Baada ya Kashfa ya Trump, Ulaya kwa kauli moja wamuambia Zelensky your not Alone you never walk alone alipo wapo ulipo tupo simamia nchi yako

Kwa nini walikuwa wanateswa?
 
ULaya ni maneno matupu, wanasema u r not alone huku wakijua wazi marekani ndio anayetoa pesa nyingi na silaha zake kila siku, ulaya hawawezi kumsaidia zelensky , waangalie tu jinsi ya kumbembeleza trump hakuna namna
 
Russia haina capabilities wala nia ya kupigana na kuitawala Europe, hii ni propaganda kina Zelensky wanatumia kuendelea kujistify hiyo vita
Utakuwa hauijui vizuri Urusi hususani Putin. Putin anaamini kwamba Ulaya inapaswa kuwa chini ya mamlaka ya Urusi, na yeye Putin ndio Mtu sahihi wa kufanikisha suala hili.
 
Mbi
Mbona kwasasa ulaya ni mateka wa US chini ya NATO na hakuna shida yoyote. Kwann ulaya ukiwa chini ya Russia ndio kuwe na shida.

Kama lengo la Russia ni kuitawala ulaya yote ilikuwaje akaruhusu USSR Ivunjike?
 

Nafikiri bado hauna taarifa za kutosha kuhusiana na Utawala wa Urusi, tambua kwamba Wananchi wa Ukraine wengi wao waliwahi kuwa Raia wa Urusi hapa kabla ya Nchi hizo hazijatengana. Watu wa Ukraine wanaufahamu vizuri Sana Utawala wa Urusi.
Je, umeshawahi kujiuliza hivi ni kwa nini hasa Wananchi karibia wote kabisa wa Ukraine kwenye Vita hii wameungana Sana na kwa moyo mmoja wanapigana ili kukataa kabisa kuwa chini ya Utawala wa Urusi? Unajua ni kwa nini hasa hali ipo hivi? Unajua ni kwa nini Majeshi ya Putin yameshindwa kabisa kupata uungwaji mkono kutoka kwa Raia wa Ukraine kwenye hii Vita yake huko Ukraine??? Unazijua sababu zake??
Tangu Vita hiyo ilipoanza huko Ukraine, Je, umeona kuna dalili za kugawanyika miongoni mwa Watu wa Ukraine dhidi ya Majeshi ya Putin???.

Kimsingi, unapaswa utambue ya kwamba, ndani ya nchi hiyo ya Urusi tangu zamani Sana kumekuwa na tatizo sugu Sana la Watu wa majimbo mbalimbali kwenye nchi hiyo kutaka kujitenga na kujitegemea wao wenyewe wakiwa katika nchi huru. Tatizo hilo la kutaka kujitenga na Urusi huko Ulaya ya Mashariki linafahamika Sana kwa jina la "SEPARATISTS," kwa wale watu waliopo Urusi au ambao wamewahi kuwepo Urusi nafikiri wanalijua vizuri Sana jambo hili.
 
Utakuwa hauijui vizuri Urusi hususani Putin. Putin anaamini kwamba Ulaya inapaswa kuwa chini ya mamlaka ya Urusi, na yeye Putin ndio Mtu sahihi wa kufanikisha suala hili.
Kwa umri wake mbona atakuwa amekifa kabla ya kukamilisha Hilo? Hivi jaribu kufanya conceptualization ya vita ya Russia Vs NATO (Ulaya na Marekani) kichwani; yaani military command yake mwenyewe itamuua kabla hajaribu kufanya hivyo maana atakuwa anacheza na mwisho wa dunia
Hata rais wa Marekani atakayekuwa na hizo ambitions ataminywa tu
 
Russia haina capabilities wala nia ya kupigana na kuitawala Europe, hii ni propaganda kina Zelensky wanatumia kuendelea kujistify hiyo vita
Nashangaa huu ujinga unaosambazwa na watu wanaojitoa ufahamu. NATO au tuseme Ulaya bila USA wepesi sana hawana lolote na Trump analijuwa hilo udhaifu wao. Kwa sasa Ulaya wafunge kamba wasubiri tu Trump miaka yake minne vinginevyo hawana jeuri ya kijeshi wala kipesa. USA anatoa 50% ya kila kitu cha NATO.
 
Tatizo kubwa la wasovieti ni rushwa Russia rushwa na Ukraine rushwa zaidi... misaada ya Marekani na ulaya imeishia mifukoni mwa wala rushwa... so ukiona mmoja ameshindwa jua rushwa hapo..

Russian walifikia kuiba battery za magari na vifaru vya vita kwenda kuuza.. including starter ortanator n.k kamba ilikua magari mapya yasiyo ibiwa kila kitu...
 
