Baada ya Dr. Slaa kufunua nyongeza; Sheria ya "mbwembwe" ni batili?

Baada ya Dr. Slaa kufunua nyongeza; Sheria ya "mbwembwe" ni batili?

Napata shida kuamini kwamba "Muungwana" hakuusika na nyongeza ya kipengele cha 7(3).) Ninukuu kipengere chenyewe:
7(3)For the purposes of subsection (2), "campaign team" means a group of' persons formed by a candidate in the nomination process or a contested election for purpose' of presenting or assisting that candidate in the election campaigns, who have been approved-
(a) in the case of a Presidential candidate, by the Registrar;
(b) in the case of a Member of Parliament, by the District Administrative Secretary; and
(c) in the case of a Councilor, by the Ward Executive Officer.
Source:Election expences Act 2010.

Ukicheck vipengere (a) na (b) ina maana Rais mpaka anasaini halikua hajui kwamba timu yake ya kampeni inatakiwa kupitishwa na Msajili wa vyama? ukija kipengere (b) Ingewezekanaje DAS afanye kazi ya kupitishatisha timu ya kampeni ya mbunge/wabunge wa eneo lake bila Mwenyekiti wa chama husika kutojua(Rais ni mwenyekiti wa chama kimojawapo) Uyo DAS anateuliwa na nani?Hata kama DAS ana WEO wapo chini ya TAMISEMI-je waziri husika wa TAMISEMI anaweza kufanya jambo bila kumuhusisha bosi wake?

Nionavyo hiki kipengele walikiongeza makusudi kupata information za wabunge na wapambe wao ili kuwabana kisiasa. "Muungwana" kuonyesha amefura ni harakati zake kisanii za kujiengua na haibu wakati ni muhusika.Pili siamini kama ofisi ya AG wanaweza kuongeza icho kipengere bila maagizo kutoka juu.Kama amefura AG anasubiri nini kujiengua?

Mawazo yako ni mazuri lakini yameingia doa........... kiswahili cha kingumbaru...
.
 
BAADA ya Mbunge wa Karatu (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa kuibana serikali kuhusu vipengele vilivyoongezwa kinyemela katika muswada uliosaniwa na Rais Jakaya Kikwete kwa mbwembwe wiki iliyopita, taarifa mpya zinasema Rais amefura, akitaka maelezo ya kina ya walioingiza vipengele hivyo.
Tanzania Daima lilipozungumza na mmoja wa wasaidizi wa Rais Kikwete kuhusu sakata hilo jana, alidokeza kwa maneno machache, na kwa msisitizo, akisema: “Rais amefura.”
Kwa habari zaidi, Soma Tanzania Daima.

Kuna wakati nilisema kuwa Dr Slaa ni kati ya watu watatu katika nchi hii wanaohitaji kupewa tuzo ya heshima. Huyu mtu anajali na kuipenda sana nchi yetu. Ukiangalia kwa ukaribu utagundua kuwa anaongoza nchi hii, ndiyo kama rais.
 
FP.. kama kweli tatizo ni wasaidizi mbona hakuna aliiyewahi kuwajibishwa hadi hivi sasa? wanasema the "buck stops with the president". Kama watu walioboronga miaka minne chini ya uongozi wake ndio hao hao wanaendelea kuboronga na yeye anajua wanaboronga (case in point suala la cheki, magari, mtumbwi, helikopta, ) kwanini hakuna aliyebadilishwa? Sheria yenyewe siyo ngumu kiasi hicho na haina kurasa nyingine na kutokana na umuhimu wake angejaribu hata kukaa chini na kusikiliza opposite opinion (mimi nilielezea ubaya wake kwenye Star TV na wengine wamefanya kwa njia tofauti).

Tatizo yeye kajizungusha na watu wanaoimba sifa zake na wanaomshangilia kwa vigelegele hana mtu ambaye anamwambia kitu tofauti. Kikuungua ndio tunatakiwa kulalamikia wasaidizi. No sir.. kwa sababu yeye ndiye aliyoipigia debe sheria hii kwa mbwembwe yeye ndiyo ale uchungu wake.

Mkuu kuna baadhi ya watanzania Kikwete yeye ni malaika wakati wote, hakosei. Hata yeye hataki kuonekana kama huwa anakosea. Mimi naamini kuwa kipengele kiliingizwa makusudi, tumshukuru Dr. Slaa aliyeweka nchi katika moyo wake, anaiongoza nchi hii, ndiyo kama rais wetu.

