Atheists wana mtindio wa ubongo

Atheists wana mtindio wa ubongo

Naona umeishiwa hoja.
Hiyo ni hoja ya msingi sana na nadhani umeelewa lengo lake na ndio maana unatafuta uvungu wa kujifichia.

Huwezi kusema mtu ameona nyumba bila kuonesha uwezekano wa huyo mtu kuwa na ufahamu au ujuzi wa nyumba

Mtu akiwa na ufahamu wa nyumba maana yake, akiwa msituni akaona nyumba atawaza tu kuwa hii nyumba imejengwa (according to personal experience)

Kwa hiyo ili useme kitu flani ndio chanzo lazima uwe na backup uliyo i-exeperience inayokusapoti

Sasa ukisema ulimwengu upo na hauwezi kuwa umejiumba, je hiyo source ushawahi kui experience wapi ikifanya hivyo kwenye ulimwengu mwingine tofauti na huo?
 
Ni kweli hao jamaa wanazingua ila ukitaka kubishana nao kwa kutumia hoja hii uliyoileta wanakushinda ndani ya sekunde 1 tu
Mimi naamini uwepo wa Mungu. Ila asilimia 95% ya mijadala ya wanaoamini na wasioamini niliyopata kuishuhudia, basi wanaoamini huwa hawana hoja!

Atheists huwa wanajenga hoja za uhakika kuliko hawa waumini wenzangu!
 
uwepo wa Mungu unatambulika katika fahamu za mwanadamu kwa njia ya IMANI...na si logic. Ukitumia logic utafika mahala fulani utakwama.

Upo ushahidi wa kimazingira unaoipa nguvu hiyo IMANI ya juu ya uwepo wa Mungu. Hasa unapoangalia dunia na viumbe vilivyomo. Ukikaa chini ukatafakari kwa kina lazima utatambua uwepo wa huyo MUNGU.

Uwepo wake upo naturally katika fahamu zetu....hawa wanaokana uwepo wake wanadhani ni smart kwa kuleta maswali yenye mitego ya kilojikia...ila hata wao wenyewe hawana majibu ya chanzo chao na cha ulimwengu.
 
Salaamu wakuu.

Niende Moja kwa moja kwenye mada.

Utakuta mtu anasifia gari ; "Hii gari kiboko kweli mainjinia wake walikuna vichwa balaa katika usanifu na gari hii haina mpinzani kwani katika kila nyanja ipo okay", ilmuradi tu gari litasifiwa hata kama linazo kasoro na mapungufu fulani.

Hao hao ma atheists utawasikia tena wakisifia; "Hii computer achana nayo, inakasi kubwa balaa utadhani haikundwa na.binadamu bali imedondoka kutoka mbinguni".

Ma atheists hawaishi hapo tu, hebu wakaribishe kwenye pilau utawasikia; "Aise huu msosi kiboko, mtamu kweli, sijui kapika nani !!? Mpishi katoka wapi??!, pasi shaka umepikwa na mtu kutoka pwani kwani watu wa bara hawawezi mapishi ya aina hii !! ".

Huyo atheist anatoa madai kana kwamba huyo mpishi anamjua na kamuona!!, sasa kwa utani tu jaribu kumwaambia kwamba msosi huo umejipika wenyewe!!, utashambuliwa kwa kejeli na matusi na kupewa majina mabaya ya kukutoa akili, utawasikia wakisema; wewe unamatatizo kichwani mwako inawezekanaje chakula kijipike chenyewe??!!.

Sasa njoo kwenye uumbaji wa dunia na uwaulize; je hawaoni uzuri wa dunia na vilivyopo juu yake, navyo havijaumbwa??, hakuna nafsi iliyoumba dunia.na ulimwengu??, endelea kuwahoji; kama wapo Ma engineers waliounda lile gari, ile computer na yupo mpishi aliyepika lile pilau safi vipi akosekane Yule aliyeumba dunia safi na vilivyomo??--- hapo akili zao zinashikwa na wazimu kwani wanajua ni lazima Mungu atajwe katika uumbaji wa dunia na vilivyomo na wao kusikia jina Mungu kwao ni ugonjwa wa mzio (allergy), sasa watakuuliza; Huyo Mungu yuko wapi??!, ukiwajibu; Mungu huwa haonekani, waona wamepata silaha, watahoji; tutaaminije kitu kisichoonekana ndio kimeumba hii dunia??-- wanasahau kwamba hata ile pilau waliokula hawakumuona mpishi wake lakini wanaamini ilipikwa na mtu-mpishi lakini wakiambiwa Kuna muumba Mungu wa dunia na ulimwengu hawataki kusikia.

