Baada ya IGA ya DPW na Bandari zetu, licha ya mapungufu, HGA yake inakuja. Ombi kwa Serikali yetu sikivu, tunaomba Maximum Transparency kwenye HGA

Kwani mnajadili nini humu??.

Bunge imeridhia

Mahakama imeridhia

Serikali imeridhia.

Kelele zenu ni za chura tu azimzuii tembo wa DP WORLD kuwekeza hapo bandarini.

Hivi hamna kazi za kufanya?

Wengine wameacha kuhubir injili kamisani wamekomaa na kuhubiri mikataba huko vigangoni, kuongoza bongo lala ni kazi sana.
 
Nakwambia hivi, hata IGA hujaipata kutoka source ya serikali.

Kwanza dai serikali i release IGA kutoka source ya serikali, kabla ya kwenda popote zaidi kwenye HGA.

Kwa sababu sasa hivi tukitaka forensic papertrail yenye chain of custody inayoonesha IGA ni halali, hatuwezi kuonesha hivyo.
 
HGA ni mkataba nwepesi sana. Hauna sababu kwanini usiwe "transparent".

Sana sana unaonesha sheria, kanuni, taratibu na tamaduni zetu ambazo tumekubaliana kwenye majadiliano wageni wetu wazifate wanapokuwa hapa kwa utendaji wao.
Mambo machache sana itabidi yawe siri katika HGA ambayo ikibidi yatawekwa kwenye "concession agreements".

"Concession agreements" ndiyo sirsi ambazo hazitawekwa wazi kwa faida ya pande zote.

concession agreements zitakuwa nyingi tu.
 
