Kasongo Yeyee
JF-Expert Member
- Feb 13, 2019
- 281
- 406
Kazi kweli kweli
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mitano tenaWakuu
Baada ya kivuko eneo la Busisi kuzingua na kushindwa kutoa huduma, watu wamevunja geti la Daraja la Magufuli, kisha kuvuka kwa mguu hadi ng’ambo kama video inavyoonesha.
Soma, Pia: Vivuko vya Kigongo-Busisi havifanyi kazi leo. Daraja lifunguliwe kwa dharura kuruhusu magari
DC ASEMA HAWAJAVUNJA GETI WAMERUHUSIWA KUPITA
Alipoulizwa na JamiiForums kuhusu kilichotokea, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Senyi Ngaga anasema “Hawajavunja geti, ilikuwa jana (Januari 26, 2025) baada ya vivuko kusimama kutoa huduma kutokana na changamoto ya uwepo wa magugumaji.
"Majani hayo yalikuwa mengi kiasi kwamba ingeweza kuathiri utendaji kazi wa vivuko, hivyo kilichofanyika ulifanyika utaratibu Wananchi wakafunguliwa geti na kupitia kwenye njia ile nyingine ya Daraja.
“Sio kweli kuwa wamevunja geti, nadhani ni ile furaha tu ya kuruhusiwa kupita ndio wakajikuta wengine wanasema hivyo, geti lipo vizuri na halina changamoto yoyote.”
Mbona ufafanuzi wa mkuu wa wilaya unaonesha wamefungua makusudi ili kuwahudumia raia?Point ni kwamba, wahusika wa daraja wakifunga geti, si salama kulazimisha kutumia daraja.
Labda wamefunga kwa sababu kuna matengenezo fulani yamefanyika na kuna sehemu watu wakipita itatokea ajali.
Sasa hapo ukilazimisha kupita ikatokea ajali utamlaumu nani?
Suala si kupitisha magari mazito, suala ni kwamba hujapewa ruhusa kupita hujui daraja lina mapungufu gani bado.
Mbona ufafanuzi wa mkuu wa wilaya unaonesha wamefungua makusudi ili kuwahudumia raia?Point ni kwamba, wahusika wa daraja wakifunga geti, si salama kulazimisha kutumia daraja.
Labda wamefunga kwa sababu kuna matengenezo fulani yamefanyika na kuna sehemu watu wakipita itatokea ajali.
Sasa hapo ukilazimisha kupita ikatokea ajali utamlaumu nani?
Suala si kupitisha magari mazito, suala ni kwamba hujapewa ruhusa kupita hujui daraja lina mapungufu gani bado.
Ufafanuzi uko wapi?Mbona ufafanuzi wa mkuu wa wilaya unaonesha wamefungua makusudi ili kuwahudumia raia?