Atheists wana mtindio wa ubongo

Atheists wana mtindio wa ubongo

Ngoja nikujibu swali hili kwanza, Kisha tunaiweka kiporo unijibu maswali yangu. Baada ya hapo tutarudi hapa.

Tamko Sayansi lina maana zaidi ya Moja, kama linavyo fasiriwa na wahudika, japokuwa Mimi siyo muumini sana wa Fasiri (Definitions),

1. Sayansi ni aina yoyote au Fulani ya taaluma au ujuzi. Yaani taaluma yoyote huitwa Sayansi, ndiyo maana tunaambiwa Social Science, Environmental Science na mfano wa hivyo.

2. Science is The systematic study of the structure and behaviour of the physical and natural world through observation, experimentation, and the testing of theories against the evidence obtained.
"the world of science and technology"

Sasa weka hiki kiporo, Kisha tutarudi hapa.
Kifupi ni study of nature.
Hapa inazungumziwa Natural science.
 
Tuambie Sayasi ni nini ? Kingine mwenzako amedai Sayansi imetengeneza kila kitu. Sasa nimeuliza mnipe majibu ya maswali niliyo uliza.

Siyo tuseme tu ilimradi unatakiwa ukiri kwanza Kisha uulize kingine. Sayansi imetengeneza Jua, Uhai, Hewa ?

Unatakiwa uulize kwa kitu unachokijua. Miungu haitengezi, Mungu wa kweli ni mmoja ambaye ameumba hao wengine wanajiita tu au kuitwa. Sasa ulitakiwa udurusu tamko Mungu, Kisha uhoji kuhusu Mungu. Wengi hamumjui Mungu ila mnampinga hii ni ishara ya kuonyesha mna matatizo ya ajili.

Kingine, kama unaona Mungu hajaumna unatakiwa utupe jibu sahihi juu ya ulimwengu na mengine imekuwaje yametokea na yakawa hivi yalivyo ?
Sijaona maswali yako ila kila kitu ni Nature.
Sayansi ndio kujifunza asili
 
Kwa hiyo binti wa miaka 20 ambaye ana mama mzazi wa miezi 3, yupo?

Hivyo ndiyo nilivyotaka kumaanisha

Mungu wako ana contradiction kama huyo binti na mama yake
Kwa hiyo unakubali kuwa kuna Mungu mwenye contradictions.
 
Kwa hiyo unakubali kuwa kuna Mungu mwenye contradictions.
Kuna dhana ya Mungu yenye contradiction

Contradiction huonesha namna jambo lisivyokuwa na uwezekano wa kuwepo kihalisia
 
Sawa sawa

Umefanya logical reasoning yenye logical consistency kubaini uongo wa hoja ambayo ina contradiction

Sayansi nayo imetumia njia hiyo hiyo kuonesha Mungu wako hayupo

Mungu huyu tumeambiwa ni omnipotent, omnibenevolent na pia ni omniscient

Omnipotent: ana nguvu ya kuzuia maovu yasiweze kutokea

omnibenevolent: ana upendo wote na mwenye utayari wa kuzuia mabaya

Omniscient: Mwenye ujuzi wote wa kuelewa ni njia gani uovu unaweza ukapenya, na mwenye kujua ni njia gani ambayo inaweza kuzuia huo uovu

Mungu mwenye kujua njia zote ambazo dhambi na maovu yanaweza yakaja kutokea, Mungu mwenye uwezo wa kuzuia hayo yote yasiwepo, mwenye kila sababu ya kufanya hivyo angezuia maovu yasiwepo.

Kama kungekua na Mungu mwenye ujuzi wote, upendo wote na muweza wa yote basi uovu usingekuwepo

Uovu upo. Hiyo inamaanisha hauwezi kuwa na vyote viwili kwa mpigo (contradiction) yani kuwepo na uovu halafu at the same time kuwe na Mungu mjuzi wa yote, mwenye upendo wote na muweza wa yote

Uovu unathibitisha Mungu huyo hayupo

Kusema Mungu mwenye sifa hizo yupo inafanya kusiwe na tofauti na mtu anayesema binti wa miaka 20 ana mama yake mzazi mwenye umri wa miezi 3 wapo
Ni kweli uovu upo mwingi tu. Lakini uovu haufanywi na Mungu, bali na binadamu.

Mungu alitoa mwongozo wa kuishi bila kutenda maovu. Sisi ni kuzingatia mwongozo huo, basi. Mambo meema ya kutenda yapo mengi sana, kwa nini uchague maovu na huku unalalama ati kwa nini Mungu hakuzuii!

