Baada ya Chikwende Junior Lokosa wa Nigeria ajiunga simba

Baada ya Chikwende Junior Lokosa wa Nigeria ajiunga simba

Tunatofautiana, kwahiyo ungekua wewe ungeanza ubishi? Siyo kueleweshana?
Kwa ulivyoanza tu imeonyesha kabisa unajifanya mjuzi kwa kuelekeza lawama moja kwa moja kuwa kishingo kafukuzwa hii imeonyesha ni mtu wa aina gani ulivyo
 
Dah kama kaondoka mwenyewe hapo sasa ni mtihani. Ila hata hivyo sioni kama simba ilihitaji hawa watu 2.
anachukua dollar 30,000 halafu utakataaje kufundisha morocco ubaki bongo ambapo kuna viwanja vya ajabuajabu?ali post kwenye insta yake kwamba mo na barbra walitumia usiku ule wote kumbebembeleza abaki ila hata familia yake ilitaka ahamie morroco pale si karibu na ulaya?
Flight time ya ubelgiji to morroco ni masaa 3:15 ,belgium to Tanzania ni masaa 10:50 kwanini asiende morocoo sasa sema namuonea huruma pale hataweza kudumu hata miezi mitatu jamaa wanafukuza kama hawana akili na ni team iliyopoteza thamni na ukubwa muda sana mashabiki wake wana hasira vibaya mnoo hawana uvumilivu
Simba ilimsadia sana sababu ndiyo club yake ya kwanza kufundisha na imempa cv kubwa afrika
 
Kwa ulivyoanza tu imeonyesha kabisa unajifanya mjuzi kwa kuelekeza lawama moja kwa moja kuwa kishingo kafukuzwa hii imeonyesha ni mtu wa aina gani ulivyo
Anhaa haya. Ila taarifa ya mwanzo kabisa juu ya kuondoka kwa kocha iliyokuja jf ilisema simba ndiyo waliamua mkataba ufe. Kama baadaye ilidhihirika haiko hivyo mimi sikujua hilo swala.
 
tusubiri tuone ndiyo maana wamempa miezi sita haya mambo sa ingine ni gamble sana, sarpong alikuwa tishio rwanda, balinya, mugalu,serunkuma,mavugo walikuja hapa na rekodi za kutisha ila wakati mwingine inakuwa chenga unayemtrajia anakuangusha usiyetarajia inakua maajabu kama okwi ilivyokuwa
Kuna tatizo la kupigana misumari hilo usisahau pia
 
Ni kama Saido alivyokataa na ss ana flop. Juzi almanusra Kakolanya amuumbue kwenye p shootout.
Wewe mpira haujui kashabikie rede tu. Kwahiyo Kakolanya angedaka penati ndio ingekuwa kuumbuka kwa Saidioo kuanza ku flop?. Kwahiyo Kagere na Onyango wameflop kwavile wamekosa penati? Hata Mesi na Ronaldo hawawezi kutamba kila siku. Kuna siku wanakuwa na siku mbaya. Tuje bongo tena. Chama na Luis kuna siku game zinawakataga.

Embu tupe statistic za Saido zinaonesha kuwa kweli ameanza kufliop sasa
 
Chikwende kutufunga goli moja tu tumemsajili
shida ya simba ukitoa luis na dilunga kidogo ni kwamba wakiingia kwenye 18 ya adui speed siyo kubwa sasa unamuachaje chikwende,hata kabla ya mechi ya simba yeye ndiye aliwavusha platnum kwa ud songo alishawahi kuwagonga pirates orlando goal mbili na yuko team ya taifa zimbabwe
umesahau kuna wachezaji walionekana kwenye mapinduzi na sportspesa kama kina fei toto? unakumbuka samatta aliendaje tp mazembe?si ni ile mechi ya dar esalaam ya 3-2?cha ajabu nini sasa?tena mashabiki walimpigia kelele moise katumbi ikabidi amchukue ili kuwaridhisha mashabiki
 
Nashangaa bwalya na mugalu walikuja kichwakichwa ila hao wanigeria balaaa ingawa kwasi wa ghana naye misumari ilikolea akapotea au balinya alichofanyiwa yanga
Mugalu alianza na balaa sana pale Simba, kila akiingia sub anatupia tu kila akiingia nyavu mpaka mashabiki wakatamani apewe dakika nyingi. Sasa hivi anaonekana moja ya magarasa dah mpira wa bongo aisee mchezaji usipojipanga hauuwezi kuucheza. Unaona princess dube wa Azam saivi kimya.

