Awamu ya Sita imeshakopa Trillion 10 ndani ya miezi 9 madarakani. Tunaomba ufafanuzi

Awamu ya Sita imeshakopa Trillion 10 ndani ya miezi 9 madarakani. Tunaomba ufafanuzi

Wewe ni chawa tu ila huyo bibi yako subiri! Atakaposhindwa kulipa mishahara ndo utajua hujui! Kwanza hata akiba ya fedha za kigeni hajui ni kiasi gani anajua Mwiguru Nchemba peke yake!
Kinacho kusumbua wewe ni chuki na ukabila hakuna jambo jingine, na kwa sababu ujinga ni wa kwako na hauna madhara mama ataendelea na kazi na atafanya vizuri kabisa kama unavyo ona watoto wako na wa wadogo zako kijijini huko wanaenda kusomea madarasa yenye tiles na roofing ya gypsum board
 
Nani kazungumzia ukabila hapa! Nyinyi mkikosa hoja mnakimbilia ukabila! Wapuuzi sana nyie!
si busara tunapochangia hoja kutaja makabila ya watu.watanzania ni wamoja na mwl nyerere alitukumbusha ubaya wa watu kukumbatia ukabila ijapokuwa tunajua kuna makabila hii zana kwao ni ngumu kweli kweli lkn tujitahidi tu kuchangia mada bila subjugation.
 
Kinacho kusumbua wewe ni chuki na ukabila hakuna jambo jingine, na kwa sababu ujinga ni wa kwako na hauna madhara mama ataendelea na kazi na atafanya vizuri kabisa kama unavyo ona watoto wako na wa wadogo zako kijijini huko wanaenda kusomea madarasa yenye tiles na roofing ya gypsum board
Bado uwazi hakuna
 
Mbatia katika hotuba yake ya mwisho wa mwaka alisikika akisema mpaka sasa Serkali ya awamu ya sita imeshakopa takriban Trillion 10 tokea iingie madarakani! Nauliza kwanini serikali haiji kutoa ufafanuzi wa kutosha badala yake kufunika funika mambo?.

Mheshimiwa Spika Ndugai japo kaomba msamaha kwa maneno yake lakini nahisi kuna kitu hapa hakiko sawa hususani kwenye kukopa madeni kwenye utawala wa Rais Samia!.

Waingereza wanasema ujumbe wa Ndugai sent and delivered mambo mengine ni kuwahadaa wananchi na kuweka sawa maslahi yao!.

Tuache kumsakama tu Spika ila tujadili sasa kuhusu Trillion 10 pamoja na tozo ndani ya miezi 9 zimefanya nini?.

Serkali kama ilivyoombwa kutoa ufafanuzi kwenye akiba ya fedha za kigeni na hapa tunaomba ufafanuzi juu ya kauli ya mkopo wa trillion 10 kama Mbatia na wengineo wanavyosema.
Wewe Mnaojiita Tanzania Leaks jibu inshaallah utalipata leo.
 
Mbatia katika hotuba yake ya mwisho wa mwaka alisikika akisema mpaka sasa Serkali ya awamu ya sita imeshakopa takriban Trillion 10 tokea iingie madarakani! Nauliza kwanini serikali haiji kutoa ufafanuzi wa kutosha badala yake kufunika funika mambo?.

Mheshimiwa Spika Ndugai japo kaomba msamaha kwa maneno yake lakini nahisi kuna kitu hapa hakiko sawa hususani kwenye kukopa madeni kwenye utawala wa Rais Samia!.

Waingereza wanasema ujumbe wa Ndugai sent and delivered mambo mengine ni kuwahadaa wananchi na kuweka sawa maslahi yao!.

Tuache kumsakama tu Spika ila tujadili sasa kuhusu Trillion 10 pamoja na tozo ndani ya miezi 9 zimefanya nini?.

Serkali kama ilivyoombwa kutoa ufafanuzi kwenye akiba ya fedha za kigeni na hapa tunaomba ufafanuzi juu ya kauli ya mkopo wa trillion 10 kama Mbatia na wengineo wanavyosema.
Unataka ufafanuzi kwa porojo? Weka tawimu za ukweli uone zinavyojifafanua.
 
SIyo tu kutoa ufafanuzi bila ushahidi huku wanajisifia wanakusanya kodi sijui 2.5T lakini hatujui zinaenda wapi, tuna taka ushahidi nani amelipwa nini in details with vivid evidence
Wacha ujinga. Wewe porojo ulizokuja nazo umekuja na ushahidi upi?
 
Mbatia kasukwa kwaaajili ya 2025, leo lipumba anasema mikopo hii ni nafuu na endelevu sana kwa uchumi wa nchi hii.. Tafakarii

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Mna stress tu, hakuna zaidi.

Hasa likiwa deni limeiva kama lile lililo mfanya Mh Mwigulu kumpigia Amiri Jeshi Mkuu simu mara tatu usiku as if nchi imevamiwa.

Kwa mara ya kwanza nimesikia kumbe nchi nayo inaweza kuhamisha deni yaani kukopa kwa kazi nyingine kumbe ni ili kulipa deni lililo kwiva na chakulipa huna.Siku wakopeshaji wakijua tunakopa kwenda kuendeleza kilimo umwagiliaji kumbe ki uhalisia ni kwenda kulipia mkopo wa vyumba vya madarasa ulioiva na chakulipa hatuba mjue ndio nchi imeumia hivyo. Hatutakopesheka wataambizana.
 
Pesa zinaenda kukamilisha legacy ya SGR,Bwawa la Nyerere na miradi mingine kibao ili Legacy inayolindwa kwa nguvu zote idumu, Mama ni muungwana sana pamoja na yote bado anawakumbuka na vijana katika ajira.
 
Back
Top Bottom