TANZIA Augustino Mrema, Mwenyekiti wa chama cha TLP afariki dunia

TANZIA Augustino Mrema, Mwenyekiti wa chama cha TLP afariki dunia

Augustino Lyatonga Mrema ndiye aliyeasisi vuguvugu la mageuzi nchini kwenye ngazi za uchaguzi na ile 1995 wale mliokuwepo mnajuwa kabisa bila Nyerere kuingilia Kati Nccr Mageuzi ingekuwa Chama Tawala

Mrema amekuwa msema kweli asiyetawaliwa na tamaa

Mrema hakuwa mbinafsi ndio sababu alipowasapoti Kikwete na Maguful kwenye Uchaguzi hakuwalazimisha wanachama wa TLP kufuata Msimamo wake

Rest in peace Lyatonga

Vijana msilale bado mapambano - 1995
Mrema alikuwa mpigaji tu kama wapigaji wengine. Kapokea sana rushwa kutoka kwa makampuni aliyokuwa anayaita Kiraracha ili kuyahoji kwenye tuhuma za kukwepa kodi
 
Mrema alikuwa mpigaji tu kama wapigaji wengine. Kapokea sana rushwa kutoka kwa makampuni aliyokuwa anayaita Kiraracha ili kuyahoji kwenye tuhuma za kukwepa kodi
Kama alikuwa mpigaji Mbona hata nyumba ya kuishi pale sinza alinunuliwa na chama
 
Mwendo ameumaliza na ameitendea mema Nchi yake .ni baba wa demokrasia ya vyama vingi pamoja na mapungufu ambayo binadamu wote tunayo alijenga msingi kipindi kigumu kupita vyote.
RIP Agostino Lyatonga Mrema...mzee wa Kiraracha, mzee wa siku saba na mzee wa upigaji...

Pamoja na hayo naomba kukuuliza wewe makorere, hivi Mrema anakuwaje baba wa demokrasia?

Je unajua upepo wa mageuzi ulianza lini na wakati huo Lyatonga Mrema alikuwa wapi?

Je unajua madai ya demokrasia yalishika kasi lini na nyakati hizo Lyatonga Mrema alikuwa na msimamo gani?

Je unajua wana mageuzi walivyopambana kung'oa visiki miaka hiyo huku Lyatonga Mrema akivilinda vising'olewe?

Je unamjua aliyeendesha mapambano dhidi ya wana mageuzi na kuviongoza vyombo vya dola kutetea status quo?

Je unamjua aliyeapa kutoruhusu mfumo wa vyama vingi na kudai yeye si kichaa akiapa kulinda utawala wa kimla wa CCM?

Je unajua Lyatonga Mrema alijipa ukamanda wa vikosi vya FFU vilivyotumia silaha za moto, moshi na mbwa kuwatawanya wana mageuzi.

Je unajua kuwa hadi leo tupo ambao tulijeruhiwa na kuwa vilema tukidai demokrasia kupitia mkono wa kamanda Lyatonga Mrema?

Je unajua wakati mfumo wa vyama vingi unapitishwa rasmi mwaka 1992, Lyatonga Mrema alikuwa nani katika serikali ya CCM?

Pamoja na hayo...

Pumzika kwa amani Agostino Lyatonga Mrema, utakumbukwa kwa namna ulivyopambana kuzuia mfumo wa kidemokrasia lakini ukashindwa.

Utakumbukwa kwa namna wana mageuzi walivyokuwa wakihangaika juani kudai demokrasia ila wewe ukaja kula matunda yake kivulini.
 
Pumzika mzee wa kiraracha

Ila yule mjane vp hata ndoa haha enjoy wajameni
 
Na inaonekana hatutakuja kupata ukweli hasa ilikuaje mpaka msikiti wa mwembechai,pale Magomeni Dar warming kuuliwa pale wakiwa in a peaceful protest
 
R.I.P Lyatonga..tulipigwa bomu tukiwa na Lema Mwaka 2005 Pale Friends Corner Arusha Nikampa maji ya Kunawia Uso,Sijapost kitu kupitia ID hii nadhani toka 2017.Kwa heshima yake Nimejitokeza
 
Mwenyekiti wa chama cha TLP, Augustino Lyatonga Mrema (77) amefariki duninia leo Jumapili 21 August 2022, saa 12.15 asubuhi, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam. Mrema aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, alizaliwa Desemba 31, 1944, Vunjo mkoani Kilimanjaro.

Msemaji wa MNH, Aminieli Eligaisha amesema, Mrema alilazwa hospitalini hapo kuanzia 16 August 2022 na kufikwa na mauti asubuhi ya leo. Enzi za uhai wake, mwanasiasa huyo aliwahi kuwa mgombea urais kupitia NCCR-Mageuzi katika uchaguzi mkuu wa mwaka 1995 baada ya kujiunga na chama hicho akitokea Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mrema aliwahi kuwa Mbunge wa Moshi Vijijini (CCM), Temeke (NCCR Mageuzi) na Vunjo kupitia TLP na hadi amefikwa na mauti alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Parole.


