John Wickzer Mulholland
JF-Expert Member
- Apr 13, 2023
- 6,656
- 14,403
Kukomaa kwa Zelensky sio kukomaa kwa wananchi wa Ukraine,muhimu kuangalia hapo ni je,wananchi wake nao wanamuunga mkono,vita sio movie,ni kujitia kwenye umasikini wakutupwa kisa kupenda ligi...
Wananchi wa Ukraine wanapigana Vita ili kumzuia Putin wa Urusi asiteke Ardhi ya nchi yao, halafu Trump naye anapigana Vita na Rais wa Ukraine Bw. Zelensky ili naye aweze kuiteka nchi hiyo hiyo ya Ukraine kwa kupitia Mkataba wa Madini. Je, unafikiri Watu wa Ukraine watakuwa tayari kumkubalia Rais Trump aiteke Nchi hiyo wakati huo huo wanampiga Vita Putin kwa sababu hiyo kutaka kuiteka nchi??
Putin anapaswa azuiwe asiiteke Nchi hiyo ya Ukraine na Trump naye pia anapaswa azuiwe ili asiweze kuiteka nchi hiyo ya Ukraine. Putin na Trump wote kabisa wanapswa wazuiwe ili wasiiteke Ukraine.
Zelensky amefanya UAMUZI BORA KABISA kwa maslahi mapana zaidi ya umma wa Wananchi wa nchi yake ya Ukraine.
Zelensky amekataa kuwasaliti Wananchi wa nchi yake. Hongera kwake kwa Uzalendo Mkubwa Sana alioonyesha mbele ya Wababe wa dunia!