Baada ya kutoka jela, Emmanuel Mbasha azungumzia kuhusu Flora Mbasha

chongchung

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2013
Posts
13,277
Reaction score
40,924
ALICHOKISEMA EMMANUEL MBASHA KUHUSU MKE WAKE FLORA MBASHA.



Baada ya maneno mengi kuzaga kila kona ya Tanzania kwa wanandoa hawa wa wili.....Emmanuel Mbasha amefunguka na kuweka wazi anampenda mke
wake Flora Mbasha.

Kupitia kipindi cha Amplifaya cha Millardayo siku ya jana,Emmanuel Mbasha amesikika akisema anampenda mke wake Flora hivyo anamuomba arudi nyumbani wale familia.

 
Last edited by a moderator:
Frola Mbasha akomba kila kitu kilichobakia ndani,



sehemu ya chumba cha kupumzikia kilichobakiwa na kochi na zulia.

Ilisemekana kwamba wakati hayo yakiendelea, Mbasha alikuwa nyuma ya nondo za Mahabusu ya Keko jijini Dar es Salaam ambako alishikiliwa.Kwa mujibu wa mtu aliyeambatana na Mbasha alipopata dhamana dhidi ya kesi yake inayomkabili ya ubakaji wa shemejiye mwenye umri wa miaka 17, alipofika nyumbani kwake Tabata-Kimanga, Dar alipigwa butwaa kukuta hakuna vitu ndani!



Chumba kingine kilichosafishwa kabisa bila ya samani yoyote

Habari zilidai kwamba alipowauliza majirani kama walimuona mtu akiingia ndani walimwambia mkewe (Flora) ndiye alikuwa akiingia na kutoka mara kwa mara.

Ilielezwa kuwa vitu hivyo vilihamishwa Juni 16 ambapo Mbasha alitoka mahabusu Juni 17, yaani siku moja tu. Baadhi ya vitu vilivyodaiwa kuchukuliwa
nyumbani hapo ni kitanda cha bei mbaya walichokuwa wakilalia kwenye chumba cha baba na mama huku akimwachia neti ikiwa inaning’inia.



Vingine ni makochi huku akibakisha sofa ndogo ya mtu mmoja, vitu vyote jikoni na nguo (suti za bei mbaya, walizonunua wakati wakiwa Marekani).

Pia alidaiwa kukomba vile vidani vyote vya dhahabu.jamani hebu sikilizeni kilio cha mumewe Flora jamani daah wakati mwingine sisi wanawake tunaingia tamaa sijui yaani shetani ana nguvu sana tena sana, Flora hivi ataimbia wambi injili yake baada ya hili tukio hii inafanya watu wawaone walokole ni wanafiki sanakumbe si woteshame, shame.

 

Attachments

  • chumba.jpg
    35.8 KB · Views: 5,731
  • IMG_0150.jpg
    38.4 KB · Views: 5,693
Halafu Joyce Kiria, ndio anajitokeza kusambaratisha ndoa hii, lolote lile litakalotokea laana lazima impate Joyce Kiria!
 
Sasa wale waliokuwa wanainjinia Emma amuache Flora kimewanukia sasa mapenzi ya wawili bhana huyawezi.
 
Sioni sababu ya kufuatilia suala km hili ambalo mwisho wake hauna faida yoyote ile zaidi ya kusababisha ugomvi tu na kupoteza mda!!!
 
......................Chukua jembe ukalilime
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…