Sio kazi ya Mungu kuzuia matendo yako, ila utapimwa kwa matendo yako. Sio kazi ya Mungu kukuchunga kama mbuzi. Yeye anaelewa uwezo uliopewa wa kujua meema na maovu. Mungu haigilii uchaguzi wako. Ukichagua uovu, fanya kwa hasara yako.

Ulitaka Mungu akuchemshie chai ndiyo ujue kuwa anakupenda?
 
Ni kweli uovu upo mwingi tu. Lakini uovu haufanywi na Mungu, bali na binadamu.

Mungu alitoa mwongozo wa kuishi bila kutenda maovu. Sisi ni kuzingatia mwongozo huo, basi. Mambo meema ya kutenda yapo mengi sana, kwa nini uchague maovu na huku unalalama ati kwa nini Mungu hakuzuii!

Sio kazi ya Mungu kuzuia matendo yako, ila utapimwa kwa matendo yako. Sio kazi ya Mungu kukuchunga kama mbuzi. Yeye anaelewa uwezo uliopewa wa kujua meema na maovu. Mungu haigilii uchaguzi wako. Ukichagua uovu, fanya kwa hasara yako.

Ulitaka Mungu akuchemshie chai ndiyo ujue kuwa anakupenda?
Mungu anajua mambo yajayo ila still 'anatupima'. Ili iweje sasa? Si anajua kua sitatenda mema tu anyway kwann anilete duniani?
Magonjwa na maafa mbalimbali ni mungu pia anapanga? Ni kwasababu ya maovu ya binadamu, sindio?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli uovu upo mwingi tu. Lakini uovu haufanywi na Mungu, bali na binadamu.

Mungu alitoa mwongozo wa kuishi bila kutenda maovu. Sisi ni kuzingatia mwongozo huo, basi. Mambo meema ya kutenda yapo mengi sana, kwa nini uchague maovu na huku unalalama ati kwa nini Mungu hakuzuii!

Sio kazi ya Mungu kuzuia matendo yako, ila utapimwa kwa matendo yako. Sio kazi ya Mungu kukuchunga kama mbuzi. Yeye anaelewa uwezo uliopewa wa kujua meema na maovu. Mungu haigilii uchaguzi wako. Ukichagua uovu, fanya kwa hasara yako.

Ulitaka Mungu akuchemshie chai ndiyo ujue kuwa anakupenda?
Alieumba uovu ni nani?
 
Ni kweli uovu upo mwingi tu. Lakini uovu haufanywi na Mungu, bali na binadamu.

Mungu alitoa mwongozo wa kuishi bila kutenda maovu. Sisi ni kuzingatia mwongozo huo, basi. Mambo meema ya kutenda yapo mengi sana, kwa nini uchague maovu na huku unalalama ati kwa nini Mungu hakuzuii!

Sio kazi ya Mungu kuzuia matendo yako, ila utapimwa kwa matendo yako. Sio kazi ya Mungu kukuchunga kama mbuzi. Yeye anaelewa uwezo uliopewa wa kujua meema na maovu. Mungu haigilii uchaguzi wako. Ukichagua uovu, fanya kwa hasara yako.

Ulitaka Mungu akuchemshie chai ndiyo ujue kuwa anakupenda?
Napata mashaka kama umesoma na kuelewa post yangu.

Kwanza ukisema mabaya yanatokana na matendo yetu, itabidi utuambie vipi kuhusu matetemeko ya huko Turkey na Syria yanasababishwa na matendo ya kina nani?
 
Napata mashaka kama umesoma na kuelewa post yangu.

Kwanza ukisema mabaya yanatokana na matendo yetu, itabidi utuambie vipi kuhusu matetemeko ya huko Turkey na Syria yanasababishwa na matendo ya kina nani?
Na tutamtaka ajue kua sayari 'Jupiter' ina vimbunga vikali sana. Kwahio atwambie hio hali mbaya inasababishwa na maovu ya nani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kapanga nani na yamepangwa na nani?
Sifa za Mungu wenu si mwenye huruma, upendo na mpenda haki?

Sasa huoni hiyo inakinzana sifa tajwa?
Unarudia swali Moja mara mbili katika ibara Moja, sijui unaharakia wapi. Amepanga Allah.

Hapo umetaja baadhi ya sifa ila kadhalika ni mkali wa kuadhibu.
 
Kifupi ni study of nature.
Hapa inazungumziwa Natural science.
Kijana usiwe unajadiliana na Mimi kama huna Elimu ya haya mambo. Hakikisha unasoma vizuri ninachokiandika kuepusha kukosea na kuandika visivyo hitajika.

Maana nilizo zitoa zipo kamili na zimeweka wazi mambo.

