Ati ni kweli kuwa kuna kada hata wafanye Kazi miaka mia hawezi kuwa na nyumba kama ya Mwijaku?

Ati ni kweli kuwa kuna kada hata wafanye Kazi miaka mia hawezi kuwa na nyumba kama ya Mwijaku?

Nyumba ndio kitu rahisi kujenga kama una kipato endelevu. Kuna watu wana nyumba za 300m ukimshtukiza leo lete 5m hana, wengi tu. Kwanini? Kwasababu hakujenga kwa sababu ana 300 au 500m benki,kajenga taratibu leo kapata 1m kesho 5m keshokutwa 3m mpaka anamaliza ujenzi. Haihitaji uwe na 300m benk au zaidi ili ujenge nyumba ya 300m ni kuwa na kipato endelevu na nia thabiti.
Akili kubwa sana mkuu,watoto hawawezi kuelewa ila tuliojenga namna iyo nyumba za ndoto zetu tunajua🙌🙌
 
Habari wakuu!

Baada ya kuwakandia Machawa na kuwatukana vilivyo mpaka humu ndani uzi wangu kufutwa.

Moja ya viongozi wa bodi ya Machawa Tanzania alinipigia simu jana akiwa na furaha nyingi. Nikiwa najua kuna dili la kibiashara linakuja, nashangaa ananiambia unamuona Mwijaku huko.

Nikamwuliza kafanyaje? Akanijibu, alichofanya kuna bàadhi ya kada hata wangefanya kazi miaka mia na wapewe kiunua mgongo bado hawataweza kujenga nyumba kama ya Mwijaku.

Nikamkatia Simu. Akatuma sms wala sikuifungua. Nilijua ni mpuuzi tu. Sasa nauliza, uchawa unalipa eeeh! Lengo la kuhamasisha uchawa ni nini? Ni kwamba hawajiamini na wanatafuta kutambuliwa ndani ya jamii?

Au je Mwijaku kama moja ya viongozi waandamizi wa uchawa kuonyesha nyumba yake ni kujaribu kuwazima midomo kina siye tunaosakama shughuli yao? Au ni majibu kwa wale wanaomuona ni mwanaume wa hovyo na sasa kawajibu kivitendo kuwa yeye ni mwanaume wa aina gani?

Je, kulikuwa na ulazima upi wa Mwijaku kuonyesha mafanikio ya kazi yake?
Je, kuwawatia moyo Machawa wengine wakaze?
Àu je, kuwafungua macho vijana kuwa kazi yoyote ukiifanya kwa moyo na kwa bidii inaweza kukutoa?
Au je, kuwakatisha tamaa adui na hasimu wake?

Je, huu ndio mwanzo wa Machawa na wale wote wanaofanya kazi zinazodharauliwa ingawaje sio haramu nao kuonyesha kuwa wanapata mafanikio makubwa kwa kazi hizohizo zinazodharaulika. Tuliona kwenye kazi ya muziki ikiwa miongoni mwao kazi zilizodharaulika, kwa sasa wanamuziki kwa kiasi chake wanakaheshima kadogo na bado wanahangaika kujenga heshima?

Kazi ya udalali nayo je viongozi wake waandamizi nao watajibu kwa vitendo kama walivyofanya Machawa?

Wakati sisi Wasomi na wenye elimu za juu na pengine kazi kongwe ambazo zinaheshimiwa kwenye jamii tukiwa hatuna maisha mazuri na hata vijumba vyetu vikiwa dhoofu hali, je tuna haja ya kubadili mtazamo kuhusu maisha na kazi?

Hii inawaambia nini vijana waliomaliza chuo na waliokochuoni kuhusu fursa zilizoko kwenye jamii baada ya kumaliza masomo yao?

Je, tutabdilike ikiwa dunia itatuletea mabadiliko ya kazi mpya na zile za zamani kupitwa na wakati?

Kazi kama utengenezaji wa Memes, Stand up comedy, maigizo mafupi mafupi mtandaoni, online business, n.k je ni wakati wa kuzitambua na kuziheshimu ikiwa watumiaji wake wanapata pesa za kuendesha maisha yao na kuishi maisha mazuri ingawaje wale kina siye hatutaki kuona hilo?

Embu Acha nipumzike.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Unauliza jibu? Alafu hiyo nyumba ya mwijaku haiwezi kuwa chini ya mill 600 labda kama unampigia mahesabu kwa kujenga tandahima
 
Ukiwa unalipwa take home ya 1M (ambayo kwa bongo ni wachache wenye nayo) na ukafanya kazi kwa miaka 35, utakuwa umelipwa jumla ya 420M, kwa kuwa mshahara unapanda utakuwa umelipwa kama 500M hiv,

Kwa 500M unajenga nyumba kama ile, changamoto ndugu zangu walimu, manes, polisi, na wengine wenye take home ya 500k
 
Acheni tu tuendelee kusoma mpaka tupate madigrii hata kama hayana hela nyingi kwa kazi zake inatosha. Hawa wanaofanya kazi za ajabuajabu na kupata mafanikio makubwa kuliko sisi wasomi wapate tu. All in all wasomi wawepo tu
 
Wewe si ndio Kuna waraka wako Ulikuwa unakataza watu wasiwe machawa?unaona Sasa unavyolipa uchawa?umeonaaa?