Kipengele hiki kina uhusiano na juhudi zilizokwishaanza za kuzuia wanachama wa CCM kumkabili JK kwenye uchaguzi. Nadhani pia Dr. Slaa anaonekana ni tishio kwenye uchaguzi ujao. Sasa hapo rais ni yupi, anayesaini bila kusoma sheria, au anayefanya kazi kama rais kuhakikisha kuwa nchi inaendeshwa kwa misingi ya sheria za haki? Tumpe haki yake Dr Slaa anayositahili kuiongoza nchi hii octoba 2010.
 
wadau mimi nilikuwa sijasoma gazeti la Tanzania Daima, kweli hii ishu imetokea, lakini sioni kama kweli raisi alikuwa halijui hili, maana yake ni kwamba yeye hajui kama kwenye bunge hicho kipengele hakikujadiliwa so asingeweza just from no where agundue hilo, kwa mantiki hii mimi namtetea Mr. President, has got nothing wrong done, waliofanya vibaya ni waale kwa makusudi yao binafsi wamepindisha ukweli wa kipengele chenyewe
Kwa nini asaini kitu asichokijua
 
Jamani nipeni shule. JK ana kosa gani? kweli mnataka rais achukue ORIGINOL (iliyopelekwa bungeni) kisha alinganishe na anaotaka kusaini (mpya)!!! come on naona tunazidi kumlaumu sasa.

Prezidaa ana wasaidizi kibao wa kuweza kufanya kazi hiyo.

Mnyonge mnyongeeni ila haki yake mpeni

wadau mimi nilikuwa sijasoma gazeti la Tanzania Daima, kweli hii ishu imetokea, lakini sioni kama kweli raisi alikuwa halijui hili, maana yake ni kwamba yeye hajui kama kwenye bunge hicho kipengele hakikujadiliwa so asingeweza just from no where agundue hilo, kwa mantiki hii mimi namtetea Mr. President, has got nothing wrong done, waliofanya vibaya ni waale kwa makusudi yao binafsi wamepindisha ukweli wa kipengele chenyewe
Type ya watu kama nyie ndiyo aina ya wasidizi alionao Mkulu wanamwambia mambo poa tu mzee kanyaga twende, sasa mfano Kabuche1077 na FairPlayer wawe washauri wa rais kwa mambo ya bunge na katiba na wanashauri hivi wanavyosema na mkulu anawaamini taifa litegemee nini
 
Hivi, kuna ugumu gani kwa Mh Kikwete kuchukua msimamo wa kutovumilia utendaji usioridhisha? Ingekuwa ni mtu mdogo kwenye ofisi ya umma kafanya kakosa kadogo angeshatimuliwa tena kwa mbwembwe!!

Kinachohitajika hapa ni yeye kuchukua hatua juu ya mzembe MMOJA TU kati ya hao wengi wanaomzunguka na wengine watashika adabu.

Yaani napata hisia ya kumtingisha, labda kalala ataamka!!
 
Dr. Slaa yuko sahii hapa, hawa wakuu wamefanya makosa, hakuna haja ya ku SPIN, badala yake ni kukubali makosa na kurekebisha hiyo sheria. Kikubwa zaidi ni kujifunza ili makosa kama hayo yasifanyike tena huko mbeleni. Ndio maana wenzetu walioendelea, huunda tume ili kugundua kwanini makosa yamefanyika na kisha kuziba mianya ili yasifanyike tena.

Inaudhi unapoona watu wanajaribu ku SPIN hata pale walipokosea, why? Kila mtu anakosea na muhimu ni kujifunza ili kuepuka makosa kama hayo.

Dk Slaa awashukia Spika Sitta na Werema
Hemed Kivuyo, Arusha

MBUNGE wa Karatu Dk Wilbrod Slaa, amewashukia spika wa bunge, Samuel Sitta na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Warema kuhusu rais kudanganywa katika sheria ya matumizi ya fedha katika uchaguzi.

Kutokana na hali hiyo,amewataka waache kutoa majibu mepesi kwenye hoja nzito tena bila kufanya utafiti.

Dk Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ametaka sheria hiyo irudishwe bungeni katika kikao cha 19 kinachotarajiwa kuanza Aprili ili kifungu ambacho rais Jakaya Kikwete amekisaini bila kujadiliwa bungeni, kiondolewe.

Katika barua yake aliyomwandikia spika wa bunge kulalamikia kauli hizo, Dk Slaa alisema kifungu hicho namba 7(3) cha sheria ya uchaguzi kimemhadaa rais Kikwete na hivyo kwenda kinyume na demokrasia.