Nakumbuka misimu miwili iliyopita Miraji aring'ara sana dogo pindi yupo uchebe kama kocha na Boko akiwa majeruhi. Dogo nyota iling'ara kisha ikafifia mazima mpaka leo hii kuja kuibukia kwenye mapinduzi. Sasa fikiria sasa anaongezeka straika mwingine kutoka naijeria hapo nyasi zitawaka mzee
 
Anhaa haya. Ila taarifa ya mwanzo kabisa juu ya kuondoka kwa kocha iliyokuja jf ilisema simba ndiyo waliamua mkataba ufe. Kama baadaye ilidhihirika haiko hivyo mimi sikujua hilo swala.

Kocha toka mwanzo alikuwa anatafutiwa timing ya kupigwa chini, hivyo naye akawa anatafuta timu kimya kimya.

At the same time, mkataba ulikuwa umeisha na Simba hawakutaka kufika bei. Hivyo akaamua aondoke.
 
Anhaa haya. Ila taarifa ya mwanzo kabisa juu ya kuondoka kwa kocha iliyokuja jf ilisema simba ndiyo waliamua mkataba ufe. Kama baadaye ilidhihirika haiko hivyo mimi sikujua hilo swala.
sasa unaokota info mitandaoni halafu unakuja kuvimbia watu humu
 
kishingo hajafukuzwa kaka morroco anapata mshahara mara tatu aliokuwa anapata simba na ni karibu na ubelgiji hata family yake kumfata ni rahisi na league ya morroco ni kubwa na tajiri kuliko yetu alitaka kuondoka mwenyewe,hayo mengine sikubishii lakini tangu lini kocha bongo akasema namtaka mchezaji fulani kalatewa?labda wa kibongo hawa wa milioni 30 kuna kipindi uchebe alimtaka Justin shonga wakaambiwa bei milioni 800 story iliishia hapohapo
Bongo kocha anasema nataka kiungo,beki,mshambuliaji analetewa yoyote ndiyo maana wanakuja ma free agents au cheap wa kutoka burundi ,kenya , congo zimbabwe zambia
hawa mashabiki mandazi utadhani wanachangia hata mia kazi kupiga mikelele tu. wanajua bei ya hao wachezaji hatari?
 
takwimu zake siyo mbaya naangalia comments za wanigeria kwenye hiyo page wanasema ni striker mzuri,simba walitaka wamfanyie majaribio akakataa nahisi ndiyo maana kapewa mkataba wa miezi 6 alikaa muda bila team
Ni Morrison mwingine.
 
shida ya simba ukitoa luis na dilunga kidogo ni kwamba wakiingia kwenye 18 ya adui speed siyo kubwa sasa unamuachaje chikwende,hata kabla ya mechi ya simba yeye ndiye aliwavusha platnum kwa ud songo alishawahi kuwagonga pirates orlando goal mbili na yuko team ya taifa zimbabwe
umesahau kuna wachezaji walionekana kwenye mapinduzi na sportspesa kama kina fei toto? unakumbuka samatta aliendaje tp mazembe?si ni ile mechi ya dar esalaam ya 3-2?cha ajabu nini sasa?tena mashabiki walimpigia kelele moise katumbi ikabidi amchukue ili kuwaridhisha mashabiki

Sikubaliani na wewe...

Kuhusu fei toto yanga walicheza bahati nasibu kwa bahati nzuri ilitiki kwa upande wao na isitoshe dogo alionyesha ana potential kulingana na umri wake.

Kuhusu mbwana sammata kwenda mazembe ni kweli zile mechi mbili za dar na Lubumbashi zilichangia Sana usajili wake kwenda mazembe lakini mazembe wenzetu ni wajanja na si wakurupukaji km Sisi kwani walichukua tahadhari Kwanza kwa kumpeleka kikosi cha akiba Kwanza ili athibitishe uwezo wake ndyo aingie timu kubwa.

Simba kwa chikwende wamecheza bahati nasibu,all in all tusubiri muda ndyo utakaohukumu
 
Back
Top Bottom