Uchaguzi 2020 Baada ya Dkt. Kigwangalla kujibizana na Mo Dewji Twitter. Dkt. Bashiru amshukia Kigwangalla, amtaka am-tweet Dkt. Magufuli

Uchaguzi 2020 Baada ya Dkt. Kigwangalla kujibizana na Mo Dewji Twitter. Dkt. Bashiru amshukia Kigwangalla, amtaka am-tweet Dkt. Magufuli

Yeah I agree but lets blame the system for that the Individuals are willing to use English but the system of our education couldn't prepare them effectively
Ndicho alichozungumza LISSU tujadiliane kuhusu mfumo wetu wa elimu maana hauleweki kabisa
 
Mimi Sina elimu yeyote ni haki yangu kuchapia,[emoji16][emoji16][emoji16] ila Dr kuandika kingereza kibovu vile ni aibu kwa Taifa na waliomchagua kuwa waziri.
Sasa kama huna elimu yoyote ujasiri wa kukosoa umeupata wapi ? Umeoteshwa nini ?

Nani amekwambia ya kuwa mjinga anatakiwa achapie ? Hivi huoni kama mjinga naye hupenda kuambiwa ana elimu ?

Sasa uache uongo. Lakini nani alikwambia Tabibu lazima ajue Kiingereza ? Ukizingatia ya kuwa Lugha hiyo si lugha yake mama ?
 
Yaani kuanzia kidato cha kwanza Hadi PhD umesoma kwa kimombo Kisha usijue kukiongea?hio ndio tunaita elimu ya kukaririshwa
Siyo kweli, utajuaje kiingereza hali ya kuwa ni Lugha ya kufundishia tu ?

Labda nikuulize, wewe ulizaliwa unajua Kiswahili ? Imekuwaje ukajua Kiswahili ? Sasa huwezi kumlaumi mtu au kumshangaa mtu hajui Kiingereza hali ya kuwa lugha husika si Lugha ya kwanza ya mtu husika.

Pili, kuelewa mambo kuna njia nyingi sana, hasa kuyafanyia kazi mambo hayo. Kwahiyo naweza kuyaelewa mambo hata kama mambo hayo si kwa lugha yangu, na hili liko wazi na mimi ni shuhuda wa hilo. Ulitakiwa ujue Elimu ni nini kisha ujadili hili.
 
Yaani kuanzia kidato cha kwanza Hadi PhD umesoma kwa kimombo Kisha usijue kukiongea?hio ndio tunaita elimu ya kukaririshwa
Hivi ushawahi kusoma masomo ya lugha fulani kama fani ?

Kwenye masomo mengine tunasoma kwa Kiingereza ila yaani matumizi ya lugha hiyo, ila hatusomi kama fani.

Ili uijue lugha fulani lazima uchukue muda mrefu na ukae na watu wanao zungumza lugha hiyo muda wote, ila kinyume na hapo huwezi kuijua lugha hiyo kwa kuiongea.
 
Hivi ushawahi kusoma masomo ya lugha fulani kama fani ?

Kwenye masomo mengine tunasoma kwa Kiingereza ila yaani matumizi ya lugha hiyo, ila hatusomi kama fani.

Ili uijue lugha fulani lazima uchukue muda mrefu na ukae na watu wanao zungumza lugha hiyo muda wote, ila kinyume na hapo huwezi kuijua lugha hiyo kwa kuiongea.
Ndiyo nakubaliana na wewe Mimi siwezi kushangaa mtu kuwa na elimu na asijue kuongea kiingereza VP kama angekuwa bubu je ungemuweka kundi hilo pia?

Kiingereza waweza jifunza mtu yeyote ukitaka tunachohitaji ni taaluma siyo lugha
 
Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally amemtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamisi Kigwangalla kumzungumzia Mgombea wa Urais wa CCM, Dkt. Magufuli badala ya kuendelea na malumbano yake yanayohusu mpira dhidi ya Mmiliki wa Simba SC, Mohammed Dewji.

Dkt. Bashiru amaema“Naona Hamis Kigwangalla yupo mitandaoni kujibizana na Mohammed Dewji mambo ya mipira, tupo kwenye uchaguzi. Nataka nione ana-tweet na wafuasi wake namna Mwenyekiti na Mgombea Urais wetu atakavyoshinda.”

Ameongeza, “Siingilii maisha binafsi, hakuna maisha binafsi unapokuwa mgombea wa CCM".

Dkt. Kigwangalla na Mo Dewji walianza kujibishana mtandaoni baada ya Kigwangalla kuhoji namna alivyopatikana CEO mpya wa Simba ambaye anaelewa kuwa PA wa Mo Dewji.

Katika kujibu hoja hiyo Mo aliendelea hadi kumuomba msamaha Waziri Kigwangalla kutokana na mkopo wa pikipiki kutofanikiwa (hali iliyotafrisiwa kuwa Mo anadhani Kigwangalla anafanya hivyo kutokana na kunyimwa mkopo).

Hata hivyo, Kigwangalla aliendelea na kusema mkopo hauhusianj bali tu yeye anahoji kama Mwanachama wa Klabu ya Simba. Aliweka bayana barua pepe aliyoombea mkopo wa pikipiki na pia alionesha tweet zake za nyuma ambazo pia alikuwa a ahoji mambo kadhaa ndani ya Simba.


Huu mchezo umemgharimu Hamisi
 
Lakini huu mchezo ulikuwa unaleta watalii pamoja na covid..waliendelea kufurika. Wamemuonea tu jamaa.[emoji3][emoji3]
 
Hivi anaweza kuwa kakosa uwaziri kisa mwamedi? Sidhani, mwamedi nae mjanja mjanja sana inabidi wawepo majasiri kina Kigwangala kumuhoji maswali magumu
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Bashiru Ally mchana wa leo ametoa maelekezo kwa wagombea wa Ubunge kubaki katika maeneo yao ya jimbo na kufuata maelekezo na taratibu zilizopangwa na Kamati za Siasa za Wilaya husika.

Katibu Mkuu amewataka wabunge kuzingatia ratiba za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na ratiba za Kamati za Siasa za Wilaya kuungana na Viongozi wengine kuwatafutia Kura wagombea Udiwani pamoja na kumuombea Kura mgombea Urais wa CCM Ndugu John Pombe Magufuli.

Sambamba na maelekezo hayo, amewataka wabunge kutumia mitandao ya kijamii katika kutafuta kura za Chama Cha Mapinduzi kwa kufafanua ilani yetu ya Chama kwa mwaka 2020- 2025 kwa kuwaeleza wananchi kipi kimetekelezwa na kipi tunatarajia kukitekeleza pamoja na kuhamasisha wananchi kwenda kupiga kura siku ya tarehe 28 Oktoba 2020.

Nidhamu ya Chama inatuongoza kusikiliza maelekezo ya Viongozi wetu na bila kinyongo kuyatii na kujisahihisha.

Tunasema tumesikia na tumetii...!

View attachment 1560618View attachment 1560618View attachment 1560620

Kumekuch a tena
 
Back
Top Bottom