Awamu ya Mama Samia Suluhu Hassan itakuwa kama ya Mzee Ruksa

Awamu ya Mama Samia Suluhu Hassan itakuwa kama ya Mzee Ruksa

Son of Gamba

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2012
Posts
4,720
Reaction score
6,957
Kwa jicho la tatu nauona utawala wa Samia Suluhu Hassan (SSH) ukienda kufanana ama kushahabiana na utawala wa awamu ya pili wa Mzee Ruksa. Samia Suluhu Hassan ni Mzanzibari na Mzee Mwinyi pia alikuwa Mzanzibari. Hata kimuonekano tu na jinsi wanavyoongea, wote hawa wawili wana haiba fulani hivi ya "upole".

Hii itakuwa neema kubwa sana kwa "wafanyabiashara" hasa ikitokana na ukweli kwamba kipindi cha marehemu JPM, biashara nyingi "zilikufa" ama "kudumaa". Hii inafanana na kipindi cha Mwalimu Nyerere, mliokuwepo wakati ule, kuanzia mwaka 80 mpaka 85 biashara nyingi zilikufa Sana, lakini alipoingia Mzanzibari, Mzee Ruksa, biashara zilishamiri kama uyoga wakati wa masika.

Kwa mtazamo wangu hali hii inaenda kujirudia tena! Kipindi cha "Ruksa" part two, kinajirudia tena! History has a tendency of repeating itself. Historia huwa inajirudia, na Mama Samia atalithibitisha hilo.

Wafanyabiashara, kaeni mkao wa kula, kipindi cha mavuno kinakuja. Tena naona hata yale maduka yakubadilishia fedha za kigeni yakiruhusiwa upya. Kitendo cha kufunga yale maduka (Bureau De Change) kilikuwa ni kitendo cha "dhuluma" na ukandamizaji. Sioni kama Mama Samia Suhusu Hassan atakuwa ni mwenye "dhuluma" kama mtangulizi wake alivyokuwa.

Tena kutokana na uswahiba uliopo kati ya Mama SSH na Jakaya Kikwete, hakika naiona Tanzania iliyojaa furaha na tabasamu. Sasa "pesa" itakuwa mifukoni mwetu.

Farewell Magufuli, till we meet again

IMG_20210322_095923.jpg
 
Kwa jicho la tatu nauona utawala wa Samia Suluhu Hassan (SSH) ukienda kufanana ama kushahabiana na utawala wa awamu ya pili wa Mzee Ruksa. Samia Suluhu Hassan ni Mzanzibari na Mzee Mwinyi pia alikuwa Mzanzibari. Hata kimuonekano tu na jinsi wanavyoongea, wote hawa wawili wana haiba fulani hivi ya "upole".

Hii itakuwa neema kubwa sana kwa "wafanyabiashara" hasa ikitokana na ukweli kwamba kipindi cha marehemu JPM, biashara nyingi "zilikufa" ama "kudumaa". Hii inafanana na kipindi cha Mwalimu Nyerere, mliokuwepo wakati ule, kuanzia mwaka 80 mpaka 85 biashara nyingi zilikufa Sana, lakini alipoingia Mzanzibari, Mzee Ruksa, biashara zilishamiri kama uyoga wakati wa masika.

Kwa mtazamo wangu hali hii inaenda kujirudia tena! Kipindi cha "Ruksa" part two, kinajirudia tena! History has a tendency of repeating itself. Historia huwa inajirudia, na Mama Samia atalithibitisha hilo.

Wafanyabiashara, kaeni mkao wa kula, kipindi cha mavuno kinakuja. Tena naona hata yale maduka yakubadilishia fedha za kigeni yakiruhusiwa upya. Kitendo cha kufunga yale maduka (Bureau De Change) kilikuwa ni kitendo cha "dhuluma" na ukandamizaji. Sioni kama Mama Samia Suhusu Hassan atakuwa ni mwenye "dhuluma" kama mtangulizi wake alivyokuwa.

Tena kutokana na uswahiba uliopo kati ya Mama SSH na Jakaya Kikwete, hakika naiona Tanzania iliyojaa furaha na tabasamu. Sasa "pesa" itakuwa mifukoni mwetu.

Farewell Magufuli, till we meet again
Na iwe hivyo.
 
Kwa jicho la tatu nauona utawala wa Samia Suluhu Hassan (SSH) ukienda kufanana ama kushahabiana na utawala wa awamu ya pili wa Mzee Ruksa. Samia Suluhu Hassan ni Mzanzibari na Mzee Mwinyi pia alikuwa Mzanzibari. Hata kimuonekano tu na jinsi wanavyoongea, wote hawa wawili wana haiba fulani hivi ya "upole".

