Athlete Crown sio gari la kubishana nalo ukiwa barabarani acha liende

Pia tafuta toyota makes za ulaya uone dashboards zake kama hazilingani na hao kina bmw benz audi na vw
True...Japanese car yoyote ile ambayo ipo designed specifically for Europe or North America dash yake kusoma zaidi ya 180 ni Jambo la kawaida.

Sisi gari nyingi tunanunua mtumba kutoka japan na ndiyo maana zinaishia 180 kulingana na sheria zao..

Lakini chonde chonde ndugu zangu nawasihi bongo bado sijaona barabara ya kumaliza dash...ni kifo..
bado nawapenda vijana wenzangu.
 
Eneo walilopatia ajali naishi jirani...kila nikipita hapo nikiona ule mti waliounga nasisimka....kila nikiona mark x nasisimka...dah...
Nadhani zile gari zina injini kubwa na powerful kuliko uwezo wa body
Body yake ni nyepesi mno. Huwa wanadai body nyepesi ni kwa ajili ya fuel economy na safety.
 
Mkuu kuna Passo ya cc880 na ina kisahani cha 180 kph, na hiyo Brevis yako cc 3000 ina kisahani cha 180 kph. Gari zote hizo zinaweza kufika speed 180, ila tofauti ni kuwa mwenye power (engine) kubwa ndio atawahi kuifikia hiyo speed maana Mkuu issue hapa ni gearbox sio engine pekee. Brevis ya cc2500 ina kisahani cha 180 kwa sababu wametaka iwe hivyo, wangetaka ifike 300kph ingewezekana kwa engine hiyo hiyo. Sidhani kama una uelewa wa mechanics.
 
Mi nilishajaribu kijitoyota flani kufika 140 nilihisi ni kifo tu ndio kinanifuata. Nilishusha speed maana Gari ilikuwa nyepesi kama karatasi. Steering inaenda hata kwa kidole ila huyo myumbo wake sasa wacha kabisa. Boeing 747
 
Yap, huu ndio ukweli ila majitu yanaminyana. Sasa kama gari ya mjerumani yenye 140HP inaweza gonga speed ya 260kph kwanini gari ya Toyota yenye 190HP ishindwe kufika hapo?

Ni mpangilio wa gear na jinsi control unit ilivyosetiwa kuruhusu peak speed kwenye speedometer. Thats all! Naimani hizo gari zote za Toyota jamii ya brevis na crown zinaweza vuka speed ya 180 kama control unit ikifanya ruhusa.
 
Brevis yenye 1JZ ina hp 200
Haiwezi ishinda
Crown yenye 3GR yenye hp 250

Mkipelekana sehemu moja na kuanza Crown atamaliza mapema.

Gari yenye sahani ya 260km/h ila ina cc,hp,piston chache haiwezi maliza mbele ya gari yenye 180km/h yenye cc,hp,piston zaidi
 
Mi nilishajaribu kijitoyota flani kufika 140 nilihisi ni kifo tu ndio kinanifuata. Nilishusha speed maana Gari ilikuwa nyepesi kama karatasi. Steering inaenda hata kwa kidole ila huyo myumbo wake sasa wacha kabisa. Boeing 747
Mkuu haya magari yetu yenye 4 cylinders ni mepesi mno ukifisha speed kuanzia 120 na kuendelea ndio maana naona bora utoke asubuhi na mapema uanze safari ili kuepusha ajali zisizo na lazima
 
Mi nilishajaribu kijitoyota flani kufika 140 nilihisi ni kifo tu ndio kinanifuata. Nilishusha speed maana Gari ilikuwa nyepesi kama karatasi. Steering inaenda hata kwa kidole ila huyo myumbo wake sasa wacha kabisa. Boeing 747
hahahahaa....nilikuwa nq tabia ya kukimbia kimbia...nina nissan note nilikuwa na tabia ya kwenda nayo 140kph hii barabara ya Arusha babati kipindi cha nyuma tochi si nyingi...ila tangu nione wale jamaa wa mark x pale usa river...nimejirekebisha mwendo wangu ni 80-120 safari ya mbali...
ila hii nissan ipo stable sana barabarani..140 sijahi kuiona imekuwa nyepesi
 
Hahahahah utafariki aisee, nissan wanajitahidi sana kwenye aerodynamics!
 
Mi nilishajaribu kijitoyota flani kufika 140 nilihisi ni kifo tu ndio kinanifuata. Nilishusha speed maana Gari ilikuwa nyepesi kama karatasi. Steering inaenda hata kwa kidole ila huyo myumbo wake sasa wacha kabisa. Boeing 747



 
ndo hvyo afu pia zikifika 180 ..ECU inaanza block baadh ya vitu ili kupunguza perfomance ya gari isiendelee mwaga moto
 
kwa kuanza hamna passo ya cc 880 hiyo ka unayo labda ww na si passo itaftie jina ....pili passo ya cc 1000 haifiki 180 hata siku moja ...mimi umenambia sina uelewa wa mechanics basi ww physics hujui ...

ki science zaid hiyo passo ya 1L inaweza fika 180 kama itakuwa nyuma ya gari kubwa lililofika 180 ...WHY then??

sababu air resistance ilioko wakati uko na spidi kubwa ni kubwa sana hivo engine ya passo yenye 64-69hp haiwez i overcome hiyo resistance afu ka passo kanaishia 165kph mkuu


afu kingne hujui why gari nyingi zilizonchini zina dash ya 180 hiyo katafute mwenyewe au pitia huu huu uzi utaona
 

kutembea 180 kwa dk 20 nzima utakuwa umeenda 60km kifupi hamna road hiyo tz yenye 60km bila obstacle
 
Hapo ndio mnapochanganya mambo,kwani kinachofanya gari kwenda speed ni nini?
 
ngoja nkupe mfano wa kawaida ..hivi mtt wa darasa la pili anaweza kukuacha na baskel akakupita kabisa kisa ana baskel yenye gia nyingi let say saba na ww una nne tu ?? ukipata jibu weka hapo ......hako ka korola cha cc hizo labda kama kana body ya kirikuu ila body yake yenye tani moja plus asee haiwezekan ...ingewa hivo gari zote zingekuwa na cc ndogo afu gia box ndo ifanye kazi ya kupaisha gari but kuna pulling powe inapatikana kwa 4GR ama 2GR where hako cha cc 1700 hakana
 

hapo kuflash ECU ....isiweke restriction yoyote gari ikifika spid ilioekwa .... mi napenda gari ya ma mbio impreza wrx 330hp ila sizidishi 90-100 safari ndefu labda kwa ajil ya kumuonesha mtu ubabe pale anapotaka ligi la dk mbili baada ya hapo unamuacha aende
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…