Azimio La Arusha: Why We Were Dead Wrong!

Azimio La Arusha: Why We Were Dead Wrong!

- Kuhusu Jefferson, nimesema very clear kwamba Declaration aliyoitoa, ilijali sana kuwepo kwa mazungumzo ya UN kule NYC, na pia by origin Jefferson asili yake ilikuwa ni France, ambako kulikuwa na vugu vugu kubwa la kukataa utumwa, DEclaration aliyoiandika ilijali hayo na pia hata alipofariki, huku nyuma ilikuwa bado inatekelezeka na nido maana Lincoln akaweza kuitekeleza lakini kwa kupitia The American Civil War, ambapo wananchi wengi sana walimwaga damu, sasa sisi katika kutekeleza Azimio, wananchi wengi walipoteza maisha wakati wa kuhamishwa, lakini matokeo yamekuwa zero! WHY? Ni kwa sababu Azimio lilikuwa halitekelezeki na mpaka leo huwezi kulitekeleza!


William.

Thomas Jefferson Genealogy

[TABLE="align: right"]
[TR]
[TD]
Thomas%20Jefferson.jpg
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Thomas Jefferson, third president of the United States, was of English descent, but with deep and wide Virginia roots. His father and paternal grandparents were Virginians; his mother was born in London to English parents


Sina haja ya kucopy na kupaste..... United Nations was the result of WWII

GET YOUR FACTS RIGHT HOMMIE!!
 
Mkuu Kichuguu,


Sifa nyingine ya katiba ni lazima iwe ni sheria kuu ya nchi. Sheria zingine za nchi zinakuwa extension ya katiba. Hivyo CCM wana wabunge wengi na wana rais. Hivyo wanaweza kubadilisha vitu kukidhi mahitaji yao.
Zakumi,
Believe me it won't be for long.
 
- Duh!

William.

Kaka yangu william,

Soma vizuri historia ya nchi yako uelewe ilikuwa vipi kijamii na kiuchumi kabla ya ujio wa mkoloni compared to nchi kama Kenya; pia soma mchakato wote mwalimu alioupitia wakati alipomuachia Mzee Kawawa uongozi wa nchi ili kwenda kujenga chama na alipata feedback gani huko. Wananchi walikuwa na hamu na matunda ya uhuru kwani walipewa ahadi nyingi sana na vuguvugu la kutaka mabadiliko ya haraka from the bottom-up lilianza kuchochoea kwani tofauti ya kipato/maisha miongoni mwa watanzania ilikuwa kubwa sana na watanzania waliendelea kuwa watumwa ndani ya nchi yao kwani ni watanzania wachache pamoja na wahindi na wazungu ndio waliokuwa wamekamata uchumi wa nchi. Bila ya Mwalimu kuleta azimio la arusha, wananchi vijijini wange - revolt na nchi isingekuwa hii tunayoiongelea. Kwa kifupi, Azimio la Arusha lilikuwa endorsed hata na wasomi wa chuo kikuu, let alone wananchi wengi vijijini. Ukikaa kusikiliza mawazo ya viongozi juu ya nini kilitokea, utapotoka kwani wengi wao walitegemea uhuru ungewaletea faida wao, sio wananchi. Nadhani upo Tanzania hivi sasa, zunguka vijijini na tafuta wasaa wa kuongea na wazee wa zamani huko vijijini kuhusu suala zima la uhuru na azimio la arusha.
 
Hizo rekodi unazosema zipo za vifo vya watu waliokufa kutokana na Azimio la Arusha ziweke hapa JF. Here we dare talk openly. Kama huna basi ni uwongo.

Tunalumbana hapa si kwa sababu hatujui tunakotoka na tunakokwenda. Tunalumbana hapa kwa sababu the likes of you mmeamua makusudi kutupotosha tusimulike madhambi yanayofanywa na serikali za post Arusha declaration na sera mbovu za Mkapa/ Kikwete.

Tanzania leo ina matatizo makubwa kwa sababu uongozi wa sasa hauna dira, hauna ruuya (vision) na umekithiri kwa wizi mtupu. Kama hicho ni kitu cha kushabikia, nakusikitikia sana na ndoto zako za uongozi kwa sababu inavyoonekana hautakuwa tofauti na hawa unaowashabikia.

I am out!

Mkuu wangu Jasusi:-

1. Unasema hujui kwamba wananchi wengi waliliwa na fisi, baada ya kuachwa maporini kutoka kuhamishwa kwenye miji yao ya asili eti kwenda kupelekwa kwa nguvu kuanzisha vijiji vya ujamaa, I mean vipo wapi sasa hivyo vijiji? Hayo yote yamefanywa under false ideology za Azimio la Arusha, look leo Azimio hakuna wala Vijiji hakuna what a waste?

2. Unasema umulike madhambi yanayofanywa toka Azimio liuliwe kule Zanzibar, lakini husemi kwamba madhambi against Azimio yalianzia the very Awamu ya kwanza iliyotuletea hilo janga la taifa, Viongozi walioliunga mkono waliruhusiwa kuiba as much they wanted bila kuulizwa, lakini waliolipinga wakasingiziwa majungu mengi, ukiona nyumba ina matatizo muhimu ni kwenda kuchungulia msingi wake, utakuta matatizo yalipoanzia, ukweli ni kwamba Azimio wa s a myth, na infact it was a complete lie nido maana halikuwa na njia zaidi tu ya kufa!

3. Kama dira ya taifa haikuwepo toka awamu ya kwanza, haiwezi kuwa ajabu kama haipo leo, wizi haukuanza leo umeanzia awamu ya kwanza, we were here, mpaka siku hili taifa kwa pamoja tutakapo kubali kwamba Azimio na maazimio mengi ya awamu ya kwanza ndio yametufikisha hapa tumekwama, ndio tutaanza kusonga mbele, maana taifa lisilojua linakotoka, haliwezi kujua linapokweda!

Willliam.
 
