Baada ya kifo cha Magufuli, Wapinzani walituaminisha chuki zitaisha kumbe bado?

Baada ya kifo cha Magufuli, Wapinzani walituaminisha chuki zitaisha kumbe bado?

Uoga wa nini...Diamond ni CCM.. CCM ni wengi kuliko Chadema na Inapendwa so wana CCM nao si wahamasishane Kumpigia kura Diamond na kwa kuwa CCM inapendwa sana basi hata Chadema wapige kampei bado haitafaa kitu. Kulalamikia hizi kampeni za Chadema ni kuonesha uoga wa CCM
Kuna utani kuwa wapo watu wanakula ugali kwa picha ya samaki!
Ccm ni kama ugali usio na mboga. Huliwa tu pale picha ya samaki ikiwekwa mbele. Sasa inategemea ni samaki wa aina gani!
Watu walisha kinai bila picha ya samaki mzuri ugali hauliki.
 
hahaaaa wanakimbia nchii ya asali na maziwa wanamuogopa nani? wacha tule matunda ya nchi yetu hao wakae hukohuko
Kurudi watarudi tu tatizo ni yule aliyeota ndoto za alinacha eti anapenda kuwa raisi wa malaika,huku akijua alikuwa mtekaji,muuwaji,aliyejaa dharau na kejeli ATARUDI????Acha tujinafasi kutesa kwa zamu.
 
Kuna msemo unaosema, asifuye mvua imemnyea.

Wakati wa Hayati Dkt. Magufuli, CHADEMA walikuwa na propaganda kali sana kwamba Magufuli ameshindwa kuleta umoja kwa taifa. Kwa vile Mara nyingi wanalalamika kwenye mitandao mambo yao yakaenda hadi nje ya nchi.

Kuna wengine hadi wakaomba uhamisho kwa mbwembwe kwamba ni wakimbizi wa kisiasa na sababu ni Hayati Magufuli.

Sasa Hayati Magufuli hayupo, Ila bado wanalazimisha chuki miongoni mwa Watanzania.

Mwenyekiti wa chama ana hubiri chuki za ukabila.

Wanachama wanahubiri chuki zaidi ya Diamond asipigiwe kura.

Hawa watu ni watu wa aina gani?

Ungekuwa wewe Ndio Rais wa nchi unawafanya nini Hawa? Unaweza ukawaalika ikulu kula nao mesa Moja na kugonga nao cheers?

Nahisi Dkt. Magufuli alikuwa sahihi kuwatuliza.

Nini maana ya democracy. Mtu yupo huru kudai anachoona ni sahihi wao wanatetea haki zao wanaanzaje kunyamaza sasa. Tatizo lenu mnataka watu waiabudu ccm kila mnachokifanya watu wakubali na sie hatutaki
 
Unawazungumzia hawa wananchi waliyoenda kuvunja gate la Airport na kujazana barabarani wakitandika kanga kwenye msiba wa Magufuli? kilichofanyika hakuna ambaye alitarajia kama kungekuwa na wananchi wa kufanya vile sasa watu kama wale wasiotabirika ni ngumu pia kujua watapigia chama gani.

Walikuwa wangapi? Hata hivyo sina tatizo na wao kuipigia kura ccm, ila nataka ushindi wa halali. Hili ni jambo lisilo hitaji mjadala kuwa kukiwa na mazingira sahihi ya ushindani, hakuna uwezekano wa ccm kushinda zaidi ya 55% ya uchaguzi. Ccm hawataki ushindani halali maana wanajua chama chao sio cha kizazi hiki, ukweli huu unawaumiza kupita maelezo.
 
Walikuwa wangapi? Hata hivyo sina tatizo na wao kuipigia kura ccm, ila nataka ushindi wa halali. Hili ni jambo lisilo hitaji mjadala kuwa kukiwa na mazingira sahihi ya ushindani, hakuna uwezekano wa ccm kushinda zaidi ya 55% ya uchaguzi. Ccm hawataki ushindani halali maana wanajua chama chao sio cha kizazi hiki, ukweli huu unawaumiza kupita maelezo.
Sijui idadi yao ila ni wengi hakuna aliyetarajia hasa kwa jinsi ambavyo huyo Marehemu alivyokuwa anazungumziwa na hadi sasa jinsi anavyoendelea kuzungumzwa hakuna angetaraji kitu kama kile na hatuwezi kusema ndio wale tu pengine kuna wengine hawakuwa wakitoka tu majumbani. Sasa kwa watu wa aina hiyo mie napata shida sana kuamini kwamba et ccm haitaki ushindani halali kwa kuogopa CDM tu kwamba CDM ina mtaji wa kula wa kutosha kuwaingiza Ikulu.
 
Sijui idadi yao ila ni wengi hakuna aliyetarajia hasa kwa jinsi ambavyo huyo Marehemu alivyokuwa anazungumziwa na hadi sasa jinsi anavyoendelea kuzungumzwa hakuna angetaraji kitu kama kile na hatuwezi kusema ndio wale tu pengine kuna wengine hawakuwa wakitoka tu majumbani. Sasa kwa watu wa aina hiyo mie napata shida sana kuamini kwamba et ccm haitaki ushindani halali kwa kuogopa CDM tu kwamba CDM ina mtaji wa kula wa kutosha kuwaingiza Ikulu.
Narudia tena, sio kwamba ccm hakuna sehemu hawapati ushindi halali, ndio maana nikakuwekea percent ambayo hawawezi kuvuka kukiwa na ushindani halali. Na iwapo watapata ushindi finyu kulingana na matamanio yao, uwezekano wa wao kupoteza chaguzi za mbeleni ni mkubwa, kwani ccm sio chama cha kizazi hiki.
 
Narudia tena, sio kwamba ccm hakuna sehemu hawapati ushindi halali, ndio maana nikakuwekea percent ambayo hawawezi kuvuka kukiwa na ushindani halali. Na iwapo watapata ushindi finyu kulingana na matamanio yao, uwezekano wa wao kupoteza chaguzi za mbeleni ni mkubwa, kwani ccm sio chama cha kizazi hiki.
Na mimi nilichoeleza ni kwamba si kwamba ccm haitaki ushindani halali kwa kuogopa Chadema kama ambavyo wengi wanafikiri, mimi binafsi sioni hivyo. Kitu gani kinakufanya useme ccm sio chama cha kizazi hiki?
 
Sijui idadi yao ila ni wengi hakuna aliyetarajia hasa kwa jinsi ambavyo huyo Marehemu alivyokuwa anazungumziwa na hadi sasa jinsi anavyoendelea kuzungumzwa hakuna angetaraji kitu kama kile na hatuwezi kusema ndio wale tu pengine kuna wengine hawakuwa wakitoka tu majumbani. Sasa kwa watu wa aina hiyo mie napata shida sana kuamini kwamba et ccm haitaki ushindani halali kwa kuogopa CDM tu kwamba CDM ina mtaji wa kula wa kutosha kuwaingiza Ikulu.
Achana naye huyo nyumbu atakuambia hao watu waliovunja geti pale airpot waliletwa na maroli na mabasi kutoka mikoani.
 
Back
Top Bottom