Ewe Mungu wasamehe hawa viumbe wako na uwaongoze katika njia zako na uwaondoshee kibri na majivuno.
Mkuu, vipi kuhusu huyu MUNGU aliyeumba Dunia na huu ulimwengu wote? Kwa mantiki hii uliyotumia lazima atakuwa ameumbwa na MUNGU mkubwa zaidi, na hata huyo MUNGU mwingine naye atakuwa ameumbwa na mkubwa zaidi yake( there is no ending).

Kwa maneno rahisi ni hivi, kama haiwezekani ulimwengu kujitokeza wenyewe basi vile vile haiwezekani MUNGU mwenye uwezo wa ajabu WA kuumba ulimwengu kujitokeza mwenyewe bila kuumbwa.
 
Hukuweka hoja zaidi ya kuzua jambo ambalo linakutoa katika lengo. Unapo ulizwa uwepo wa kitu huonyesha nini Kisha ukaleta jambo ambalo liko nje ya madam na halihitajiki wala kudhuru ni upunguani, kwamba mtu wa miguu sita mara kadha. Huu ni muendelezo kama ulio uleta hapa kwamba kuhusu uelewa wa nyumba, Sasa nani asiye jua nyumba ni nini ? Kijana kutetea ujinga ni ngumu sana.

Nakupa tena nafasi nyingine, jalia sijui au sina uelewa wa nyumba. Tuambie nyumba inaweza kujitengeneza au kuwepo pasi na chochote ?
Nilikuambia kuwa sababu ya mimi kunifanya nifikirie kuwa ni sahihi kuwaza nyumba imejengwa imetokana na awareness yangu katika mazingira yaliyonizunguka yanayonifanya nitambue nyumba zipo.

Awareness ndio imejenga personal experience ya kunipa utambuzi wa kujua hii ni nyumba

Awareness ya kujua mechanism ya jinsi nyumba zinatengenezwa ndio iliyonifanya nione ni sahihi kufikiria nyumba haijajijenga.

Those are facts based on personal experience

Sasa ukitoka katika mfano huo ukasema utumie hoja ya universe katika kujua chanzo ishu inakuwa ni irrelevant

Kuna maswali ya kujiuliza kabla ya kuendelea

Je huo ulimwengu ni wapi uliwahi kushuhudia ukiumbwa ili iwe sahihi kufikiria kuwa ulimwengu huu uliumbwa?

Una awareness yeyote based on personal experience ikionesha ulimwengu ukiumbwa?
 
Hatujibu kirahsii hivi. Onyesha huo utoto ulipo fanya kama navyofanya Mimi. Mimi nakosoa hoja yako wewe hatahija yangu huigusi unaruka ruka.
Kisema huo ni utoto ndio kuonesha kuwa ni utoto?
 
Ina maana hujui Sayansi na jambo Moja na ngano ni jambo lingine ? Nilipokwambia usome Second law of Thermodynamics Kuna kitu kinaonyesha ukomo wa jambo na chanzo kadhalika Entropy. Sasa Hawa wameafikiana uhalisia. Sasa kuna zile ngano kama vile Sun is Stationery au Earth rotates, hizi ni ngano. Vitu ambavyo hata Sayansi yenyewe inashindwa kuvithibitisha kisayansi na vipo katika Sayansi hizi huitwa ngano. Haya mambo ya Special Relatiy au Black hole ni ngano.
Hao walioafikiana ni kina nani?

Mambo yao wanayafanya wakiwa chini ya mwamvuli gani usiohusika na sayansi ambayo wewe unaiita ngano?

Ni ngano kutokana na disprove ipi ambayo umewa challenge?
 
Hiyo ni hoja ya msingi sana na nadhani umeelewa lengo lake na ndio maana unatafuta uvungu wa kujifichia.

Huwezi kusema mtu ameona nyumba bila huyo mtu kuwa na ufahamu au ujuzi wa nyumba

Mtu akiwa na ufahamu wa nyumba maana yake, akiwa msituni akaona nyumba atawaza tu kuwa hii nyumba imejengwa (according to personal experience)

Kwa hiyo ili useme kitu flani ndio chanzo lazima uwe na backup uliyo i-exeperience inayokusapoti

Sasa ukisema ulimwengu upo na hauwezi kuwa umejiumba, je hiyo source ushawahi kui experience wapi ikifanya hivyo kwenye ulimwengu mwingine tofauti na huo?
Kijana haya unayo andika hayana maana, naandika kwa Kiswahili chepesi sana. Nyumba inaweza kujijenga au kutokea pasi na chochote ?