Thomas Jefferson Genealogy

[TABLE="align: right"]
[TR]
[TD]
Thomas%20Jefferson.jpg
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Thomas Jefferson, third president of the United States, was of English descent, but with deep and wide Virginia roots. His father and paternal grandparents were Virginians; his mother was born in London to English parents


Sina haja ya kucopy na kupaste..... United Nations was the result of WWII

GET YOUR FACTS RIGHT HOMMIE!!

- Hapo sio mwisho wa historia ya Jefferson, soma zaidi mkuu utaona asili yake hasa inatokea wapi ni zaidi ya hapo ulipoishia!

William.
 
Kaka yangu william,

Soma vizuri historia ya nchi yako uelewe ilikuwa vipi kijamii na kiuchumi kabla ya ujio wa mkoloni compared to nchi kama Kenya; pia soma mchakato wote mwalimu alioupitia wakati alipomuachia Mzee Kawawa uongozi wa nchi ili kwenda kujenga chama na alipata feedback gani huko. Wananchi walikuwa na hamu na matunda ya uhuru kwani walipewa ahadi nyingi sana na vuguvugu la kutaka mabadiliko ya haraka from the bottom-up lilianza kuchochoea kwani tofauti ya kipato/maisha miongoni mwa watanzania ilikuwa kubwa sana na watanzania waliendelea kuwa watumwa ndani ya nchi yao kwani ni watanzania wachache pamoja na wahindi na wazungu ndio waliokuwa wamekamata uchumi wa nchi. Bila ya Mwalimu kuleta azimio la arusha, wananchi vijijini wange - revolt na nchi isingekuwa hii tunayoiongelea. Kwa kifupi, Azimio la Arusha lilikuwa endorsed hata na wasomi wa chuo kikuu, let alone wananchi wengi vijijini. Ukikaa kusikiliza mawazo ya viongozi juu ya nini kilitokea, utapotoka kwani wengi wao walitegemea uhuru ungewaletea faida wao, sio wananchi. Nadhani upo Tanzania hivi sasa, zunguka vijijini na tafuta wasaa wa kuongea na wazee wa zamani huko vijijini kuhusu suala zima la uhuru na azimio la arusha.

Mkuu Mchambuzi:-

1. Tafadhali sana usiongelee Kenya, maana wao walipo sasa kimaendeleo na sisi tulipo ni aibu sana kusema anaything kuhusu historia zetu, please usinilazimishe kwenda huko.

2. Unasema wananchi walikuwa na hamu ya Uhuru na matunda yake, Really? Wananchi wapi hao mkuu wangu, I mean it took Mwalimu kuja mjini kuwaamsha kwa sababu walikuwa wamelala ndio maana aliposhika TAA cha kwanza aliwaondoa wale wote aliowakuta na kuleta wapya, unajua sababu mkuu? Ni kwa sababu aligundua kwamba wote walikuwa hawana any idea ya uhuru, so kwenye hili pia huna ukweli mkuu!

3. Wananchi wa Tanzania then wenge-revolt? Hapana kama ni kweli then wange-revolt walipohamishiwa maporini na kuliwa na simba na Fisi, kama hawaku-revolt on that basi wasingewezaa ku-revolt kwa sababu ya the myth, simply ni kwamba they did not know anything ndio maana kuna kati yenu mnaamini kwamba mpaka leo sisi wananchi ni kama wale wa zamani kwamba hatujui anything, ni wanajeshi tu waliokuwa na akili za ku-revolt na only because kuna waliokuwa wametoka kusoma nje, ama sivyo hata wao wasingeweza kutuhubutu!

4. Unsema Azimio lilikuwa endorsed na wasomi wa then, please! wasomi hao ni kina nani hasa ambao walikuwa objective mbele ya Mwalimu, hebu mtaje mmoja tu aliyekwua na openmind juu ya Azimio na Mwalimu akamkubali, wote walitishiwa walioktaaa wakaambiwa waondoke nchi, please Mchambuzi ulianza vizuri sasa unaanza kutoka nje kabisa ya mstari I mean how can you say this with your very clear mind kwamba Azimio, lilikuwa endorsed n wasomi wa wakati huo, huku tunasikia waliopingwa waliitwa Ikulu na kuchapwa viboko, watu wazima na akili timamu, pleasee!

5. Mkuu toka nirudi nimetembea vijiji vingi sana, sijasikia mwananchi hata mmoja akikumbuka zamani wote wapo mbio mbio kujaribu kupata a piece of cake ya sasa, na hio ndio hasa maana ya ubepari kila mmoja kujituma kutafuta nafasi yake kwenye keki ya uchumi wa taifa, sio rahisi lakini kwa sababu njia imeshaonyeshwa ni lazima twende nayo!

MCHAMBUZI, ULIANZA VIZURI KULE WMANZO, LAKINI SASA UNAANZA KUTOKA NJE YA MSTARI WA UTETEZI WAKO WA AZIMIO LA ARUSHA!

William.
 
Kobello,
Umefunga mjadala juu ya miiko. Kumbe Marekani wana miiko. Ni mleta mada tu ndiye alikuwa halijui hilo.

- Labda mngetuletea mifano ili kuridhisha hoja yenu, ni ishu gani ya kisheria huko US iliwahi kuamuliwa kwa kutotumia sheria, badala yake wakatumia miiiko ya uongozi kama zile enzi za Azimio, kiongozi mwizi anaitwa kwenye kamati kuu badala ya kuepelekwa kwenye Sheria!

- I mean kuishi kwangu kote US, sijawahi kusikia ishu ya sheria imeamuliwa kwa miiiko ya uongozi, labda muweke mfano hapa!

William.
 
Mkuu William Malecela,

Unaposema Azimio la Arusha ndio kiini cha matatizo yanayotukabili leo kama taifa, una maana gani hasa, kwani azimio la arusha per se ni pana sana. Ungefunguka kidogo tungeweza pata mjadala mzuri zaidi.

Azimio la Arusha haliwezi kulaumiwa kuwa ndio limetukwamisha kimaendeleo kwasababu katika Azimio lile kuna sehemu inayosisitiza KUJITEGEMEA kama msingi wa maendeleo badala ya kuwa omba omba !! Kujitegemea implicitly maana yake kuweza kuzitumia rasilimali za nchi vizuri ili kukidhi mahitaji ya ndani ya nchi kwanza badala ya kutegemea kukidhi mahitaji kwa kuagiza toka nchi za nje. Nchi kujitegemea kuna faida kisiasa kwani nchi huheshimiwa internationally na haiwezi kuyumbishwa katika kufanya maamuzi yake ya sera; kiuchumi nchi inayojitegemea kwa kuzalisha mahitaji yake yenyewe huweza kuuza ziada nchi za nje na pia huzuia mfumuko wa bei unaotokana na kuagiza mahitaji toka nje ya chi hivyo kuchangia kuboresha maisha ya wanannchi!!
 
Azimio la Arusha haliwezi kulaumiwa kuwa ndio limetukwamisha kimaendeleo kwasababu katika Azimio lile kuna sehemu inayosisitiza KUJITEGEMEA kama msingi wa maendeleo badala ya kuwa omba omba !! Kujitegemea implicitly maana yake kuweza kuzitumia rasilimali za nchi vizuri ili kukidhi mahitaji ya ndani ya nchi kwanza badala ya kutegemea kukidhi mahitaji kwa kuagiza toka nchi za nje. Nchi kujitegemea kuna faida kisiasa kwani nchi huheshimiwa internationally na haiwezi kuyumbishwa katika kufanya maamuzi yake ya sera; kiuchumi nchi inayojitegemea kwa kuzalisha mahitaji yake yenyewe huweza kuuza ziada nchi za nje na pia huzuia mfumuko wa bei unaotokana na kuagiza mahitaji toka nje ya chi hivyo kuchangia kuboresha maisha ya wanannchi!!



- Mhhhh!, Azimio lilisisistiza kujitegemea na huku Awamu ya kwanza ndio iliyoanza tabia ya kuomba omba, I mean nakumbuka mkutano mmoja na Mwalimu mwishoni mwa uhai wake, akisema kuna wakati taifa liliishiwa mahindi akamtuma Salim kwenda India kuomba Dola USD $ 3 million tu!

- I mean huenda Azimio lilikuwa na maneno mazuri sana kwa kuyasoma tu, lakini tatizo ni kwamba ililikuwa halitekelezeki, na ndio maana limetufikisha hapa tulipo Taifa hatuelewani ni kwa sababu tulikuwa tunaongozwa na dead theories za Azimio, saa ni wakati wa kuachana na ile myth for good twende mbele tu na ubepari!

William.
 
-

1. Unasema hujui kwamba wananchi wengi waliliwa na fisi, baada ya kuachwa maporini kutoka kuhamishwa kwenye miji yao ya asili eti kwenda kupelekwa kwa nguvu kuanzisha vijiji vya ujamaa, I mean vipo wapi sasa hivyo vijiji? Hayo yote yamefanywa under false ideology za Azimio la Arusha, look leo Azimio hakuna wala Vijiji hakuna what a waste?

Willliam.
W. J. Malecela
Mkuu Umefocus sana kwenye -VE na mbaya zaidi kama hii ya kuliwa na fisi ni story za kahawa.Try to be analytical an unbiased

Ukweli ni kwamba uwepo wa hivi vijiji vya ujamaa ndio uliwezesa na ulisaida kupapatikana kwa taarifa kirahis kuhusu watu kupotea( kuliwa na wanyama) . Kabla ya hapo bado watu walikuwa wanaliwa sana na hao fisi/simba mamba lakini haku kuwepo information . --- Tumia SImple logic Kama watu 10 wameweza kuliwa na simba kwa mwkaa wakati wanahisi kwenye community vipi ni wangapi walikuwa wanaliwa bila taarifa wakati wakati kila mtuyuko kivyake .

Fact nyingine ukiwa na resources ndogo unahitaji Organisation na managemnt . Hivi
  • utawahudumia vipi wakazi 15,000 waliotapakaa maeneo mbaimbali ?. famiia moja na nyingine ziko one mileapart
  • Shule ya msiingi utaijenga wapi au kisima cha maji utachimba wapi?
  • Bwana shamba wa kusadia uhamasihaji wa kiimo bora atakuwa stationed wapi kama watu hawaishi katika community

Pamoja na hivyo vijiji vya ujamaa bado mpaka sasa kuna baadhi ya maeneo wanafunzi wanatembea(Msisitizo wanatembea) hata KM 5 kufika kwenye shule au hospitali au seheu za hudumaza jamii sasajiuzlie bila hivyo ingekuwaje.

BTN

  • je unajua kufuta ujinga wa kutojua kusoma na kuandika tanznia ifanikiwa tena kidunia na sababu mojawapo ni ingawa hakukuwa na resource za kutosha ni azmioa la rushana navijiji vya ujamaa.
  • Je unajua hivi sasa hata baada ya azimio kuzikwa kuna watoto wanafika hata darasa la tatu hawajui kuandika.Je na hilini kosa la Azimio arusha.
  • Je unajua pamoja na kukuwa kwa uchumi ,GDP, illiteracy ya watanzania inaogezeka


Fact Nyingine


Vijiji vya ujaama haikuwa kitu kipya sana labda kwa baahi ya mikoaau jamii kama dodoma na singida amabapo watu wanaishi scattered . Kwenye Baddhii ya jamii hata kabla zoezi halijanaza ni kama tayari walikuwa wanaishi kwenye vijiji vya ujamaa. Na unaweza kuona hata tofauti ya kimaendeleo(Japo ni ndogo) jamii zilizokuwa zinaishi kwenye hali hiyo na zile jamii amabazo so called kijiji kimoja lakini nyumba moja na nyigine iliyo karibu ziko umbali wa Km 2.......


NB
William dodoma city
Nadhani unahitajika kuelewa Maudhui ya AZimio la Arusha Vizuri ili uje na version II ya thread hii useme hapa palikuwa na tatizo na hapa pangerekebishwa hivi.

Unawasifia kenya wako mbali lakini kuna donda kuu kulela "class struggles". No wonder na sisi tumeshaingia kwakasi yaajabu kwenye donda hilo
 
Last edited by a moderator:
Mkuu wangu Jasusi:-

1. Unasema hujui kwamba wananchi wengi waliliwa na fisi, baada ya kuachwa maporini kutoka kuhamishwa kwenye miji yao ya asili eti kwenda kupelekwa kwa nguvu kuanzisha vijiji vya ujamaa, I mean vipo wapi sasa hivyo vijiji? Hayo yote yamefanywa under false ideology za Azimio la Arusha, look leo Azimio hakuna wala Vijiji hakuna what a waste?

2. Unasema umulike madhambi yanayofanywa toka Azimio liuliwe kule Zanzibar, lakini husemi kwamba madhambi against Azimio yalianzia the very Awamu ya kwanza iliyotuletea hilo janga la taifa, Viongozi walioliunga mkono waliruhusiwa kuiba as much they wanted bila kuulizwa, lakini waliolipinga wakasingiziwa majungu mengi, ukiona nyumba ina matatizo muhimu ni kwenda kuchungulia msingi wake, utakuta matatizo yalipoanzia, ukweli ni kwamba Azimio wa s a myth, na infact it was a complete lie nido maana halikuwa na njia zaidi tu ya kufa!

3. Kama dira ya taifa haikuwepo toka awamu ya kwanza, haiwezi kuwa ajabu kama haipo leo, wizi haukuanza leo umeanzia awamu ya kwanza, we were here, mpaka siku hili taifa kwa pamoja tutakapo kubali kwamba Azimio na maazimio mengi ya awamu ya kwanza ndio yametufikisha hapa tumekwama, ndio tutaanza kusonga mbele, maana taifa lisilojua linakotoka, haliwezi kujua linapokweda!

Willliam.
William,
Ungesema waliliwa na simba hapo ningekusikiliza kwa sababu kesi za watu kuliwa na simba mpaka sasa zipo huko Ruvuma. Lakini kwa kawaida fisi hali mtu aliye hai. Try another myth.
 
- I mean huenda Azimio lilikuwa na maneno mazuri sana kwa kuyasoma tu, lakini tatizo ni kwamba ililikuwa halitekelezeki, na ndio maana limetufikisha hapa tulipo Taifa hatuelewani ni kwa sababu tulikuwa tunaongozwa na dead theories za Azimio, saa ni wakati wa kuachana na ile myth for good twende mbele tu na ubepari!

William.

W. J. Malecela. Vyema.

Umeshajiuliza hayo maneno mazuri kuyasoma kwanini hayakutekelezeka? Wewe umeleta suala la Jefferson,hivi unajua ni kwa muda gani hiyo declaration imeanza kuleta matunda? Azimio limedumu kwa miaka 19 tu,lakini licha ya changamoto za hapa na pale,taifa liliweza kuwa na viwanda vya kusaidia wakulima wa pamba,korosho na mkonge. Liliweza kuleta uwajibikaji,watumishi wa umma walikuwa waoga kuiba mali za umma,hata walioiba ilikuwa sio katika kiwango cha sasa. Ambapo wizi wa mali za umma upo waziwazi. Azimio kwa kipindi hicho kifupi liliweza kujenga misingi,ambayo kwa hakika kama Azimio la Zanzibar lingeweza kubeba misingi mizuri ya Azimio la Arusha,taifa lingekuwa limepiga hatua.

Tungefanya blending kidogo,lakini taifa likaamua kuingia mazima kwenye ubepari. Na sasa taifa linapiga nyimbo za kijamaa huku likicheza kibepari. Matokeo yake ndiyo haya:badala ya kusonga mbele tunarudi nyuma,vilivyokuwa viwanda vya korosho vimegeuzwa kwa matumizi mengine. Wakulima wa korosho wako hoi,huku wahindi wanao-export korosho hizo wakizidi kutajirika.

Pia mkuu, kuna jambo moja ambalo mimi uwa naamini aidha Mwalimu hakuwa mwalimu mzuri katika kufundisha falsafa zake au wanafunzi wake enzi hizo hawakuwa waelewa. Ndiyo pengine ikawa ni rahisi kwao kulitupia mbali azimio. Sasa taifa lina wasomi ambao wanaelewa falsafa za Mwalimu vyema kabisa. Na kwa kuwatumia hao,taifa laweza amua kuzipitia upya falsafa hizo katika msingi wa kutumia mazuri ya azimio na kuyaweka katika mazingira ya sasa.

Ndio maana mkuu Mchambuzi alikwambia mambo ya NIA, MCHAKATO na MATOKEO ya azimio. Kama umekiri azimio lina mambo mazuri kuyasoma,hauoni lilikuwa na NIA nzuri?
 
Last edited by a moderator:
William,
Ungesema waliliwa na simba hapo ningekusikiliza kwa sababu kesi za watu kuliwa na simba mpaka sasa zipo huko Ruvuma. Lakini kwa kawaida fisi hali mtu aliye hai. Try another myth.

Huyu jamaa anajichanganya sana. Mara Jefferson na UN,mara Jefferson alikuwa mnafiki juu ya kupiga marufuku utumwa,kwavile alikuwa ana watumwa nyumbani kwake. Mara Jefferson ana asili ya Ufaransa. Yote hayo anasahau kutoa facts za ni kwa vipi Azimio la Arusha limetufikisha hapa. Na je ni yapi ya kujivunia kutoka kwenye mbadala wa azimio?

Kuna mambo mawili naanza kufikiri juu ya mkuu W. J. Malecela: moja,pengine anakuwa mbishi kama njia ya kujifunza na kuelewa juu ya Azimio. Jambo la pili ni pengine jamaa anakuwa mbishi kwavile haelewi anachokibishia,anabishia nini?

Le Mutuz,naomba nimalize kwa kurudia tena,azimio halikuwa perfect kwa 100%,ila kwa uhakika nakwambia lilikuwa na bado lina relevance kwa taifa letu kuliko haya "maazimio" tuliyo nayo sasa. Kama wataka mema kwa taifa letu kwa kikazi hiki na vijavyo,tujadili ni yapi ya kuchukua kutoka kwenye azimio ili taifa liweze ktwa na dira yenye kuendana na mazingira yetu,si dira zinazotengenezwa Washington, New York na Geneva.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu wangu Jasusi...............

Willliam.

Unarudi kwenye tatizo lile lile la kutojali kabisa kujadili and appreciate 'NIA' ya Sera ya Azimio la Arusha, badala yake unazidi kupotea kwani kwako wewe muongozo wa hoja zako ni 'MCHAKATO' na 'MATOKEO'. Kwa mwendo huo, itakuwa ni vigumu sana kwako kuja na Sound Argument iliyo coherent and that is near the Quality and Character ya Azimio la Arusha. Kwa mfano hapa chini unamjibu Jasusi and I quote:

Unasema hujui kwamba wananchi wengi waliliwa na fisi, baada ya kuachwa maporini kutoka kuhamishwa kwenye miji yao ya asili eti kwenda kupelekwa kwa nguvu kuanzisha vijiji vya ujamaa, I mean vipo wapi sasa hivyo vijiji? Hayo yote yamefanywa under false ideology za Azimio la Arusha, look leo Azimio hakuna wala Vijiji hakuna what a waste?

Kaka William, madhara ya tabia yako ya kutopendelea kujisomea/kufanya utafiti zinazidi kujitokeza hapa. Kwa mfano, kama umesoma historia ya afrika mashariki, wakati wa ujenzi wa Reli ya Kisumu – Mombasa, (waingereza) wazungu wengi pamoja na waafrika waliliwa sana na Simba katika nyika ya Voi. Kuna filamu moja by ‘Michael Douglas' inaitwa ‘Ghost of the Darkness', inaelezea vizuri sana nini kilijiri, lakini maudhui yake sio mchakato au matokeo bali NIA. Kwa vile NIA ya waingereza haikuwa kuwalisha Simba wa Porini nyama za binadamu bali kuleta maendeleo ya miundombinu kama kichocheo cha kujenga uchumi imara, suala la watu kupoteza maisha halikupewa uzito wowote zaidi ya kuchukuliwa kwamba ni suala la ‘ajali kazini'. Inashangaza watu kama wewe kuzidi kung'a'ng'ania hoja ya wananchi kuliwa na ‘Fisi'. Hoja kama hii haitakiwi kutoka kwa mtu mwenye upeo mkubwa kama wewe kaka William.

Unaelewa nini ilikuwa ni Nia ya vijiji vya ujamaa? Nia ilikuwa ni kuvifanya vijiji hivi view the basis of a socialist system of production, ultimate aim ikiwa kuifanya Tanganyika liwe taifa linalojitegemea kutokana na nguvu kazi ya wananchi wake, lakini muhimu zaidi katika mazingira ya people-centered development ambayo yanazingatia a Bottom-Up approach to development badala ya Top-Bottom approach.

Kaka William, kama umewahi kutumia muda wako japo kidogo kujosomea historia ya nchi yetu, by the time tunapata uhuru (mwaka 1961), takibran 85% ya Tanganyika ilikuwa ni vijiji. Pia usisahau kwamba nch yetu mpaka leo hii ni moja ya nchi chache sana duniani ambayo imezungukwa na mbuga za wanyama. Hivi una taarifa kwamba mwaka jana Simba alitokea Mbagala Rangi Tatu na kuleta maafa?

Wakoloni walipokuja walikuta mazingira ya Tanganyika ni pori kwa kiasi kikubwa sana. Fahamu tu kwamba hawakujenga miji huko porini na badala yake waliwafuata watanganyika huko huko na kuwatumikisha katika kilimo cha mazao ya biashara. Nadhani unatambua kwamba wakoloni hawakuwa na mkakati wowote wa kuwahamishia watanganyika mijini au kuwajengea industrial centres. Je, katika mazingira ya mwaka 1961, Mwalimu ilitakiwa afanye nini kama njia yaku ‘transform' jamii hizi? Kumbuka kwamba ilikuwa ni miaka sita tu tokea uhuru na nchi ilikuwa haina fedha za kutosha kuwa na options nyingi za kufikishia wananchi huduma, wananchi ambao asilimia 90 walikuwa hawajui kusoma na kuandika, hawana huduma za afya, hawana ajira, na wanaishi mazingira ya porini and in a very sparse manner. Kaka William, nadhani una ufahamu mzuri kwamba nchi yetu hata leo, population yake imetapakaa sana, kwani ni sehemu chache tu ndio zenye concentration kubwa ya watu. Je, ulitegemea Mwalimu afanye nini ili kuwafikishia wananchi huduma muhimu, wananchi ambao walikuwa na kiu ya maendeleo baada ya miaka mingi ya colonial exploitation, wananchi ambao walishapewa ahadi nyingi sana wakati wa harakati za ukombozi? Mwalimu angezitimizaje ahadi za matunda ya uhuru in terms of kuwapatia wananchi huduma za kijamii pamoja na ajira? Inawezekana una mawazo tofauti juu ya nini Mwalimu angefanya, huu ni wasaa wako kutueleza ili tujue tulikosea wapi na tusonge vipi mbele.

Vinginevyo kwa mtazamo wangu ambao unaweza kuwa finyu – kwa kifupi tu – Njia sahihi ilikuwa kuja na mkakati/sera ambayo ingepelekea watanganyika kuishi kwa pamoja na kwa wingi katika maeneo kadhaa ili iwe rahisi kuwafikishia huduma za kijamii pamoja na kuwapatia mazingira ya kujishughulisha kiuchumi ili kujipatia kipato. Kwa maana hii, ilibidi vijiji vya ujamaa vinazishwe kwa wingi ili kuwaondoa wananchi kutoka maeneo ambayo mengi yalikuwa na watu wachache kwani Economies of Scale zisingewezekana huko walipo. More importantly, a system of production inayokidhi level ya maendeleo ya wakati ule pamoja na mazingira ilibidi iwe devised, so by default it had to be Kilimo. Kumbuka, jamii zote zilianza na Kilimo kwani huo ndio msingi wa kukupelekea kwenye Mapinduzi ya Viwanda. Ukipunguza uvivu wa kufanya utafiti utalibaini hilo mapema sana.

Unasema umulike madhambi yanayofanywa toka Azimio liuliwe kule Zanzibar, lakini husemi kwamba madhambi against Azimio yalianzia the very Awamu ya kwanza iliyotuletea hilo janga la taifa, Viongozi walioliunga mkono waliruhusiwa kuiba as much they wanted bila kuulizwa, lakini waliolipinga wakasingiziwa majungu mengi, ukiona nyumba ina matatizo muhimu ni kwenda kuchungulia msingi wake, utakuta matatizo yalipoanzia, ukweli ni kwamba Azimio wa s a myth, na infact it was a complete lie nido maana halikuwa na njia zaidi tu ya kufa!

If one reads between the lines, atabaini kwa upesi tu kwamba inaonyesha ‘inside information' kuhusu viongozi Fulani Fulani kuruhusiwa kuiba mali ya umma wakati wa Ujamaa. Kwa vile sisi hatuna hizo taarifa na hapa JF We Dare to Speak Openly, please speak up ili hoja yako iache kupepesuka na badala yake iwe na mashiko.

Kuhusu hoja yako juu ya Kifo cha Azimio la Arusha, nakushauri jaribu kufanya utafiti japo kidogo kuhusu internal and external factors zilizopelekea kifo chake kwani kwa haraka sana utagundua kwamba, ni kweli partially ilikuwa ni poor implementation ya sera lakini kwa kiasi kikubwa sana ilitokana na juhudi za makusudi on part of viongozi waliopewa dhamana ya kulitekeleza kum ‘black mail' Mwalimu. Viongozi wengi walikuwa wanashirikiana na wahindi pamoja na mabepari wa nje kuharibu uchumi wa nchi yetu, na wengi wa hawa ndio waliopewa dhamana kusimamia mashirika ya umma. Kama William, unafahamu kwamba nchi yetu ina rasilimali nyingi sana na wazungu walikuwa wanatafuta kila njia ya kuhakikisha Ujamaa haufanyi kazi ili waweze pata nafasi ya kuja kutufilisi kupitia ubepari chni ya soko huria holela lisilojali maslahi ya Watanzania, jambo ambalo sasa wamefanikiwa chini ya Structural Adjustment Policies na Azimio la Zanzibar.

Hivi nikuulize - Kwanini Ujamaa wa Sweden ulifanikiwa? Tusidanganyake kwamba Ujamaa hauwezekani. Ujamaa unawezekana, hivyo Azimio la Arusha bado lina nafasi katika Tanzania yetu ya leo, lakini linahitaji kufanyiwa marekebisho. Kwa mtazamo wangu, huo ndio uwe msingi wa mjadala wetu – kubaini success and failures za Azimio la Arusha, iwapo kweli tuna nia nzuri na taifa letu changa.

Kama dira ya taifa haikuwepo toka awamu ya kwanza, haiwezi kuwa ajabu kama haipo leo, wizi haukuanza leo umeanzia awamu ya kwanza, we were here, mpaka siku hili taifa kwa pamoja tutakapo kubali kwamba Azimio na maazimio mengi ya awamu ya kwanza ndio yametufikisha hapa tumekwama, ndio tutaanza kusonga mbele, maana taifa lisilojua linakotoka, haliwezi kujua linapokweda!

Kwa kweli inasikitisha kuona kwamba, licha ya wadau wengi hapa kujaribu kukuelezea jinsi gani taifa letu lilikuwa na dira huko nyuma, wewe bado unazidi kupingana na hilo. Lakini ukiulizwa je, dira ya sasa ni nini? Majibu hauna zaidi ya kuleta hoja zinazoelwa juu ya ubepari na utawala wa kisheria. Na ni nani anaesema kwamba wizi unaweza kudhibitiwa kwa asilimia mia moja? Hakuna nchi inayoweza kuzuia hilo, lakini nchi makini zinaweza kuja na leadership code na mambo kama hayo kupunguza tatizo husika. Na hivyo ndivyo alivyofanya Mwalimu chini ya Azimio La Arusha. Leo hii we are facing a major social evil – UFISADI, and this is a by-product ya hatua ya kuachana na azimio la arusha. Sidhani kama utapingana na hili. Azimio la Arusha served as an ‘orbit' ya kisiasa, kijamii na kiuchumi; Chini ya Azimio la Arusha, na katika mazingira ya nchi changa iliyokuwa na umri wa miaka sita tu ya uhuru (1961 – 1967), ajira ndio ilikuwa ni kipato halali kwa kila mtanzania; lakini leo hii chini ya azimio la Zanzibar, equation imepanuliwa na sasa Rushwa na Ubadhirifu pia vimekuwa sehemu halali ya viongozi kujipatia kipato. Hii ndio nature of leadership that we have nurtured chini ya azimio la Zanzibar. Viongozi wameacha kuwa watumishi wa umma, sasa wanashindana kwa utajiri and lifestyle huku wale waliowapa dhamana wakizidi kudidimia.

Tangia mwaka 1995, wanasiasa wote wenye nia ya kuongoza nchi hii hawafanyi hivyo kwa maslahi ya umma bali maslahi binafsi na ushahidi ulio wazi juu ya hili ni jinsi gani wanatumia mamilioni ya pesa kununua wajumbe wa mkutano mkuu wa taifa. Wengi wa hawa wanakamatwa na pesa hizo chafu wakati wa michakato ya kupata mgombea wa Urais kupitia CCM, lakini kwa vile Azimio La Zanzibar linakamata wengi zaidi, masuala kama haya yanapotezewa. Je, hii ndio Tanzania yako ya sasa yenye Dira?
 
Mimi nadhani tatizo la William, na hili ameshaligusia awali kwingineko, ni kumkubali Julius Nyerere. He has a personal beef with Mwalimu. After all, hata kama mimi mtu angeandika kitabu juu ya baba yangu ambacho kinaonyesha madhaifu yake, halafu mtu huyo awe mkubwa na mwenye ushawishi kama Julius Nyerere, sijui ningejisikiaje. William amekiri kuwa hajasoma azimio la Arusha, na wakati huo huo anasema lilikuwa ni waste of time, badala ya kutoa uchambuzi ni wapi azimio lilikuwa na kasoro anatuambia watu waliliwa na fisi. Hawezi kuona lolote zuri katika azimio kwa sababu ana beef na mwandishi wake, na hence the only way he can deal with it ni kuli dismiss kama waste of time na kuwakumbatia kama mashujaa, wale ambao waliwezesha kufutwa kwake. They fought his battle for him. Ukimuuliza juu ya matatizo yaliyopo hivi sasa katika uongozi anasema ni kwa sababu hatujui tulikotoka na tunakwenda wapi. Azimio lilitupa dira walioizima dira hiyo, ambao William anawashabikia, hivi sasa wanaitafuna nchi karibia ibaki mfupa tu, yeye anaona it is fine as long as it does away with Mwalimu's legacy. Hence thread yake ya kumsifia Mkapa na ubinafsishaji wake. Halafu kilichonistua zaidi ni kwamba kama hawa ndio viongozi vijana tunaowategemea kutuelekeza karne ya 21 then we are doomed. Lakini kwa angalizo tu, yeyote anayepambana na Julius Nyerere anapambana na historia. Tumeona wamekuja hapa JF vijana wa Kikwete, akina FF, etc. wakijaribu kupaka tope legacy ya Mwalimu lakini wakapambana na akina Nguruvi3, akina Kigarama akina Mag3, mwisho wake wameishia kubadili majina tu.
 
Huyu jamaa anajichanganya sana. Mara Jefferson na UN,mara Jefferson alikuwa mnafiki juu ya kupiga marufuku utumwa,kwavile alikuwa ana watumwa nyumbani kwake. Mara Jefferson ana asili ya Ufaransa. Yote hayo anasahau kutoa facts za ni kwa vipi Azimio la Arusha limetufikisha hapa. Na je ni yapi ya kujivunia kutoka kwenye mbadala wa azimio?

Kuna mambo mawili naanza kufikiri juu ya mkuu W. J. Malecela: moja,pengine anakuwa mbishi kama njia ya kujifunza na kuelewa juu ya Azimio. Jambo la pili ni pengine jamaa anakuwa mbishi kwavile haelewi anachokibishia,anabishia nini?

Le Mutuz,naomba nimalize kwa kurudia tena,azimio halikuwa perfect kwa 100%,ila kwa uhakika nakwambia lilikuwa na bado lina relevance kwa taifa letu kuliko haya "maazimio" tuliyo nayo sasa. Kama wataka mema kwa taifa letu kwa kikazi hiki na vijavyo,tujadili ni yapi ya kuchukua kutoka kwenye azimio ili taifa liweze ktwa na dira yenye kuendana na mazingira yetu,si dira zinazotengenezwa Washington, New York na Geneva.

- Ulianza vizuri na hoja sasa umeanza personal, vipi mkuu lets stick kwenye hoja, sihitaji kukujadili wewe nanajadili taifa!

William.
 
Mimi nadhani tatizo la William, na hili ameshaligusia awali kwingineko, ni kumkubali Julius Nyerere. He has a personal beef with Mwalimu. After all, hata kama mimi mtu angeandika kitabu juu ya baba yangu ambacho kinaonyesha madhaifu yake, halafu mtu huyo awe mkubwa na mwenye ushawishi kama Julius Nyerere, sijui ningejisikiaje. William amekiri kuwa hajasoma azimio la Arusha, na wakati huo huo anasema lilikuwa ni waste of time, badala ya kutoa uchambuzi ni wapi azimio lilikuwa na kasoro anatuambia watu waliliwa na fisi. Hawezi kuona lolote zuri katika azimio kwa sababu ana beef na mwandishi wake, na hence the only way he can deal with it ni kuli dismiss kama waste of time na kuwakumbatia kama mashujaa, wale ambao waliwezesha kufutwa kwake. They fought his battle for him. Ukimuuliza juu ya matatizo yaliyopo hivi sasa katika uongozi anasema ni kwa sababu hatujui tulikotoka na tunakwenda wapi. Azimio lilitupa dira walioizima dira hiyo, ambao William anawashabikia, hivi sasa wanaitafuna nchi karibia ibaki mfupa tu, yeye anaona it is fine as long as it does away with Mwalimu's legacy. Hence thread yake ya kumsifia Mkapa na ubinafsishaji wake. Halafu kilichonistua zaidi ni kwamba kama hawa ndio viongozi vijana tunaowategemea kutuelekeza karne ya 21 then we are doomed. Lakini kwa angalizo tu, yeyote anayepambana na Julius Nyerere anapambana na historia. Tumeona wamekuja hapa JF vijana wa Kikwete, akina FF, etc. wakijaribu kupaka tope legacy ya Mwalimu lakini wakapambana na akina Nguruvi3, akina Kigarama akina Mag3, mwisho wake wameishia kubadili majina tu.