"Hivyo,Naomba Serikali ichukue hatua kuwasilisha "miscellaneous Amendment" katika Mkutano wa 19 yaani Bunge la Aprili, ili kifungu hiki ambacho ni kinyume na demokrasia kiondolewe kwenye aheria ambayo rais ameisaini,"inasema sehemu ya taarifa ya Dk Slaa

"Angelikuwa amesoma Mhe. Spika angelikuwa mwangalifu kutamka aliyoyatamka. Mheshimiwa Spika anakiri kulikuwa na mjadala, lakini hakutamka mjadala ulihusu nini, na wala hakumnukuu mwenyekiti wa siku hiyo ambayo alikuwa Mhe. Naibu Spika alitoa maagizo gani.

"Ni hatari kwa viongozi wetu kutoa matamko kwa mambo mazito bila kufanya utafiti angalau mdogo. Mhe. Spika atakubali kuwa kwenye Hansard, hakuna popote ambako imejadiliwa achilia mbali kukubaliwa kuwa timu ya kampeni itathibitishwa na msajili(kwa mgombea urais) au katibu tawala (kwa mgombea ubunge) au na mtendaji wa kata kwa (mgombea udiwani). Hii ni dhana mpya kabisa, siyo tu haijajadiliwa wala haikufikiriwa kama Hansard inavyoonyesha," alisema Dk Slaa.

Alifafanua kilichokuwa kimejadiliwa katika mjadala huo ni hoja ya mbunge wa Bariadi Mashariki Andrew Chenge ambaye alitaka kufanyia mabadiliko hoja ya mabidiliko kuhusu pendekezo la serikali kwamba kifungu cha 7(2) na alitaka makundi ya sanaa yaingizwe baada ya neno "Voters".

"Hivyo ni vyema naye Spika akiri tu kuwa utaratibu wa kutunga
sheria umekiukwa. Haifai kubishana kwa sababu wakati Hansard ndiyo ushahidi wa wazi wa jambo hilo, anaeleza katika barua hiyo.

Dk Slaa anaeleza kwamba anamwona mwungwana mwanasheria mkuu wa serikali kukiri mapungufu hayo, lakini anasikitishwa na kauli yake kwamba anastushwa na kauli ya Dk Slaa.

"Kwanini mwanasheria mkuu aanze kufikiria siasa badala ya kuchukua Hansard,Bill iliyowasilishwa Bungeni, na kuisoma ili kujua kilichoazimiwa na Bunge. Huu ndio utafiti siyo kukurupuka kujibu mambo mazito, hata kama anatumia nafasi yake ili kuficha makosa yake, hali hii haikubaliki katika dunia ya sasa kwa sababu watu ni waelewa.

"Hivyo,Naomba Serikali ichukue hatua kuwasilisha miscellaneous Amendment" katika ,kutano wa 19 yaani Bunge la Aprili, ili kifungu hiki ambacho ni kinyume na demokrasia kiondolewe kwenye Sheria ambayo Rais ameisaini.

Dk Slaa aliyasema hayo huku akionyesha nakala ya barua aliyomtumia Spika wa Bunge, Samuel Sitta akimtahadharisha kuwa makini na matamshi ambayo amekuwa akitoa mara kwa mara bila kufanya utafiti wa kina. Alisema baadhi ya vyombo vya habari viliwanukuu kwa nyakati tofauti Spika Sitta na Jaji Werema wakisema kuwa hawaamini na hawadhani kama tuhuma hizo zina ukweli na kwamba Dk Slaa anapaswa kuelimishwa zaidi ili kufahamu vifungo hivyo vya sheria ya gharama za uchaguzi na kudai kuwa kauli zao zinakiri na kukataa hivyo kujichanganya .
 
Wasaidizi wanamtesa sana Rais wetu......timuatimua wote unipe mimi unikulu hapo ikulu!!!!
 
Kwa uzembe wa ofisi yake mara kwa mara unaofanywa na wasaidizi aliowateua yeye mwenyewe na kushindwa kuwawajibisha, angefanya jambo moja muhimu ili akumbukwe kama shujaa. ASIJIUZULU ILA ATANGAZE KWA MBWEMBWE KUBWA KWAMBA OCTOBER 2010 HATAGOMBEA TENA KITI HICHO KWA VILE KIMEMSHINDA
 
Huyu bwana hajafura lolote wala nini, he is an artist and comedian just like others. Who knows may be he's the one who ordered them to be inserted!
 
