Tetesi: Baada ya kivuko Busisi kuzingua, wananchi waruhusiwa kupitia katika Daraja la Magufuli na kuvuka kwa mguu hadi ng’ambo

Tetesi: Baada ya kivuko Busisi kuzingua, wananchi waruhusiwa kupitia katika Daraja la Magufuli na kuvuka kwa mguu hadi ng’ambo

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakuu

Baada ya kivuko eneo la Busisi kuzingua na kushindwa kutoa huduma, watu wamevunja geti la Daraja la Magufuli, kisha kuvuka kwa mguu hadi ng’ambo kama video inavyoonesha.

Soma, Pia: Vivuko vya Kigongo-Busisi havifanyi kazi leo. Daraja lifunguliwe kwa dharura kuruhusu magari


DC ASEMA HAWAJAVUNJA GETI WAMERUHUSIWA KUPITA
Alipoulizwa na JamiiForums kuhusu kilichotokea, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Senyi Ngaga anasema “Hawajavunja geti, ilikuwa jana (Januari 26, 2025) baada ya vivuko kusimama kutoa huduma kutokana na changamoto ya uwepo wa magugumaji.

"Majani hayo yalikuwa mengi kiasi kwamba ingeweza kuathiri utendaji kazi wa vivuko, hivyo kilichofanyika ulifanyika utaratibu Wananchi wakafunguliwa geti na kupitia kwenye njia ile nyingine ya Daraja.

“Sio kweli kuwa wamevunja geti, nadhani ni ile furaha tu ya kuruhusiwa kupita ndio wakajikuta wengine wanasema hivyo, geti lipo vizuri na halina changamoto yoyote.”
 
Hata hivyo ni kakipandeeee🤣🤣🤣😅 daraja liishe tu
 
Kwa hiyo ni sherehe hapo busisi
Na je magari yaliyokuja nao na probably yana mizigo Yao!?
 
Hawa waafrika wengi ni watu wa kuishi kwa kudura sana.

Yani hawajui kuwa kitendo cha kutofunguliwa geti inawezekana daraja halijakamilika/halijaandaliwa kwa matumizi, na huko wanakokimbilia wanaweza kusababisha ajali kubwa.
 
Hawa waafrika wengi ni watu wa kuishi kwa judura sana.

Yani hawajui kuwa kitendo cha kutofunguliwa geti inawezekana daraja halijakamilika/halijaandaliwa kwa matumizi, na huko wanakokimbilia wanaweza kusababisha ajali kubwa.
Hilo walilopita ni lile la dharura mzee ambalo linatumika kupitishia malighafi za ujenzi wa hilo daraja

Lakini vilevile magari ya serikali na viongozi siku hizi hawatumii vivuko huwa wanapita tu hapo sizani kama linaweza kupitisha magari mazito then liwe threat kwa waenda kwa miguu!
 
Hawa waafrika wengi ni watu wa kuishi kwa judura sana.

Yani hawajui kuwa kitendo cha kutofunguliwa geti inawezekana daraja halijakamilika/halijaandaliwa kwa matumizi, na huko wanakokimbilia wanaweza kusababisha ajali kubwa.
HALF HUMANS HALF ANIMALS🤗
 
Hawa waafrika wengi ni watu wa kuishi kwa judura sana.

Yani hawajui kuwa kitendo cha kutofunguliwa geti inawezekana daraja halijakamilika/halijaandaliwa kwa matumizi, na huko wanakokimbilia wanaweza kusababisha ajali kubwa.
Likitokea la kutokea maafa yake sio madogo, lawama itatupiwa serikali kumbe ilikuwa ni jambo la uelewa tu.
 
Wakuu

Baada ya kivuko eneo la Busisi kuzingua na kushindwa kutoa huduma, watu wamevunja geti la Daraja la Magufuli, kisha kuvuka kwa mguu hadi ng’ambo kama video inavyoonesha.

Soma, Pia: Vivuko vya Kigongo-Busisi havifanyi kazi leo. Daraja lifunguliwe kwa dharura kuruhusu magari


DC ASEMA HAWAJAVUNJA GETI WAMERUHUSIWA KUPITA
Alipoulizwa na JamiiForums kuhusu kilichotokea, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Senyi Ngaga anasema “Hawajavunja geti, ilikuwa jana (Januari 26, 2025) baada ya vivuko kusimama kutoa huduma kutokana na changamoto ya uwepo wa magugumaji.

"Majani hayo yalikuwa mengi kiasi kwamba ingeweza kuathiri utendaji kazi wa vivuko, hivyo kilichofanyika ulifanyika utaratibu Wananchi wakafunguliwa geti na kupitia kwenye njia ile nyingine ya Daraja.

“Sio kweli kuwa wamevunja geti, nadhani ni ile furaha tu ya kuruhusiwa kupita ndio wakajikuta wengine wanasema hivyo, geti lipo vizuri na halina changamoto yoyote.”
Ila wasukuma bhana sasa wansvyochekelea yaani..😃😃
 
Hilo walilopita ni lile la dharura mzee ambalo linatumika kupitishia malighafi za ujenzi wa hilo daraja

Lakini vilevile magari ya serikali na viongozi siku hizi hawatumii vivuko huwa wanapita tu hapo sizani kama linaweza kupitisha magari mazito then liwe threat kwa waenda kwa miguu!
Yaani unakuja hapa na nadharia zako za unadhani kutetea huu ujinga wa kutofata utaratibu.

SHITHOLE COUNTRIES NI SHIDA SANA
 
Hilo walilopita ni lile la dharura mzee ambalo linatumika kupitishia malighafi za ujenzi wa hilo daraja

Lakini vilevile magari ya serikali na viongozi siku hizi hawatumii vivuko huwa wanapita tu hapo sizani kama linaweza kupitisha magari mazito then liwe threat kwa waenda kwa miguu!
Point ni kwamba, wahusika wa daraja wakifunga geti, si salama kulazimisha kutumia daraja.

Labda wamefunga kwa sababu kuna matengenezo fulani yamefanyika na kuna sehemu watu wakipita itatokea ajali.

Sasa hapo ukilazimisha kupita ikatokea ajali utamlaumu nani?

Suala si kupitisha magari mazito, suala ni kwamba hujapewa ruhusa kupita hujui daraja lina mapungufu gani bado.
 
Back
Top Bottom