kidambinya
JF-Expert Member
- Jan 11, 2016
- 1,177
- 1,721
Ok
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu hizi ni kampuni mbili tofauti hata ukisoma hiyo kesi mkurugenzi hakuwa shikaHuu ni mradi wa kujenga hoteli huko Dublin ilio pelekea kufunguliwa kesi ya mazingira miaka hiyo ya 1999
Na hizi ni namba zake za simu enzi hizo 70951399186 (sina uwakika kwa sasa nani anazimiliki) so kuwa mwangalifu ukitaka zitumia kwa lolote.
View attachment 634465
Sawa Kiongozi ngoja niondoe hii picha na kubakiza maneno ila namba nina uwakika nazoa hata @britanicca ana weza kuprove huko aliko kuwa namba hizo zilikuwa ziki muhusu DrMkuu hizi ni kampuni mbili tofauti hata ukisoma hiyo kesi mkurugenzi hakuwa shika
Poa kiongozi yani tunavyomsaka shika hadi kama alikuwa na michepuko lazima ijulikane hakuna jiwe litakalobaki bila kuondolewa...Sawa Kiongozi ngoja niondoe hii picha na kubakiza maneno ila namba nina uwakika nazoa hata @britanicca ana weza kuprove huko aliko kuwa namba hizo zilikuwa ziki muhusu Dr
Kwa Tanzania sio jambo geni, mnakumbuga Mzee wakikombe@ ambikie mwakipasileLancefort Ltd ni kampuni iliyosajiliwa nchini Russia miaka kadhaa iliyopita, na kwasasa haifanyi kazi kwa kipindi kirefu baada ya watendaji wake kupotea gafla kwa mazingira ya kutatanisha.
Kutoka mjini Rostov on don napokaa mpaka Moscow ni mwendo mrefu kidogo ambao ni km 1200 na zaidi, kwa mwendo wa trein ni 5hrs,
nimefika mjini moscow na kuanza kuuliza hasa legality ya kampuni hiyo ndani ya moscow na Urusi kwa ujumla, nimefanikiwa kupata maelekezo ya kukutana na Mtanzania mmoja anaisha mtaa wa Tverskaya Street, ambaye kanikaribisha na kuanza kufanya uchunguzi wangu, nikaamua kwanza nipate hifadhi ndani ya hotel ya Sputnik.
Baada ya kwenda kwa watanzania wanaoishi huku nimegundua huyu mzee alipata matatizo kwa kuhisiwa ni spy wa Marekani, ambaye kapandikizwa kutokea Afrika, na amekuwa akitafutwa na kufuatiliwa nyendo zake zote kuanzia kwenye kampuni yake na nyumbani alipokuwa anaishi.
Mke wake bi Luisa Kvonkov ndo alibanwa na kueleza kwao ni Tanzania Magu, Lakini inasemekana kwamba kuna kampuni kubwa la kimarekani aidha shirika la upelelezi ambalo liko nyuma ya kampuni ya Lancefort, ndio chanzo cha kutiwa msuko suko uko alikokuwa anamiliki kampuni hiyo.
Shirika la Lancerfort limekuwa likimiliki asset kubwa nchini urusi na kwingineko duniani wakati chanzo cha hela yao hakijulikani, hivyo moja kwa moja kuhisiwa ni miongoni mwa mashirika ma spy ambao wafadhili wake ni wamarekani ambao wana uhasama wa mda mrefu na Urusi.
Wametelekeza mali nyingi kukiwemo na private jets na magari ya thamani.