Hii itakuwa neema kubwa sana kwa "wafanyabiashara" hasa ikitokana na ukweli kwamba kipindi cha marehemu JPM, biashara nyingi "zilikufa" ama "kudumaa". Hii inafanana na kipindi cha Mwalimu Nyerere, mliokuwepo wakati ule, kuanzia mwaka 80 mpaka 85 biashara nyingi zilikufa Sana, lakini alipoingia Mzanzibari, Mzee Ruksa, biashara zilishamiri kama uyoga wakati wa masika.

Kwa mtazamo wangu hali hii inaenda kujirudia tena! Kipindi cha "Ruksa" part two, kinajirudia tena! History has a tendency of repeating itself. Historia huwa inajirudia, na Mama Samia atalithibitisha hilo.

Wafanyabiashara, kaeni mkao wa kula, kipindi cha mavuno kinakuja. Tena naona hata yale maduka yakubadilishia fedha za kigeni yakiruhusiwa upya. Kitendo cha kufunga yale maduka (Bureau De Change) kilikuwa ni kitendo cha "dhuluma" na ukandamizaji. Sioni kama Mama Samia Suhusu Hassan atakuwa ni mwenye "dhuluma" kama mtangulizi wake alivyokuwa.

Tena kutokana na uswahiba uliopo kati ya Mama SSH na Jakaya Kikwete, hakika naiona Tanzania iliyojaa furaha na tabasamu. Sasa "pesa" itakuwa mifukoni mwetu.

Farewell Magufuli, till we meet again
Si mbaya kukubwa atoe ajira
 
Wafanyabiashara huu ndo wakati sasa. Wenye vyeti huu ndo wakati sasa wa ajira. Mshawishini mama kuwa nchi inaweza kuendelea na raia wakawa na pesa pia.

WAFANYABIASHARA JPM TUMUENZI KWA KULIPA KODI SAHIHI.
Unalipa kodi kwa biashara iliyokufa au haipo? Think again!

Mfumo wa kodi ilikuwepo ulikuwa mbovu kabisa. Umeua biashara nyingi. Na mpya jazifunguliwi. Nani anafungua biashara kwenye nchi ambayo TRA wanakubambinkia kodi, halafu wanakuja na polisi kuchukua kodi au unaenda benki unakuta pesa zako TRA walishachukua!
 
Jpm Alibana hela,nadhani baada ya siku 21 tutaanza kuokota hela mabarabarani

Hela mtaani hazikuonekana kwa sababu zifuatazo
1: utekelezaji wa miradi ya maendeleo
2 alidhibiti ufisadi na rushwa kwa kiwango kikubwa
3 mfumo mzuri wa ukusanywaji kodi

Kwa sababu hizo ni ngumu sana hela kuonekana sana kama ilivyokuwa awamu ya JK.
Kama mama SHS atafata utendaji mzuri ulianzishwa na JPM ni dhahiri hali itaendelea vile vile.
 
Unalipa kodi kwa biashara iliyokufa au haipo? Think again!

Mfumo wa kodi ilikuwepo ulikuwa mbovu kabisa. Umeua biashara nyingi. Na mpya jazifunguliwi. Nani anafungua biashara kwenye nchi ambayo TRA wanakubambinkia kodi, halafu wanakuja na polisi kuchukua kodi au unaenda benki unakuta pesa zako TRA walishachukua!
Hayo yalikuwa ni makosa.
 
Hela mtaani hazikuonekana kwa sababu zifuatazo
1: utekelezaji wa miradi ya maendeleo
2 alidhibiti ufisadi na rushwa kwa kiwango kikubwa
3 mfumo mzuri wa ukusanywaji kodi

Kwa sababu hizo ni ngumu sana hela kuonekana sana kama ilivyokuwa awamu ya JK.
Kama mama SHS atafata utendaji mzuri ulianzishwa na JPM ni dhahiri hali itaendelea vile vile.
Point yako namba 1 ndio valid.

Hizo 2 na 3 ni porojo tu, hazina uhalisia wowote. Mfumo mzuri wa kukusanya kodi unaenda na polisi? We vipi? Inaonekana unasomaga biashara kwenye vitabu tu. Haujawahi miliki hata genge!
 
Point yako namba 1 ndio valid.

Hizo 2 na 3 ni porojo tu, hazina uhalisia wowote. Mfumo mzuri wa kukusanya kodi unaenda na polisi? We vipi? Inaonekana unasomaga biashara kwenye vitabu tu. Haujawahi miliki hata genge!

Hongera wewe Mo dewji ila uhalisia ndio huo, nawashangaa sana mnaodhani kifo cha JPM ndio kitairudisha hela mtaani. Hii Tz sio ile ya miaka 10 iliyopita mambo yalikuwa shagala bagala maendeleo ya nchi hakuna wachache wanajinufaisha wao bila kujali maslahi ya wananchi hasa wanyonge.
 
Back
Top Bottom