Azam wana timu nzuri, wana wachezaji wazuri na jana kaondolewa kwenye michuano

Azam wana timu nzuri, wana wachezaji wazuri na jana kaondolewa kwenye michuano

Leonel Ateba Mbinda

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2023
Posts
644
Reaction score
2,695
Sawa Azam walishika nafasi ya pili sisi tukaumia sana lakini tukumbuke sisi tulijiumiza wenyewe, sisi hatukuwa watu wa kushika nafasi ya pili, hata sasa hivi tunakwenda vizuri lakini mbeleni huko tutakorofisha tena mtani abebe ndoo na Injinia kashasema Simba haimnyimi usingizi, anajua anachokifanya ndani ya timu yetu, yaani Yanga kumfunga Simba ni sure bet kwenye kamari sasa hivi.

Azam wana timu nzuri, wana wachezaji wazuri na jana kaondolewa kwenye michuano, mimi kwa maoni yangu haikufungwa Azam, imefungwa nchi, aibu ni ya nchi, viongozi wakuu wa nchi wanaweza kuwa wanatambiana kuwa Rwanda ana timu nzuri kuliko Tanzania, ndio ukweli wenyewe.

Azam kuondoshwa kwenye michuano ya mabingwa hatua za awali kabisa ni msiba ndugu zangu watanzania, sio jambo la kuleta utani, matusi, au kujiona mjanja kuwadhalilisha viongozi wao na wachezaji, mimi naheshimu sana uhuru wa kutoa maoni lakini tunapoiombea mabaya Azam aondolewe kwenye level ya kimataifa wewe kama mtanzania unaona ni sawa kweli?

Haya mambo lazima tuyaangalie vizuri, humu ndani tupambane na kutaniana wenyewe kwa wenyewe lakini utani hadi tunapokwenda kupambana na nchi nyingine, kweli? Mbona jana hatukuona timu za Rwanda zikishangilia Azam? Hatukuiona Rayon wala Polisi jana, mashabiki wote waliungana kuwa kitu kimoja kuisapoti APR ambayo kiukweli imedhamiria kufanya vizuri ingawa kwa namna walivyocheza jana hawana timu nzuri bado, jana dakika za mwishooooni Jibril Sylla alikuwa awalize warundi wale lakini bahati haikuwa kwetu watanzania.

Tuache habari hizi za kijinga jinga, tushauriane kwenye level za kimataifa tufanye nini kwa sababu mwisho wa siku inatajwa Tanzania, sio Azam.Huu ni ujinga, ulofa, upumbavu sana.
 
Andika Wanyarwanda sio Warundi.
Azam ni wendawazimu haiwezekani kutolewa mapema hivyo kila msimu wanaoshiriki Mashindano ya Caf huo ni uzezeta wa kiwango cha broiler.....Timu tajiri maskini wa mafanikio mpira unachezwa hadharani unaona kabisa shida ipo kuanzia kufungwa 4 na wydad,kufungwa 4 na Yanga,kushinda goli moja la penati katika uwanja wa nyumbani basi unaona kuna vilaza wamejazana Azam fc kula pesa za Bakhresa unaliabisha Taifa halafu usichekwe kweli?
 
Wameshaondolewa, kuna sababu kadhaa ambazo wadau walipendekeza lakini uongozi ulisweka pamba nzuri kwenye masikio yao moja wapo ilikuwa ni ufanisi duni wa kocha, swali fikirishi kama hao matajiri wa chamazi hawawasikilizi wadau nini kifanyike
 
Mimi ni mwananchi, ila sikupenda kabisa Azam amalize nafasi na pili maana nilijua tu ataleta aibu, Bora Simba na Yanga waendelee kui boost ligi yetu kimataifa tuwe ma giant wa kuogopeka....