Siyo lazima uwe na uzoefu na kitu ndiyo ujue hakika yake. Uwepo wa kitu husika huonyesha uwepo wa mengine.

Kuna ulimwengu ngapi kijana ? Hili sharti la ku experience kitu ndiyo ujue uhakika wa mambo umelipata wap I? Sababu ni sharti mfu mno na halifanyi kazi katika uhalisia ndiyo maana nikasema hivi huna hoja unaleta utoto.

Siyo lazima uwe na backup, unapo ona uwepo wa nyumba kujua uwepo wake unahitajika kuwa na nini ? Kwahiyo wewe unapo dai Mungu hayupo ushawahi ku experience kutokuwepo kwa Mola katika ulimwengu (kama upo huo ulimwengu ) mwingine ?
 
Hao walioafikiana ni kina nani?

Mambo yao wanayafanya wakiwa chini ya mwamvuli gani usiohusika na sayansi ambayo wewe unaiita ngano?

Ni ngano kutokana na disprove ipi ambayo umewa challenge?
Kijana unafatikia mambo ya Sayansi ? Unaweza kunipa jaribuo lolote la Kisayansi lililo fanyika kuonyesha Dunia inazunguka ? Sasa kama huijui Sayansi achana na jambo hili. Utakimbia hii nada kijana.

Au ni jaribio gani la Kisayansi lililo fanyika kuonyesha Jua lipo katikati na Dunia inazunguka jua ?

Naposema ngano namaanisha mambo yakutungwa yakawekwa katika Sayansi. Ushawahi kuniuliza kwanini Einstein alikuja na ishu ya Special Relativity ? Lengo ni kumuhujumu Albert Michelson aliyethibitisha ya kuwa Dunia haizinguki kwa kutumia Light Beams. Sababu Einstein alikuwa muumini wa wa theory ya Copernicus akaamua kumuhujumu mwenzake.

Siyo Mimi tu wenyewe tu walisha chalenjiana kijana kitambo sana. Fatilia haya mambo. Kisha jibu maswali niliyo kuuliza.
 
Nilikuambia kuwa sababu ya mimi kunifanya nifikirie kuwa ni sahihi kuwaza nyumba imejengwa imetokana na awareness yangu katika mazingira yaliyonizunguka yanayonifanya nitambue nyumba zipo.

Awareness ndio imejenga personal experience ya kunipa utambuzi wa kujua hii ni nyumba
Ndiyo maana nakwambia unaleta utoto, nilipo kuuliza wewe swali ukiona nyumba unaona nini au unajulishwa uwepo wa nini ni kule kutambua uhalisia, Sasa unakataa nini na unakubali nini ? Haya ndiyo madhara ya uoga na kutofikiria jambo liko wazi unalipinga na kulikiri, kwani hapa nilikuwa naongelea mambo ya maabara ?

Kwa maana hiyo kwa kukiri kwako hili, hayo mengine yote uliyo yaandika yafute hayana maana.

Na ujue tunaposema uhalisia tunamaanisha utambuzi ule wa kawaida kutokana na jambo lilivyo katika dhati yake.
 
Mkuu mi kama atheist nashukuru kwa busara yako kwa namna ulivyoamua kutuita

Ila ulichosahau ni kitu kimoja

Watu wanasifia magari, Pc nk kutokana na comparison walizofanya za kuangalia ufanisi wa bidhaa moja dhidi ya bidhaa nyingine.

Hao atheist wanaosifia magari, computer nk, wanafanya hivyo kwa references.

Kwamba watu wanasema hii bidhaa ni bora kwasababu kuna specs hii ambayo kwenye bidhaa hii nyingine haipo

Viwanda vinavyotengeneza hizo bidhaa vinathibitishika kuwa vipo bila kuhitaji kitu kingine cha ziada kama ishara ya kuonesha ndio source ya hizo bidhaa

Huyo mtu hawezi kushindwa kukuthibitishia kampuni la Dell au Hp kuwa lipo.

Ni maswala ya taaluma ambayo kila mtu anaweza akafanya endapo akifundishwa.

Sasa

Unaposema huu ulimwengu umesababishwa na Mungu, references yako inakuwa nini?

Tunaweza tukathibitisha hicho chanzo bila kutumia kitu kingine kinachopimika kuwa ndio uthibitisho wa Mungu asiyepimika?

