Azam mabingwa kombe la mapinduzi

Boniphace Kichonge

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2017
Posts
1,605
Reaction score
1,957
Wadau
Azam FC ya Tanzania wametwaa Kombe la Mapinduzi baada ya kuwafunga URA ya Uganda kwa bao 4 kwa 3 kupitia mikwaju ya penati katika mchezo wa fainali uliofanyika uwanja wa Aman Zanzibar. Mpira umemalizika saa 4: 45 usiku huu.
Timu za Simba na Yanga zilishindwa kufurukuta baada ya kutolewa mapema katika mashindano hayo.
Mgeni rasmi katika mchezo huo alikuwa Rais wa Zanzibar Dkt Ally Mohameid Shein.
 
Hivi ukiambiwa kabisa utaje Kombe la Kimashindano kabisa na lenye ' Tija ' kwa nchi na Maendeleo ya Soka utalitaja kweli Kombe la Mapinduzi?
Huwezi kulitaja kombe la Mapinduzi.
Nashangaa kwanini timu yenu pendwa Simba ilipeleka timu kwenda kuaibishwa kwa vichapo.
 
Wadau
Azam wametwaa Kombe la Mapinduzi baada ya kuwafunga URA ya Uganda kwa bao 4 kwa 3 kupitia mikwaju ya penati.
Mpira umemalizika saa 4: 45 usiku huu.
Mgeni rasmi katika mchezo huo alikuwa Rais wa Zanzibar Dkt Ally Mohameid Shein.
Asante kwa taarifa
 
brother vip mbona povu wakati hii ni taarifa tu

Wewe ukishaona tu Kombe lolote lile Fainali ama Simba au Yanga hazipo ' automatically ' tu jua kwamba hilo halikuwa Kombe lenye ' hadhi ' bali ni Kombe ' Upuuzi ' tupu!
 
Huwezi kulitaja kombe la Mapinduzi.
Nashangaa kwanini timu yenu pendwa Simba ilipeleka timu kwenda kuaibishwa kwa vichapo.

Simba SC hatukuenda kushindana bali tulienda kujaribu Wachezaji wetu wa Kikosi B na pia kutafuta tu ' fitness ' ili tukirudi bara kuendelea na Ligi yetu ya Vodacom kama kawaida tuzidi kutoa ' Vichapo ' tu na tuwaache hao Azam FC na ' Washamba ' wasiojua mpira kabisa duniani kote Yanga FC.
 
Nimekupata mdau.

Naomba maoni yako. Je lilikuwa jambo sahihi kumkatishia mkataba Omog? Au ndio itakuwa kama kosa walilo fanya Yanga kwa kumletea zengwe Babu Pluijm? Maana kule wenye akili washajua kiufundi babu alikuwa muhimu kwa Yanga kuliko Lwandamana.
 
Hongera sana Azam,,, kuna wengine imewauma timu zao kutolewa mapema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…