kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 277
Mshambuliaji nyota wa Liverpool, Fernando Torres ameitosa timu hiyo na kujiunga na timu ya Chelsea huku akiacha washabiki wengi wa Liverpool wakiwa na hasira juu yake wengine wakimaliza hasira zao kwa kuzichoma jezi za Liverpool zenye jina lake.
Fernando Torres amekamilisha usajili uliovunja rekodi ya usajili ya Uingereza kwa kuitosa Liverpool na kujiunga na vijana wa darajani, Chelsea.
Torres amehamia Chelsea baada ya Liverpool kukubali kumuuza mchezaji huyo nyota kwa kitita kinono cha paundi milioni 50.
Chelsea pia imetumia kitita cha zaidi ya paundi milioni 25 kukamilisha usajili wa mlinzi hodari wa Benfica ya Ureno, David Luiz.
Wakati dirisha dogo la usajili likifungwa, Liverpool imeamua kuzitumia pesa za usajili wa Torres kwa kumsajili mshambuliaji hatari wa Newcastle Andy Carrol kwa usajili uliovunja rekodi ya uhamisho ya Newcastle, paundi milioni 35.
Carrol alipelekwa Liverpool kwa helikopta ili kutia saini mkataba huo.
Kiungo wa Arsenal, Jack Wilshere amemtabiria Carrol kuwika zaidi akiwa na jezi ya Liverpool.
Fernando Torres amekamilisha usajili uliovunja rekodi ya usajili ya Uingereza kwa kuitosa Liverpool na kujiunga na vijana wa darajani, Chelsea.
Torres amehamia Chelsea baada ya Liverpool kukubali kumuuza mchezaji huyo nyota kwa kitita kinono cha paundi milioni 50.
Chelsea pia imetumia kitita cha zaidi ya paundi milioni 25 kukamilisha usajili wa mlinzi hodari wa Benfica ya Ureno, David Luiz.
Wakati dirisha dogo la usajili likifungwa, Liverpool imeamua kuzitumia pesa za usajili wa Torres kwa kumsajili mshambuliaji hatari wa Newcastle Andy Carrol kwa usajili uliovunja rekodi ya uhamisho ya Newcastle, paundi milioni 35.
Carrol alipelekwa Liverpool kwa helikopta ili kutia saini mkataba huo.
Kiungo wa Arsenal, Jack Wilshere amemtabiria Carrol kuwika zaidi akiwa na jezi ya Liverpool.