Baada ya kufuatilia uendaji wa chooni wa huyu dada muuza mgahawa, nimejiapiza sili tena migahawa ya uswahilini

Wahudumu wengi wa chakula huwa hawana tabia ya kumpa mteja sabuni ya kunawa mikono kabla ya kula, na ukitaka wakupe wengine wanakuona msumbufu, ila huwa wanaileta ukimaliza kula!
 
Ukimchunguza sana bata, hutokuja kumla kamwe.
Usafi sio bata, na bata akisafishwa hana shida. Wahadumu wa chakula wanapaswa kuanda chakula katika mazingira ya usafi, tuachane na mambo ya uswahili mwingi usio na tija.
 
Wahudumu wengi wa chakula huwa hawana tabia ya kumpa mteja sabuni ya kunawa mikono kabla ya kula, na ukitaka wakupe wengine wanakuona msumbufu, ila huwa wanaileta ukimaliza kula!
Wakati kunawa kwa sabuni kabla ya kula ni kwa usalama wako ila kunawa baada ya kula ni ustaarabu tu!

Ustaarabu unapewa kipaumbele kuzidi afya😀
 
Wakati kunawa kwa sabuni kabla ya kula ni kwa usalama wako ila kunawa baada ya kula ni ustaarabu tu!

Ustaarabu unapewa kipaumbele kuzidi afya[emoji3]
Ipo haja ya kuweka somo la usafi na afya ya binadamu kuanzia primary hadi chuo kikuu katika nchi hii.
 
Huyo ni msafi.

Umewahi kuona mkaanga au mchoma chapati wewe? Sema hapana, hapa kijiweni yupo, akimsafisha mtoto ni kwamba kazi inaendelea.

Mungu tu analinda walaji
Hawa wanawake wachoma chapati ndo funga kazi🙌, At least wale wanaume unakuta wanazichoma wakiwa wamesimama na wanavaaga kikazikazi na chapati zao huanzia 500+, Ila hawa wamama wa chapati za 250 hawa ni mziki kwenye suala la uchafu
 
Ipo haja ya kuweka somo la usafi na afya ya binadamu kuanzia primary hadi chuo kikuu katika nchi hii.
Sijui kama itasaidia sana! Labda kama ingewezekaba kuwekwa mkakati utakaoilazimisha kila familia kujenga tabia ya usafi, pengine ingesaidia.

Naamini usafi ni tabia ambayo mtu anapaswa kujengewa tokea akiwa mchanga.

Inashauriwa na wataalam, kwa mfano, mtoto tokea akiwa mchanga, kila anapojisaidia, akishafanyiwa usafi, anawishwe mikono kwa maji na sabuni. Afanyiwe hivyo pia kabla na baada ya kulishwa chakula.

Vitendo hivyo vitaishia kujikita kwenye kumbukumbu ya ndani na hivyo inakuwa kama vile ni tabia ya kuzaliwa nayo. Wengine wakikutana na mtu wa aina hiyo, watakuambia usafi upo kwenye damu, kumbe ni tabia aliyofundishwa tokea akiwa mchanga.
 
Hawa wanawake wachoma chapati ndo funga kazi🙌, At least wale wanaume unakuta wanazichoma wakiwa wamesimama na wanavaaga kikazikazi na chapati zao huanzia 500+, Ila hawa wamama wa chapati za 250 hawa ni mziki kwenye suala la uchafu
Kweli kabisa, anapokea pesa mkono huo huo na kushika chapati mkono huo huo, yaani ni kama hawaelewi kabisa.
 
Migahawa ya level ya kati hizi hand wash zikiisha wanajaza tena maji kwenye kile kichupa ndio maana unaona ni nyepesi. Maji yenyewe ya ndoo hayakufanyi ukanawa kabisa kabisa 100%. Bongo ni shida sana.
 
Kweli kabisa, anapokea pesa mkono huo huo na kushika chapati mkono huo huo, yaani ni kama hawaelewi kabisa.
Mazoea! Kafanya hivyo tokea akiwa mtoto na hakuna aliyewahi kumwambia kuwa ni vibaya.

Wengine, hata ukisema uwaelekeze, wanaweza wakakuona una majivuno. Watakuambia wamekuwa wakifanya hivyo tokea zamani na haijawahi kuwaletea shida.

Sasa mtu kama huyo unafikiri itakuwa rahisi kumbadilisha?
 
Migahawa ya level ya kati hizi hand wash zikiisha wanajaza tena maji kwenye kile kichupa ndio maana unaona ni nyepesi. Maji yenyewe ya ndoo hayakufanyi ukanawa kabisa kabisa 100%. Bongo ni shida sana.
Kazi ipo.
 
Kuna mwaka mkuu wa mkoa wa lringa , kreluuu alifariki na kipindupindu, jiulize kwake vijakazi wangapi wa usafi, kwenye magonjwa kuomba mungu tu.
 


Kuna mugahawa mikubwa wanaweka kikombe kimoja cha maji ya maiti kwenye vyakula vyao kila siku, usile kabisa, kajipikie.
 
Mtu na akili timamu anategemea kweli elfu 2 itamoatia mlo? Serious???
 
Hakika hili ni janga,migahawani hadi mahotelini ni majanga,mamantilie ndio funga kazi uchafu kuanzia vyombo,vyakula hadi usafi wao binafs hasa wapemba ogopa sana migahawa ya wapemba.

Mahotelini wanajitajidi kwa usafi ila mnalishwa sana expired products pia na chakula kilicholala.

Kama una option achakula huko kale chakula cha kupikwa nyumbani kwako.
 
Kuna mwaka mkuu wa mkoa wa lringa , kreluuu alifariki na kipindupindu, jiulize kwake vijakazi wangapi wa usafi, kwenye magonjwa kuomba mungu tu.
Umesoma ulichoandika?
Kwa hiyo alivofariki huo mwaka
Baadae mwaka uliofuata akafufuka?

Halafu akauwawa tena na mwanamalundi?
Ebu weka sentence yako vzr
 
Bila kapicha haieleweki
 
Huko siyo uswahilini, huko ni ushenzini. Waswahili usafi ni jadi yetu. Koma.

Si kila anaeongea Kiswahili ni Mswahili.
Endelea kujifariji na kuwafiriji hivyo uswahilini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…