Azam FC 1-2 Yanga SC|| Uwanja wa Chamazi|| NBC Premier League

Bangala inabidi aingie licha ya tatizo la viungo mabeki nao wamepoteana, nadhani Kaseke hii mechi inamhusu kuliko hawa madogo wa pembeni.
Ngoja tuone ,naona mabeki wanapata wakati mgumu hawapumui kabisa
 
Ni swala la mda ice cream 🍨 italambwa tu
Hii mechi tukishinda litakuwa jambo la kushukuru. Maana viungo wetu katikati wanakimbia kimbia tu muda mwingi, kiasi Mayele kule mbele anakosa kabisa mipira.

Nitashangaa kama Zawadi Mauya ataachwa acheze dk 90! Hii mechi inawafaa mafundi kama Balama Mapinduzi. Mauya control ya mpira iko chini sana.
 
Mkuu unaichambua mechi vilivyo,
 
Nadhani kocha analiona ilo
 
Refa amepanick, hii faulu ni Nyepesi Sana Kutoa kadi
 
Profesa awe makini na Sure Boy! Ameshakula kadi ya njano. Akimuacha mpaka mwisho, atapigwa kadi ya pili ya njano + red kadi!

Ni mwepesi wa kupaniki na kutoka nje ya mchezo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…