ZUMARI TV AZAM: KIPINDI MAALUM CHA MALKIA ELIZABETH (1926 - 2022) JAFFAR MPONDA NA MOHAMED SAID LEO USIKU SAA TATU
Picha ya kwanza Malkia Elizabeth 1953.
Picha ya Pili barua ya viongozi wa TAA kwenda kwa Malkia Elizabeth wakimpongeza kwa kuwatawazwa kuwa malkia 1953.
Mwandishi kulia akiwa nje ya Buckingham Palace 1992.
Randy...
Inawezekana labda kwa kukosa kutambuana ukadhani kuwa unaweza ukanidhihaki.
Ikiwa lipo jina lakini kwa sababu hii au ile wanahistoria waliotangulia wakawa hawalitaji au kuna historia lakini kwa sababu moja au nyingine ikawa haiandikwi, mimi huona nina wajibu wa kuifahamisha jamii kile wasichojua.
Hii haiwezi kuwa ''hukawii.''
Jana kipindi cha Zumari kuhusu Malkia Elizabeth kilirushwa na baada ya kipindi baadhi ya watazamaji wameniandikia.
Watazamaji wanasema wamefaidika na baadhi ya mambo niliyoeleza.
Wengi hawakuwa wanajua kuwa uongozi wa TAA 1953 President alikuwa Julius Nyerere na Vice President Abdul Sykes.
Lakini kilichowashangaza sana ni jina la Secretary General wa TAA Dome Okochi Budohi mzalendo kutoka Kenya.