Na bila kuwa kazini hata akilipwa huo mshahara, hayo ma deal (rushwa) hawezi kufanya.

Basi Mzee Mwinyi akawa kapatq elimu fulani kuhusu ukubwa wa suala la rushwa serikalini.
 
Hiyo mishahara ni shs ngapi

Weka Salary slip hapa za wafanyakazi

Ukubwa wa hela kwako unaanzia shs ngapi?

Unapiga kelele sana hapa JF bila takwimu za mishahara

Wewe hujui kupanga matumizi, Ukiweka salary slip hapa, Ficha details zingine

Wewe umekosa elimu ya Finance na Economics

Tangu lini mahitaji ya mtu yakatimizwa, Ukinunua helcopter utahitaji Dreamliner

Furaha ni wewe binafsi na sio pesa

Kuna watu wanafuraha na hata hawajawahi kuajiriwa na wala hawajajiajiri ni wakulima wa kawaida tu wasiotambulika

Kaa kimya wewe Mwanaume, Mkeo itakuwaje sasa?
If you think money can't buy happiness go and ask the homeless and the jobless...

#YNWA
 
Mkuu lack of vision ya hawa wahuni inairudisha nyuma sana Nchi yetu. Mtu mmoja tu kwa sababu ana Phd fake ya kuunga unga basi kila kinachotoka kinywani mwake hata kama kinakiuka sheria na taratibu mbali mbali za nchi ni sheria ya Nchi na kinapigiwa makofi kama yote.

Kajisemea Jenerali Ulimwengu tumerudi nyuma miaka 50, mimi naona tumerudi nyuma miaka 70 na miaka mitano ijayo kutakuwa na vilio vya kusaga na meno kwani Watanzania wengi wataingia kwenye kundi la ufukara wa kutisha.
Mark my words Mkuu unless there is a huge change in the leadership and the direction of our beautiful country.


Mishahara duni ina athari kubwa sana kwa watumishi wa umma na Taifa kwa ujumla na hizi ni baadhi ya athari hizo kwa watumishi na Taifa letu.

1. Low purchasing power
Mishahara duni inapunguza uwezo wa mtumishi kufanya manunuzi na hivyo wakati mwingine humlazimisha mtumishi kukimu mahitaji yake kwa kukopa kugharamia basic needs na sio kukopa ili afanye biashara au kuongeza mtaji wa biashara yake.

Mtumishi wa nchi hii hata kununua tv ya shilingi 500,000/=, inabidi akakope Benki au katika vicoba, n.k vinginevyo atalaza watoto njaa.

2. Stress
Mishahara duni ni moja ya chanzo kikubwa cha stress kwa watumishi wa umma kwani hela anayopata mwisho wa mwezi haitoshi kumfikisha mwezi unaofuata kwa sehemu kubwa ya mshahara huo mdogo inatumika kulipa madeni na hivyo kumuacha mtumishi akiwa na mawazo(stress) ya namna ya kumaliza mwezi.

3. Uwezo mdogo wa kujiwekea akiba
Mishahara duni inafanya kuwa ni vigumu kwa mtumishi wa umma kuweka akiba katika Maisha yake na matokeo yake akipata dharau solution yake ni kwenda kutafuta mkopo.

4. Uwezo mdogo wa kukopesheka
Moja ya athari ya mishahara duni ni mtumishi kuwa na nafasi ndogo ya kupata mikopo inayokidhi mahitaji yake kwani wakopeshaji hutoa mikopo kulingana na mshahara (take home) ya mtumishi husika.

Matokeo ya hali ni kuwaweka watumishi katika mazingira magumu ya kujilwamua kimaisha iwe ni katika kutafuta mitaji,kugharamia ujenzi, n.k.

5. Mishahara duni ni chanzo watumishi kuwa na mikopo mingi mitaani (multiple loans)
Mtumishi mwenye mshahara mdogo hulazimika kukopa sehemu tofauti tofauti ili kukidhi mahitaji yake kwani taasisi nyingi za mikopo hukwepa kuwa mikopo mikubwa kwa hofu ya kushindwa kurejesha hivyo watumishi hulazimika kukopa katika taasisi zaidi ya moja na hata kwa watu binafsi mitaani.

6. Chanzo cha watumishi kujiingiza katika rushwa, ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma
Pamoja na ukweli kwamba siku zote binadamu hatishiki na mshahara hua hautoshi, lakini ni kweli pia mishahara duni isiyokidhi mahitaji ya msingi ya mtumishi na familiar yake, humsukuma mtumishi kutumia nafasi yake katika Utumishi wa umma kupata fedha za ziada hata kwa njia zisizo halali ili aweze kumudu maisha tofauti na wale wanaotumia madaraka yao kujilimbikiza mali.

7. Chanzo cha mafao madogo ya uzeeni
Wote tunajua kuwa mafao ya kustaafu anayolipwa mtumishi baada ya kustaafu hutegemea na mshahara wake wakati anastaafu.Hivyo, watumishi wenye mishahara midogo hata mafao ya huwa madogo.

8. Maisha magumu ya uzeeni
Mtumishi ambae kwa bahati mbaya mpaka anastaafu ameshindwa kuwekeza, mtumishi huyu ataishia kuishi maisha magumu bada ya kustaafu hasa ikitokea anastaafu huku bado ana watoto wanaomtegemea.

9.Mifuko ya hifadhi ya Jamii kuathirika kiuchumi
Kama mishahara ni duni na haiongezeki, tafsiri take ni kuwa hata makato yanayoingia katika mifumo hii yanakuwa madogo na pia hayaongezeki kwani makato hukatwa kwa asilimia ya basic salary ya mtumishi. Hivyo, mama mshahara hauongezeki, maana yake hata pato la mifumo hii nalo haliongezeki.