Kaka Paskali,
Mimi naganda hapo kwenye sehemu ya heading ya bandiko lako., NANUKUU... "licha ya mapungufu" ... MWISHO WA KUNUKUU..!! na baadhi ya maeneo kwenye bandiko lako.
Mkuu Ngali, Ngalikihinja , karibu sana!.
Ni kwenye TEC wako correct 100% kutoa maoni yao, ila kuyafanya ndio maoni ya Wakatoliki wote is not right!. Kitendo cha kuyasomea mimbarini, madhabahuni na alterini is not right!, ni kuchanganya dini na siasa Mpeni Mungu yaliyo ya Kimungu na Kaisari yaliyo ya Kaisari! Hiki kinachofanywa na Baraza la Maaskofu Katoliki, sio kuchanganya dini na siasa?
1. Kwanini unadhani IGA iendelee huku mkataba una mapungufu?
IGA iendelee kwasababu IGA sio mkataba ni makubaliano tuu ya kuingia mkataba, HGA ndio mkataba, licha ya IGA mbovu save for illegality, unaweza kuwa na HGA nzuri kama nilivyoeleza hapa Wajua kuna ndoa halali, batili na batilifu? Ndoa ya TPA na DPW, ni Ubakaji? Wajua ubakaji unaweza kuwa alali? IGA batili yaweza kuzaa HGA halali?
2. HGA yake unayoizungumzia, unadhani itaondoa mapungufu yanayotajwa?
HGA inaweza kuondoa mapungufu yote save for mapungufu ya illegality, kukiisha kuwa na illegality, the contract is null and void ab initio!. Hapa nilieleza Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee!
3. Hivi HGA huwa haifuati IGA imesema nini? Hapa naomba kuelimishwa ni kwa namna gani HGA inaweza ikaongea kinyume na IGA.
Sio lazima kila mkataba kuwa na IGA, HGA inaweza kuwa nzuri as if IGA has never been there!. Kama lile Bunge full of vilaza walipopitisha lile Azimio batili la kutopokea ripoti ya CAG, kisha likaipokea as if sio Bunge hilo lililotoa Azimio batili!. Je, Wajua Bunge linaweza kutoa azimio batili? CAG yuko kikatiba. Je, Bunge lina uwezo kutopokea ripoti ya CAG? baada ya kutoa Azimio batili hili, nikawaonya Je, Wajua Bunge linaweza kuvunjwa Siku 7 Zijazo?. lisipopokea ripoti ya CAG, Bunge linavunjwa kwa mujibu wa Katiba waliipokea Ripoti ya CAG kimya kimya as if nothing happened!. Hivyo HGA inaweza kuwa nzuri as if there has never been an IGA ya ajabu ajabu!.
4. Unadhani transparency itaondoa mapungufu?? Kwani hawawezi weka transarency huku mapunguvu yakiongezeka?
Yes transparency itasaidia sana!, kwa vile Samia sio mwanasheria, Mbarawa sio mwanasheria, hiyo IGA ingekuwa transparent halafu Samia akaona hoja hizi Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee! amini nakuambia asinge saini ile POA!.
Unadhani mapungufu yametokana na kutokuwa wawazi?
Mapungufu yametokana na wanasheria vilaza!. Nimemsikia yule head of government negotiation team, kiukweli I serious doubt his credentials as a competent lawyer!, makosa ya the capacity to contract ni LW 101 contract law, Ist Year!.
5. Kwa kutumia hiyo hiyo kawaida ya HGA, kuwa huwa ni confidential, unadhani wataweka wazi yatakayokuwemo kwenye HGA?
Yes naamini wataweka for public interest.
Nini kitawalazimisha kuweka wazi wakati kawaida yake ni USIRI?
Hizi kelele kuhusu mapungufu ya hii IGA, serikali yetu ikaahidi kuzingatia ushauri, then HGA ya itawekwa open ili tuone kweli mapungufu ya IGA yamerekebishwa!.
Wasipokuwa OPEN what will be the next step?.
We have nothing to do, ila tunaweza kuwatumia wawakilishi wetu Bungeni kuomba kuiona HGA ya DPW na Bandari zetu!.
Huoni kwamba unataka tucheze kamari au pata potea?
No hii sio kamari au pata potea, no let's give it a try!.
6. Kwenye content yako, kuna maelezo haya, nanukuu .."Wale wote mlioipinga hii IGA kwa hoja za kisheria, hoja zenu zote zitakuwa zimezingatiwa kwenye HGA.".. Mwisho wa kunukuu. Nini kinakufanya uamini hicho ulichokiandika?
PM Majaliwa aliahidi serikali itazingatia.
Wasipozingatia je?
Ni Waziri Mkuu kutufanya tena Watanzania wote kama watoto wa chekechea kama ile "ni mzima, anachapa kazi", kumbe mtu was no more long ago!.
Ni kweli ndio maana na mimi nimeiomba serikali yetu Sikivu HGA ziwekwe wazi, tuondoe mashaka.
Kaka Paskali, naheshimu sana uelewa wako kwenye mambo mbalimbali.
Thanks for this nami wewe kwangu ni mwalimu wangu wa quo warranto!.
Binafsi nimekuuliza maswali kadhaa kwenye posts zako mbalimbali. Yapo uliyoyakwepa na hujawahi kuyajibu hadi sasa, kwa ahadi kwamba utarudi na majibu, lakini hujarudi
Kwa hili naomba unisamehe sana, kuna baadhi ya mabandiko yangu ni just info pack, huwa sijibu kitu mule!. Ila kama kuna mahali niliahidi nitarudi halafu sikurudi, if haina limitations clause, ni rejelee bandiko langu lolote ambalo sikujibu, ni tag, nitajibu!.
KWA MASWALI HAYA NITAKUWA KINGÁNGÁNIZI KWAKO KAKA, ILI UJIBU KILA MOJA KWA UFASAHA.

Ngali K.
Nimejibu yote and no stone is left unturned
P
 
Asante sana Dada kipenzi, tumsaidie huyu Mama, kumoonyesha what is expected of her.
P
 
nyie mliofilisika kimawazo ndo mnaleta masuala ya kidini.TEC wanatoa WARAKA miaka yote haijalishi rais ni muislam au ni mkristo.

kwanini waraka wa sasa wa TEC muone wa kidini?
Waraka huu ni tofauti na huko nyuma. Kuupinga uwekezaji ambao ni mwendelezo wa utendaji wa tangu awamu zilizopita kwa baadhi inachukuliwa ni kama uasi, na haswa namna ulivyosambazwa na kusomwa makanisani.

Masuala ya kiuchumi unapoyapinga unaongea na serikali iliyotumia nguvu kuelimisha maaskofu juu ya nini kinachokusudiwa kufanyika, unaiambia hiyo hiyo serikali moja kwa moja kwamba sikubaliani na mnachotaka kukifanya na sio kwenda kwa waumini na kuwasomea waraka wa kupinga uwekezaji.

Kwa kufanya hivyo unawakwaza hata wataalam wakatoliki kwa kuwataka waipinge serikali yao, vipi kama baadhi yao walitumika katika kuuandaa huo uwekezaji?.