Lakini pia

Unaposema huu ulimwengu ni bora au umekamilika unakuwa umeupima na kuufananisha na ulimwengu gani mwingine mpaka ukafikia hitimisho kuwa ulimwengu huu ni mzuri?

Aliyesema laptop Hp omen ya gaming ni bora aliangalia toleo la chini yake au alifananiaha na brand nyingine kwenye maswala ya kiuwezo akaona Hp Omen ni laptop bora

Sasa ulimwengu huu mnaosema ni mzuri au ni bora, ni bora ukiufananisha na ulimwengu upi?
What an answer!
Kudos mkuu
 
Awareness ya kujua mechanism ya jinsi nyumba zinatengenezwa ndio iliyonifanya nione ni sahihi kufikiria nyumba haijajijenga.

Those are facts based on personal experience
Maana yake uhalisia na ndiyo unao hukumu huu.

Ndiyo maana nilikwambia huko mwanzo kwa hali hiyo hakuhitajiki mtu kupewa ushahidi ya kuwa baba ni mkubwa kiumri kuliko mtoto, sababu uhalisia wa kimaumbile Usha hukumu na jambo ni lenye kujulikana.
 
Sasa ukitoka katika mfano huo ukasema utumie hoja ya universe katika kujua chanzo ishu inakuwa ni irrelevant

Kuna maswali ya kujiuliza kabla ya kuendelea

Je huo ulimwengu ni wapi uliwahi kushuhudia ukiumbwa ili iwe sahihi kufikiria kuwa ulimwengu huu uliumbwa?

Una awareness yeyote based on personal experience ikionesha ulimwengu ukiumbwa?
Inakuwa Irrelevant kivipi ? Dunia IPO haipo ?

Uhalisia ambao timeutumia katika nyumba ndiyo uhalisia ambao upo katika dunia.

Kwamba uwepo wa kitu huonyesha uwepo wa vingine. Ndiyo maana huwa tunawaomba ushahidi mtuambie kama Dunia haijajiumba basi imejiumba. Je unao ushahidi huo au utuambie imetokana pasi na chochote.
 
Kijana haya unayo andika hayana maana, naandika kwa Kiswahili chepesi sana. Nyumba inaweza kujijenga au kutokea pasi na chochote ?
Hilo unalolizungumza wewe ni jambo la mbele baada ya hatua kadhaa kuzipita huku nyuma.

Hoja yangu imejikita kwenye hatua za mwanzoni kuhusu utambuzi wa kujua hii ni nyumba na inajengwa

Nazungumzia mazingira yaliyokujengea ufahamu wa kujua hii ni nyumba
 
Mimi naamini uwepo wa Mungu. Ila asilimia 95% ya mijadala ya wanaoamini na wasioamini niliyopata kuishuhudia, basi wanaoamini huwa hawana hoja!

Atheists huwa wanajenga hoja za uhakika kuliko hawa waumini wenzangu!
Mimi kwa mtazamo wangu wanaoamini uwepo wa Mungu wana hoja kuliko wale ambao Wanaamini hakuna Mungu
 
Siyo lazima uwe na uzoefu na kitu ndiyo ujue hakika yake. Uwepo wa kitu husika huonyesha uwepo wa mengine.
Kama huna uzoefu hukijui utajuaje kuwa hii ni nyumba?
 
.

Kuna ulimwengu ngapi kijana ? Hili sharti la ku experience kitu ndiyo ujue uhakika wa mambo umelipata wap I? Sababu ni sharti mfu mno na halifanyi kazi katika uhalisia ndiyo maana nikasema hivi huna hoja unaleta utoto.
Hilo ndio swali ambalo unatakiwa ujibu pale unapotaka kutoa tafsiri ya kitu ambacho hakijawahi kufanyika

Mtu anayesema nyumba inajengwa anakuwa na sababu ya kiuzoefu na hicho kitu inayomsapoti hoja yake kuwa nyumba zinajengwa.

Wewe unayesema ulimwengu umeumbwa, wapi uliwahi kushuhudia ulimwengu ukiumbwa ili iwe rahisi kufikiri huu ulimwengu nao uliumbwa?
 
Siyo lazima uwe na backup, unapo ona uwepo wa nyumba kujua uwepo wake unahitajika kuwa na nini ? Kwahiyo wewe unapo dai Mungu hayupo ushawahi ku experience kutokuwepo kwa Mola katika ulimwengu (kama upo huo ulimwengu ) mwingine ?
Kama huna backup inayokusapoti basi utakosa authenticity ya kusema habari za kuumba/kuumbwa
 
Back
Top Bottom