Ila Simba mlivyo ma mbumbumbu mlishangilia sana Azam kutufunga na kumuumiza pacome, hivo pambaneno na Hali zenu
 
Kwangu Mimi nimeona vitu vichache:-
1:Kocha ni mpole wachezaji wanafanya makosa yaleyale lkn hakuna maamuzi at least ya kuwaweka benchi wachezaji,jana unaona kabisa wachezaji wanacheza kibinafsi na sio kitimu
2: Utoto mwingi sana goal walilofungwa ni uzembe/kukosa uzoefu wa mechi kubwa kwenye kushambulia unaongoza goli moja la nyumbani kwanini usilinde mpk half time then unakuja tafuta surprise kipindi cha pili?.
3: wanatakiwa kua na wakongwe km Nyoni awasaidie hawa watoto wakue otherwise wote wanaona wapo sawa and vichwa vikubwa kwao
 
Andika Wanyarwanda sio Warundi.
Azam ni wendawazimu haiwezekani kutolewa mapema hivyo kila msimu wanaoshiriki Mashindano ya Caf huo ni uzezeta wa kiwango cha broiler.....Timu tajiri maskini wa mafanikio mpira unachezwa hadharani unaona kabisa shida ipo kuanzia kufungwa 4 na wydad,kufungwa 4 na Yanga,kushinda goli moja la penati katika uwanja wa nyumbani basi unaona kuna vilaza wamejazana Azam fc kula pesa za Bakhresa unaliabisha Taifa halafu usichekwe kweli?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mimi ni mwananchi, ila sikupenda kabisa Azam amalize nafasi na pili maana nilijua tu ataleta aibu, Bora Simba na Yanga waendelee kui boost ligi yetu kimataifa tuwe ma giant wa kuogopeka....

Ila Simba mlivyo ma mbumbumbu mlishangilia sana Azam kutufunga na kumuumiza pacome, hivo pambaneno na Hali zenu
Unajua unachokizungumzaa weyeee? Umevurugwaaaaa?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Unajua unachokizungumzaa weyeee? Umevurugwaaaaa?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Ndo ukweli huo, sikupenda Azam kumaliza wa pili nilijua tu atazingua, ila sasa na nyi makolo Azam alivyotufunga mlizidi mdomo
 
Sawa Azam walishika nafasi ya pili sisi tukaumia sana lakini tukumbuke sisi tulijiumiza wenyewe, sisi hatukuwa watu wa kushika nafasi ya pili, hata sasa hivi tunakwenda vizuri lakini mbeleni huko tutakorofisha tena mtani abebe ndoo na Injinia kashasema Simba haimnyimi usingizi, anajua anachokifanya ndani ya timu yetu, yaani Yanga kumfunga Simba ni sure bet kwenye kamari sasa hivi.

Azam wana timu nzuri, wana wachezaji wazuri na jana kaondolewa kwenye michuano, mimi kwa maoni yangu haikufungwa Azam, imefungwa nchi, aibu ni ya nchi, viongozi wakuu wa nchi wanaweza kuwa wanatambiana kuwa Rwanda ana timu nzuri kuliko Tanzania, ndio ukweli wenyewe.

Azam kuondoshwa kwenye michuano ya mabingwa hatua za awali kabisa ni msiba ndugu zangu watanzania, sio jambo la kuleta utani, matusi, au kujiona mjanja kuwadhalilisha viongozi wao na wachezaji, mimi naheshimu sana uhuru wa kutoa maoni lakini tunapoiombea mabaya Azam aondolewe kwenye level ya kimataifa wewe kama mtanzania unaona ni sawa kweli?

Haya mambo lazima tuyaangalie vizuri, humu ndani tupambane na kutaniana wenyewe kwa wenyewe lakini utani hadi tunapokwenda kupambana na nchi nyingine, kweli? Mbona jana hatukuona timu za Rwanda zikishangilia Azam? Hatukuiona Rayon wala Polisi jana, mashabiki wote waliungana kuwa kitu kimoja kuisapoti APR ambayo kiukweli imedhamiria kufanya vizuri ingawa kwa namna walivyocheza jana hawana timu nzuri bado, jana dakika za mwishooooni Jibril Sylla alikuwa awalize warundi wale lakini bahati haikuwa kwetu watanzania.

Tuache habari hizi za kijinga jinga, tushauriane kwenye level za kimataifa tufanye nini kwa sababu mwisho wa siku inatajwa Tanzania, sio Azam.Huu ni ujinga, ulofa, upumbavu sana.
Hivi,APR ni timu ya Warundi au Wanyarwanda?
 
Kwasababu malengo Yao yameegemea kuzifunga Simba na Yanga tu.
 
Back
Top Bottom