Baada ya kukaa masaa matatu kwenye foleni, nauliza, hatuwezi kujenga flyover juu ya Mfugale bridge?

Baada ya kukaa masaa matatu kwenye foleni, nauliza, hatuwezi kujenga flyover juu ya Mfugale bridge?

Mi mwenyewe nimepita sasa hivi.
Waliamua kujijengea wenyewe wakitoka airport wapite kiulaini.

Mi nadhani wangeteneza roundabout buguruni ili kuruhusu magari kutoka tazara yawe yanasogea haraka.

Kwa sasa traffic police wa tazara akiruhusu magari kuja buguruni, wa buguruni anakuwa ameyazuia yanayotoka tazara. Hawana mawasiliano. Kwa hiyo, pale kwa mfugale yatavuka magari machache tu na foleni ya buguruni inakuwa darajani tayari.

Roundabout buguruni ingesaidia sana kama pale ubungo.

Au hadi awepo mchina?
Bandari kuwa bagamoyo ingepunguza stress

Pia reli au kutengeneza outer road ndio solution
 
inawzekana kabisa! inaanzia buguruni matumbi all the way mpaka mbele ya tazara kule

Ushauri:- magari yote yanayotoka gongo la mboto kwenda mjini kupitia barabara ya Uhuru yote yapite daraja la mfugale, kisha barabara ya buguruni Rozana inyooshwe kwenda barabara ya Nyerere ikiungia pale NBC, magari kutoka Tabata na Kwa Mnyamani ndiyo yapite buguruni shell kufuata barabara ya Uhuru kwenda mjini. Magari kutoka Gongo la mboto kwenda Ubungo tu ndiyo yakunje pale tazara kwenye daraja la Mfugale, pale buguruni shell kutoka tazara magari yasipinde kulia kufuata barabara ya uhuru. Abiria wote kuelekea Gongo la mboto kutoka mjini wapande na kuteremka kwenye kona ya Rozana.

Abiria kutoka Ubungo kwenda Gongo la mboto na mbagala ndiyo wapande na kuteremka buguruni shell kituo cha sasa.

Magari yanayotoka mbagala kwenda Rozana nayo yaungane na yale yanayotoka gongo la mboto kwenye daraja la Mfugale.

Daraja la Mfugale liongezwe mpaka pale NBC ili magari yanayotoka Rozana yapite chini kuingia barabara ya Nyerere.

Nina uhakika foleni ya Tazara kutoka bandarini na mbagala itapungua.

Injinia Mfugale weka mchoro.
 
Nafikiri construction inayofanyika pale buguruni SGR inaweza kuchangia tatizo pale tazara, lakini pia uamuzi wa haraka ufanyike pale Buguruni, either ijengwe flyover nyingine au ijengwe roundabout kubwa itakayoenda sambamba na ujenzi SGR.. ili lile daraja la SGR likiisha na round about iwe imeisha..
 
pale tazara chini ya daraja la mfugale wangeweka mzunguko na mzunguko mwingine buguruni pia na mataa ya chang'ombe. Kiasi kikubwa ingepunguza foleni.

Taa zinachangia sana kuongeza foleni mijini.
Foleni ya sehemu hii inachangizwa na vitu viwili kwanza malori yanayotoka bandarini ukiona umefika njia hii pita service road kuanzia pale sokota utapitia nyuma huku kwenye maduka ya hardware utokee karibu na TCC kisha ingia nyerere rd au pitia njia ya mchicha kutokea magorofani au kuna rough road pale njia ya wizara ya kilimo kisha ingia nyerere road pili uwepo wa traffic police tazara junction na buguruni sijui hawa jamaa wana watu wao wanawavusha kutoka town yaani upande huu wa bandari zikizidi sana ni dakika mbili kuvuta na kiukweli taa zinafanya vizuri kuliko hawa jamaa either way


Sent from my iPhone using JamiiForums

Sent using Redmi Y2
 
Ushauri:- magari yote yanayotoka gongo la mboto kwenda mjini kupitia barabara ya Uhuru yote yapite daraja la mfugale, kisha barabara ya buguruni Rozana inyooshwe kwenda barabara ya Nyerere ikiungia pale NBC, magari kutoka Tabata na Kwa Mnyamani ndiyo yapite buguruni shell kufuata barabara ya Uhuru kwenda mjini. Magari kutoka Gongo la mboto kwenda Ubungo tu ndiyo yakunje pale tazara kwenye daraja la Mfugale, pale buguruni shell kutoka tazara magari yasipinde kulia kufuata barabara ya uhuru. Abiria wote kuelekea Gongo la mboto kutoka mjini wapande na kuteremka kwenye kona ya Rozana.

Abiria kutoka Ubungo kwenda Gongo la mboto na mbagala ndiyo wapande na kuteremka buguruni shell kituo cha sasa.

Magari yanayotoka mbagala kwenda Rozana nayo yaungane na yale yanayotoka gongo la mboto kwenye daraja la Mfugale.

Daraja la Mfugale liongezwe mpaka pale NBC ili magari yanayotoka Rozana yapite chini kuingia barabara ya Nyerere.

Nina uhakika foleni ya Tazara kutoka bandarini na mbagala itapungua.

Injinia Mfugale weka mchoro.
Nimesoma hadi mwisho ila kuanzia paragraph ya tatu maelezo ya hizo ruti mpya ni full kuchanganyika na kama ikiwa hivyo aysee gari zitagongana kila uchao.
 
Inabidi wapige nyingine ya juu kama wachina wanavyo fanya ubungo kwa aliji ya magari yanayo toka bandarini kuelekea buguruni.


Pili vituo vyote vya daladala vitolewe karibu na junction ya tazara.

Pia njia za chochoro ziongzwe.

Mfano mtu katoka bandarini kuelekea airport kwanini apite tazara?

Daraja la tazara halija jengwa kuondoa foleni bali limejengwa wakubwa wasifiwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku hizi mtu akimaliza pale Mlimani au hata DIT analazimisha jina lake lianze na Eng. eh Eng. Kilaza Mshiko. Eng. M. Shirikina, Eng. Mambo Kisawa etc. Ukimleta kwenye ground a design kitu ndio unakuta hela inatumika nyingi halafu foleni iko pale pale. What we need in Dar is an outer ring road kama Nbi au Kla. Hata pale Ubungo pakiisha, as long as Buguruni kuna zile four busy ways, hakuna tatizo litakalotatuliwa kwa wanaokwenda na kutoka port.
 
Round Imeonyesha zinweza kutatua tatizo. Buguruni waweke round about kubwa. Ushahidi wa round about ni pale ubungo.
Ningekuwa mimi ningezuia kabisa magari yanayotoka mjini na.uwanja wa ndege kupita chini. Yote yangepita juu.
Hakuna sababu ya gari.kutoka mjini kwenda Airpot lipiye chini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bandari kuwa bagamoyo ingepunguza stress

Pia reli au kutengeneza outer road ndio solution
Nadhani SGR ikianza kazi hii pressure itapungua maana malorry yatachukulia mizigo huko Morogoro..
 
Zinashindwa kazi huku zikiwa zinawaka katika utaratibu wake!?
Kuna nyakati za rush hours Human Intelligence inahitajika for maximum efficiency. Taa zinaweza zikaita hata kama hakuna gari uoande huo na ikasimamisha uoande ambao una magari kwa sababu ni kama programmed robot, halifikirii kama binadamu, umenielewa?
 
Back
Top Bottom