Maaskofu wetu wakatoliki wamechemka.
 
CCM waliishasema uwekezaji wa bandari liko kwenye ILANI yao ni lazima litekelezwe mtake msitake, with or without transparency. Mkataba mbaya mzuri wao wataleta muwekezaji, they don't care nchi hii ni yao.
 
Asante kwa majibu, narudi tena kwa maswali ili nielewe vizuri zaidi;

1. Nanukuu ... "Ni kwenye TEC wako correct 100% kutoa maoni yao, ila kuyafanya ndio maoni ya Wakatoliki wote is not right!. Kitendo cha kuyasomea mimbarini, madhabahuni na alterini is not right!, ni kuchanganya dini na siasa Mpeni Mungu yaliyo ya Kimungu na Kaisari yaliyo ya Kaisari! Hiki kinachofanywa na Baraza la Maaskofu Katoliki, sio kuchanganya dini na siasa?" .. Mwisho wakunukuu

Kusema kwamba tamko la TEC kufanya ndiyo maoni ya wakatoliki wote is not right, kwangu mimi, YOU ARE NOT RIGHT..!! Kwa mtazamo huu, hakuna viongozi wa kundi lolote, watakaotoa tamko halafu litambulike ndo msimamo wa kundi hilo. Maulamaa wakitoa tamko linakuwa si la waislamu wote, shura ya maimam nao hivyo..!! The same kwa rais wa nchi, akisema kitu, ni cha watanzania wote, hakiwi chake peke yake...!!

Usisahau TEC ni wakatoliki wakisema wao tumesema wakatoliki. LABDA NIKUULIZE SWALI, ILI LILE TAMKO LIWE MSIMAMO WA WAKATOLIKI WOTE, NINI KIFANYIKE? SWALI HILO HILO KWA MAKUNDI MENGINE..!!

2. Majibu yako mengi yako based on imani..!! Not facts. Yako based na maombi not facts. Hao hao unaoamini watafanya unachokiamini, walishawahi kutudanganya huko nyuma. Mfano, nani amepata ripoti ya kuungua kwa soko la Kariakoo ambayo iliahidiwa kutolewa baada ya wiki tangu kutolewa kwa amri ile? Au lile la YUPO ANACHAPA KAZI KUMBE KAFARIKI..!! Kuwaamini akina "Majaliwa" ndo kumetufikisha hapa ambapo ahadi zinatiliwa shaka. Usisahau, kilichokutokea kwenye maisha yako ya jana, ndicho kinakufanya uamue namna ya kuishi leo.

3. TAMKO kusomwa mimbarini, sababu inajulikana. Mpaka leo umewahi sikia chombo gani cha habari kimerusha kwa ufasaha tamko lile? Hapa TEC waliliona hilo mapema na ndiyo maana wakatumia mimbari. Haya, umesema kusoma tamko mimbarini ni kuchanganya dini na saisa, wao viongozi wanapotumia mimbari kutangaza ya kisiasa, huwa hawachanganyi dini na siasa? Kwanini wakiongea TEC mimbarini kuhusu tamko lao, iwe ni kuchanganya dini na siasa lakini akiongea Kikwete mimbarini, tena ni muislamu kwamba hakwenda kule kufanya ibada, iwe si kuchanganya dini na siasa?? Hii ni double standard.
 