Kupitia wapelelezi wa ndani ya urusi ambao walilichunguza shirika ambalo inasemekana rais wake ni Dr Luis Shika kwa kipindi kile, waligundua mawasiliano ya karibu na baadhi ya mashirika yafuatayo AMNESTY INTERNATIONAL, CIA, FBI , HGRE, OKLE, ambayo mara nyingi huwa ni waanzilishi wa upelelezi katiKa nchi nyingi,
Baada ya kugundua hayo walitekwa na kuwekwa mateka na wawili kuuwawa, mmoja wapo akiwa mkenya Edward Koinange na mwingine wa Siera Leone Yunusu AKhbu, Na wawili kukimbilia Tanzania lakini Rais wao akapelekwa hospitali baada ya kuwatoroka akiwa ameumizwa vibaya, hakutibiwa Urusi alitoroshwa kinyemela mpaka mjini Dnipro Ukraine, na kutoroshewa Tanzania,
Baada ya kufika Tanzania hakuenda moja kwa moja kwao akajificha mjini Dar es salaam, (Haya ni maelezo kwa mujibu wa mtu wake wa karibu)
Baadae kutorokea Uhispania Mjini Malaga , amekaa malaga miez 8 Na kurudi Tanzania,
Mwaka 2012 wakaidhinisha malipo kutoka marekani ambayo bado yapo kwenye mlolongo wa
kukamilisha mchakato,
WITO KWA BALOZI ZETU TUNAOMBA MUWASAIDIE HAWA WATANZANIA WANAOKUWA NA MATATIZO MUWASAIDIE
Tukiachana na Shika wapo watanzania wengi wanaokosa msaada wa karibu sana kutoka Kwa balozi zetu hizi ,
Ukisoma ukatafakari haitadhuru
Tufanye nimemaliza
KUNA MENGI SITAYAANDIKA HAPA KUTOKANA NA KUJUA KWAMBA KUMBE HII ISHU NI CRUCIAL , NA KULINDA USALAMA WA DR,
PIA YATAENDELEA KUWA KUMBUKUMBU ZANGU NA KUZIPELEKA MAALI ZITAITAJIKA KWA KUMSAIDIA DR,
USIKURUPUKE KUKOPI HABARI HII, MAANA CODES ZOTE NINAZO MIMI UTASHINDWA KUITETEA,MTU PEKEE MWENYE UWEZO WA KUWEKA EVIDENCE NI MIMI, IKITOKEA UKAKOPI SEMA UMEITOA WAPI,
Britanicca
![]()
=============Muendelezo=========
Kurbashnov Max Ni Kijana mwenye Umri wa miaka 34, ambaye ni mdogo wa Bwana Falz kurbashnov ambao wote walikuwa wameshaanza kujitambua mwaka 2001 na kujua kilichoendelea baina ya baba yao na Dr Luis Shikamwanafunzi aliyetokea Africa Akitaka kuwekeza wakati akisoma, nimekutana naye baada ya kuuliza ni kina nani walikuwa na hisa katika kampuni ya Lanceford na kupelekwa moja kwa moja kwa kijana ambaye baba yake alikuwa na hisa,
ambaye kanipa mkasa mzima ulivyoenda mpaka familia yake kuhusika kwenye Biashara hiyo na kuingia matatizoni, aeleza uhusiano wa Shika na kikosi cha marekani.
Anaanza
"Mara ya mwanzo walikutana na Baba yetu bwana Kurbashnov katika mgahawa unaoitwa Istoriya unaopatikana,Verkhnyaya Krasnoselskaya ulitsa, Krasnoselsky, 107140 Moscow,
''Baba yetu alipenda sana uwekezaji hasa kujificha nyuma ya wawekezaji kutoka nje ya Urrusi ni jambo ambalo lilimfanya kila anapokutana na mtu anayeonekana kutoka nje ya Rusia lazima amuulize juu ya Fursa za kufanya au kuwekeza kwa kutumia jina la mgeni, maana kwa kipindi kile kulikuwa ni vigumu kuanzisha biashara kwenye sera za kikomunist na ukiangalia ndipo tulikuwa tuna mda mchache tumejitenga katika USSR hivo nchi nyingi zilizojitoa mfano uzerbakistan tunapotokea sisi walikuwa na ushirikiano na Slovenia, na macedonia, ziliona kama zimekosa soko la uwekezaji na wakitaka kurudi hapa walichajiwa hela nyingi kwa kuwakomoa, ndiyo maana warusi wengi waliona ni bora kuwekeza kwa kutumia majina ya wageni ila kwa makubaliano maalumu,''
alielezea bwana kurbashnov Max
Anaendelea:
"Baba yeye ni mbobezi wa masuala ya finance aliyosoma chuo kikuu cha moscow university touro kwahiyo alihisi ni vema kupata mwekezaji ambaye ni mtaalamu wa upande wa finance pia, ila kwa bahati Mbaya Dr shika alionekana kutaka kuwekeza zaidi kwenye chemical na mbolea suala ambalo baba hakulipenda maana watu wa kilimo walipata moja kwa moja msaada toka serikalin hivyo ilikuwa ni ngumu kupata wateja." anaeleza
Anaendelea:
"Baada ya Dr shika kuonekana ana hela kulingana na maelezo ya mzee Shika alikuwa na Russian ruble 2,900,000 ambayo ni sawa na dollars 50,000 za marekani kwa kipindi hicho ambayo ingetosha mtaji mzee wangu akaona ni fursa wangeweza kuchanganya na kupata mtaji mkubwa na hiyo ndo ilikuwa njia iliyomshawish baba yangu kuwekeza kwa kampuni ya mbolea ila aliweka asilimia 25 tu kama jaribio na Dr Shika akaweka 75,"
Baada ya miez kadhaa wakafungua kampuni kwa jina Lancerford ambayo ilikuwa maarufu kwa sababu iliendeshwa na mtu mweusi maana ilikuwa vigumu kupata mweusi anamiliki kampuni wengi wao walikuwa mawazo yao ni kuajiriwa kwenye migahawa kama waiters na kusafisha kama celaners au hotel attendant hata kama ana masters, maana kutokana na ubaguzi wa rangi ilikuwa vigumu kupata kazi za juu"
Kaka yangu Falz kurbashnov akaanza kupata msuko suko kutoka kwa watu wa usalama wakihisi kwamba anatumika na watu wa nje na anapanga mashambulizi ya kigaidi Kutokana na habari hizo kusambaa baba familia nzima ilianza kuyumbbishwa hata miradi yetu ikafungwa na baba mdogo akafungwa jela miaka 10 , baba yangu akakimbia nchi , akabaki Mr shika tu kwenye kampuni ile,
Mama yangu alijuana na afisa mmoja na akataka kufuatilia stahiki za mme wake yaan mzee wetu, lakin afisa mmoja ambaye alimwambia kwamba kuna vijana wameajiriwa katika kampuni ya Lanceford kama maspy wa KGB kujua ni nani hasa mmiliki na amepata wapi hela,mmoja ni muhasibu na mwingine ni wa security,
Baada ya kaka yangu Falz kurbashnov kuajiriwa pale kama mweka hazina msaidizi alisingiziwa kesi akafungwa miaka 20 jela kwa kosa la ugaidi, na kusaidia maspy wa nje,
alifuatwa kazini tulipouliza majirani walisema wameskia akisema kama amekabwa na watu akitamka
“I’m not a terrorist. I’ve never been one,” mbaya zaidi marekani iliweka shinikizo kumfunga jela za kwao kwamba kuna mambo wanayataka toka kwake, ilileta mzozo kidogo lakin baadae wakawekeana masharti na Rusia, urusi nayo ilisema wanamtaka, lakini marekani wakampeleka kwa kubadirishana wafungwa,
Siku wametekeleza ilo tukio ndipo tukaogopa kusogelea maeneo yale kabisa na baadae kuona ofisi imefungwa Tiyari na hatukumuona Tena Dk shika na tulidhani amekufa maana tumepoteza mawasiliano yake,"
Maeneo ambayo Dr shika alipenda kuyatembelea sana ni pamoja na pirogoviskiy ,Pushkino na nikorina gola uko ndipo walipokuwa wamarekani weusi ambao walikuwa marafiki zake na wengi walikuwa command force ya USA kikosi 32 ambacho ni kikosi cha ushirikiano na russia kwa wakati uo,
Hayo ndo maelezo ya kurbashnov Max ambaye anaonekana kwenye picha chini
![]()
Nimefanikiwa kufika maeneo yote ya matukio kwanza nimefika eneo ambalo kulikuwa na office ile bameshabomolewa na kujengwa nyumba nyinginezo
Pili, Eneo ambalo limesemekana alitekwa nimefika lhukovisty nje ya mji wa moscow na kupaona ila liyetuonesha hakusema ndipo alipata mateso dr shika ila ametueleza tukio lililotokea maeneo hayo na muafrica aliyelipotiwa kuwa billionea aliyetekwa na kuwekwa hapo tukaoanisha picha na kuconect dot
Picha yake ni hii:
![]()
Nyumba inasemekana ni ile ile ila imefanyiwa marekebisho mara kadhaa
Imeadaliwa na Britanicca
Acknowledgement muhimu unapokopi plz
Itaendelea baadae na nitasimulia nani alimtorosha na alitumia mbinu zipi, nani anashikiria hela yake na kwanini anaambiwa ailipie bima.
Ninakutana na muhusika kesho Jumatatu asubuhi njema
huyo ni mwehu anahangover ya siasamkuu mbona dr. hausiani na mambo ya siasa
mambo mengi ya Urusi hayapo googlyau mtandaoni unless otherwise uandike kwa kirusinakataa kabisa,ukiangalia hiyo website hakuna picha za ofisi,adress ya kampouni hakuna, e mail wanatumia msn wakati proffesionally ilitakiwa labda drshika@lancefortltd.ru then angalia vizuri website yao..www.lancefort.narod.ru ni free hosting sio za kulipia thats why kuna narod katikati ni kama .blogspot.com au .yola.com,website kwa mjanja akiingalia kwa macho tu changa la macho
Uki search google hawana rekodi ya kueleweka no results kabisa,kampuni moja inafanya shughuli kama 40,kuanzia fertilisers,petroleum,pharmaceutical hakuna hata picha za ma executives,mnadanganyika sababu kuna website tena ya free hosting?
CIA,FBI watengeneze bogus company in a foreign soil ambayo ina deal hadi na gesi na petrol?they must be crazy,CIA,FBI wakitaka info nzuri za nchi kama Russia huwa wanatumia wan KGB wa kulekule ndani(MOLES)refer story ya OLEG KALUGIN
nakataaa nakataaaa nakataaaaa ,mtoa mada hata kama kaeleza alichoambiwa simply ni kwamba mzee LUNYALULA KIDOLA aliwanywesha chai ya moto wabongo wa huko ku explain issue yake ya kukatwa vidole na kupoteza meno aka acome up with a fascinating story. NOOOOO
mwisho wake unakaribiaNgoja niendelee kuwa msomaji kwenye sakata la huyu daktari.
ndo maana watu wanahisi kwamba alikuwa anatumiwa na watu wenye masilahi binafsibritanicca hii sukari guru unayotupikia ni kwq hisani ya nani?!
Mtu alikuwa mtumishi wa umma kama daktari ila a kapata scholarship ya kuongeza elimu huko Urusi,ghafla awe milionea?! Moscow kwa anaeifahamu ni ngumu sana kwa mwafrica hata uwe mtoro wa waziri fisadi ukafika na kuwa mfanyabiashara mkubwa na ukwasi!!
Wengi wanaosoma Russia toka Tanzania wanategemea boom ambalo huwa halitoki hadi waandamane kwenye ubalozi kipindi cha baridi kali na enzi za kina Dr Shika boom lilikuwa hali zizi dola 3500$ kwa mwaka
Kwa kumbukumbu zangu ni kuwa vibarua vya inostranii wakati wa summer havizidi ruble 500 kwa siku ambayo kwa exchange rate ya dolar ni 1$ kwenye 60 ruble kwa sasa na vichache sana iwe kwenye mahotel ama migahawa kwa hawapendi kuajiri chornii/bblacks.
Mnatoka tuamini ghafla alienda huko na utajiri wake?!!