Sasa bila shaka tumeshakubaliana ya kuwa hizo ni maana za Sayansi. Sasa nataka mniambie Sayansi imetengeneza kila kitu kivipi ? Jua likeyengenezwa vipi na Sayansi ?
 
Sijaona maswali yako ila kila kitu ni Nature.
Sayansi ndio kujifunza asili
Kote kwenye alama ya kuuliza Kuna maswali. Hujaona alama za kuuliza ? Zifatilie Kisha ujibu.
 
Salaamu wakuu.

Niende Moja kwa moja kwenye mada.

Utakuta mtu anasifia gari ; "Hii gari kiboko kweli mainjinia wake walikuna vichwa balaa katika usanifu na gari hii haina mpinzani kwani katika kila nyanja ipo okay", ilmuradi tu gari litasifiwa hata kama linazo kasoro na mapungufu fulani.

Hao hao ma atheists utawasikia tena wakisifia; "Hii computer achana nayo, inakasi kubwa balaa utadhani haikundwa na.binadamu bali imedondoka kutoka mbinguni".

Ma atheists hawaishi hapo tu, hebu wakaribishe kwenye pilau utawasikia; "Aise huu msosi kiboko, mtamu kweli, sijui kapika nani !!? Mpishi katoka wapi??!, pasi shaka umepikwa na mtu kutoka pwani kwani watu wa bara hawawezi mapishi ya aina hii !! ".

Huyo atheist anatoa madai kana kwamba huyo mpishi anamjua na kamuona!!, sasa kwa utani tu jaribu kumwaambia kwamba msosi huo umejipika wenyewe!!, utashambuliwa kwa kejeli na matusi na kupewa majina mabaya ya kukutoa akili, utawasikia wakisema; wewe unamatatizo kichwani mwako inawezekanaje chakula kijipike chenyewe??!!.

Sasa njoo kwenye uumbaji wa dunia na uwaulize; je hawaoni uzuri wa dunia na vilivyopo juu yake, navyo havijaumbwa??, hakuna nafsi iliyoumba dunia.na ulimwengu??, endelea kuwahoji; kama wapo Ma engineers waliounda lile gari, ile computer na yupo mpishi aliyepika lile pilau safi vipi akosekane Yule aliyeumba dunia safi na vilivyomo??--- hapo akili zao zinashikwa na wazimu kwani wanajua ni lazima Mungu atajwe katika uumbaji wa dunia na vilivyomo na wao kusikia jina "Mungu" kwao ni ugonjwa wa mzio (allergy), sasa watakuuliza; Huyo Mungu yuko wapi??!, ukiwajibu; Mungu huwa haonekani, waona wamepata silaha, watahoji; tutaaminije kitu kisichoonekana ndio kimeumba hii dunia??-- wanasahau kwamba hata ile pilau waliokula hawakumuona mpishi wake lakini wanaamini ilipikwa na mtu-mpishi lakini wakiambiwa Kuna muumba, Mungu wa dunia na ulimwengu hawataki kusikia.

Ewe Mungu wasamehe hawa viumbe wako na uwaongoze katika njia zako na uwaondoshee kibri na majivuno.
wewe ndio una mtindio wa ubongo wala sio wao...

nani kakwambia uumbaji alifanyaga an entity called "god"?

Where do you invent that nonsense?
 
Ukamilifu ni kutokua na matetemeko yanayouwa watu, vimbunga, mafuriko etc... cha ajabu hivi vitu haviko duniani pekee...

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo hapo mnasema haya mambo ni nature, maana yake asili inakuwaje na dosari ?

Maana yake haya mambo yanatokana pasi na chochote au yanatokea bahati mbaya ? Kinyume chake huwezi kusema ni dosari vitu ambavyo havitokei kwa bahati mbaya au pasi na chochote.

Kwahiyo Sasa ili uwe sahihi unatakiwa ututhibitishie haya yanatokea pasi na chochote na kwa bahati mbaya.
 
Hapo hapo mnasema haya mambo ni nature, maana yake asili inakuwaje na dosari ?

Maana yake haya mambo yanatokana pasi na chochote au yanatokea bahati mbaya ? Kinyume chake huwezi kusema ni dosari vitu ambavyo havitokei kwa bahati mbaya au pasi na chochote.

Kwahiyo Sasa ili uwe sahihi unatakiwa ututhibitishie haya yanatokea pasi na chochote na kwa bahati mbaya.
Haya yanatokea pasi na chochote ila bahati mbaya, haiitaji hata akili kubwa kufikiria hili... kwani kuna anaepanga mvua inyeshe au isinyeshe? Kuna anaepanga matetemeko au vimbunga? Ivo ni vitu vinatokea venyewe na ni nature...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom