Baada ya Changamoto uwezo wangu wa akili umepungua

Baada ya Changamoto uwezo wangu wa akili umepungua

Mrs Gudman

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2015
Posts
613
Reaction score
1,297
Habari Wana Jamii Forum

Nianze Kwa historia kidogo ,

Takribani miaka minne iliyopita nilikuwa napitia vipindi vigumu sana Kwa sababu nilimpoteza mwenzangu, malezi na majukumu kuniwia mengi

Kutoka kwenye hali ya kutokujishughulisha kivile (kama mjuavyo wadada wamama wa Kiafrika ukiwa na mwanaume kuna majukumu automatically anayasimamia yeye na wewe Kuna majukumu Yako) mpaka kwenye hali ambayo Kila kitu kinakuangalia alafu Wakati huo huo nilikuwa nalea ,alafu Wakati huo huo nilikuwa nasimamia miradi yangu na kazi pia nilijikuta nafanya mambo makubwa peke yangu ambayo sikuwahi kufanya before bila msaada wa mtu wa karibu.

Imagine naenda Kazini ,natoka Kazini naenda Biasharani ,natoka Biasharani naenda site nikifika site nasikiliza matatizo mara nimeibiwa mara Sijui kitu gani kimeisha (Wakati mwingine nimeishiwa) nikitoka naenda nyumbani mara mtoto anaumwa mara Sijui kimepanda kimeshuka ,nikajikuta Nina tumia akili yangu kupita kiasi kitu ambacho sikuzoea hapo mwanzo .

Ule Wakati ulipita salama maumivu yakaisha, shughuli zangu zikaenda vizuri lakini nimebaki na tatizo, tatizo lenyewe ni kusahau.

Mimi Nina mdada wa miaka 31 lakini naweza kukutana na mtu ambaye tunafahamiana na nikamsahau completely, naelewa kabisa huyu si mgeni machoni pangu ila nashindwa kumkumbuka jina mpaka nimuulize (siyo wote ila ishatokea Kwa watu wanne)

Napoteza vitu mfano flash, funguo, Hela, nikiwa na Hela ndogo ndogo sikumbuki nilipoweka na mara nyingine zinapotea au kuja kuzikuta siku nyingine.

Sifanyi kazi zangu kwa ufanisi kama mwanzo, mara nyingi kazi zangu zinakuwa na dosari kitu ambacho naonekana nimekuwa mzembe while najijuwa kabisa Mimi siyo mzembe, siyo mvivu Wala nini.

Hayo ni machache tu, naombeni nijue nifanyeje kurudi katika hali yangu ya mwanzo.
 
Pole. Ni muda muafaka wa kutafuta mwenza,ni ishara kubwa single hukuwezi. Wengi hujikaza, na ndio maana humalizia yuko single ,alafu anaenjoy. Kisaikolojia mtu akidai ana kitu fulani sana, kiuhalisia hana hiko kitu.
Olewa na muungwana
 
Pole Sana sister. Jitahidi ujiweke sawa Kwa Sasa na vile vile ni wakati wa kutafuta mwenza wa kuwa naye. Ila tu awe mtu sahihi Ili aweze kukupa furaha Kwa kipindi hiki ulichokuwa mpweke.... Then punguza majukumu yale ambayo hayana ulazima Sana
 
Pole Sana sister. Jitahidi ujiweke sawa Kwa Sasa na vile vile ni wakati wa kutafuta mwenza wa kuwa naye. Ila tu awe mtu sahihi Ili aweze kukupa furaha Kwa kipindi hiki ulichokuwa mpweke.... Then punguza majukumu yale ambayo hayana ulazima Sana
Yupo kwenye tatizo la afya badala ya kutafuta matibabu atafute mwenza? Mimi nashauri nenda clinic za magonjwa ya akili utashauriana na Dr upate dawa gani za kupumzisha akili Ili akili yako ikae sawa.
 
Pole sana ndugu, pole kwa kufiwa na mwenzi wako.

Anza maisha mapya ya mahusiano, fungua moyo na atakayekuja ukaona anafaa mpe nafasi.

Huna changamoto kubwa, ila hakikisha ukiingia kwenye mahusiano ubongo na moyo vifanye kazi pamoja.

Usisahau malezi ya watoto na majukumu yako kikazi na biashara.

Do it just for funny na Wala usiweke matarajio yeyote makubwa.

Utavuka, mimi sioni kama una tatizo lolote zaidi ya Hili.
 
Habari Wana Jamii Forum

Nianze Kwa historia kidogo ,

Takribani miaka minne iliyopita nilikuwa napitia vipindi vigumu sana Kwa sababu nilimpoteza mwenzangu, malezi na majukumu kuniwia mengi

Kutoka kwenye hali ya kutokujishughulisha kivile (kama mjuavyo wadada wamama wa Kiafrika ukiwa na mwanaume kuna majukumu automatically anayasimamia yeye na wewe Kuna majukumu Yako) mpaka kwenye hali ambayo Kila kitu kinakuangalia alafu Wakati huo huo nilikuwa nalea ,alafu Wakati huo huo nilikuwa nasimamia miradi yangu na kazi pia nilijikuta nafanya mambo makubwa peke yangu ambayo sikuwahi kufanya before bila msaada wa mtu wa karibu.

Imagine naenda Kazini ,natoka Kazini naenda Biasharani ,natoka Biasharani naenda site nikifika site nasikiliza matatizo mara nimeibiwa mara Sijui kitu gani kimeisha (Wakati mwingine nimeishiwa) nikitoka naenda nyumbani mara mtoto anaumwa mara Sijui kimepanda kimeshuka ,nikajikuta Nina tumia akili yangu kupita kiasi kitu ambacho sikuzoea hapo mwanzo .

Ule Wakati ulipita salama maumivu yakaisha, shughuli zangu zikaenda vizuri lakini nimebaki na tatizo, tatizo lenyewe ni kusahau.

Mimi Nina mdada wa miaka 31 lakini naweza kukutana na mtu ambaye tunafahamiana na nikamsahau completely, naelewa kabisa huyu si mgeni machoni pangu ila nashindwa kumkumbuka jina mpaka nimuulize (siyo wote ila ishatokea Kwa watu wanne)

Napoteza vitu mfano flash, funguo, Hela, nikiwa na Hela ndogo ndogo sikumbuki nilipoweka na mara nyingine zinapotea au kuja kuzikuta siku nyingine.

Sifanyi kazi zangu kwa ufanisi kama mwanzo, mara nyingi kazi zangu zinakuwa na dosari kitu ambacho naonekana nimekuwa mzembe while najijuwa kabisa Mimi siyo mzembe, siyo mvivu Wala nini.

Hayo ni machache tu, naombeni nijue nifanyeje kurudi katika hali yangu ya mwanzo.
Ni tatizo la wengi hilo na tiba yake ni mapumziko.. Unahitaji complete rest yenye ku refresh mind... Walau kwa mwezi mzima huku ukiwa unafanya yale ya muhimu tuu na ukae mbali na majukumu yote na kati ya hicho kipindi upande siku 3 kamili bila simu bila kelele yoyote bali ni kunywa, kula na kuupa mwili mapumziko kumbukumbu zako zote zitakaa sawa
 
Na mimi nina tatizo kama la kwako siku hizi nasahau sana watu naweza kukutana na mtu ninayemfahamu ila sikumbuki jina wala nilikutana nae wapi, nilichoamua ni kusimama kuvuta bangi na pombe na kuanza kufanya mazoezi, ni wiki ya pili sasa I hope hali yangu itarudi kuwa sana ila tatizo la afya ya akili is real tusichukulie poa.
 
Ubongo ni kama processor ya computer. Ukifungua mafaili mengi kwa wakati mmoja au uka-save mafaili mengi kwenye desktop lazima utaona slow down. Kanuni ni kupata muda wa kulala usingizi, kupita njia tofauti wakati wa kwenda kazini na kurudi nyumbani, kutembea kwa mguu mara kadhaa, kujumuika kanisani, msikitini, n.k. Mwisho kabisa ni kuhakikisha kwamba una mpenzi hata kama hakupatii hela as long as anaweza kukuchakata vizuri.
 
1.Meditation.

2.Achana na hio addiction uliyo nayo(eg.porn,faping)

3.Visit nature(forest, waterbodies)

4.pata usingizi wa kutosha.

5. Punguza matumizi ya simu kupitiliza.

6. Soma vitabu riwaya mbali mbali

7. Have safe sex (frequently). Trust me sex inatuliza akili hasa ikiwa shiriki.

8. Kunywa maji mengi matunda(ndizi,tikiti,papai,nanasi na tango).

The imp
 
Na mimi nina tatizo kama la kwako siku hizi nasahau sana watu naweza kukutana na mtu ninayemfahamu ila sikumbuki jina wala nilikutana nae wapi, nilichoamua ni kusimama kuvuta bangi na pombe na kuanza kufanya mazoezi, ni wiki ya pili sasa I hope hali yangu itarudi kuwa sana ila tatizo la afya ya akili is real tusichukulie poa.
Angalau tatizo lako umelielewa punguza kuvuta bange au acha Kama unaweza pombe nayo punguza maana kuacha sio rahisi
 
Habari Wana Jamii Forum

Nianze Kwa historia kidogo ,

Takribani miaka minne iliyopita nilikuwa napitia vipindi vigumu sana Kwa sababu nilimpoteza mwenzangu, malezi na majukumu kuniwia mengi

Kutoka kwenye hali ya kutokujishughulisha kivile (kama mjuavyo wadada wamama wa Kiafrika ukiwa na mwanaume kuna majukumu automatically anayasimamia yeye na wewe Kuna majukumu Yako) mpaka kwenye hali ambayo Kila kitu kinakuangalia alafu Wakati huo huo nilikuwa nalea ,alafu Wakati huo huo nilikuwa nasimamia miradi yangu na kazi pia nilijikuta nafanya mambo makubwa peke yangu ambayo sikuwahi kufanya before bila msaada wa mtu wa karibu.

Imagine naenda Kazini ,natoka Kazini naenda Biasharani ,natoka Biasharani naenda site nikifika site nasikiliza matatizo mara nimeibiwa mara Sijui kitu gani kimeisha (Wakati mwingine nimeishiwa) nikitoka naenda nyumbani mara mtoto anaumwa mara Sijui kimepanda kimeshuka ,nikajikuta Nina tumia akili yangu kupita kiasi kitu ambacho sikuzoea hapo mwanzo .

Ule Wakati ulipita salama maumivu yakaisha, shughuli zangu zikaenda vizuri lakini nimebaki na tatizo, tatizo lenyewe ni kusahau.

Mimi Nina mdada wa miaka 31 lakini naweza kukutana na mtu ambaye tunafahamiana na nikamsahau completely, naelewa kabisa huyu si mgeni machoni pangu ila nashindwa kumkumbuka jina mpaka nimuulize (siyo wote ila ishatokea Kwa watu wanne)

Napoteza vitu mfano flash, funguo, Hela, nikiwa na Hela ndogo ndogo sikumbuki nilipoweka na mara nyingine zinapotea au kuja kuzikuta siku nyingine.

Sifanyi kazi zangu kwa ufanisi kama mwanzo, mara nyingi kazi zangu zinakuwa na dosari kitu ambacho naonekana nimekuwa mzembe while najijuwa kabisa Mimi siyo mzembe, siyo mvivu Wala nini.

Hayo ni machache tu, naombeni nijue nifanyeje kurudi katika hali yangu ya mwanzo.
Nimeona hapo maoni mengi ya wadau ni mazuri na mengine nakubaliana nayo,tafuta mwenza yote hayo yatakaa sawa,
 
Pole. Ni muda muafaka wa kutafuta mwenza,ni ishara kubwa single hukuwezi. Wengi hujikaza, na ndio maana humalizia yuko single ,alafu anaenjoy. Kisaikolojia mtu akidai ana kitu fulani sana, kiuhalisia hana hiko kitu.
Olewa na muungwana
Asante Kwa ushauri nilishaolewa Toka mwaka Jana , I am very happy ila tatizo langu halijaisha
 
Ubongo ni kama processor ya computer. Ukifungua mafaili mengi kwa wakati mmoja au uka-save mafaili mengi kwenye desktop lazima utaona slow down. Kanuni ni kupata muda wa kulala usingizi, kupita njia tofauti wakati wa kwenda kazini na kurudi nyumbani, kutembea kwa mguu mara kadhaa, kujumuika kanisani, msikitini, n.k. Mwisho kabisa ni kuhakikisha kwamba una mpenzi hata kama hakupatii hela as long as anaweza kukuchakata vizuri.
Kwa sasa Nina mume ,nimeolewa mwaka Jana December
 
Ni tatizo la wengi hilo na tiba yake ni mapumziko.. Unahitaji complete rest yenye ku refresh mind... Walau kwa mwezi mzima huku ukiwa unafanya yale ya muhimu tuu na ukae mbali na majukumu yote na kati ya hicho kipindi upande siku 3 kamili bila simu bila kelele yoyote bali ni kunywa, kula na kuupa mwili mapumziko kumbukumbu zako zote zitakaa sawa
True inatakiwa afanye disc formation yaani aanze upya.Afanye rest pia ale virutubisho viongezavyo akili na kumbukumbu,maana amepita kwenye hard time.
Mungu alipoumba wawili alikuwa na makusudio yake.
 
Thamani ya mtu asipokuwepo, unakuta mwanamke mpumbavu umwambia mumewe mwanaume suruari wewe, mbona nilikuwa naishi kabla yako na blah blah kibao.
Mume akiondoka ushinda kwa Mwamposa kumsumbua awarudishie
 
Back
Top Bottom