Uchawa ni umavi huo ndio msimamo wangu.
Hasa kwa mwanaume.
Bora Mwanamke akiwa Chawa japo najua wanawake kiasili wao ndio wanataka tuu kusifiwa na sio kusifia.

Hata Chawa ajenge Jengo refu zaidi duniani bado kwangu atakuwa katika nafasi ya hadhi ya chini Daima
 
Ukiwa unalipwa take home ya 1M (ambayo kwa bongo ni wachache wenye nayo) na ukafanya kazi kwa miaka 35, utakuwa umelipwa jumla ya 420M, kwa kuwa mshahara unapanda utakuwa umelipwa kama 500M hiv,

Kwa 500M unajenga nyumba kama ile, changamoto ndugu zangu walimu, manes, polisi, na wengine wenye take home ya 500k

Ukilipwa Milioni moja huwezi kuwa na nyumba ya milioni mia mbili hata ufanyaje, labda uwe na vyanzo vingine vya mapato.

1 month = 1M
1 Year = 12M
10 Years = 120M
30Years = 360M

Hapo hujala, hujavaa, hujaoa, hujasaidia ndugu, hujanunua gari, hujasomesha. Thubutu!
 
Ukilipwa Milioni moja huwezi kuwa na nyumba ya milioni mia mbili hata ufanyaje, labda uwe na vyanzo vingine vya mapato.

1 month = 1M
1 Year = 12M
10 Years = 120M
30Years = 360M

Hapo hujala, hujavaa, hujaoa, hujasaidia ndugu, hujanunua gari, hujasomesha. Thubutu!
Bila vyanzo vingine kutoboa ngumu sanaaaa
 
Uchawa ni umavi huo ndio msimamo wangu.
Hasa kwa mwanaume.
Bora Mwanamke akiwa Chawa japo najua wanawake kiasili wao ndio wanataka tuu kusifiwa na sio kusifia.

Hata Chawa ajenge Jengo refu zaidi duniani bado kwangu atakuwa katika nafasi ya hadhi ya chini Daima
Aaah Kwa hiyo hujaziheshimu Juhudi za Mwijaku?
 
Ufaransa, China....!! Ana haki ya kusema Kuna kada haziwezi kujenga hiyo nyumba.... Mwijaku ni agent na dealer wa mtu mkubwa kwenye Mambo ya unga!. Achana na watu kujifyatua akili wana mengi usiyoyajua.
 
Una dharau sana Robert 🤔🤔

Hapana!
Kuwaweka Watu katika makundi yao sio dharau.kwenye biolojia nilifundishwa Classification na hiyo ndio Application yake Mkuu.

Mbona mimi sijali wengine wakiniweka vile waonavyo (mitazamo yao ilivyo) na sioni kama wamenidharau?
 
Hapana!
Kuwaweka Watu katika makundi yao sio dharau.kwenye biolojia nilifundishwa Classification na hiyo ndio Application yake Mkuu.

Mbona mimi sijali wengine wakiniweka vile waonavyo (mitazamo yao ilivyo) na sioni kama wamenidharau?
🤣🤣🤣🤣🤣Kwa hiyo Mwijaku yupo kwenye kingdom animalia ,class Insecta au vipi?...(ilinisumbua sana hii topic😁😁)
 
Nyumba ndio kitu rahisi kujenga kama una kipato endelevu. Kuna watu wana nyumba za 300m ukimshtukiza leo lete 5m hana, wengi tu. Kwanini? Kwasababu hakujenga kwa sababu ana 300 au 500m benki,kajenga taratibu leo kapata 1m kesho 5m keshokutwa 3m mpaka anamaliza ujenzi. Haihitaji uwe na 300m benk au zaidi ili ujenge nyumba ya 300m ni kuwa na kipato endelevu na nia thabiti.
Well said mkuu
 
🤣🤣🤣🤣🤣Kwa hiyo Mwijaku yupo kwenye kingdom animalia ,class Insecta au vipi?...(ilinisumbua sana hii topic😁😁)

Ile topic NI rahisi,nzuri, na Applicable.
Ukiijua hiyo na kuitumia hakuna mwanadamu atakayekuchezea wala hutamlaumu yeyote.

Kwani Kunguru utamuweka kwenye Kunguru wenzake
Njiwa kwa njiwa
Kenge kwa kenge
mbzui kwa mbuzi
Popo kwa Popo
N.k

Kosa kubwa ni kumlazimisha Mbwa awe paka. Yaani mtu ushamuona yupo class Hii alafu unataka utumie mawazo na matamanio yako awe vile utakavyo. Hilo ni kosa.

Mbwa m-treat kama mbwa
Paka m-treat kama paka
Kuku m-treat kama kuku.
Wote ni muhimu ila zingatia matumizi yao tuu
 
Back
Top Bottom