Asante kwa majibu, narudi tena kwa maswali ili nielewe vizuri zaidi;
Karibu tena na tena, formula yangu ni ile ile, I leave no stone unturned!
Kwanza nakubaliana na wewe msimamo wa mtu yoyote kuhusu jambo lolote is not necessarily awe right, sometimes I might be wrong, na kuambiwa I'm wrong, nakupokea very positively.
hakuna viongozi wa kundi fulani, watakaotoa tamko halafu litambulike ndo msimamo wa kundi hilo.Maulamaa wakitoa tamko linakuwa si la waislamu wote, shura ya maimam nao hivyo..!!
Dini ni imani, hivyo viongozi wa kiimani wanaaminika zaidi na waumimi wao kuliko viongozi wa siasa. Tamko la TEC, japo limekuwa formulated na Maaskofu, tamko hilo lilivalishwa Umungu kwa kufanywa ni kauli ya wengi, " Vox Populi is Vox Dei" na kitendo cha kulisoma tamko hilo mimbarini, madhabahuni, altareni, kumelifanya tamko hilo kuwa ni sehemu ya ibada!. Wakatoliki wanawaamini sana viongozi wao wa dini wakiamini hiyo ni sauti ya Mungu. Hivyo Wakatoliki wote waliopo CCM na serikalini wanao ikubali DPW, tamko hilo la TEC linatuweka katika wakati mgumu!. Vivyo hivyo tamko la Sheikh Mkuu ni tamko la Waislamu wote!. Kuna wakati wa mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhan, siku ya mfungo 29, mwezi ulionekana Mombasa, huku haukuonekana, Sheikh Mkuu kupitia Bakwata akasema mwezi haujaandama, hivyo Tanzania sio Iddi, watu wa Answar Sunna walikaidi wakaswali Eid el Fitri. Kesho yake mfungo 30, mwezi mwandamo ukaonekana ni mkubwa kabisa!, hivyo waliswali Iddi jana yake they were right!, serikali ikawataka Waislamu wote wa Tanzania kuifuata Bakwata, even if they are wrong!, hivyo Wakatoliki wa Tanzania watafuata msimamo wa TEC hata kama Maaskofu wa Katoliki are wrong!. Niliwahi kutoa angalizo hili humu kuhusu kuabudu Angalizo: Kuna Wengi Wanamwabudu Shetani Wakidhani ni Mungu!. Jee Wewe Unajijua?, Jitambue!.
The same kwa rais wa nchi, akisema kitu, ni cha Watanzania wote, hakiwi chake peke yake...!!
Rais ni mamlaka halali au serikali ni mamlaka halali, ikitoa tamko ni amri halali inafuatiwa na utekelezaji
Usisahau TEC ni wakatoliki wakisema wao tumesema wakatoliki. LABDA NIKUULIZE SWALI, ILI LILE TAMKO UWE MSIMAMO WA WAKATOLIKI WOTE, NINI KIFANYIKE? SWALI HILO HILO KWA MAKUNDI MENGINE..!!
Tamko la TEC ni tamko la Wakatoliki wote!, kitu ambacho sio kuwatendea haki Wakatoliki wanao ikubali DPW!. Serikali yetu ikiwapuuza Wakatoliki, mwaka 2025 wanaweza kutoa waraka wa kuwatakia Wakatoliki wasikichague chama kinacho puuza Vox Populi is Vox Dei!.
It's true kuna vitu tunaahidiwa na havitekelezwi, ila Watanzania hivi ndivyo tulivyo tunaishi kwa matumaini, hili dubwana ni li zimwi ila ni zimwi likujualo halikuli likakwisha, hivyo licha ya kututenda yote haya ukifika wakati wa uchaguzi, tunalichagua tena na tena!.
.Kuwaamini akina "Majaliwa" ndo kumetufikisha hapa ambapo ahadi zinatiliwa shaka. Usisahau, kilichotokea kwenye maisha yako jana, ndo kinakufanya uamue namna ya kuishi leo.
We are living in a jungle, the law of the jungle applies, it's a constant struggle for existence, survival for the fittest, to be fit, one has to be adaptive to the changing environments, be adaptive and survive, if you can't adapt you just perish!. Angalia tarehe ya bandiko hili Elections 2015 - If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's pray for him! na sasa Mama huu ukimya wake na kuna vitu anavisema kwa sisi wa jicho la tatu vinatuogopesha hivyo tumejisalimisha mapema Mama, I'm here to support you, to serve our country. I'm here sio tu kuonesha ujuzi wangu kwa nchi yangu, bali pia kuutumia. But...
3. TAMKO kusomwa mimbarini, sababu inajulikana. Mpaka leo umewahi sikia chombo gani cha habari kimerusha kwa ufasaha tamko lile?
Kwa urefu wa tamko lile hakuna media angeweza kulitangaza lote kwa ufasaha, makanisa ya wenzetu wanapotoa public information announcements, Padri anashuka kutoka mimbarini, altareni na madhabahuni anakuja kwenye podium ya Walei, na kutoa tangazo hilo, hivyo kutenganisha tangazo la kumwabudu Mungu na tangazo la kawaida.
Haya umesema kusoma tamko mimbarini ni kuchanganya dini na saisa, wao viongozi wanapotumia mimbari kutangaza ya kisiasa, huwa hawachanganyi dini na siasa?
Pia wanafanya makosa, mimi ni muumini wa Parokia ya St .Peters, ndipo nimepatia Komunio, nikatumikia, nikapatia Kipaimara, nikafungia ndoa na ile sherehe yangu ya mwisho pia itakuwa hapo!, enzi za Mwalimu Nyerere alikuwa anasali bila kupanda altareni kusalimia!.
Kwanini wakiongea TEC iwe ni kuchanganya dini na siasa lakini akiongea Kikwete mibari, ten ni muislamu kwamba hakwenda kule kufanya ibada, iwe si kuchanganya dini na siasa?
Kwenye hili naendelea kusisitiza tusichanganye dini na siasa!.
P
 
