Tetesi: Baada ya kuangukia Pua kwenye ubunge, Kafulila Mbioni kutimikia CHADEMA

Tetesi: Baada ya kuangukia Pua kwenye ubunge, Kafulila Mbioni kutimikia CHADEMA

Lizaboni

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2013
Posts
33,895
Reaction score
20,392
Hii si siri tena.

NCCR Mageuzi ni kama imeshakufa Kigoma. Mtu pekee ambaye pengine alionekana anaweza kuwakilisha chama hicho kwenye Dunia ya Mawese Ni David Kafulila. Amefanya majaribio kadhaa kuhakikisha anarudi mjengoni lakini amekwama. Sasa analia, kutweta na kusaga meno. Ubunge kaukosa. Kilichobaki ni kulea mtoto.

Hata hivyo, taarifa za ndani zinasema kuwa Mwanasiasa huyo kijana na machachari ambaye alitikisa hapo nyuma kwenye sakata la ESCROW Akaunti kwa sasa anajiandaa kutimikia CHADEMA. Mazungumzo yanaendelea vema chini ya ushawishi wa Kada wa CHADEMA, Malisa Godlisten Joseph.

Taarifa zinasema kuwa Malisa na Kafulila ambaye alibatizwa jina la 'Tumbili' wameshakaa vikao kadhaa na kuna mambo wameafikiana. Hata hivyo kuna jambo moja ambalo ndilo kiini na masharti ya Kafulila kuhamia CHADEMA. Kama litafanikiwa basi njia nyeupe kuhamia Ufipa. Jambo hilo ni uwezeshwaji kifedha. Kafulila anataka alipwe kiasi cha shilingi milioni 5 kwa Mwezi kwa kipindi chote ambacho amekosa ubunge. Kwamba, kiasi hicho kitamsaidia kujenga utulivu wa kiakili na hivyo kupata fursa ya kutosha kukitumikia chama chake kipya, CHADEMA kwa masharti kuwa mkoa wa Kigoma uwe na wabunge wa CHADEMA angalau 2 kwenye uchaguzi Mkuu wa 2020.

Je masharti hayo CHADEMA watatekeleza? Na je kama watatekeleza, Kafulila ataweza kupambana na CCM na ACT ambao wameshaweka mizizi kwenye mkoa huo? Tusubiri na tuone.
 
KAFULILA KABLA YA KUHAMIA NCCR ALIKUWA CHADEMA LAKINI KIPINDI YUPO CHADEMA ALIWAHI KUITWA MSALITI LEO HII ANARUDI CHADEMA ,

DAA SIASA HIZI JAMANI
 
Lizabon naona agizo la kurudisha posho limekuchanganya sana....
Kwanza huo uongo wako tambua kuwa vyama washirika wa UKAWA hairuhusiwi kuchukuliana wanachama unless kwa ishu maalum sana na hasa za kikatiba kama ilivyofanyika kwa Juma Duni...Kwahyo hiyo mada yako ni hang overs za kurejesha posho ya mwenge
 
Huko ndio anaelekea kubaya kabisa kisiasa sasa anapotea...

Kwanini mnapenda kuwa Watabiri?

Kubaya wapi wakati ndiko alikotokea, hivyo anarudi kwenye chama kilimjenga.

Lizaboni, kwani akirudi kuendeleza harakati zake kwani atakuwa amekosea? au ulitaka arudi CCM au aende ACT ndio umsifie?

Hilo suala la hela naona umeweka kama propaganda tu kwani hakuna asiyekufahamu.
 
Duuuh!!wewe Jamaa!!Hivj Kafulila akija ni kwa faida yake au ya CHADEMA?Sasa kweli alipwe 5mil kirahisirahisi tu?!Hebu peleka stori zako za kupika huko maana hata mtoto mdogo huwez kumdanganya kwa ulichokiandika hasa kuhusu hela
 
We Jamaa ni Muongo na Mzushi khaa! Et milion 5 kila mwezi... Hahahaaa...daa ndo mana kusini hakuna maendeleo kutokana hiz tabia kama zako
 
Kwanini mnapenda kuwa Watabiri?

Kubaya wapi wakati ndiko alikotokea, hivyo anarudi kwenye chama kilimjenga.

Lizaboni, kwani akirudi kuendeleza harakati zake kwani atakuwa amekosea? au ulitaka arudi CCM au aende ACT ndio umsifie?

Hilo suala la hela naona umeweka kama propaganda tu.
Badala ajenge chama chake anatangatanga nini.. kwan kuanguka kwake ubunge tatizo ni chama au ni yeye binafsi?
 
Hii si siri tena.

NCCR Mageuzi ni kama imeshakufa Kigoma. Mtu pekee ambaye pengine alionekana anaweza kuwakilisha chama hicho kwenye Dunia ya Mawese Ni David Kafulila. Amefanya majaribio kadhaa kuhakikisha anarudi mjengoni lakini amekwama. Sasa analia, kutweta na kusaga meno. Ubunge kaukosa. Kilichobaki ni kulea mtoto.

Hata hivyo, taarifa za ndani zinasema kuwa Mwanasiasa huyo kijana na machachari ambaye alitikisa hapo nyuma kwenye sakata la ESCROW Akaunti kwa sasa anajiandaa kutimikia CHADEMA. Mazungumzo yanaendelea vema chini ya ushawishi wa Kada wa CHADEMA, Malisa Godlisten Joseph.

Taarifa zinasema kuwa Malisa na Kafulila ambaye alibatizwa jina la 'Tumbili' wameshakaa vikao kadhaa na kuna mambo wameafikiana. Hata hivyo kuna jambo moja ambalo ndilo kiini na masharti ya Kafulila kuhamia CHADEMA. Kama litafanikiwa basi njia nyeupe kuhamia Ufipa. Jambo hilo ni uwezeshwaji kifedha. Kafulila anataka alipwe kiasi cha shilingi milioni 5 kwa Mwezi kwa kipindi chote ambacho amekosa ubunge. Kwamba, kiasi hicho kitamsaidia kujenga utulivu wa kiakili na hivyo kupata fursa ya kutosha kukitumikia chama chake kipya, CHADEMA kwa masharti kuwa mkoa wa Kigoma uwe na wabunge wa CHADEMA angalau 2 kwenye uchaguzi Mkuu wa 2020.

Je masharti hayo CHADEMA watatekeleza? Na je kama watatekeleza, Kafulila ataweza kupambana na CCM na ACT ambao wameshaweka mizizi kwenye mkoa huo? Tusubiri na tuone.
lizaboni rudisha pesa za mwenge
 
Chadema inaokoteza okoteza tu wanasiasa imekosa uwezo wa kukuza na kutengeneza wanasiasa mahiri!
 
Chadema inaokoteza okoteza tu wanasiasa imekosa uwezo wa kukuza na kutengeneza wanasiasa mahiri!
downloadfile-2.jpeg

swissme
 
We Jamaa ni Muongo na Mzushi khaa! Et milion 5 kila mwezi... Hahahaaa...daa ndo mana kusini hakuna maendeleo kutokana hiz tabia kama zako
Dr. Alikua akilipwa mshahara wa Mbunge! Naona mnasahau haraka sana!
 
Back
Top Bottom