Hii inatoa mwanga kidogo kuona jinsi ambavyo nchi hii inaendeshwa. Ikiwa hivi ndivyo ni sheria ngapi zimeshakuwa doctored namna hii? Mie bado sijaamini na ninasubiri maelezo ya serikali. Fikiria sasa mikataba ya madini, ndo maana inabidi iwe siri!

Haiwezekani kuwa jambo hili (kama kweli limefanyika) lilikuwa limefanyika kwa mara ya kwanza. Sema sasa hivi kuna mtu amejisumbua kuthibitisha kuwa kweli kinachosainiwa ndo kile kile? Na pengine na yeye amepata TIP kutoka kwa watu wanaojua kuwa mambo huwa yanakuwa hivyo! So we know sheria zinatungwa then wale ambao wanahisi kuna kitu ambacho kama wangepekipeleka bungeni kisingepita, wanapata muda wa kukipenyeza, then sheria inatiwa sahihi.

Ingekuwa ni omission ungesema ni typing error, lakini addition? Haiwezekani. Lazima kipengele hiki walishapanga kukitumia mahali. Nchi hii sheria huwa wanatungiwa watu na mazingira fulani tu! Ndo maana sheria nyingi baada ya kutumikia kile ilichotungiwa hubaki bila kutekelezwa na yeyote hata kama zinavunjwa kila siku!
 
Jamani kama kuna mambo ambayo mimi binafsi huwa yananiudhi ni lack of seriousness and censorship on the part of our Accounting officers in the government. Ukienda hata kwenye maonesho yao pale mnazi mmoja au Karimjee documents nyingi hazifanyiwi editing hata kidogo. Sasa kama hilo la cheque kweli wameshindwa kuliona hilo kama siyo uzembe ni nini?
 
Hapa wakuu hakuna kutafuna meno mengi yalishasemwa kuwa hatuna uongozi na hii ni mbaya sana kwani inaonyesha jinsi raisi wetu alivyozungukwa na watu wasiowahaminifu kwake. Yaani wanamfanyia usanii live. Hii ni hatari. Inawezekana kuna mengi yanafanyika jamaa anasign kumbe watu wanatafuna kona. HATUNA UONGOZI KWAKWELI.
 
Kiutaratibu sheria hiyo ni batili na haiwezi kutumika. Nilazima irudiswe bungeni ikafanyiwe marekebisho tena. Ila nachelea kusema itafumbiwa macho.
 
Kwa mtazamo wangu hakuna namna ambavyo ingeweza kutokea kuongezwa kipengele hiki bila kufahamika au kugundulika, kwani raisi makini anazo mbinu zote za kuhakikisha jambo hilo halitokei. Hata kuunda timu maalum ya wabunge kuipitia kuihakiki ingesaidia. Lakini kama mpaka leo ameshindwa kutoa tamko la ni namna gani imetokea na ni nani mhusika aliyeipitia na kumhakikishia iko sawa na anakusudia kuchukua hatua gani, basi huu ni usanii kama walivyosema Wakuu hapo juu!
 
Hongera sana Dkt Kikwete, keep it up!

Siamini macho yangu, Jamani hii nini? ila naye amezidi mno upole,kwanini asiwabadilishe hawa wanaomsaidia,hivi ni kweli alikuwa mwanajeshi au ulikuwa ni usanii?
 
Kuna wakati nilisema kuwa Dr Slaa ni kati ya watu watatu katika nchi hii wanaohitaji kupewa tuzo ya heshima. Huyu mtu anajali na kuipenda sana nchi yetu. Ukiangalia kwa ukaribu utagundua kuwa anaongoza nchi hii, ndiyo kama rais.

Nakubaliana na wewe kwa asilimia zote, maana kama siyo Dr Slaa mambo mengi yalishapita tu hivi hivi, na pia amesaidia kuondoa ile kauli ya yule kiongozi wa Kenya aliyemwambia JKN kuwa anatawala marehemu
 
Hivi, kuna ugumu gani kwa Mh Kikwete kuchukua msimamo wa kutovumilia utendaji usioridhisha? Ingekuwa ni mtu mdogo kwenye ofisi ya umma kafanya kakosa kadogo angeshatimuliwa tena kwa mbwembwe!!

Kinachohitajika hapa ni yeye kuchukua hatua juu ya mzembe MMOJA TU kati ya hao wengi wanaomzunguka na wengine watashika adabu.

Yaani napata hisia ya kumtingisha, labda kalala ataamka!!

Kama anashindwa kuwatimua, basi tumtimue yeye
 
Back
Top Bottom