Awamu ya Tano iliua UDART, hili tuliseme wazi si kumung'unya maneno

Awamu ya Tano iliua UDART, hili tuliseme wazi si kumung'unya maneno

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
Uache siasa za changa la macho, Serikali ya JPM ndiyo imeua utendaji wa UDART.

Barabara za UDART kweli ni mali ya serikali lakini mradi wa mabasi mwendo kasi ulikuwa toka mwanzo ni mradi binafsi (private investment) uliowekezwa na mtanzania, Nd Kisenha.

Serikali ilifanya kila njia kumnyima pumzi mwekezaji huyu wa UDART. Alipoagiza mabasi alinyimwa katakata kuyatoa bandarini mpaka hela yote ipatikane kulipa kodi.

Huku ni kukosa ushirikiano kwa muwekezaji, ambapo wale wa kigeni hupewa Tax Holiday au Mkataba maalum kwa malipo ya kodi kubwa.

Hii ingewezesha huduma iendelee, biashara iendelee na kodi ilipwe. Hili ni kosa, maana serikali haikuwa na msaada wowote kwa muwekezaji.

Pili, tunasikia tetesi kuwa sasa UDART ni mali ya Serikali maana baada ya Nd Kusenha kufunguliwa madai ya Uhujumu uchumi, kwawaida ya modus operadi ya Awamu ya 5kwa wafanyabiashara, serikali imejimilikisha uendeshaji.

Serikali zote toka Awamu ya kwanza hadi nafikiri Mwinyi (miaka zaidi ya33) mfupa wa DMT (Dra es Salaam Motor Transport) na UDA (Usafiri Dar es Salaam), ziliwashinda.

Sasa sijui Awamu ya 5 ndio wangeweza Kuendesha UDART?

Mbaya zaidi serikali inaua moyo wa wazalendo kuingia miradi mikubwa kiuwekezaji, kinyume cha wanachoongea majukwaani. Ziara ya Waziri Mkuu Majaliwa kwa UDART kweli sioni mantiki yake zaidi ya kusema Serikali imachukua na kuanza mradi huu on a false start.

Sana sana ni kujikosha kwa wananchi kwa failures za serikali yenyewe, kusaidia wazalendo kuwekeza nchini mwao.
 
Marehemu POMBE alikuwa anapigwa daily na wajanja aisee nashangaa ule ubabe wake wote lkn bado wahuni wa mjini wamepiga hela ndefu Sana hakika wezi WA nchi hii wanatisha
Tatizo kubwa si hilo.

Tatizo ni kutaka kulazimisha serikali kufanya biashara ambazo haiwezi, pamoja na "kuwafanyizia" wafanyabiashara wazalendo.
 
Marehemu POMBE alikuwa anapigwa daily na wajanja aisee nashangaa ule ubabe wake wote lkn bado wahuni wa mjini wamepiga hela ndefu Sana hakika wezi WA nchi hii wanatisha
Acha kupotosha wewe,

Ukweli ni kwamba huyo marehemu ndiye alikuwa anapiga. Ubabe wake ulikuwa ni zuga tu na uhuni wake. Marehemu amepiga hela ndefu Sana mfano alitumia 1.2 trillion kununua ndege by cash ambapo alilipwa 10% ya hiyo hela ,unafikiri ni sh ngapi?

Yeye alikuwa ni mwizi Namba 1 wa nchi hii.

Usijifanye hujui wakati unajua acha kudemka.
 
Rais hawezi kusimamia kila kitu, mpaka pen maofisi au sindano mahospitali. Mh. Spika juzi kasema, vijana wa kitanzania bila kuiba hawana raha moyoni, mradi huu, unafilisiwa na watu walioaminiwa na wala sio tax holiday au uwekezaji.

Kumbuka bado kuna mabasi 100 yanazurula mitaani, lakini mapato yake yanaishia mifukoni kwa wale wanaojiita watoto wa mjini.
 
Rais hawezi kusimamia kila kitu, mpaka pen maofisi au sindano mahospitali. Mh. Spika juzi kasema, vijana wa kitanzania bila kuiba hawana raha moyoni, miradi huu, unafilisiwa na watu walioaminiwa na wala sio tax holiday au uwekezaji. Kumbuka bado kuna mabasi 100 yanazurula mitaani, lakini mapato yake yanaishia mifukoni kwa wale wanaojiita watoto wa mjini.
Sasa hivi Serikali ndio inaendesha UDART badala ya muwekezaji aliyeondolewa kihuni.

Mfupa wa DMT na UDA uliishinda serikali, huu wa kisasa wa UDART ndio kabisa imejaribisha ulaji wa mameneja na wafanyakazi wake.
Hakuna cha ajabu hapo, serikali awamu iliyopita ilivurunda.
 
Rais hawezi kusimamia kila kitu, mpaka pen maofisi au sindano mahospitali. Mh. Spika juzi kasema, vijana wa kitanzania bila kuiba hawana raha moyoni, miradi huu, unafilisiwa na watu walioaminiwa na wala sio tax holiday au uwekezaji. Kumbuka bado kuna mabasi 100 yanazurula mitaani, lakini mapato yake yanaishia mifukoni kwa wale wanaojiita watoto wa mjini.
Yeye spika aliingia bungeni kwa uadilifu? Pale jizi la kura linapowatuhumu watu kuwa sio waaminifu.
 
Nilikuwa siamini kwamba kwenye kila analogusa Magufuli huwa ana haribu Ila kwenye Mwendokasi ndo sehemu niliyokuja kuamini kwa Mara ya kwanza!

Kwanza inabidi wote tujiulize mwendokasi ilianzia wapi?