Ni ngumu mno mno kwani watu walishakula ''hela za watu'
CCM haya mnayofanya kumbukeni ni dhuluma kwa mali za wananchi maskini!
Mkono wa Mungu ni mrefu sana na ni mkono wenye haki na nguvu sana.

Ole wenu enyi wezi na vizazi vyenu kwani Bwana atashusha gharija juu yenu.
 
https://www.facebook.com/
View: https://fb.watch/mTLTQUYlL6/?mibextid=NnVzG8&startTimeMs=204921
 
Mikataba inayofuata yote itakuwa siri, hiyo transparency unayoiomba ni ipi?
Yes kikawaida HGA ni confidential ila kufuatia mauzauza ya IGA ya DPW na Bandari, kumetengeneza public interest itakayo ilazimu HGA zake ziwe transparent ili tuone na kujiridhisha zile kasoro za kisheria za IGA ya DPW haziko reflected kwenye HGA.
Public interest surpluses everything!.
P
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu ya kuwaletea trends mbalimbali, leo naomba niwaletee hii trends za kinachoendelea kwenye hii issue.

Baada ya IGA ya DPW na Bandari Zetu, HGA yake iko njiani inakuja!

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
Ukiacha kutetea DP world tutakuunga mkono
Mkuu JakiDubai, kuna watu wanaandika jf ili waungwe mkono?, utaniunga mkono ili iweje?.
Anyway karibu, hili ni moja ya mabandiko yangu kuunga mkono IGA ya DPW na Bandari zetu, angalia tuu tarehe ya bandiko hili ili ulinganishe na wengine, na ikitokea una uwezo wa kusoma contents, soma contents uone jinsi ninavyoisupport DPW na Bandari zetu!.

Karibu

P
 
Wanabodi,

Baada ya IGA ya DPW na Bandari Zetu, HGA yake iko njiani inakuja!

The issue ni moja tu, jee HGA ya DPW na Bandari zetu itakuwa open kama hii IGA?.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
Mzigo wenyewe sasa ndio huu
Fuatilia yanayojiri kutoka Ikulu kwenye Halfa ya utiaji saini wa Mikataba mahsusi 3 ya uwekezaji Bandari ya Dar es salaam, leo Oktoba 22, 2023.

Asante kwa taarifa, hizi sasa ndio HGA
Huu sasa ni muda muafaka wa kuyatekeleza haya Baada ya IGA ya DPW na Bandari zetu, licha ya mapungufu, HGA yake inakuja. Ombi kwa Serikali yetu sikivu, tunaomba Maximum Transparency kwenye HGA

P
 
Ushauri wako ni mzuri kwamba watu wasichanganye dini na siasa lakini ushauri huu hautafua dafu !
 
Licha ya HGA ya DPW na Bandari zetu kusainiwa, hoja ya transparency ya kilichosainiwa ni nini, bado iko valid.
P
 
Licha ya HGA ya DPW na Bandari zetu kusainiwa, hoja ya transparency ya kilichosainiwa ni nini, bado iko valid.
P
Labda ni confidential kama ulivyosema ! Na hii iko vile kwenye mikataba yote ya kibiashara iliyokwisha sainiwa kwenye Nchi hii na makampuni ya kimataifa. !!
Kwenye madini ni hivyo hivyo na kwenye gesi nako ni vile vile mpaka alipokuja Yule Mheshimiwa ndio tukaanza kujua jua kidogo kuwa kumbe tumepigwa za uso !!
Kwahiyo nathubutu kusema hii njo iko vile hakuna namna !! Kanuni zinazohusu mikataba ya kimataifa kama hiyo ni lazima itazingatiwa !! 🙏🙏
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…