10. Uwezo wa Mifumo ya Hifadhi ya Jamii kuchangia maendeleo ya nchi kushuka
Wote ni mashahidi wa jinsi mifumo hii inavyotumia fedha za wanachama kujenga vitega uchumi kama kujenga malengo,n.k pamoja na kuiokpesha serikali.

Hivyo, vipato vya hii mifuko vinapkuwa haviongezeki, maana yake ni mchango wa mifuko hii katika shughuli za kiuchumi za nchi hushuka pia.

11. Mishahara kutoongezewa kunaathiri mzunguko wa fedha
Ukiwalipa vizuri watumishi, maana yake ni kuwa umeongeza uwezo wao wa kufanya manunuzi mitaani na hivyo kuongeza mzunguko wa fedha mitaani.

12.Kunaathiri utoaji wa mikopo katika mabenki na taasisi nyingine za kifedha
Ukiongeza mishahara, maana yake pia umeongeza uwezo wa mtumishi kukopesheka, na hivyo ku-boost biashara ya mabenki katika kukopesha na kwahiyo kuongeza faida ya mabenki na automatically kodi ya serikali kutoka katika mabenki na taasisi zingine za kifedha inaongezeka.

13. PAYE kutoongezeka na serikali kukosa mapato
Kwasababu PAYE hutegemea mshahara mtumishi anaolipwa, mshahara inapokuwa mdogo au kutoongezeka, maana yake ni mchango wa PAYE katika mapato ya nchi unafubaa na matokeo yake kuipunguzia serikali mapato.

14. Kushusha ana kuondoa morali ya kazi miongoni mwa watumishi
Mishahara inapokuwa midogo au kutoongezeka kwa muda mrefu, hali hiyo kushusha morali ya kazi miongoni mwa watumishi na hivyo kupunguza ufanisi wa kazi na madhara ni kwa nchi na wananchi wanaotafuta huduma katika ofisi za umma

15. serikali na chama tawala kuchukiwa
Hii ndio athari ya kisiasa kwa chama tawala na serikali iliyoko madarakani na ni advantage kwa vyama vya upinzani.

Unafika katika hospitali ya umma unakutana na Daktari au Nesi mwenye stress zake(anawaza ada ya mwanae,madeni mtaani n.k) unaishia kupata huduma mbovu inayotishia afya na hata uhai wa mgonjwa kisa kikiwa kipato kidogo kinachowaweka watumishi hawa katika mazingira magumu kimaisha.

16. Nchi kuendelea kushuka nafasi za juu miongoni mwa nchi ambazo raia wake hawana furaha
Kutoka na stress na ugumu wa maisha unaotokana na mishahara duni,watu watakosa furaha ya maisha na hivyo kuchangia nchi yetu kuwa ni miongoni mwa nchi ambazo raia wake hawana furaha kama ilivyo sasa na kama ambavyo itaendelea kuwa unless hatua zinachukuliwa kuboresha standard of living ya watu wetu.

Hizi ni baadhi ya athari ambazo, kwa mtazamo wangu, zinatokana na mishahara duni na pia kutoongeza kabisa mishahara ya watumishi wa umma kwa miaka sita sasa.

CC: Waziri wa Fedha na Waziri wa Utumishi
 
Kuna Wapumbavu ndani ya maccm na hii Serikali haramu ambayo 2024 wanaweza kabisa kuanza kampeni ya nguvu ya kumshawishi huyo anayejiita mwendawazimu aendelee mitano mingine au kuongeza awamu kwa miaka miwili.

Katiba ya Nchi imeshachezewa sana, imeshadharauliwa sana ni kama vile hatuna katiba ni bora liende tu chochote kitakachotoka kinywani kwa nanihii basi ni sheria mpya ya Nchi.

Inasikitisha sana lakini Tanzania na Watanzania tunapitia kipindi kigumu sana ambacho wengi hatukutegemea kukiona.
Hili lisitokee tafadhali 10 inatosha.
 
Mkuu lack of vision ya hawa wahuni inairudisha nyuma sana Nchi yetu. Mtu mmoja tu kwa sababu ana Phd fake ya kuunga unga basi kila kinachotoka kinywani mwake hata kama kinakiuka sheria na taratibu mbali mbali za nchi ni sheria ya Nchi na kinapigiwa makofi kama yote.

Kajisemea Jenerali Ulimwengu tumerudi nyuma miaka 50, mimi naona tumerudi nyuma miaka 70 na miaka mitano ijayo kutakuwa na vilio vya kusaga na meno kwani Watanzania wengi wataingia kwenye kundi la ufukara wa kutisha.
Mark my words Mkuu unless there is a huge change in the leadership and the direction of our beautiful country.
Ukweli mtupu na hata mwaka huu hatatoa nyongeza ya mishahara labda kwa wajeda tu ili wasije kumgeuka. Kwahiyo, tutarajie vilio zaidi kutoka watumishi na hata wasio watumishi kwani uchumi teyari umevurugwa.

Kwakuwa ameshaharibu uchumi, tusitarajie eti ataongeza mishahara ya wafanyakazi maana hela sasa hana, hivyo ataishia kutisha watu au kuendelea kuwapa watumishi matumaini hewa ya kuboresha masilahi yao kama ambayo amekuwa alifanya tangu aingie madarakani.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Umejitahidi Sana lakini sijui Kama hao watumishi wa umma wamekuelewa. Ili wskuelewe inabidi wastaafu halafu wakutane na adha za dunia hii........ Ila kwa mbaaaalsomo linaanza kuwaingia kwa namna Bei ya vitu vinavyopanda bila kushuka
 
Back
Top Bottom