Mbi

Mbona kwasasa ulaya ni mateka wa US chini ya NATO na hakuna shida yoyote. Kwann ulaya ukiwa chini ya Russia ndio kuwe na shida.

Kama lengo la Russia ni kuitawala ulaya yote ilikuwaje akaruhusu USSR Ivunjike?

Nchini Urusi kuna historia ndefu sana ya tangu zamani Sana kuhusiana na suala la kuwepo kwa Utawala wa mabavu na wa kikatili, usiokuwa wa Haki, ambao hauzingatii Haki za binadamu, demokrasia, Wala kujali Uhuru wa Watu.

In Russia, There is a serious problem of the Dictatorship Regime that amongst the most brutal and repressive Regine in the world.
Kumbuka historia ndefu ya madhila na misukosuko ambayo Wananchi wengi zaidi wa huko Urusi (USSR) waliyopitia chini ya Utawala wa nchi hiyo enzi hizo chini ya Mamlaka za Ujasusi wa nchi hiyo ambayo inaitwa KGB, sasa hivi inaitwa FSB.

Kimsingi, unapaswa utambue ya kwamba, ndani ya nchi hiyo ya Urusi tangu zamani Sana kumekuwa na tatizo sugu Sana la Watu wa majimbo mbalimbali kwenye nchi hiyo kutaka kujitenga na kujitegemea wao wenyewe wakiwa katika nchi huru. Tatizo hilo la kutaka kujitenga na Urusi huko Ulaya ya Mashariki linafahamika Sana kwa jina la "SEPARATISTS," kwa wale watu waliopo Urusi au ambao wamewahi kuwepo Urusi nafikiri wanalijua vizuri Sana jambo hili.
 
Shida wana maneno uwezo hawana. Ulaya sasa hivi haieleweki ni kama the shadow of itself. Uchumi wake hoii wakato utakua kwa 1.7 waliyemwekea vikwazo yani russia unategemewa wake mwaka huu ukue kwa about 4 point something.
Ulaya imabidi irudi mezani ijipange upya. Marekani ashaitosa
 
Wadanganye wasiofuatilia mambo kwa undani ila sio mimi

Unasema eti wananchi wa Ukraine wameungana kuikabili Urusi wakati tunajua wanapelekwa vitani kwa lazima? Mikoa aliyochukua Urusi wananchi alishangilia sana na kuna sehemu magari ya deraya ya Slovakia yalipita yakiwa na bendera raia wa Ukraine wakadhani ni majeshi ya Urusi sababu bendera ya Slovakia na Urusi ni kama zinakaribia kufanana, basi wakaanza kuwashangilia huku wakionesha alama ya Z baadae wakagundua sio majeshi ya Urusi wakavunga kama sio wao.
WaUkraine wanakimbia nchi yao hadi wengine wanafia msituni wskitoroka kushikwa kwa nguvu... Hata huyu punguani wao Zelensky alitoa oda waUkraine walioko nchi za nje wanyang'anywe paspoti wakamatwe warudishwe nchini mwao wakapigane na Urusi, hili nalo hulijui au ni unaa tu umekujaa 😁
WaUkraine wanapelekwa vitani kwa kuswagwa kama manamba na hawana pa kusemea sababu huyo mwehu wao hajali chochote ilimradi nae aonekane anapambana na wakubwa.
 
Baadhi ya masharti ya Ukraine kuwa huru ni haya
1. Kutokumiliki silaha za nuclear
2. Kuwa na jeshi dogo
3. Kutojiunga NATO
4. Kumkodishia Russia bandari ya kijeshi
Kitendo cha Ukraine kwenda kinyume na makubaliano haya ni uchokozi wa wazi Russia na kutishia uchumi n usalama wa Russia
 
Zelensky ameishashindwa vita na Nchi imeshamegwa hao EU ni maboya waliomlaghai Zelensky na magobole ya misaada aibu inawakumba🤣🤣 lazima wajitoe kimasomaso sasa hivi Hangary anawacheka tu hao EU kwa kuangukia pua
Vita haijaisha , ameshindwaje?
 
Russia haina capabilities wala nia ya kupigana na kuitawala Europe, hii ni propaganda kina Zelensky wanatumia kuendelea kujistify hiyo vita
Aliyeanzisha vita ndiye aliye justify vita, acha kuziba jicho moja.
 
Tafuta habari kuhusu mikataba ya NATO na Urusi, Ukraine na Urusi na kilichokuwa kinafanya na serikali ya Zelensky kwenye mipaka ya Urusi.
Kwamba Crimea haikuwa ya Ukraine kwa hiyo kuidai ni kuichokoza Urusi?.Hapo hapo pamoja na ile okt 7 kule Israel bado una kipeperushi cha free Palestine!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…