Augustino Mrema ni mwanasiasa wa Tanzania aliyezaliwa tarehe 31 Desemba 1944 na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania. Alibadilisha uanachama wa chama Februari 1995 na kujiunga na NCCR-Mageuzi na baadaye akabadilika tena na kuwa Tanzania Labour Party (TLP) ambako aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa chama. Aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Vunjo mara kadhaa kabla ya kushindwa katika uchaguzi wa kitaifa na James Mbatia wa NCCR MAGEUZI mwaka 2015. Kisha akachaguliwa na Rais John Joseph Pombe Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Parole Tanzania mwaka 2016.

Augustino Mrema ni wa pili kati ya ndugu watano na ni wa kabila la Wachaga wa kijiji cha Kiraracha karibu na mlima Kilimanjaro. Augustino Mrema alisoma shule ya msingi na sekondari mjini Moshi mwaka 1955 hadi 1963, kisha akajiunga na Chuo cha Ualimu cha Mtakatifu Patrick ambako alimaliza elimu yake ya sekondari mwaka 1965. Augustino Mrema aliendelea kuandika mitihani ya Chuo Kikuu cha Cambridge O-level mwaka 1968 kisha akaendelea na masomo, kujiunga na Chuo cha Elimu ya Siasa, Kivukoni. Baadaye alienda Marangu kuendeleza masomo yake.

Augustino Mrema Nafasi Serikalini

Augustino Mrema ameshika nyadhifa kadhaa katika Serikali ya Tanzania, Shirika la Usalama wa Taifa na chama cha CCM tangu mwaka 1966; nafasi 5 alizoshika ni pamoja na zifuatazo:

  1. Mwalimu wa Uraia Vijijini 1974-1980
  2. Mwalimu katika Chuo cha Usalama cha Taifa 1980-1982
  3. Naibu Msaidizi wa Usalama wa Taifa katika Mkoa wa Dodoma 1982-1984
  4. Naibu Mkuu wa Usalama wa Taifa Mkoa wa Dodoma 1983-1984
  5. Naibu Mkuu wa Usalama wa Taifa Mkoa wa Shinyanga 1985-1987

Augustino Mrema Kisiasa

Ingawa Augustino Mrema alikuwa akigombea urais nchini Tanzania tangu jimbo hilo lilipoanzisha demokrasia ya vyama vingi mwanzoni mwa miaka ya 1990, maisha yake ya kisiasa yalianza mwaka 1985 alipogombea ubunge katika jimbo alilozaliwa la Kilimanjaro. Ugombea wake ulizuiwa na Mahakama ya Juu, hata hivyo, baada ya mchakato mrefu wa kukata rufaa, alitangazwa rasmi kuwa mshindi mwaka wa 1987. Alifanikiwa kushika kiti chake mwaka 1990 bila ushindani mkubwa. Kuwa Mbunge kulimruhusu Rais kumteua katika nyadhifa mbalimbali za Baraza la Mawaziri. Kuanzia 1990 hadi 1995 Mrema alishika nyadhifa mbalimbali za Baraza la Mawaziri na za juu serikalini:
  1. Waziri wa Mambo ya Ndani 1990-1994
  2. Waziri wa Kazi, Maendeleo na Michezo 1994-1995

Mwaka 1995 Augustino Mrema alihama CCM na kujiunga na Mkutano Mkuu wa Taifa wa Ujenzi na Mageuzi-Mageuzi ambacho kilikuwa chama kipya wakati huo. Katika uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995, alisimama kama rais wa NCCR-Mageuzi ambayo ilikuwa ni muungano kati ya Mkutano Mkuu wa Taifa wa Ujenzi na Chama cha Mageuzi-Mageuzi, alifanikiwa kupata asilimia 27.77 ya kura zote akishika nafasi ya tatu baada ya wakati huo aliyekuwa Rais Benjamin Mkapa aliyekuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Ibrahim Lipumba aliyesimama kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF).

Katika uchaguzi uliofuata alisimama kwa tiketi ya TLP na kupata asilimia 7.80 ya kura zote. Katika uchaguzi wa Desemba 14, 2005 alichaguliwa tena kuwa rais wa TLP na kumaliza wa nne na kupata 0.75% ya kura. Hayati Magufuli alimteua kushika wadhifa wa Mwenyekiti wa Bodi ya Parole kuanzia 2016 hadi 2019.
Kumbe Kweli mrema alikuwa Ni Mtu wa Tiss( usalama wa Taifa) hakuwai kuwa mpinzani wa kweli
 
Back
Top Bottom