Baada ya Heri James kuwa DC, Mwenyekiti Mpya wa UVCCM kutokea tena Zanzibar?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Ikumbukwe kwamba Kabla ya Heri James kuwa Mwenyekiti wa UVCCM nafasi hiyo ilishikwa na Hamad Masauni, japo baadaye aling'olewa kwa kashfa ya kufoji umri, baada yake akaja Sadifa, ambaye rekodi yake ya lugha chafu sidhani kama itakuja kuvunjwa. Hawa wote walitoka Zanzibar.

Sasa swali langu ni hili: Baada ya aliyepo kung'olewa kijanja na kupewa u-DC, anayefuatia atatoka bara au sasa ni zamu ya visiwani?
 
Najiuliza nikwavipi kijana toka nchi ya Zanzibar anakuja kuwa mkuu wa wilaya huku bara?

Mbona hakuna mtanganyika mkuu wa wilaya nchini kwao Zanzibar?

Ifike mahali tuwe na katiba current inayoakisi yasasa.

Vijana tubishane vya msingi sio kutwa taifa linabishana kama dayamondi atashinda biitii... Vijana wanaofanya hiyo ajenda ya kitaifa no vijana PUMBAFU KABISA
 
Sio ajabu nao ni Watanzania wanahaki ya kushiriki katika nafasi mbalimbali za uongozi kwenye nchi yao.
 
Muungano wetu ulivyo, ukiwa Mtanzania kutoka Zanzibar una haki zote za Zanzibar na Tanganyika, ila ukiwa Mtanzania wa Tanganyika haki zako ni huku Bara tu.

La mkuu wa Wilaya mbona dogo sana, Mbarawa ni Mpemba na alikuwa waziri wa Ujenzi na baadae Maji wakati sio mambo ya Muungano. Wenyewe wanasema tuna Muungano wa kipekee.
 
Akitoka Zanzibar hatakuwa na nguvu bara, na hiyo tutarudi enzi za Makonda.

Makonda huku bara alikuwa nguvu ndani ya UVCCM kuliko Sadifa Juma.
 
Halafu Cha ajabu wao hao hao wa kutoka huko ndio hawautaki Muungano huu
 
Halafu Cha ajabu wao hao hao wa kutoka huko ndio hawautaki Muungano huu
Walipoteza nchi yao, sio jambo jepesi. Ni sawa na kuporwa shamba, halafu mporaji anasema usijali nitakuwa nakuletea chakula πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…