- Mkuu Jasusi, kuna mahali ulisema uko out, sasa umeingia perosnal, kichwa cha mada ni Azimio la Arusha how we were wrong, sina uhakika ya Mwalimu an vitabu vya baba yametokea wapi, kama huna hoja tena ni bora kukaa pemebeni kuliko speculations bila FCATS, siwezi kuwa na beef na Mwalimu ambaye wala simjui na nothing to do na my level, please kama umeishiwa hoja sio vibaya ukakaa pembeni, huwa sijadili watu mara nyingi sana najaribu kujadili hoja tu za taifa!

William.
 
William,
Ungesema waliliwa na simba hapo ningekusikiliza kwa sababu kesi za watu kuliwa na simba mpaka sasa zipo huko Ruvuma. Lakini kwa kawaida fisi hali mtu aliye hai. Try another myth.

- For sure huwafahamu sana fisi, sio wote wanaofanana mkuu, labda wa Musoma ni tofauti na wa Dodoma!

William.
 
Mimi nadhani tatizo la William, na hili ameshaligusia awali kwingineko, ni kumkubali Julius Nyerere. He has a personal beef with Mwalimu. After all, hata kama mimi mtu angeandika kitabu juu ya baba yangu ambacho kinaonyesha madhaifu yake, halafu mtu huyo awe mkubwa na mwenye ushawishi kama Julius Nyerere, sijui ningejisikiaje. William amekiri kuwa hajasoma azimio la Arusha, na wakati huo huo anasema lilikuwa ni waste of time, badala ya kutoa uchambuzi ni wapi azimio lilikuwa na kasoro anatuambia watu waliliwa na fisi. Hawezi kuona lolote zuri katika azimio kwa sababu ana beef na mwandishi wake, na hence the only way he can deal with it ni kuli dismiss kama waste of time na kuwakumbatia kama mashujaa, wale ambao waliwezesha kufutwa kwake. They fought his battle for him. Ukimuuliza juu ya matatizo yaliyopo hivi sasa katika uongozi anasema ni kwa sababu hatujui tulikotoka na tunakwenda wapi. Azimio lilitupa dira walioizima dira hiyo, ambao William anawashabikia, hivi sasa wanaitafuna nchi karibia ibaki mfupa tu, yeye anaona it is fine as long as it does away with Mwalimu's legacy. Hence thread yake ya kumsifia Mkapa na ubinafsishaji wake. Halafu kilichonistua zaidi ni kwamba kama hawa ndio viongozi vijana tunaowategemea kutuelekeza karne ya 21 then we are doomed. Lakini kwa angalizo tu, yeyote anayepambana na Julius Nyerere anapambana na historia. Tumeona wamekuja hapa JF vijana wa Kikwete, akina FF, etc. wakijaribu kupaka tope legacy ya Mwalimu lakini wakapambana na akina Nguruvi3, akina Kigarama akina Mag3, mwisho wake wameishia kubadili majina tu.

Umemsahau Ngongo ha ha ha ha ha.
 
W. J. Malecela. Vyema.

Umeshajiuliza hayo maneno mazuri kuyasoma kwanini hayakutekelezeka?
Wewe umeleta suala la Jefferson,hivi unajua ni kwa muda gani hiyo declaration imeanza kuleta matunda? Azimio limedumu kwa miaka 19 tu,lakini licha ya changamoto za hapa na pale,taifa liliweza kuwa na viwanda vya kusaidia wakulima wa pamba,korosho na mkonge. Liliweza kuleta uwajibikaji,watumishi wa umma walikuwa waoga kuiba mali za umma,hata walioiba ilikuwa sio katika kiwango cha sasa. Ambapo wizi wa mali za umma upo waziwazi. Azimio kwa kipindi hicho kifupi liliweza kujenga misingi,ambayo kwa hakika kama Azimio la Zanzibar lingeweza kubeba misingi mizuri ya Azimio la Arusha,taifa lingekuwa limepiga hatua.

Tungefanya blending kidogo,lakini taifa likaamua kuingia mazima kwenye ubepari. Na sasa taifa linapiga nyimbo za kijamaa huku likicheza kibepari. Matokeo yake ndiyo haya:badala ya kusonga mbele tunarudi nyuma,vilivyokuwa viwanda vya korosho vimegeuzwa kwa matumizi mengine. Wakulima wa korosho wako hoi,huku wahindi wanao-export korosho hizo wakizidi kutajirika.

Pia mkuu, kuna jambo moja ambalo mimi uwa naamini aidha Mwalimu hakuwa mwalimu mzuri katika kufundisha falsafa zake au wanafunzi wake enzi hizo hawakuwa waelewa. Ndiyo pengine ikawa ni rahisi kwao kulitupia mbali azimio. Sasa taifa lina wasomi ambao wanaelewa falsafa za Mwalimu vyema kabisa. Na kwa kuwatumia hao,taifa laweza amua kuzipitia upya falsafa hizo katika msingi wa kutumia mazuri ya azimio na kuyaweka katika mazingira ya sasa.

Ndio maana mkuu Mchambuzi alikwambia mambo ya NIA, MCHAKATO na MATOKEO ya azimio. Kama umekiri azimio lina mambo mazuri kuyasoma,hauoni lilikuwa na NIA nzuri?

- Ahagaaaahhh, jamani kwa nini nipoteze muda wangu kusoma Azimio, ambalo limtufikisha hapa Tanzania tulipo kwama?
I mean Azimo ndio hasa chanzo cha confusion tuliyonayo hili taifa, siamini kwamba kuna anything good kwenye Azimio zaidi tu ya a myth, kweli Azimio lilijenga Viwanda halafu Azimio hilo hilo likaviua kwa kuingiza saisa kwenye uchumi, sasa mimi nilisome sasa ili linisaidie nini jamani na huku madhara yake nayaona kwa macho yangu kila mahali hapa bongo?

William.
 
Back
Top Bottom