Mradi wa mabasi ya mwendokasi ukianzishwa na kuasisiwa na Rais wa Awamu ya nne. Kwa Jinsi mradi ulivyokuwa umeandaliwa ulitakiwa kusimamiwa na kampuni binafsi na tangu mwanzo ulisimamiwa kwenye mfumo huo. Mradi huu ulikuwa chini ya Kampuni na Kisena na wakati unaanza kila kitu kilikuwa kinaendeshwa katika dunia ya kisasa. Ticket zilikatwa kielectronic na watu waliweka hadi kuwa na kadi ya kutumia mwezi mzima.

Alipokuja Magufuli kwanza alianza ku deal na kisena kwa sababu kisena hakuwa kwenye kundi la watu waliomuunga mkono kwenye uchaguzi wa mwaka 2015. Alimtesa kisena kumpa kesi za uhujumu uchumi na mkewe na baadae kumnyang’anya mradi na hatimaye akaondoa utaratibu wote mzuri uliokuwa umewekwa kwa ajiri ya kuendesha mradi.

Matokeo yake akawapa wanajeshi, na hapo ndo Tatizo lilipoanza. Mradi ulianza kuendeshwa kwa tabia za kiswahili na watu wakaanza kukata ticket kama daladala.

Mradi huu hadi kufikia sasa ulitakiwa uwe umeshaanza kujiendesha kwa faida Ila kwa roho mbaya ya magufuli na tabia zake za kuchukia matajiri ndo amefanya mradi ule uwe kituko na usifike popote.

Polee kisena. Buriani Mwendokasi.
 
Rais hawezi kusimamia kila kitu, mpaka pen maofisi au sindano mahospitali. Mh. Spika juzi kasema, vijana wa kitanzania bila kuiba hawana raha moyoni, miradi huu, unafilisiwa na watu walioaminiwa na wala sio tax holiday au uwekezaji. Kumbuka bado kuna mabasi 100 yanazurula mitaani, lakini mapato yake yanaishia mifukoni kwa wale wanaojiita watoto wa mjini.
Anayasema hayo leo..!!
 
marehemu POMBE alikuwa anapigwa daily na wajanja aisee nashangaa ule ubabe wake wote lkn bado wahuni wa mjini wamepiga hela ndefu Sana hakika wezi WA nchi hii wanatisha
Na inashangaza sana, mabasi karibu nusu yako juu ya mawe na yaliyopo hayana ubora badala yake ni kero...

Yale yaliyo juu ya mawe ukisikia matatizo yake utaambiwa gear lever mbovu au matairi yameisha, au gear box au sterling rod imekatika nk nk..

Cha kushangaza kingine ni, mabàsi yana matatizo ya injini au matairi nk nk lakini, unakuta vitu vingine kama viti, vioo nk vinavyofolewa ktk namna ya hujuma moja kwa moja...

Kwa kifupi ni kuwa, hakuna kipindi ambacho wizi na ufisadi na uharibifu wa mali ya umma na mifumo ya utendaji ulishamiri kama kipindi cha uongozi wa Mwendazake...
 
Sasa hivi Serikali ndio inaendesha UDART badala ya muwekezaji aliyeondolewa kihuni.
Mfupa wa DMT na UDA uliishinda serikali, huu wa kisasa wa UDART ndio kabisa imejaribisha ulaji wa mameneja na wafanyakazi wake.
Hakuna cha ajabu hapo, serikali awamu iliyopita ilivurunda.
Mwekezaji alikuwa sio mtu wa kuaminika, ana makado-kando mengi sana tokea alivyokuwa Mwanza. Hata kupata huo miradi aliupata kimagumashi maana hajawahi kuendesha miradi kama huo popote pale duniani. Kwanza tatizo lilikuwa kwenye upangaji wa nauli ambapo yeye alitaka iwe juu zaidi, serikali ikamkatalia kupandisha nauli. Akaona apunguze mabasi kwa kusingizia mabovu ili asitumie gharama kubwa kuyaendesha na alinde mgao wake, kitu ambacho ni kinyume na dhana ya miradi huo. Matokeo yake, uhaba wa mabasi uliongezeka, abiria kujazana kwenye mabasi na mwisho watu kuyasusa kurudi kutumia magari yao.

Lakini tokea 2015, awamu ya tano imejaribu kutafuta wawekezaji wanaoelewa maswala ya usafirishaji mijini, lakini kila mwekezaji anayekuja anakutana na Madudu ya uzembe, anakimbia. Ili kupata mwekezaji mwenye nia, lazima serikali wasafishe wahuni wote waliokuwa kwenye miradi huo na kurudisha shirika kwenye hadhi ya kubinafshwa.
 
h
Tatizo kubwa si hilo.
Tatizo ni kutaka kulazimisha serikali kufanya biashara ambazo haiwezi, pamoja na "kuwafanyizia" wafanyabiasgara wazalendo.
ivi zile shell aka vita vya Mafuta kila Mkoa vya serikali kwa minajil ya kufanya biashara bado mpango unaendelea au ulidancha na mwendazake kupitia mawaziri wenye ubunifu wa abunwasi na adabu za kimbwa koko
 
Kisena yule Fisadi! Enzi za JK alikuwa na nguvu hatari,aliwahi kumpiga OCD wa Maswa mtama lol.huyu atakuwa alikamatwa kwa uhalali.
Kisena aliwekwa kama chambo tu. Ile kampuni ya SIMON GROUP ina wahusika wengi sana wakubwa, akiwepo Profesa Kapuya na Marehemu Idd Simba. Kuna vigogo kadhaa wamo mle. Ukipekua humu JF kuna mada inayoongelea SIMON GROUP, utayaona mengi sana
 
Back
Top Bottom