Azam TV Limited yaingia mkataba wa kuonesha Matangazo ya Ligi Kuu kwa miaka 10. Mshindi misimu mitatu ijayo kulamba bonus Tsh 500m

Hatua nzuri lakini 10yrs ni mingi sana kwa hii mikataba.

Premier League wanafanya kwa mnada na ni kwa miaka 3. Halafu wanarudi tena kwenye mnada, kufunga mkataba wa miaka 10, labda kama wameweka vifungu vya kulinda pia thamani ya fedha. Hiyo hela baada ya miaka 10 inaweza kushuka thamani by 50%.
 
Nchi yetu kibiashara bado sana.

Mambo mengi bado serikali inafanya biashara yenyewe kwa yenyewe. Sera ya nchi haivutii hata FDI ( Foreign Direct Investment ).

Na wafanyabiashara wetu wengi wazawa ni wachuuzi kutoka China wakishirikiana na machinga.

Imagine kwenye Database ya TRA ndani ya nchi ya watu 60M kuna walipa kodi 3M pekee.

Na kila wakati serikali ikitaka kupandisha makusanyo ya kodi, badala ya kutafuta walipa kodi wapya wao wanawaongezea kodi watu hao hao.

Na wenyewe wanachofanya sasa ili waishi kila mara wanatafuta mbinu za kukwepa kodi.
 
Wamejitahidi kuonesha mechi zote za ligi kuu, ombi muhimu waongeze camera hasa kubainisha matukio yenye utata kwenye mechi ..mfano zile goli za simba na yanga za kona hapo ndo unaona upungufu kidogo wa camera
 
Hivi Mo akiona huu mkataba wa bil. 225 anajisikiaje yeye anaposhindwa kutoa bil. 20? [emoji23][emoji23]
Hizo ni pesa mkuu, huwezi kuzitupa kama vile unapanda ma-apple hapa bongo. Kama hakuna mazingira mazuri hata kama ningekuwa mimi ningesubiri tu. Au kwa akili zako unadhani matajiri kama Bakhresa na Mo hawaumii wakipoteza pesa?
 
Vilabu lazima vihusishwe, amini usiamini bila Simba au Yanga kwenye ligi ya VPL, Azam hawezi kupata faida hata arukeruke vipi.
 
Aboreshe na viwanja vyetu jamani pitch mbovu sana...
 
Sorry
So hiyo 500m anapewa mshindi wa kwanza kwa kila msimu ktk miaka mitatu mfululizo, ambayo ni tofauti na atakayo pewa na mdhamini wa ligi ?

Na sahizi mshindi wa kwanza anapewa sh. Ngapi
 
Ishu sio udogo wala ukubwa
Ishu miaka 10?
DStv akija na ofa mara tatu ya hiyo baaada ya miaka 5 hawawezi vunja mkataba?
Hilo wameliona Azam. Ndiyo maana ya miaka kumi. Ni mingi sana. Angalau mitano sio mbaya.
 
Halafu uhalali WA Ku saini miaka kumi unatoka wapi iwapo Viongozi wa TFF wanachaguliwa kila baada ya miaka mitatu??
Muda mrefu baada ya Msomali kuondoka TFF, mkataba bado utakuwa valid.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…